Tanzanite yaendelea kuhujumiwa,wawekezaji wauza madini ghafi nje

Mtoto wa Mkulima

JF-Expert Member
Apr 12, 2007
681
126
Tanzanite yaendelea kuhujumiwa,wawekezaji wauza madini ghafi nje
Na Mwandishi Wetu

AGIZO la serikali la kupiga marufuku usafirishaji nje ya nchi wa tanzanite ghafi lililotolewa miaka minne iliyopita, limeshindwa kutekelezwa baada ya wadau kuendelea kuuza madini hayo ghafi nje ya nchi.


Uchunguzi umeonyesha kwamba wadau wote wa madini hayo akiwamo mwekezaji wa madini tanzanite, Kampuni ya Tanzanite One ya Arusha bado wanasafirisha madini hayo ghafi kwenda nje kuyauza.


Hali hiyo inatokana na serikali kushindwa kusimamia agizo lake ililolitoa mwaka 2003.


Waziri wa Nishati na madini wa wakati huo, Daniel Yona katika hotuba yake ya bajeti alisema kwamba serikali imependekeza madini ya tanzanite yaanze kukatwa hapa hapa nchini kabla ya kusafirishwa kwenda nje.


Yona alisema serikali imetangaza kusudio la kupiga marufuku usafirishaji nje wa tanzanite ghafi na kwamba kufuatia tamko hilo, wizara ilituma ujumbe kutembelea nchi ambazo huchukua madini ya Tanzanite kama malighafi ikiwamo India, Thailand na Italia.


Alisema katika ziara hiyo waligundua kwamba kusanifu tanzanite nchini italeta faida kubwa na kwamba Tanzania inabidi itekeleze uanzishaji wa maeneo huru ya biashara (EPZ) kwa kukaribisha mifuko ya pensheni nchini kuwekeza katika ujenzi wa majengo ya kupangisha katika maeneo hayo na kuongeza mafunzo ya ukataji vito ndani na nje ya nchi.


Mwenyekiti wa Chama cha Wauzaji wa Madini Tanzania (TAMIDA), Sammy Mollel aliliambia Mwananchi kuwa hatua ya Kampuni ya Tanzanite One kusafirisha madini ghafi kuyapeleka Afrika Kusini kuyauza limechangia kwa kiasi kikubwa kuua soko la madini hayo nchini.


Alisema kuhamishiwa kwa soko la madini hayo Afrika Kusini kumewafanya wanunuzi wazawa kushindwa kupata nafasi ya kununua madini hayo na kuiachia Kampuni tanzu ya Tanzanite one Trading, kununua madini yote na kuyapeleka Afrika Kusini kuuzwa kwa mawakala wao.


"Biashara ya tanzanite hapa nchini imekufa, tumekubali kuhamisha soko na ajira Afrika Kusini, " alisema Mollel.


Pia alisema kupungua kwa upatikanaji wa madini katika eneo hilo kumechangiwa na uamuzi wa serikali kufunga migodi 30 ya wachimbaji wadogo kutokana na mgogoro uliokuwa ukiendelea kati yao na mwekezaji Kampuni ya Tanzanite. Zaidi ya wachimbaji wadogo 1,500 wamepoteza kazi.


Mollel alisema wachimbaji hao hivi sasa hawana kazi na kwamba uamuzi huo unaweza kuongeza idadi ya wahalifu mitaani.


Alisema ingawa sera ya madini inasema wazi kuwa mchimbaji mdogo atasaidiwa kupatiwa soko, ufundi na elimu ili aweze kuzalisha zaidi , lakini wachimbaji wa Mererani serikali imewaacha kama yatima.


Alitoa mfano wa serikali ya Thailand ambayo imeendeleza sekta ya madini kwa kuwawezesha wananchi wake kuchimba badala ya kukumbatia wawekezaji kutoka nje.


Hata hivyo, Afisa Uhusiano wa Kampuni ya Tanzanite One, David Marealle aliliambia Mwananchi kuwa tatizo linalowakabili wachimbaji wadogo Mererani ni kukosa mitaji kwa ajili ya kuwekeza katika uchimbaji.


Alisema madai kwamba madini katika eneo hilo yamekwisha na kwamba kampuni yao ndiyo ambayo imehodhi eneo lenye madini zaidi hayana msingi.


Marealle alisema wachimbaji wadogo kama wangeweza kuungana na kupata mtaji mkubwa wanaweza kupata uwezo wa kununua vifaa vya kisasa vya kuchimba na hivyo kuendelea kupata madini mengi.


"Wachimbaji wadogo, waungane wapate mtaji wa kununua vifaa vya kisasa , madini yapo, lakini kama wataendelea kubaki mmoja mmoja hawawezi kupata madini mengi," alisema.


Kuhusu kampuni yao kuhodhi soko la tanzanite na kupeleka madini hayo ghafi Afrika Kusini kuyauza, Merealle alisema kitendo cha Tanzaniate One kununua madini mengi kimesaidia serikali kupata makusanyo makubwa ya kodi inayotokana na madini.


Alisema kampuni yao inailipa serikali hela nyingi tofauti na zamani ambapo watu walikuwa wakitorosha madini hayo kinyemela na kuyauza nchi jirani bila ya serikali kupata chochote.


Afisa Uhusiano huyo alisema kampuni hiyo hivi sasa imehamishia mjini Arusha makao makuu yake kutoka Afrika Kusini na kwamba ipo mbioni pia kulirejesha soko la madini hayo hapa nchini.


Katibu Mkuu Wizara ya Nishati na Madini, Athur Mwakapugi alipoulizwa kuhusu suala hilo, alikiri kuwa bado makampuni ya madini ya tanzanite yanaendelea kusafirisha madini hayo ghafi kwenda nje ya nchi.


Hata hivyo, alisema angetoa maelezo zaidi kuhusiana na suala hilo baadaye.


Kupungua kwa shughuli za madini Mererani kumesababisha kupungua kwa mzunguko wa hela na hivyo kuwalazimisha baadhi ya wachimbaji wadogo na wafanyabiashara kuanza kuondoka katika eneo hilo.


Mji wa Mererani ambao miaka mitatu iliyopita ulikuwa umefurika watu muda wote wengine wakiwa baa na maeneo mengine ya starehe huku wengine wakiwa katika mashimo wakichimba madini ya Tanzanite hivi sasa, umeaanza kupungua watu.
 
Ikizingatiwa madini haya yanapatikana Tanzania tu...kuwepo na chombo kama OPEC au kuwe na msimamo kama wao, au iundwe kampuni ya serikali na iendeshwe kibiashara kama de-beers(wauza almasi)!
????????????????????????????????????????????????????????????????
Tutanufaika!
 
Ikizingatiwa madini haya yanapatikana Tanzania tu...kuwepo na chombo kama OPEC au kuwe na msimamo kama wao, au iundwe kampuni ya serikali na iendeshwe kibiashara kama de-beers(wauza almasi)!
????????????????????????????????????????????????????????????????
Tutanufaika!

Ni kweli kabisa kwa sabu sisi tuna natural monopoly tuliyopewa na Mungu. Haya madini yanapatikana Tanzania tuu lakini cha kushangaza hatupo hata kweny top five ya wauzaji wa Tanzanite duniani. Ndugu zetu wa kenya na India ndio wanaongoza kwa uuzaji wa Tanzanite. kama kunatamko kama hili kwanini lisifanyiwe kazi mara moja? Jamaa anasema eti wanalipa kodi kubwa. Unalipa kodi na wakati unaexport madini yetu na ajira zote nje? unalipa kudi na wakati una export uchumi wetu unatuachia mashimo?
 
Kipande cha Tanzanite yaani chenye urefu na mapana 8*10mm oval shaped na 2.5 carat kinaweza kununuliwa na dola $2400!

Hii ilikuwa inauzwa kwenye luninga moja huko ughaibuni...chakushangaza ni pale walipodai Tanzanite ina miaka kumi tu kabla ya kutoweka!
Hivi hii ni kweli? Na kama ni miaka kumi tu ndio iliyobaki basi tuiachilie kama kitega uchumi?
 
Ikizingatiwa madini haya yanapatikana Tanzania tu...kuwepo na chombo kama OPEC au kuwe na msimamo kama wao, au iundwe kampuni ya serikali na iendeshwe kibiashara kama de-beers(wauza almasi)!
?????????????????????????????????????????????????? ??????????????
Tutanufaika!


Ni kweli kabisa kwa sabu sisi tuna natural monopoly tuliyopewa na Mungu. Haya madini yanapatikana Tanzania tuu lakini cha kushangaza hatupo hata kweny top five ya wauzaji wa Tanzanite duniani. Ndugu zetu wa kenya na India ndio wanaongoza kwa uuzaji wa Tanzanite. kama kunatamko kama hili kwanini lisifanyiwe kazi mara moja? Jamaa anasema eti wanalipa kodi kubwa. Unalipa kodi na wakati unaexport madini yetu na ajira zote nje? unalipa kudi na wakati una export uchumi wetu unatuachia mashimo?



Mtoto wa Mkulima,
Walahu sala zetu zimefika kunako!




Mizengo Pinda atahadharishwa
2008-02-11 10:20:04
Na Restituta James, Dodoma


Kambi ya Upinzani Bungeni imemtahadharisha Waziri Mkuu, Bw. Mizengo Pinda, kuandaa sera ya Taifa ya kulinda, kutunza na kusimamia matumizi ya rasilimali za nchi ili kuzuia uporaji wa maliasili hizo kupitia mikataba mibovu na ufisadi.

Ilisema madini, gesi asilia na wanyamapori ni miongoni mwa maeneo yenye mikataba ya kinyonyaji iliyotokana na kukosekana sera na taratibu za kulinda, kusimamia na kutunza maliasili hizo.

Kiongozi wa Kambi hiyo Bungeni, Bw. Hamad Rashid Mohamed, alisema katika mahojiano maalum na Nipashe kuwa sera hiyo itakayoambatana na sheria, ndiyo pekee itakayoelekeza kila mwekezaji wa nje na ndani kujua msimamo wa nchi juu ya rasilimali zake.

Alimshauri Waziri Mkuu kuimarisha kitengo cha kutambua na kutafiti rasilimali za Taifa ili zijulikane na kusimamiwa kisheria kwa mujibu wa sera zinazohakikisha kuwa kunakuwa na manufaa kwa umma.

``Tunahitaji kuwa na sera ya kulinda mali za Taifa ili kila anayewekeza ajue msimamo na masharti, siyo kuwakaribisha wawekezaji ambao wanatunga sheria na kutoa masharti yao tunayoyafuata lakini kwa manufaa yao licha ya kuwa rasilimali ni mali yetu,`` alionya.
Bw. Mohamed alisema sera ya madini na sheria zina upungufu na zinawapendelea wawekezaji zaidi kuliko wananchi na kwa upande mwingi haitofautishi aina za madini, mathalani tanzanite, rubi na dhahabu.

``Tanzanite ni madini pekee duniani, yalitakiwa kuwa na sera na sheria yake na masharti na muda wa kuyachimba na kubainisha wajibu wa wazawa na mwekezaji kiasilimia na kuchimbwa kwa wakati,`` alisema Bw. Mohamed.
Alitoa mfano wa Australia ambapo wawekezaji pamoja na kuwa na leseni ya kuchimba yureniam, sheria inakataza uchimbaji hadi serikali kwa wakati wake itakaporuhusu.

``Sheria iwe wazi kwa kila maliasili iwe gesi, mafuta, dhahabu au shaba kuhakikisha zinawanufaisha wananchi kuondoa umaskini na si kuingia mikataba mibovu inayoendeleza unyonyaji,`` alisema kiongozi huyo wa upinzani.

Mwishoni mwa wiki, Mbunge wa Same Mashariki (CCM) Bi. Anne Kilango Malecela, alisema ni lazima serikali izitambue na kuzilinda maliasili kama madini, wanyama, samaki na gesi bila kujali matakwa ya mataifa ya nje ama kupewa masharti ya wawekezaji.

``Tuige mfano wa Waarabu. Wanasimamia mafuta yao bila kujali maslahi ya Marekani, Uingereza wala Japan. Wamezingatia sera na sheria na kulinda maliasili yao kwa vizazi na vizazi,`` alisisitiza.
Bi. Kilango alisema kukosekana sera na sheria ya ulinzi wa maliasili kumesababisha mikataba mibovu ya madini ambayo Rais ameunda tume kupitia sheria na sera za madini.

SOURCE: Nipashe
Atleast we are moving towards somewhere
Mimi ningeomba kusitisha mara moja Uuzaji Uchimbaji wa Tanzanite mpaka hii mada itakapo eleweka..
 
Written by ADIUE HUMBLE
Saturday, 23 May 2009


ARUSHA, TANZANIA - TanzaniteOne has paid nearly TShs16 billion to Tanzania treasury in five years.

TanzaniteOne is the leading mining firm dealing in tanzanite in Tanzania's northern parts of Mererani Hills.

The London Stock Exchange listed firm has since 2004 been mining a rare gemstone in the 100-square kilometre Block C, in Mererani Hills, some 70 kilometres south-east of Arusha.

"We have paid TShs15.7 billion in form of taxes into the Tanzanian treasury in the course of five years," TanzaniteOne Chairman, Ambassador

Ami Mpungwe said in a statement. The breakdown shows five years down the line, the firm has paid close to TShs8.4 billion in Corporate Tax; TShs7 billion in Royalties and TShs319 million in Gemstone Service Levy; making a total of 15.7 billion. Besides the taxes, Mpungwe said, TanzaniteOne has also contributed significantly to the formalization, modernization and integration of the tanzanite industry.

"We have struggled immensely in stabilizing supply lines of Tanzanite to the world markets, undertaking a number of promotional and marketing initiatives for tanzanite worldwide, contributing significantly to the social and economic infrastructure of the neighbouring communities," Mpungwe noted. Tanzanite a precious blue gemstone exclusively mined in Tanzania.

It is a US$500 million a year industry although Tanzania gets barely $20 million annually, with the lion's share going to Indian and American dealers.

Discovered by Ali Juwa Watu in 1967 at what is now known as Block C area in Mererani Hills, the gems have been mined for 42 years.

Tanzania earns $12m from tanzanite mines .
 
Written by ADIUE HUMBLE
Saturday, 23 May 2009
ARUSHA, TANZANIA - TanzaniteOne has paid nearly TShs16 billion to Tanzania treasury in five years.

TanzaniteOne is the leading mining firm dealing in tanzanite in Tanzania's northern parts of Mererani Hills.

The London Stock Exchange listed firm has since 2004 been mining a rare gemstone in the 100-square kilometre Block C, in Mererani Hills, some 70 kilometres south-east of Arusha.

"We have paid TShs15.7 billion in form of taxes into the Tanzanian treasury in the course of five years," TanzaniteOne Chairman, Ambassador

Ami Mpungwe said in a statement. The breakdown shows five years down the line, the firm has paid close to TShs8.4 billion in Corporate Tax; TShs7 billion in Royalties and TShs319 million in Gemstone Service Levy; making a total of 15.7 billion. Besides the taxes, Mpungwe said, TanzaniteOne has also contributed significantly to the formalization, modernization and integration of the tanzanite industry.

"We have struggled immensely in stabilizing supply lines of Tanzanite to the world markets, undertaking a number of promotional and marketing initiatives for tanzanite worldwide, contributing significantly to the social and economic infrastructure of the neighbouring communities," Mpungwe noted. Tanzanite a precious blue gemstone exclusively mined in Tanzania.

It is a US$500 million a year industry although Tanzania gets barely $20 million annually, with the lion's share going to Indian and American dealers.

Discovered by Ali Juwa Watu in 1967 at what is now known as Block C area in Mererani Hills, the gems have been mined for 42 years.
Tanzania earns $12m from tanzanite mines .
Huyu Mpungwe Kapungukiwa akili kabisa. Tanzanite One inaingiza zaidi 1bil dolar hapa anatuambia tax ya dola mil 10$........ huyu ni wa kupigwa mawe.

Huu mkataba usitishwe au tuwarudishie hela zao waon=doke
 
Back
Top Bottom