1. Kunapokuwa na habari mbaya katika image ya nchi ni jukumu la ubalozi, wizara ya mambo ya nje na hata idara nyingine mbali mbali kujaribu kubadili hilo, njia zipo nyingi na kazi kubwa ya ubalozi ni ku-redress the negative image. Hivi ndio vipimo vinavyotumika kuangalia effectiveness ya balozi husika, in fact who knows kwa kuweka ukweli bayana unaweza vutia watalii na wawekezaji....precisely Membe's point!!
2. Ziara za muungwana ni ku-capitalise jitihada za balozi, hivi jamani mnadhani Mheshimiwa Rais ataibuka tu aende ziarani, it all begins with proper co-ordination ya ubalozi, idara za itifaki, ikulu na respective departments on the host governments, akiondoka rais wanaofuatia ndio wanacapitalize on the promises, pledges nk....Wawekezaji wakisikia from the horses mouth na ubalozi ukiwa effective kufuatilia ndio matunda yanaokana... UbAlozi mzuri ndio utafuatilia vizuri...Precisely Membe's point ''Tutawapima kwa kuleta wawekezaji''
3. '' Tengeza nyumba wapangaji watakuja tu'' sounds nice Mkandara lakini I am afraid though it is a true statement but incomplete, wakati mwingine you need wapangaji ili uweze kujikwamua upate fedha ndio ukarabati, they need to go hand in hand... Tuna uwezekano wa kupata mafuta as dalili zipo, uwezo wa ku-explore hatuna hivi tusiombe misaada nje kuwaalika wawekezaji kwa vile bara bara ni mbovu? Tuna gesi nyingi sana, utaalam wa kui-convert into usable energy hatuna hivi tusitangaze tender ya kampuni za kigeni kuja kuredress this kwa vile kuna matatizo ya umeme?! Waziri akisema mabalozi watapimwa kwa kuvutia wawekezaji kuna kosa gani? Kukarabati nyumba YES mkandara lakini wapangaji tunawahitaji as well...
Wanabodi,
Mimi hapa mtu wa kale na elimu yangu ni ya madrasa lakini nitasema yanayonisumbua.
Hakuna cha digrii ya MA wala Phd ikiwa digrii hiyo hifanyii kazi kulingana na mazingira yako. Hizo digrii zenu za International relations mnazo zipatia nje zinatazama mazingira ya uhusiano wa Uingereza ama Marekani nje na sio kutoka nje kuingia nchi hizo. Hizi ni Academic na lazima kuzifanyia majaribio ndani mwako ambayo unayatazama kwa mtazamo wa kutoka Tanzania kwenda nje ili ziweze kufanya kazi vizuri na sio kutazama nje ili uibadilishe Tanzania kukidhi nchi hizo.
Nitakwambieni kitu kimoja walichokifanya nchi kama China, Maleysia, India na hata Ireland kwa kipindi kifupi sana. Hawa jamaa zetu wametazama nchi zao mapungufu yake ya ndani wakayafanyia kazi kuyaweza katika mazingira bora. Mazingira ambayo ni pamoja na kuelemisha wananchi wake ktk sekta ambazo wameziwekea mikakati ya muda mfupi na mrefu, badala ya wao kutumia muda mrefu kunadi nchi zao.
Hujasikia hata siku moja viongozi wa nchi hizi wakikimbia huku na kule kutafuta soko kwa sababu walikuwa wakifagia kumbi zao kuondoa taka kwanza kwa zaidi ya miaka kumi na ushee. Na hadi kesho huwezi kuona viongozi wao wakijipendekeza ktk nchi za Magharibi isipokuwa hushusha nyanga zao mezani na kusema:- This is what my county can offer! Wakiweka imani kwamba kizuri siku zote hujiuza na kibaya hujitemmbeza!...
Ukiwa na elimu na uwezo wa kufanya kazi siku zote CV (resume) yako itasema, kinachofuata ni interview na pengine kuiapata kazi sio kuzunguka na resume mkononi kila bar kuongea na wajomba wakutafutie ajira. Something is wrong!
Tunachofanya Tanzania ni biashara ya Umalaya kusimama pale Joly na kuhamia viwanja vya Maggot, Skyway, Kwa macheni na Kinondoni Block... kwa hiyo hata kama una digrii gani ukiwa malaya wewe malaya tuu!...na hiyo digrii ittakusaidia zaidi ktk kutafuta soko la Umalaya, sana sana advantage yako kubwa itakuwa lugha. usichokifahamu ni kwamba huyo mzungu mtalii anachotaka sii lugha yako ila mwili wako ambao hauna tofauti na mwanamke mwingine yeyote isipokuwa wewe ni kati ya wanawake rahisi kupatikana.
Viongozi wetu na hasa JK pleeease tengeneza kwanza nyumba yako ili upate wapangaji, watakuja tu kama walivyoweza kufanya wenzetu. Nitanukuu msemo mmoja wa rais wa maleysia akiwaambia raia wake kuwa
"Huu ni wakati mgumu sana kwenu kwa haya nitakayo waeleza!..Kuna wengi hamtaweza kunielewa lakini nakuombeni uvumilivu wenu na kesho mtakuja kunikumbuka.
Leo ni siku ambayo Maleysia imefikia Uamuzi wa kutupa magongo na wananchi kujaribu kutembea bila magongo. Malesia sio taifa lemavu lenye kilema cha uchumi ila tulipata ajari mbaya ya kiuchumi tukavunjika miguu yetu.
Kwa muda mrefu sana tumeyatumia magongo hayo, na sasa hivi ni wakati wa kujaribu kutembea wenyewe bila msaada wa magongo!..
Ukizoea kutembea kwa magongo ni rahisi kujenga imani kwamba hujapona vizuri na hautaweza kuelewa kama kweli umepona ikiwa hutajaribu kutembea bila magongo!.."
Maneno hayo ni mazuri sana na amsho kubwa kwa mataifa kama yetu kutoendelea kutegemea IMF na misaada ya nchi za magharibi ambayo ndiyo kiini cha safari zote hizi. Kuendeleza imani hizi za kuwa taifa tegemezi hata siku moja hatuwezi kwenda kokote.
Sijui kama mnalifahamu hili kuwa nafasi ya Afrika leo hii katika soko la dunia imeshuka hadi asilimia 2 kutoka aslimia 8 ambayo ilikuwa imesimama miaka ya bara hiri kupata Uhuru. sasa hii habari ya Utandawazi inatupa picha gani ikiwa nafasi yetu imepungua zaidi ktk soko hilo kuliko zamani?...
Ina maana moja tu! - Hatuwezi kushindana! na utaweza vipi kushindana ikiwa wewe mwenyewe umesha kubali huwezi kuzalisha kisha unamwita mgeni ambaye anachukua mali yako na kuiweka ktk soko la dunia kwa jina lake!..
Kisha tazameni ni vitu gani nchi kama marekani inaagiza kutoka tanzania kiasi kwamba wanadai leo kuwepo na mahusiano mazuri ya kibiashara kati yetu na wao!...Nini hasa watu hawa wananunua kutoka kwetu? Utaona ni sahani, vinyago, mbachao, mananazi, fulana za t-shrit na sijui maua, hali vitu vyote vikubwa ambavyo vinaweza kujenga uchumi wetu wanavitaka wao kuvikamata kwa kutumia majina yao.
Leo mnakimbilia Ulaya kuitangaza TZ ili ipate kukamatwa zaidi ktk vitu ambavyo vinapatikana tanzania. Why hao wawekeshaji wasije jenga viwanda vya uzalishaji wa vitu ambavyo sisi hatuna i.e magari? Electonic parts na hata mazao yetu kuwa ktk finished product ndani ya nchi?
nakuamini DR WHO sio hawa wengine wanakurupuka na kuandika, fanya research kijana na uje hapa tuonyeshane hoja.
Maliza masomo tunahitaji critical minds kama wewe pale makao makuu Foreign na pia vituoni, kazi nzuri na i wish you good research...
wengine igeni mfano, arguments zenu hazina kichwa wala miguu labda MIKUKI na BRUTUS ambao nitawajibu eventually...
Mkandara unaboa majibu yangu nitakutumia kwenye PM manake umekosa nidhamu kabisa nchi yako unalinganisha na Kahaba? ama kweli wazaliwa kisutu mpo wengi....