Tanzanian Political Opposition is Not Ready Yet!

Rev. Kishoka

JF-Expert Member
Mar 7, 2006
4,526
1,529
Pamoja na juhudi zetu kubwa za kuking'oa CCM, ukweli ni kuwa vyama vya Upinzani havijajiandaa vizuri kuliongoza Taifa letu.

Hili linatokana na ukweli kuwa havina watu wa kutosha ambao wanaweza kuwa Wabunge na kuendelea kwa migongano na kukosekana kwa watu wenye nguvu za kukubalika na jamii na hasa majimboni kuwa Wabunge.

Ni bahati mbaya sana Mzee Victor Kimesera mgombea uchaguzi wa CHADEMA Kiteto, yupo hoi bin taabani Dar kwa ajili ya matibabu. Wengi tumekimbilia "sumu" wengine watasema lwao. Lakini ukweli ni kuwa kama Mtoa uhai angemtwaa Malaika wake, je CHADEMA wangemsimamisha nani? Do opposition have a back up plan?

Kama sikosei, Mzee Kimesera anaweza kuwa na umri kati ya miaka 65-72. Hivyo basi CHADEMA wamekimbilia kumpa tunu hiii mtu mzee. Uzee si hoja au dhambi, bali jee hapakuwa na mtu mwingine yeyote ila Kimesera? Kumbukumbu zangu ni kuwa yeye Kimesera aligombea Kiteto 1995, hivyo miaka 12 baadaye, anaendelea kuwa mgombea pekee mwenye utashi na kukubalika kwa wananchi wa Kiteto?

Leo hii miye nimeshupalia Kikwete avunje Bunge na baraza la Mawaziri. Akifanya hivyo na kuitisha uchaguzi mkuu baada ya miezi 6 au hata mwaka mmoja, je Upinzani una watu wa kutosha wenye uwezo na ushawishi kukubalika katika majimbo? au ni kusubiri mabaki kutoka CCM?

Nilipoleta ile mada ya Chadema must Reform na Focus 2010, niligusia vitu kama hivi, je kina Mnyika, Kitila na Zitto, mko tayari kuchukua nchi nzima?

Zaidi la hofu ambalo ndili linalofikia kusababisha wananchi waendelee kuchagua CCM (Zimwi likujualo) ni ukweli kwamba hata kama Upinzani ukishika hatamu, je unauwezo kuongoza nchi? wanawatendaji wa kutosha wanao waamini kufanya kazi na kutekeleza mikakati na sera za vyama hivi vikichukua madaraka?

Si nia yangu kuviogofya au kuvunja nguvu za upinzani, ila ni ukweli usiopinguika na hali halisi! Upinzani upo tayari kimaneno, lakini kiutendaji sidhani hata kama wana uwezo japo 40%. Upinzani umejaa misuguano na kikubwa ambacho wanafahamika sana sasa hivi ni kuhusu vita vya ufisadi vya Slaa na Zitto.

Swali ni hili, ikiwa CCM kesho watajirudi na kujisafisha kuhusiana na Richmond, BOT, ATCL, RADA na IPLT, je upinzani utakuwa na hoja gani kujiuza? watakimbilia Katiba? au ndio kula ruzuku ambazo no kodi zetu?

Napenda kutoa hoja!
 
Pamoja na juhudi zetu kubwa za kuking'oa CCM, ukweli ni kuwa vyama vya Upinzani havijajiandaa vizuri kuliongoza Taifa letu.

Hili linatokana na ukweli kuwa havina watu wa kutosha ambao wanaweza kuwa Wabunge na kuendelea kwa migongano na kukosekana kwa watu wenye nguvu za kukubalika na jamii na hasa majimboni kuwa Wabunge.

Ni bahati mbaya sana Mzee Victor Kimesera mgombea uchaguzi wa CHADEMA Kiteto, yupo hoi bin taabani Dar kwa ajili ya matibabu. Wengi tumekimbilia "sumu" wengine watasema lwao. Lakini ukweli ni kuwa kama Mtoa uhai angemtwaa Malaika wake, je CHADEMA wangemsimamisha nani? Do opposition have a back up plan?

Kama sikosei, Mzee Kimesera anaweza kuwa na umri kati ya miaka 65-72. Hivyo basi CHADEMA wamekimbilia kumpa tunu hiii mtu mzee. Uzee si hoja au dhambi, bali jee hapakuwa na mtu mwingine yeyote ila Kimesera? Kumbukumbu zangu ni kuwa yeye Kimesera aligombea Kiteto 1995, hivyo miaka 12 baadaye, anaendelea kuwa mgombea pekee mwenye utashi na kukubalika kwa wananchi wa Kiteto?

Leo hii miye nimeshupalia Kikwete avunje Bunge na baraza la Mawaziri. Akifanya hivyo na kuitisha uchaguzi mkuu baada ya miezi 6 au hata mwaka mmoja, je Upinzani una watu wa kutosha wenye uwezo na ushawishi kukubalika katika majimbo? au ni kusubiri mabaki kutoka CCM?

Nilipoleta ile mada ya Chadema must Reform na Focus 2010, niligusia vitu kama hivi, je kina Mnyika, Kitila na Zitto, mko tayari kuchukua nchi nzima?

Zaidi la hofu ambalo ndili linalofikia kusababisha wananchi waendelee kuchagua CCM (Zimwi likujualo) ni ukweli kwamba hata kama Upinzani ukishika hatamu, je unauwezo kuongoza nchi? wanawatendaji wa kutosha wanao waamini kufanya kazi na kutekeleza mikakati na sera za vyama hivi vikichukua madaraka?

Si nia yangu kuviogofya au kuvunja nguvu za upinzani, ila ni ukweli usiopinguika na hali halisi! Upinzani upo tayari kimaneno, lakini kiutendaji sidhani hata kama wana uwezo japo 40%. Upinzani umejaa misuguano na kikubwa ambacho wanafahamika sana sasa hivi ni kuhusu vita vya ufisadi vya Slaa na Zitto.

Swali ni hili, ikiwa CCM kesho watajirudi na kujisafisha kuhusiana na Richmond, BOT, ATCL, RADA na IPLT, je upinzani utakuwa na hoja gani kujiuza? watakimbilia Katiba? au ndio kula ruzuku ambazo no kodi zetu?

Napenda kutoa hoja!

Sad but true!

Mimi nimeanza kumtafuta Balali ili tugawane pesa zake za wizi... maana kama mambo ndio hivi basi tumekwisha......lol
 
kuna ujumbe mzito hapa. Inawezekana wapinzani na wenyewe wanafuata sera ile ile kuwa wanasiasa Tanzania hawastaafu wanazunguka tu toka huku kwenda kule. Si Msekwa alidhaniwa katoka, na nani yule mwingine aliyepewa Ukuu wa Chuo Kikuu Dodoma or something.

Nadhani bado watawala na wapinzani hawaamini kuna Watanzania wengine wenye uwezo wa kuongoza.

On the other hand, kama anastahili na ana uwezo why not? Mtu kuwa mzee hakumfanya anapungukiwa na haki zake kama raia.

Unless kuna sababu nyingine ya kimsingi naamini kuwa Kimesera anawakilisha mawazo ya wapinzani.

Ila hilo la miaka 12 limenigusa kidogo kwani limenikumbusha mzee Malecela ambaye nadhani anakaribia miaka 40 Bungeni na wananchi wa Mtera bado wanamkubali. Mwingine ni Mbunge wa Kwela, C. M. Mzindakaya, na yeye amekuwa Bungeni kwa karibu miaka 40 na ushee na watu wa Kwela sidhani kama wanafikiria kumpa mtu mwingine.

Na upande mwingine (assuming kuna pande zaidi ya mbili) kuna Mbunge kama Zitto na kina Slaa na kina Selelii na wengine, kwa muda mfupi walioingia Bungeni wanajitutumua kuliko vigogo wengine waliokaa Bungeni muda mrefu.

So, to me the verdict is still out there..
 
1. Ni kitu gani kinafanya upinzani leo hii 17 years baada ya Multi-party bado kuzidi kuwa dhaifu Tanzania?

2. May be mda wa kukaa Bungeni uwe na ukomo kama ilivyo kwa Raisi?
Yaani Maximum mtu kuwa mbunge iwe vipindi vitatu vya miaka 5 yaani 15 years- ili pia kutoa nafasi kwa wengine!
 
1. Ni kitu gani kinafanya upinzani leo hii 17 years baada ya Multi-party bado kuzidi kuwa dhaifu Tanzania?

2. May be mda wa kukaa Bungeni uwe na ukomo kama ilivyo kwa Raisi?
Yaani Maximum mtu kuwa mbunge iwe vipindi vitatu vya miaka 5 yaani 15 years- ili pia kutoa nafasi kwa wengine!

Maswali yako yanaweza kujibiwa na hotuba ya kiongozi moja mkubwa kabisa wa ccm anayejisifia kuwa alifanikiwa kupunguza upinzani ndani ya bunge kutoka ...... mwaka 95 mpaka..... mwaka 2005.

Wakati mzuri sana huu wa kujiunga na ccm .....lol kama kuna kampeni mahsusi ya kupunguza wabunge wa upinzani
 
Swali ni hili, ikiwa CCM kesho watajirudi na kujisafisha kuhusiana na Richmond, BOT, ATCL, RADA na IPLT, je upinzani utakuwa na hoja gani kujiuza? watakimbilia Katiba? au ndio kula ruzuku ambazo no kodi zetu?

CCM kujisafisha na kashfa hizi maana yake ni kufagia safu nzima ya uongozi. Kuanzia Muungwana mwenyewe, EL na wengineo. EL, Kara na wengineo hawatakubali wafe peke yao itabidi wamtumbukize na bosi wao. Hivyo itakuwa mwisho wa CCM. Kuhusu kama upinzani una watu wa kutosha, jibu ni kuwa watu wapo wa kutosha. Nani alimfahamu Zitto kama anaweza kuwa mwiba kwa mafisadi bungeni? Napenda umma wa Watanzania wajue kuwa tuna vijana wengi wanao-graduate Vyuo mbalimbali nchini na diaspora na wana-uwezo wa kuiongoza nchi ila wanakuwa frustrated na watawala ambao huhakikisha kuwa kama wanaingia kwenye siasa basi maisha yao yanaandamwa. Ukitaka kujua kuwa CCM inaelea hewani, ni wakati wagombea binafsi watakaporuhusiwa kikatiba.
 
Hakuna hata siku moja opposition yoyote duniani itakuwa ready.

Wakati ukuta.
 
Mugo"The Great";135184 said:
Swali ni hili, ikiwa CCM kesho watajirudi na kujisafisha kuhusiana na Richmond, BOT, ATCL, RADA na IPLT, je upinzani utakuwa na hoja gani kujiuza? watakimbilia Katiba? au ndio kula ruzuku ambazo no kodi zetu?

CCM kujisafisha na kashfa hizi maana yake ni kufagia safu nzima ya uongozi. Kuanzia Muungwana mwenyewe, EL na wengineo. EL, Kara na wengineo hawatakubali wafe peke yao itabidi wamtumbukize na bosi wao. Hivyo itakuwa mwisho wa CCM. Kuhusu kama upinzani una watu wa kutosha, jibu ni kuwa watu wapo wa kutosha. Nani alimfahamu Zitto kama anaweza kuwa mwiba kwa mafisadi bungeni? Napenda umma wa Watanzania wajue kuwa tuna vijana wengi wanao-graduate Vyuo mbalimbali nchini na diaspora na wana-uwezo wa kuiongoza nchi ila wanakuwa frustrated na watawala ambao huhakikisha kuwa kama wanaingia kwenye siasa basi maisha yao yanaandamwa. Ukitaka kujua kuwa CCM inaelea hewani, ni wakati wagombea binafsi watakaporuhusiwa kikatiba.

Nakubaliana nawe hapa,

CCM kujisafisha inaweza kumaanisha kuondoa generation nzima ya viongozi wa ccm maana saasa waliopo wameanza kuambukiza watoto wao wizi na ufisadi!
 
kishoka ur too general,yaani issue moja kama hii ndio basi upinzani wote ushaona hawako tayari,hiyo ni juu yako na haki yako kusema chochote ingawaje ni tafauti sana na unayoandika kila siku, ila sisi tupo na tutaendelea kussuport wapinzani na hata hayo mafanikio madogo madogo amabayo yamekufanya uwe na issue ya kuandika humu kwangu mimi hiyo tosha na hatua moja mbele...bila hao ambao hawako tayari usingejua BOT,Richmond,Buzwagi etc na mafisadi wangeendelea bila kujulikana,anyway safari hii ni ya wachache wenye moyo.
 
17yrs Upinzani dhaifu sababu kubwa ni Katiba , pili Tume ya Uchaguzi , Hongo na vitisho toka Serikalini kwa wananchi . Sumaye alisema kule Mwanza ukichagua Upinzani biashara yako na jimbo lako limetengwa .Kwa maneno haya watu wa kule kijijini ni big deal maana kasema waziri mkuu na wakiangalia wanaona wana jeshi na polisi na mahakama na kila kitu wanaamini .

Rev.Kishoka na Mwafrika Mwanamke hakua haja ya kukata kitumaini kwa mwenendo huo . Usiseme wapinzani wanaweka wazee . Nani kijana toka JF kafika kafika ana sifa za kusimama pale Kiteto akanyimwa . It is time now slowly tuhamie majimboni na kuomba hata kama ni kupitia CCM as long una ajenda ya Tanzania ni sawa . So wapinzani ni watu na watu ndiyo sisi . Lawama kwa nani ?
 
Sasa hapa Mnyika alikuja hapa akawasihi wenye interest na upinzani wawasiliane nae- sasa hata JF hakuna aliyemjibu!

We stay 'there' na kusema 'wale dhaifu'- sasa kama sii mimi na wewe ni nani ataimarisha upinzani?

Watz tunapenda chakula kilichoiva tu- yaani tupakue na kula!

Ila kulaumu- ni wa kwanza!
 
kishoka ur too general,yaani issue moja kama hii ndio basi upinzani wote ushaona hawako tayari,hiyo ni juu yako na haki yako kusema chochote ingawaje ni tafauti sana na unayoandika kila siku, ila sisi tupo na tutaendelea kussuport wapinzani na hata hayo mafanikio madogo madogo amabayo yamekufanya uwe na issue ya kuandika humu kwangu mimi hiyo tosha na hatua moja mbele...bila hao ambao hawako tayari usingejua BOT,Richmond,Buzwagi etc na mafisadi wangeendelea bila kujulikana,anyway safari hii ni ya wachache wenye moyo.

Mkuu,

Inawezekana issue ya Mchungaji iko too general, lakini ukiangalia mbele dakika tano, ina ukweli mkubwa ndani yake. Kwa mfano, chukulia tupo mwaka 2010 wakati wa kampeni, halafu bahati mbaya iwatokee Mzee Ndesamburo, Cheyo, Zitto na hata mgombea urais kama ilivyotokea kwa Kimesera. Hivi kuna watu wenye uwezo (uongozi, fedha etc)na upeo ambao wako standby wa kuchukua nafasi zao? Of course the chances of this happening are slim but its still a possibility and if it is, what will happen?

Nafikiri wapinzani inabidi wafanye kazi kubwa ya ziada ya kurecruit vijana kama Zitto ili isiwe shida kushindana na watawala, na kuwa na vyama mahiri.
 
kishoka ur too general,yaani issue moja kama hii ndio basi upinzani wote ushaona hawako tayari,hiyo ni juu yako na haki yako kusema chochote ingawaje ni tafauti sana na unayoandika kila siku, ila sisi tupo na tutaendelea kussuport wapinzani na hata hayo mafanikio madogo madogo amabayo yamekufanya uwe na issue ya kuandika humu kwangu mimi hiyo tosha na hatua moja mbele...bila hao ambao hawako tayari usingejua BOT,Richmond,Buzwagi etc na mafisadi wangeendelea bila kujulikana,anyway safari hii ni ya wachache wenye moyo.

Koba,

I have to face reality. Yes I have been fighting for good governance even pushing opposition to stand tall so that good governance and fairness will rule and lead Tanzanians. the fact remains the opposition is weak.

Let me throw you a challenge. Create a Tanzanian government using anyone in opposition. This includes President, Vice, President of Zanzibar, Prime Minister, Cabinet, speaker, RC, DC!
 
Tatizo la baadhi ya watu humu wana akili lakini hawaitumikishi akili hiyo.Kama upinzani ni dhaifu ilikuwa ni wakati mzuri basi wa serikali kurekebisha Katiba ili iweze kukidhi mahitaji ya vyama vyingi na kuweka mazingira sawa ya mchezo.Wanaojua ukali wa wachezaji wa Upinzani wanamwaga MBIGIRI uwanjani na kuwaambia kwa kuwa wao ni upinzani hakuna kucheza na viatu.
Mimi nilikuwa natumaini kama upinzani ungekuwa weak,basi uwanja ungeondolewa mbigiri na sheria ya kuwaambia wasicheze bila kiatu ingeondolewa pia.
 
Koba,

I have to face reality. Yes I have been fighting for good governance even pushing opposition to stand tall so that good governance and fairness will rule and lead Tanzanians. the fact remains the opposition is weak.

Let me throw you a challenge. Create a Tanzanian government using anyone in opposition. This includes President, Vice, President of Zanzibar, Prime Minister, Cabinet, speaker, RC, DC!

Kilichotokea Kiteto hata kama tutadai faulo za CCM ni dhahiri kuwa bado Upinzani haujaweza kujiuza kikamilifu kwa Taifa la Tanzania.

Mwalimu Kitila atakuja na kudai tuwape nafasi, Mnyika atasema tembeleeni tovuti, lakini juhudi za wao kujijenga (opposition) zinaelekea ni kwenye kutoa uozo na nyakati za uchaguzi. je ni lini watajiuza kukiwa na heri?

Tangu sakata la Lowassa kuaonguka, yaelekea kana kwamba upinzani umetimiliza kazi. Matamko waliyoyatoa kutaka mapendekezo ya Mwakyembe yafanyiwe kazi yanaonekana ni mepesi na si tya nguvu mpaka Serikali iamke.

Je n lini Upinzani utaanza kujijenga na kujiuza kwa Watanzania kwa umakini?

je ni lipi lililo tokea Kiteto ambacho kilisababisha Upinzani kushindwa kama tukiondoa fujo na faulo za CCM?
 
Kilichotokea Kiteto hata kama tutadai faulo za CCM ni dhahiri kuwa bado Upinzani haujaweza kujiuza kikamilifu kwa Taifa la Tanzania.

Mwalimu Kitila atakuja na kudai tuwape nafasi, Mnyika atasema tembeleeni tovuti, lakini juhudi za wao kujijenga (opposition) zinaelekea ni kwenye kutoa uozo na nyakati za uchaguzi. je ni lini watajiuza kukiwa na heri?

Tangu sakata la Lowassa kuaonguka, yaelekea kana kwamba upinzani umetimiliza kazi. Matamko waliyoyatoa kutaka mapendekezo ya Mwakyembe yafanyiwe kazi yanaonekana ni mepesi na si tya nguvu mpaka Serikali iamke.

Je n lini Upinzani utaanza kujijenga na kujiuza kwa Watanzania kwa umakini?

je ni lipi lililo tokea Kiteto ambacho kilisababisha Upinzani kushindwa kama tukiondoa fujo na faulo za CCM?

Kiteto ni mfano mzuri kwamba kumbe wananchi wakiamua upinzani unashinda. Kata zote za mjini CHADEMA ilishinda, Huko ndio wanapojua maana ya ufisadi. CCM wamecheza rafu huko vijijini ndani ndani kwa wamasai wasiojua hili wa lile kuhusu ufisadi. Wanachujua ni ng'ombe zao. Inaelekea CHADEMA wameshindwa pia kulinda vizuri kura huko remote areas. Hebu waje watueleze kwa kina hapa ilikuwaje, tazama matokeo hapa: http://www.chadema.net/uchaguzi/matokeo/kiteto/index.php

Hapa ilikuwa ni kabla ya matokeo maruhani ya asilimia 15 iliyobaki

Asha
 
Sasa hapa Mnyika alikuja hapa akawasihi wenye interest na upinzani wawasiliane nae- sasa hata JF hakuna aliyemjibu!

We stay 'there' na kusema 'wale dhaifu'- sasa kama sii mimi na wewe ni nani ataimarisha upinzani?

Watz tunapenda chakula kilichoiva tu- yaani tupakue na kula!

Ila kulaumu- ni wa kwanza!


It couldn't put it better. Kwa maneno mengine unachosema ni kwamba watanzania wengi tunapenda kuwa sehemu ya mafanikio lakini sio sehemu ya mapambano!
 
It couldn't put it better. Kwa maneno mengine unachosema ni kwamba watanzania wengi tunapenda kuwa sehemu ya mafanikio lakini sio sehemu ya mapambano!

umenifurahisha sana kuweka mafanikio rangi ya kijani, huo ndio ukweli na mapambano huenda ikawa ni buluu sasa pambaneni ila mafanikio njooni CCM
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom