TANZIA Wakili mtetezi wa ICTR Prof. Jwani Mwaikusa auawa Tanzania

Habari ambazo zimeingia sasa hivi ni kuwa Prof. Jwani Mwaikusa ameuawa. Pamoja naye taarifa zinadokeza kuwa mwanae pia ameuawa. Tunaendelea kufuatilia taarifa hizo kwa karibu ili kuweza kupata taarifa za uhakika zaidi.

Wengi tunamfahamu hivi karibuni katika kesi ya wagombea binafsi akiwa mmoja wa walioitwa kuwa "marafiki wa mahakama" yeye akitetea haki ya wagombea binafsi na kusisitiza kuwa mahakama ina uwezo wa kusikiliza kesi hiyo. Siku za karibuni amekuwa ni mwanasheria katika Mahakama ya Kimataifa ya Mauaji ya Rwanda na mmoja wa wanasheria waliobobea wa Katiba amefariki duniani.

Taarifa zinadokeza kuwa mauaji hayo yametokea nyumbani kwake usiku wa kuamkia leo.

Taarifa bado zina kiza kuna uwezekano wa zaidi ya watu wawili kuwa wameuawa kwenye tukio hilo..



sina details zaidi.. vyanzo vyetu vinafuatilia..

Hapo kwenye bold kama ni kweli we need to think twice.....! Gen. Nyamwasa, Prof. Mwaikusa.......who is next?
 
Duh Hii si habari njema mwenye habari kamili atujulishe

Extreemly sad! Ngoja tuone uhusiano wa mauaji haya na kesi hizi mbili ambazo alionekana kuhusika nazo kwa namna yenye dalili za ushindi.
1. Mauaji ya Rwanda
2. Mgombea binafsi

RIP Prof. Mwaikusa
 
R.IP. Prof

what a loss...........

some of us tutakukumbuka kwa mengi!!!!
 
Akiwa anakaribia kutaja mgombea binafsi naomba nimnukuu RAIS,DK KIKWETE

Mimi napenda niwaonye kabisa yoyote atakaeshabikia ama kutaka kufanya kitu kitakachotutenganisha
nawaambia kweli hii serikali si sehemu ya kutafuta umaarufu,,nasema hili nikimaanisha nawambia ili mtu asishangae ..kuna walioanza chokochoko tuliwashugulikia na wengine (

tumewasahau)

kabisa

Mwenye akili utajua ana maana Gani!!!nawaambia ukweli tutakushugulikia mpaka mwisho..mi nawaambia msidanganyike bwana kitu kikija kwangu nikisema no ni no hata iweje..utahangaika kwa haki za binadamu ,,mahakama kuu na vyombo vingine vya sheria nikisema no itaishia no

DK KIKWETE TUELEZE PROF WETU ALIPO...HILI JAMBO WANA JF SI LA KUCCHUKULIA MZAHA HATA KIDOGO..ATUITAJI KUISHI NA SERIKALI YA WAUWAJI..UTAMUUA KILA MTU SIKU YA MWISHO BABAKO ANAKUKANA UTAMMALIZA???
 
Jamani nimesikitika sana siyo tu kwasababu namfahamu huyu Pro. ila mauaji yanayoendelea Tanzania yani mtu hujui siku inaishaje kama utakuwa salama next day au la!!

I feel for Amu&Baraka+familia yote..Poleni sana kwa msiba huu wa baba yenu wapendwa!!..May he RIP,Amen!
 
Re: Prof.jwani mwaikusa auwawa na majambazi

Wanandugu tusiwasingizie MAJAMBAZI kila saa hii ni proffession Job Kama zingine


si wote ni majambazi wengine ni WAUWAJI
 
Kwa sasa hivi inafahamika kuwa ni majambazi. Nadhani uchunguzi wa kina baadaye ndio utakaoonyesha iwapo kuna mkono mwingine
R.I.P Prof

kama ni majambazi kunatakiwa kuwe na clue muhimu kama vifaa walivyotumia kuvunja milango, prints/marks etc ya vitu vilivyoibiwa na kwanini waue je? marehemu alikuwa anawafahamu? tunajua majambazi hutaka mali si uhai wa mtu. Labda kama marehemu hakutaka kuachia mali kirahisi hivyo kutakuwa na clue zinazoonyesha aina ya mapambano. Otherwise haya ni mauaji tu na suspects watakuwa (1) Govt agents (2) Watuhumiwa wa mauaji ya genocide ya Rwanda (3) masuala mengine.

Polisi have to do their best au IGP ajiuzuru kama yule wa DRC last month.
 
mi nashangaa sana! yale maeneo ya mbezi beach mpaka kunduchi na kwa upande wa juu salasala yani kila kukicha majambazi, sijui polisi wako wapi..hata patrol hatuzioni! wakati mwingine inashangaza imagine hata yale maeneo yaliyo karibu na Mwamunyange pamoja na afisa wetu mkuu wa USALAMA, ujambazi kila kukicha tena mtindo ni huo huo majambazi unaingia nao getini unavyorudi. mtu akiuwa na wananchi eti watu wanachukua sheria mkononi, mkononi??? watu kuvamiwa inakua kama kitu cha kawaida....! inauma sana yani hawa jamaa sasa wamekua ni kama unavyoona inzi wanavyozunguka zunguka kwenye chakula! no STRATEGIES aaaaahh, inauma sana
 
mi nashangaa sana! yale maeneo ya mbezi beach mpaka kunduchi na kwa upande wa juu salasala yani kila kukicha majambazi, sijui polisi wako wapi..hata patrol hatuzioni! wakati mwingine inashangaza imagine hata yale maeneo yaliyo karibu na Mwamunyange pamoja na afisa wetu mkuu wa USALAMA, ujambazi kila kukicha tena mtindo ni huo huo majambazi unaingia nao getini unavyorudi. mtu akiuwa na wananchi eti watu wanachukua sheria mkononi, mkononi??? watu kuvamiwa inakua kama kitu cha kawaida....! inauma sana yani hawa jamaa sasa wamekua ni kama unavyoona inzi wanavyozunguka zunguka kwenye chakula! no STRATEGIES aaaaahh, inauma sana


good !!!mi nahisi wanakula nao ndugu yangu

Niwa pe hili la kidokezo cha POLISI KAWE...kama mmeona kwenye tv majuzi pikipiki walifunga barabara kisa polisi kukataa kwenda kwenye tukio huku gari 2 ziko nje na mafuta full kujiachia.....
baada ya kelele zile wakatoa gari moja walipofika kituon wakaja na masharti wanaenda wenyewe wakaambiwa nenda na mmoja anaekujua wakataa wakadai waelekezwe amuwezi amini waligeuza lile gari wakarudi...Baada ya muda mchana akaja mama mmoja samahani kama ilikuwa siri pale kituon saa kumi na moja yule mama anauza michicha anajulikana akaja akatukana sana wanapikipiki wakataka kumpiga kabla ya sie wenye upeo kumchukua..kumficha buchan..baada ya muda tukamtoa aeleze kilichomsibu kutukana ..wakamwekea ulinzio mama akaanza kumwaga nyie wenyepikipiki mnauwana wenyewe twendeni niwaonyeshe pikipiki mlipoificha..chumba cha jiran na wamekuja usiku saa 11 wanashindana ilale hapa au lah....akasema waliomuaa wako hapa hapa kijiwen tanki bovu na wanaendesha pikipiki...wapuuzi sana nyie ndio maana hata askari wamewadharau...anyway tatizo kubwa la askari wetu waqnataka pesa mbele biola pesa akuna msaada


Majuzi nina sehemu kimara za biashara wamiba nikamchukua mlinzi nikamweka ndani nilipofika kimara kituona wakakataa kumpokea ati mpaka wafanye uchunguzi nikawaambia ammpokei akaniita dada mmoja nimpe alfukumi..nikatoka nikampigia mkuu wa kituo kimara,nikapiga kwa mhe sana..nikawaeleza na kumpa namba za yule dada na wanaume wanazovaaga pale mbele gafla nikaona wanamchukua wanamweka ndani wakanifwata wanadai niwape alfu tano ya mafuta kumpeleka mbezi nikawambia mwacheni hapo alafu bosi wenu atakuja kumbeba

So kila sehemu ni chafu chafu zinanuka vituo vingi vya polisi vinanuka hongo rushwa usipomjua mtu ama kuwa na pesa ni aiubu ama imekula kwako
 
leo hii wale wahalifu wa kimara wamewahamishia

Mbezi sasa huu mchezo wa kuhamishana mpaka lini mh Mwema anyway
lidumu jeshi la Majambazi
 
Habari ambazo zimeingia sasa hivi ni kuwa Prof. Jwani Mwaikusa ameuawa. Pamoja naye taarifa zinadokeza kuwa mwanae pia ameuawa. Tunaendelea kufuatilia taarifa hizo kwa karibu ili kuweza kupata taarifa za uhakika zaidi.

Wengi tunamfahamu hivi karibuni katika kesi ya wagombea binafsi akiwa mmoja wa walioitwa kuwa "marafiki wa mahakama" yeye akitetea haki ya wagombea binafsi na kusisitiza kuwa mahakama ina uwezo wa kusikiliza kesi hiyo. Siku za karibuni amekuwa ni mwanasheria katika Mahakama ya Kimataifa ya Mauaji ya Rwanda na mmoja wa wanasheria waliobobea wa Katiba amefariki duniani.

Taarifa zinadokeza kuwa mauaji hayo yametokea nyumbani kwake usiku wa kuamkia leo.

Taarifa bado zina kiza kuna uwezekano wa zaidi ya watu wawili kuwa wameuawa kwenye tukio hilo..



sina details zaidi.. vyanzo vyetu vinafuatilia..

....RIP pROF MWAKYUSA
 
hizi ndio faida za EAC; ukiacha milango na madilisha wazi si hewa nzuri tu ndiyo itaingia ndani hata Nzi, na arufu ya choo cha jirani (manzese kwa mtogole -hii ni kawaida) vitaingia.

Hii inatisia ustawi wa taifa; Hawa jamaa wangekuwa mashujaa wa taifa kama wangepambana na MAFISADI; inauma sana

RIP Prof. Mwaikusa
 
Mbona uko kama unajua syndicate fulani iliyohusika.

Nadhani tunakosa taarifa kamili kuhusu mauwaji haya kama walipora kitu au la. kama hawajapora huenda ni mpango mwingine zaidi ya ujambazi. Lakini kitendo cha mashambulizi ya majambazi pale pale getini kinaweza kuzuia zoezi la uporaji maana huenda walitaka kumchukua kimya kimya na wakawa forced kumpiga risasi na kuharibu mpango mzima.

Pia Mwanakijiji ametuambia aliwahi kushiriki katika mambo ya mahakama ya Rwanda. Hawa jamaa wana chuki sana na kwa upande wowote aliokuwa tofauti nao wanaweza kufanya chochote potelea mbali mambo mengine ya Ki-TZ.

RIP Prof. Tutakukumbuka kwa kutetea katiba na uhuru halisi wa Mtanzania kupitia shauri la Mgombea binafsi

Mkuu sifahamu hata muuaji mmoja, lakini naweza kusema hakuna mnyarwanda anayeweza kuja kumuua huyo jamaa kwa kuwa judge tu wa ile mahakama. Tusiumize vichwa kwa sasa, he is already dead, in weeks and months ahead tutajua muuaji ni nani, for sure hata kamatwa and life will go on. Hii ndio haki Tanzanian style.
 
eee twaambiwa majambazi lakini kumbe hawakuiba kitu!

hapa si bure

R.I.P professa
 
Poleni wafiwa na Mola yupa nanyi katika hiki kipindi kigumu cha maombolezo.

R.I.P Prof na Mtoto Wake
 
Yaani inasikitisha sana na kutia uchungu...lakini nauliza tu kwa nia njema Prof.Mwaikusa (RIP) hakuwahi kutangaza nia???
 
Re: Prof.jwani mwaikusa auwawa na majambazi

Wanandugu tusiwasingizie MAJAMBAZI kila saa hii ni proffession Job Kama zingine


si wote ni majambazi wengine ni WAUWAJI

HABARI NILIZOZIPATA SASA HIVI NI KWAMBA HII NI ASSASSNATION. Hawa wauaji waliingia nyumbani, wakapiga risasi kadhaa kuwascare wanafamilia walio kuwa ndani. Baada ya hapo wakamshoot risasi ya kichwa na kumuua.
Katika kurusha rusha risasi za kuscare waliokuwa ndani wakampiga risasi mtoto wake aliyekuwa nje , na kumuua. Mtoto huyo anaitwa Gwamaka
Wakiwa wanatokomea, wakamwona mpitanjia ambaye walihisi (nadhani ) amewaona naye wakampiga risasi nyingi kiasi cha kusambaratika ovyo.
RIP Proffessor Jwani Mwaikusa.
Tunaomba polisi ifuatilie motive ya mauaji: Je ni visa? Ni political? au ni mambo ya Rwanda?
 
Back
Top Bottom