mama D
JF-Expert Member
- Nov 22, 2010
- 19,763
- 35,201
Nikiwa njiani najisomea na kusikiliza habari tofautitofauti za kijamii, kisiasa, kiuchumi toka mataifa tofauti; nimejikuta nikimshukuru Mungu kuwa mtanzania.
Hakika Tanzania yetu ndio nchi ya furaha.
Tumebarikiwa kuwa na waasisi bora wa taifa waliotuachia misingi imara isiyotikisika, tumajaliwa kuwa na viongozi bora wanaoendeleza yale yaliyoanzishwa miaka baada ya miaka.
Tumejaliwa kuwa na umoja ulioweza kuvunja kabisa ukabila na ukanda, leo haijalishi ulizaliwa wapi unaweza kuishi, kufanya kazi, kuoa/kuolewa, kumiliki mali... sehemu yoyote ile inayokupendeza.
Haijalishi wewe ni wa imani gani unaweza kuishi na kuwa huru popote hata kwa wale wenye imani tofauti na wewe bila hofu.
Tanzania mkristo anaweza shiriki na waislamu kwenye ibada hata muislamu kushiriki na wakristo kwenye ibada bila tatizo wala vita
Tumshukuru Mungu kwa mazuri ya nchi yetu, tushikane na tushirikiane kuboresha na kudumisha yaliyo mema
Mungu ibariki Tanzania Mungu mbariki rais wetu Samia Suluhu Hassan na wasaidizi wake wote
Hakika Tanzania yetu ndio nchi ya furaha.
Tumebarikiwa kuwa na waasisi bora wa taifa waliotuachia misingi imara isiyotikisika, tumajaliwa kuwa na viongozi bora wanaoendeleza yale yaliyoanzishwa miaka baada ya miaka.
Tumejaliwa kuwa na umoja ulioweza kuvunja kabisa ukabila na ukanda, leo haijalishi ulizaliwa wapi unaweza kuishi, kufanya kazi, kuoa/kuolewa, kumiliki mali... sehemu yoyote ile inayokupendeza.
Haijalishi wewe ni wa imani gani unaweza kuishi na kuwa huru popote hata kwa wale wenye imani tofauti na wewe bila hofu.
Tanzania mkristo anaweza shiriki na waislamu kwenye ibada hata muislamu kushiriki na wakristo kwenye ibada bila tatizo wala vita
Tumshukuru Mungu kwa mazuri ya nchi yetu, tushikane na tushirikiane kuboresha na kudumisha yaliyo mema
Mungu ibariki Tanzania Mungu mbariki rais wetu Samia Suluhu Hassan na wasaidizi wake wote