Tanzania yetu na Rais Magufuli ni wetu. Kuelekea Maisha ya kipato cha kati, Sekta ya Kilimo na Mifugo tuko wapi na tunakwenda wapi?

Freddie Matuja

JF-Expert Member
Jul 21, 2018
1,459
2,829
Nimekuwa nikijiuliza maswali mepesi au maswali magumu kutegemeana na akili yangu na kwa jinsi ninavyoona mambo yanavyokwenda Tanzania kuhusu Sekta ya Kilimo na Kifugo ambazo zinagusa Zaidi ya 60% wa wakazi wa nchi hii.

Wakati nawaza tunatokaje, jana nikakutana na taarifa Wakulima wanalamamika kuuza maziwa lita moja sh.700 mkoani Tanga, Iringa kuna kiwanda kinanunua maziwa lita Tsh 800. Maziwa haya baada ya huchakatwa yanauzwa kwa wastani wa Tsh 3200 kwa lita kwa bei ya jumla na wastani wa sh. 4,000 kwa lita kwa bei ya reja reja.

Ukilinganisha na New Zealand mwaka 2017 “The dairy sector contributes $7.8 billion (sawa na tril 11.4) (3.5%) to New Zealand's total GDP. This comprises dairy farming ($5.96 billion) (wakulima wanavuta Tril 8.74)and dairy processing ($1.88 billion) (viwanda vya kusindika maziwa vilipata Tril 2.76).

Hapa kwetu tuna tuna tajiri mmoja toka pemba anauza maziwa “reconstituted” baada ya kununua raw powdery milk toka india.
Bank ya kilimo kwa nini tusiwe na mkakati walau wa uhakika wa soko la "mpemba" anaechakata zaidi ya lita laki 1 kwa siku. Kama angenunua kwe bei nzuri, tunetengeneza ajira ngapi kwa soko la viwanda vya"mpemba". Tukifikiri kwa uchumi jumuishi ambao uwepo wa viwanda, kwanini vifaidishe india kununua maziwa ya unga ambayo yanakuwa reconstituted hapa kwa soko la ndani.

Kili nikifungua redio au TV mbona taarifa za wizara ya kilimo na wizara ya mifugo, wizara ya viwanda, wizara ya fedha hazi-address issue kama hizo. Au mimi siwazi sawia?

Kwa mwenye majibu anisaidie majibu ya maswali yafuatayo

Ni kwa kiwango gani tunatumia mkakati wa kitafiti (utafiti wa wazi au wa kificho) ya kwa ajili ya kukuza sekta ya kilimo& ufugaji kuwa za kibiashara na sekta zinazoingiliana na kilimo (mabenki, bima, usafirishaji, umeme, TBS, viwanda, TRA, maji, afya)?

Ni namna gani Tanzania kwa malengo ya muda mfupi na muda mrefu tunakuwa na taarifa za wakati ili kuwa na mkakati wa kukuza uchumi wa wakulima na wafugaji ili kutokea hapo viwanda vya ndani vifaidike na malighafi za kilimo/mifugo ili sekta zingine nazo zikue?

Tunatumia mfumo gani wa taarifa (information systems) ili Tanzania ikue kitaasisi kwa mfumo unaojinasibu na makuzi ya ukuaji wa kilimo na ufugaji ili kipato cha uchumi wa kati kiwe dhahiri zaidi katika maisha ya Watanzania?

Mkakati wetu wa kimaamuzi ukoje ili maamuzi tunayoamua yawe na mguso kwa wakulima na wafugaji wetu?

Ni kwa namna gani Tanzania ina mkakati wa muda mfupi na muda mrefu kukuza uchumi wetu ikiwemo kupunguza imports na kuongeza exports za mazao ya kilimo na ufugaji?

Benki ya maendeleo ya kilimo na Benki ya uwekezaji (TIB) wao wana picha gani ya kuhakikisha uwekezaji wa sekta ya kilimo walau unatuvusha kuhakikisha Watanzania na ukubwa wa li-nchi hili tunakwenda mahali kwa kuwa exporters wa agro-products.

Mwisho, BOT wataalamu wa analysis na kutoa reports za trend ya ukuaji wa uchumi wa Tanzania. Kwa kuchungulia figures hizi hapa chini tena, tunawezaje walau kufanya hata 10% ya kinachofanywa na New Zealand? Just 10% kwa exports za maziwa baada ya kupunguza trade deficit ya kuagiza maziwa ya zaidi ya bil 100 kila mwaka? (Maana kwa Afrika Tz ni ya pili kwa wingi wa mifugo na tuna mifugo mingi kuliko New Zealand. )


https://twitter.com/theworldindex/status/1186661362338009088?s=08
Nikichukua New Zealand tena katika sampuli;
Latest export figures from Beef + Lamb New Zealand (B+LNZ) show New Zealand's red meat exports (excluding veal and co-products) were up $1.2 billion (sawa na 1.7 Tril)(21 per cent) on 2016-17 to over $6.7 billion (sawa na 9.8 Tril) in 2017-18 on the back of sustained high value per tonne and increased volume for lamb, mutton, and beef.

JPM huwa anauliza Watanzania tunakosea wapi. Watanzania tunakwama wapi. Wapiga kura wengi wa wanasiasa wengi akiwemo Rais JPM ni wakulima. Ni kwa namna gani nao tunawaingiza kwenye equation ya kukuza kipato chao ili wanapotumia nguvu yao ya kunua huduma na bidhaa wawe na mchango kupitia kodi zao za manunuzi ya bidhaa na huduma.
Wakulima wakinunua (kama wanavyonunua wafanyakazi) tu huduma za maji, umeme, bima za afya, wakawa kwenye mifumo ya pensheni.
Wakalipoa kodi ya nyumba kama makazi bora na kulipia watoto wao shule. Serikali inaondokana na kuhudumia mahitaji ya msingi yaliyo katika matajiri hawa kama tu uwiano wa manunuzi ya "maziwa au nyama" yataendena na uwiano kwa New Zealand

Ni namna gani tunakuwa na mkakati walau kwenye exports za maziwa na nyama kwa mwana kuna $ kadhaa zina-flow in?


If you know the enemy and know yourself, you need not fear the result of a hundred battles. If you know yourself but not the enemy, for every victory gained you will also suffer a defeat. If you know neither the enemy nor yourself, you will succumb in every battle. - The Art of War by Sun Tzu, 6th century BC.
Adui zetu ujinga na umasikini tunawakabili kwa kiwango kipi kwa kujua kwenye equation ni sehemu ya kwanini tunakwama. Au hatujatambua hilo??

Nawaza tu.

Mungu ibariki Tanzania.
 
Kwanza tunaanza na mashirika la ndege Atcl kwasasa tuna 8 kufika mwakani tutafikisha ndege 11 wakulima na viwanda vitakavyo zalisha ajira badaye.
 
Nguvu na pesa JPM anazo wekeza kwenye defunct Atcl angezielekeza kwenye kilimo tungekua na 'Green revolution' ange ingia kwenye historia ya nchi hi kama kiongozi no 2.baada ya JK
 
Huwa nawashangaa sana. Mnaongelea kilimo wakati hakuna soko.
Utasema soko liko nje ila huko nje hauko peke yako. Wao wana ubora wao ambao wakulima wa Tanzania hawauwezi.
 
Kwanza tunaanza na mashirika la ndege Atcl kwasasa tuna 8 kufika mwakani tutafikisha ndege 11 wakulima na viwanda vitakavyo zalisha ajira badaye.
Unapokuwa na ugali mdogo juu ya meza inategemea watoto/wasaidizi wanaona nini na wanawezaje kumshawishi mwenye kisu cha kugawa ugali juu ya kwanini wizara ya kilimo&mifugo zipate ugali mkubwa zaidi na mrejesho wake utakuwa kwa kiasi kadhaa cha numbers kimapato.

Mathalani;
New Zeland wana Ng'ombe wa wanaotoa maziwa ambao ni wastani wa 4.mil na ng'ombe wa nyama ni 3.6 million.
Kama tukilenga kupata earnings za walau 10% nini New Zealand wanapata; ambacho ni wastani wa say 1 trillion tokana na maziwa na nyama.

Then ngozi ambayo inapatikana machinjioni ikaongezwa thamani kwa viwanda vya ndani, ripple effect yake ni kubwa.
Kwa namna hiyo ingewezekana tukatoboa.

JPM alikuwa sahihi kununua ndege kama Wizara ya Kilimo na mifugo hawajaenda mezani kujenga hoja ya nini kinaweza kufanyika kwa kutumia brains za Watanzania.

Kosa ninaloliona (niko tayari kukosolewa) kwa Mawaziri wetu ni kama wanataka wamsubiri JPM afikiri kwa niaba yao.
Wakati wao wana mandate za ku-develop investment projects.

China sasa hivi wameundiwa na wa-Israel nyama za kuzalishwa lab. Kwa ukubwa wa soko la China, ni mkakati gani ambao hata wa kufikirika ushasikia kama sio Waziri (Kilimo, Biashara, Mifugo) basi walau mkuu wa benki ya Uwekezaji au kilimo anaona kwa jicho la kibiashara namna gani tuzalishe nyama ya punda, kitmoto, mbuzi, kondoo, ng'ombe kwa ajili ya China tu kwa kuanzia.

Ukifikia hapo utagundua wengi hawaoni kwa jicho hilo. Labda mie pia sioni vema, japo nadhani niko sawa.
Kwa mtaji huo, hapakuwa na makosa kuongeza ndege kama fedha ipo na wenye wizara husika hawajaona namna gani tuwekeze kibiashara
 
Huwa nawashangaa sana. Mnaongelea kilimo wakati hakuna soko.
Utasema soko liko nje ila huko nje hauko peke yako. Wao wana ubora wao ambao wakulima wa Tanzania hawauwezi.
Tanganyika peckers ilikuwepo wakati waingereza ni wakoloni tunauza nyama. Ni ubora gani ambao sisi tunashindwa kuuiga??

Basi hata Ngozi ng'ombe tunaochinja, JKN aliacha tanneries Mwanza. Na kiwanda cha viatu Morogoro.
Hata hivi navyo vinatushinda, au hatujawaza kufanya wenyewe. Hao wanaokuja, mbona ni mitaji kiduchu na akili kidogo tu, then ni sie hao hao tunaishia kuwa laborers???

Kama EPZA kuna jeans zinazalishwa kwa soko la nje. Ni sayansi gani ambayo sisi tunashindwa.
Kama tuna ma-daktarin wanapasua matumbo ya akina mama na kutoa watoto, tunashindwaje kujua viwango vya soko la nje nasi tukaiga basi kwa kuazia.

1571827099165.jpeg


Huenda kwa vyovyote tukawa sawa...
 
Magufuli ametoa kipaumbele kwa hizo secta tuvute subra
Subra haivuti heri.

Bila shaka tuone namna gani mabilionea 100 wanatokea kwenye ahadi aliyoitoa kungali mchana kabla hawajaja watu ambao hatujui hata wanataka nini

 
Tatizo sekta za kilimo, mifugo na uvuvi hazipewi uzito unaostahili pamoja na kwamba zinaathiri maisha ya zaidi ya asilimia 60 ya watanzania. Ukiongeza uzalishaji kwenye mazao ya mifugo, tuseme nyama na maziwa unaweza kupunguza na hata kumaliza kabisa tatizo la kudumaa kwa watoto ambalo mbali ya kuathiri ukuaji wa mtoto lina madhara ya muda mrefu kwenye uwezo wa kiakili (cognitive skills). Na hili unaweza kufanya just kwa ku upscale technology rahisi kabisa mfano, kuhimiza uchanjaji wa kuku wa kienyeji vijijini dhidi ya ugonjwa wa mdondo ambalo litaogeza uzalishaji wa nyama na mayai ambalo mbali na kuboresha lishe utaboresha kipato cha kaya kutokana na kuuza kuku na mayai. Hii imekuwa implemented singida vijijini na wote tunashuhudia namna kuku wa kienyeji kutoka singida wanavyofurika kwenye soko la dar es salaam. Mfano mwingine, kwa kutumia tecnolojia ya uhamilishaji (artificial insemination) unaweza kuboresha uzalishaji wa maziwa kwa ng'ombe wetu kutoka lita 400 kwa mwaka hadi lita 1500 kwa mwaka. Sasa hizi teknolojia ni rahisi sana na zina impact kubwa. Nini cha kufanya, ongeza bajeti kwenye utafiti wa kilimo, mifugo, uvuvi unaolenga kuongeza uzalishaji, boresha maslahi ya wataalam, himiza uanzishaji wa viwanda vya kusindika mazao ya kilimo, mifugo na uvuvi, fanya utafiti wa masoko ya mazao ya kilimo, mifugo na uvuvi kwa soko la ndani na nje ya mipaka, mfano, nchi za uarabuni.
 
Unapokuwa na ugali mdogo juu ya meza inategemea watoto/wasaidizi wanaona nini na wanawezaje kumshawishi mwenye kisu cha kugawa ugali juu ya kwanini wizara ya kilimo&mifugo zipate ugali mkubwa zaidi na mrejesho wake utakuwa kwa kiasi kadhaa cha numbers kimapato.

Mathalani;
New Zeland wana Ng'ombe wa wanaotoa maziwa ambao ni wastani wa 4.mil na ng'ombe wa nyama ni 3.6 million.
Kama tukilenga kupata earnings za walau 10% nini New Zealand wanapata; ambacho ni wastani wa say 1 trillion tokana na maziwa na nyama.

Then ngozi ambayo inapatikana machinjioni ikaongezwa thamani kwa viwanda vya ndani, ripple effect yake ni kubwa.
Kwa namna hiyo ingewezekana tukatoboa.

JPM alikuwa sahihi kununua ndege kama Wizara ya Kilimo na mifugo hawajaenda mezani kujenga hoja ya nini kinaweza kufanyika kwa kutumia brains za Watanzania.

Kosa ninaloliona (niko tayari kukosolewa) kwa Mawaziri wetu ni kama wanataka wamsubiri JPM afikiri kwa niaba yao.
Wakati wao wana mandate za ku-develop investment projects.

China sasa hivi wameundiwa na wa-Israel nyama za kuzalishwa lab. Kwa ukubwa wa soko la China, ni mkakati gani ambao hata wa kufikirika ushasikia kama sio Waziri (Kilimo, Biashara, Mifugo) basi walau mkuu wa benki ya Uwekezaji au kilimo anaona kwa jicho la kibiashara namna gani tuzalishe nyama ya punda, kitmoto, mbuzi, kondoo, ng'ombe kwa ajili ya China tu kwa kuanzia.

Ukifikia hapo utagundua wengi hawaoni kwa jicho hilo. Labda mie pia sioni vema, japo nadhani niko sawa.
Kwa mtaji huo, hapakuwa na makosa kuongeza ndege kama fedha ipo na wenye wizara husika hawajaona namna gani tuwekeze kibiashara
Hapana JPM hao mawaziri wake hawapi na fasi ya kutoa long term strategic plan yeye JPM anataka kupata sifa zaharaka haraka bila planning kama ununuzi wandege ujezi wa fly over ambao returns zake ni zamda mrefu......yeye ndoanataka aonekane kila sekita ukienda kinyume nae anakutumbua
 
Hapana JPM hao mawaziri wake hawapi na fasi ya kutoa long term strategic plan yeye JPM anataka kupata sifa zaharaka haraka bila planning kama ununuzi wandege ujezi wa fly over ambao returns zake ni zamda mrefu......yeye ndoanataka aonekane kila sekita ukienda kinyume nae anakutumbua
Hata flyover haikujengwa kwa mwaka mmoja ilikuwa ni process.

Hata miradi ya kufanyika ndani ya muda mfupi na wa kati kwenye kilimo na mifugo ipo.
Ni suala la mkakati wa nini kifanyike ndani ya muda mfupi ili ku-project mafanikio ya muda mrefu.

Ili hayo yatokee, kuna suala la kufikiria nini kifanyike. Kama wenye wizara husika hawana mtazamo huo, ni kwa namna gani wako open minded ili kushirikiana na brains nje ya wizara kwa lengo la kupata matokeo ya kuwafanya wao wafanikiwe na wakati huo huo sisi wananchi tufanikiwe.

It just needs collaboration efforts to make things happen
 
2 Reactions
Reply
Back
Top Bottom