Tanzania YETU: Je, ni jamii ya vilaza na viongozi wa Kiimla na Ukurupukaji?

Steve Dii

JF-Expert Member
Jun 25, 2007
6,402
1,254
WATANZANIA WATANZANIA WATANZANIA

NIMECHOKA NIMECHOKA NIMECHOKA​

NIMENYONG'ONYEA VYA KUTOSHA, NIMESUBIRI VYA KUTOSHA, NIMEDANGANYWA VYA KUTOSHA, NIMEAHIDIWA VYA KUTOSHA, NIMECHOSHWA NA MICHOSHO YA VIONGOZI NA MAISHA DUNI YA WATANZANIA KWA UJUMLA. SAFARI HII NALIA KWA MAANDISHI KWANI SIKUBALI KUWA SOTE NI VILAZA, SI SOTE TUNARIDHIKA NA HALI ILIYOPO.....

NATAMANI KUONA NCHI YENYE MABARABARA BORA, NCHI YENYE RELI BORA, WANANCHI WALIOJAA MATUMAINI, HOSPITALI NA SHULE ZILIZO MARIDADI. NATAMANI KUONA JAMII YA WATU WAWAJIBIKAJI, NCHI YENYE WAFANYABIASHARA, WAKULIMA, WATAALAMU NA VIONGOZI WACHAPAKAZI, WAKUBWA KWA WADOGO WOTE WANAOFATA KANUNI NA SHERIA KATIKA MAZINGIRA YAO. JAMII YENYE MASHAUKU NA KUULIZA MASWALI KUJUA UKWELI, JAMII INAYOJIBIWA IKIULIZA, JAMII YENYE WATU WABUNIFU NA WATU WAJASIRI LAKINI PIA WATU WEMA NA WAUNGWANA.

Tanzania yetu, tutakuja kuona lini waziri, au walau basi naibu waziri anajiuzulu?! Iwapo kashfa ambazo mimi naamini kuwa ni kubwa kuliko zote katika nchi yetu (angalau katika kipindi cha miaka niliyo ishi na kujua yanayonizingira)zinajitokeza na kuzimika kimya kimya bila ya kuona wahusika wanafikishwa kwenye vyombo vya sheria au wao kuachia ngazi kwa kushindwa kuwajibika ipasavyo.

Kashfa kama IPTL, RICHMOND, BoT, BUZWAGI na nyinginezo kadhalika bila kusahau hii mpya kabisa, ya MUHIMBILI NA UPASUAJI/UUAJI; zote naona zinapita au zitapita na kudaiwa zimechunguzwa au zinaendelea kuchunguzwa bila kuona wahusika tuliowapatia dhamana ya kutuongoza katika nyanja mbalimbali wanawajibika kwa kujiuzulu au basi kusimamishwa kazi mara moja.

Kweli sisi wagumu hivyo kujiuzulu? Au huku ni kutojua tu maadili ya uongozi bora, kusahu kanuni za uongozi? Au basi, jamii imeharibika na kuota sugu kiasi kuwa si wananchi wala viongozi wetu tu ambao hawaoni makosa, bali jamii nzima... sielewi kwa kweli. Tunaiga mengi kutoka jamii nyinginezo huko nga'ambo; kwanini basi tusiige hili la uwajibikaji pale tukoseapo ambalo mimi kinamna fulani ndilo naona limewawezesha wao kupiga hatua moja, mbili, tatu mbele zaidi ya sisi..

Angalia, mashirika ya umma mangapi yamepukutika puchukupuchu kabla ya baadhi yake kunasuliwa na PSRC?! Kuanzia UDA, TIPA, URAFIKI, TRC, Air Tanzania, n.k. yote haya yalikuwa yanajiendesha angalau kama huduma ya jamii tu pale ambapo hayakuthamini faida zaidi au kufanya vizuri. Ila kutokana na rushwa, uzembe na ubunifu duni, yameangamia mbele ya macho yetu bila kuona hata mkurugenzi mmoja anafikishwa mbele ya chombo cha dola...

Aibu kweli kweli, wakurugenzi wamekula bila kusaza na kwenda kujipatia ukurugenzi pahala pengine au hapo hapo katika kampuni iliyo nunuliwa na "wawekezaji" kwa hela mbuzi, eti tu kuwa shirika halikuweza kujinasua au kujiongoza lenyewe kwa kutegemea ruzuku za serikali.... nini kilicholifikisha shirika hilo katika hali kama hiyo kama si wizi na uzembe?! Unajua nini, ngoja ni thubutu tu kusema....WAKAMATENI WAKURUGENZI WOTE WALIO PELEKEA MASHIRIKA YA UMMA KUFIRISIKA, WAHOJINI UTAJIRI WAO NA WANAOPATIKANA NA HATIA MALI ZAO ZITAIFISHWE MARA MOJA.

Sasa hii ni nini kama si jamii ya vilaza?!..Jamii iliyozubaa kwa kukaa kimya wakati viongozi wao wakinena na kunukuu beti za ahadi kila kukicha kwenye majukwaa na kwa mashauku yasiyo aibu katika kusubiria kupandwa vichwa kutokana na vigelegele vya watu wasio matumaini bali vilio vinavyopasika kama vigelegele? Viongozi wanaopenda kuamrisha bila kutafakari wasemayo wala kutoa mifano. Viongozi wanao taja matatizo, na kuyakemea bila kuonyesha au kutamka mbinu za kuyamudu na kuyatokomeza. Jamii yenye viongozi waliojaa utawala wa imla bila kutafakari kwa makini wasemayo yana mantiki gani katika jamii kwa sasa, kesho na mbeleni.

ZIFUATAZO NI NAKALA KUTOKA KWENYE MAGAZETI HAPA TANZANIA, AMBAZO UKISOMA NA KUTAFAKARI UTAONA NI JINSI GANI NCHI YETU INAVYO HITAJI KUCHOCHEA MAPAMBANO YA KIFIKRA NA KIVITENDO ILI NCHI YETU IPATE KUSONGA MBELE BADALA YA KUDUMAA NA HIVYO KUONEKANA INARUDI NYUMA, MAANA WENZETU HATA WALIOPIGANA VITA MIAKA MICHACHE TU ILIYOPITA WATATUPITA AU WAMESHATUPITA (sidhani kama unahitaji fizikia ya kidato cha pili kuelewa hili..) :

Most 2006/07 purchases in public institutions improper`

2007-09-14 08:57:20
By Felister Peter


Seventy-one per cent of all purchases in public institutions in 2006/07 were incorrect, and did not comply with the regulations of the Public Purchase Act of 2004.

Speaking to reporters in Dar es Salaam on Wednesday, the Chief Executive Officer of the Public Procurement Regulatory Authority, Dr Ramadhan Mlinga attributed lack of knowledge on the purchasing Act as a contributing factor to incorrect procurements.

`This is the first investigation to be carried out since PPRA`s establishment in May 2005. We began with 20 public institutions and now intend to conduct inspection to another 20 public institutions between September and December this year`, said Dr. Mlinga.

Dr. Mlinga said PPRA plans to inspect 75 institutions in the financial year 2007/08, making the total number of institutions inspected reach 115 by the end of next year.

He said in the course of investigations, it was revealed that most institutions failed to comply with regulations on preparations of the annual purchasing programme by 35 per cent, and announcing tender results by 12 per cent.

It was also revealed that institutions failed to comply with requirement to have enough time to prepare tenders by 36 per cent.

PPRA found that there was no public institution that gave priority to local companies to win their tenders.

Dr. Mlinga reassured that the goal of PPRA is to conduct investigations in public institutions to understand problem areas in purchasing and see how they can be improved.

But overall, Dr. Mlinga observed that there was a need to educate officials in public institutions on regulations of the national Public Purchases Act of 2004.

SOURCE: Guardian

Asilimia 39 ya manunuzi ya taasisi za umma hayafuati utaratibu

2007-09-13 16:12:48
Na ITV Habari


Mamlaka ya udhibiti na ukaguzi wa manunuzi ya umma- ppra, imefanya ukaguzi wa shughuli za manunuzi kwa taasisi 20 za umma na kubaini kuwa asilimia 39 ya manunuzi yanayofanywa na taasisi hizo hayafuati taratibu zilizowekwa.

Akitangaza matokeo ya ukaguzi huo jijini Dar es Salaam afisa mtendaji mkuu wa mamlaka hiyo dk. Ramadhani Mlinga, amesema kufuatia matokeo hayo, wameweka mkakati wa kuboresha hali ya manunuzi ya umma kwa kutoa mafuzo kwa asasi zisizofanya vizuri.

SOURCE: ITV

Kulingana na habari hapo juu, sijui nikisema kuwa karibu asilimia 60 za bajeti ya matumizi ya offisi za serikali zinaishia kuibiwa nitakuwa nafanya makosa kweli?! Iwapo asilimia 71 hazitumiki ipasavyo...

Ajali za magari zaua watu 2,838

2007-11-20 10:11:54
Na Futuna Seleman


Watu 2,838 wamefariki kwa ajali za magari huku 15,855 wakiwa wamejeruhiwa kwa mwaka uliopita. Hayo yalisemwa na Katibu Mtendaji wa Baraza la Ushauri la Watumiaji wa Huduma za Nchi Kavu na Majini nchini,lililo chini ya Mamlaka ya huduma za usafirishaji wa nchi kavu na majini (SUMATRA) Bw. Oscar Kikoye jijini Dar es Salaam.

Bw. Kikoye alikuwa akizungumza ikiwa ni maadhimisho ya kuwakumbuka Watanzania walioathirika na kufa katika matukio ya ajali za barabarani.

Maadhimisho hayo yalifanyika ofisini kwake kwa kuwasha mishumaa ikiwa ni mara ya kwanza tangu Baraza hilo lilipoanzishwa hivi karibuni.

Kwa mujibu wa Bw. Oscar, kuanzishwa kwa baraza hilo kunafuatia kikao cha Umoja wa Mataifa (UN) kilichofanyika Oktoba 2005 na kuamua kwamba siku hiyo iadhimishwe kila wiki ya tatu ya mwezi Novemba kwa nchi zote duniani.

Halikadhalika, Katibu wa Chama cha Kutetea Abiria Wanaotumia Daladala hapa nchini, Robert Muhangwa alisema kuwa siku hiyo ni ya muhimu katika jamii, kwani abiria anatakiwa kujua haki zake za msingi katika suala zima la utumiaji wa vyombo vya usafirishaji.

Wadau wakitoa elimu kwa abiria, watakuwa makini kwa kutambua haki zao za msingi, elimu ambayo kimsingi itolewe na serikali kwa kushirikiana na wadau, alisema Bw. Muhangwa.

Alisema kuwa, ukosefu wa elimu kwa wananchi kujua haki zao, hupelekea madereva kuzidi kuendesha mwendo wa kasi kwa vile wananchi hawajui majukumu yao katika kuwadhibiti madereva hao.

SOURCE: Nipashe

Muumba Aturehemu; sheria zisizofuatwa mabarabarani kutokana na uzembe, ubishi na ujinga; magari yaliyojaza kupita vipimo kutokana na uhaba wa usafiri, mabarabara finyu kutokana na ubunifu duni na umasikini;... nini kingine kinasababisha hizi ajali, labda nimesahau moja au mawili hivi, nisaidie kuyatambua....

Halafu basi, angalia mambo ya kiimla hapa chini...

Biashara zilizofungwa kwa nyasi, majani marufuku

2007-07-20 10:41:22
Na Grace Chilongola, PST


Halmashauri ya Manispaa ya Ilala jijini Dar es Salaam, imewapiga marufuku wafanyabiashara kuingiza kwenye masoko bidhaa mbalimbali zikiwa zimefungwa kwa nyasi, majani, pumba, matawi ya miti au migomba, kwa sababu huchafua mazingira.

Katika taarifa yake aliyoitoa kwa PST jana, Mkurugenzi wa Halmashauri hiyo, Bw. John Lubuva, alisema kuanzia Jumapili ijayo wafanyabiashara hawatakiwi kuingiza bidhaa zao kwenye masoko zikiwa zimezungushiwa takataka hizo.

Bw. Lubuva aliwataka wazalishaji, wafanyabiashara na madalali wa mazao ya chakula, kuacha kuingiza bidhaa zao kwenye masoko zikiwa na majani.

Alisema sheria ndogo ya Halmashauri ya Manispaa ya Ilala ya mwaka 2001 ya kudhibiti na ukusanyaji wa taka, inawakataza kuingiza bidhaa katika masoko, zikiwa zimefungwa na nyasi, majani na pumba.

Alisema wafanyabishara watakaokadi onyo hilo, watachukuliwa hatua kali za kisheria, ikiwa ni pamoja na kutozwa faini na kufikishwa mahakamani kuanzia Julai 22, mwaka huu.

Alisema onyo hilo analitoa kwa mara ya pili, kufuatia onyo alilolitoa awali kupuuzwa na wafanyabiashara hao.

Alisema majani, pumba, nyasi, matawi ya miti, yamekuwa yakisababisha uchafu na kuongeza wingi wa taka katika masoko.

Hivi karibuni Manispaa ya Ilala ilianzisha kampeni ya kusafisha masoko kila siku ya Jumamosi, ambapo iliwataka wananchi kununua bidhaa zao mapema kwani ifikapo saa 8:00 mchana, masoko hufungwa na shughuli za usafi kuendelea.

SOURCE: Nipashe

--adha waliyoipata watu katika maeneo hayo hadi kufikia kutolewa kwa onyo kwa mara ya pili inaweza kufikirika tu, lakini ninahuhakika ni adha ya hali ya juu.

--hata hivyo, lazima niulize; je, kwanini onyo la kwanza lilipuuziwa? utekelezaji wa onyo hilo ulikuwa dhaifu au haukuwa na nyenzo za kutekelezea? Kabla ya onyo la pili kutolewa, je uchunguzi ulifanyika kuona kwanini onyo la kwanza limeshindikana?

--je, nyenzo gani wafanyabiashara waliwekewa ili kuhalalisha tamko la onyo la kwanza kisha la pili? Walijengewa viwanja vya magunia vipya? Walionyeshwa jinsi ya kuozesha nyasi au pumba kama wanatumia? Je, walionyeshwa kitu gani badala ya nyasi, pumba au matawi ambavyo wangeweza kutumia bila hivyo navyo kuharibu mazingira pia?

Labda hizi habari zinaandika kishabiki, lakini maswali mengi yanajitokeza katika kusoma hiyo moja hapo juu, kunakuwepo na haja kubwa ya kuhoji jinsi viongozi wetu wanavyofikiria kabla ya kukemea au kutoa onyo.

Lowassa akemea uchomaji misitu ovyo

HabariLeo; Saturday,November 24, 2007 @00:01

WAZIRI Mkuu, Edward Lowassa, amekemea tabia ya wananchi wa Rukwa kuchoma misitu na ameziagiza mamlaka za mkoa huo kuwashughulikia wote watakaobainika kufanya hivyo.

Waziri Mkuu ametoa agizo hilo baada ya kubaini kukithiri kwa uchomaji moto misitu katika maeneo mengi alimopita wakati wa ziara yake ya siku nne mkoani humo.

Sasa nauliza, hili ni tambiko gani la kuchoma moto?" aliuliza Waziri Mkuu wakati akizungumza na mamia ya wakazi wa mji wa Sumbawanga katika uwanja wa Nelson Mandela.

Wakati akiwa uwanjani hapo, Lowassa alishuhudia chanzo cha maji katika milima ya Mbizi kikichomwa moto na akawataka wananchi wajionee namna wanavyoharibu mazingira hivyo kuathiri pia upatikanaji wa maji.

Ndugu zangu wana Rukwa, nawaomba kwa dhati, nilidhani mkoa wa Morogoro unaongoza kwa kuchoma moto, kumbe nyie mnaongoza, alisema Waziri Mkuu.

Katika maeneo yote alipopita, Waziri Mkuu alizungumzia suala la uchomaji moto misitu na kuonya kuwa endapo vitendo hivyo vitaendelea, wananchi watakosa pa kuishi na akawauliza wataenda kuishi wapi.

Katika ziara hiyo, Waziri Mkuu amefuatana na Waziri wa Nchi ofisi ya Waziri Mkuu Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI), Naibu Waziri ya Mambo ya Ndani, Lawrance Masha na Naibu Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Ludovick Mwananzila

Source: Habari Leo.

Cheo ni dhamana...

Lowassa: Marufuku mifugo kuingizwa bonde ziwa Rukwa

Basil Msongo, Sumbawanga
HabariLeo; Saturday,November 24, 2007 @00:05

WAZIRI Mkuu, Edward Lowassa, amepiga marufuku kuingizwa kwa mifugo katika bonde la ziwa Rukwa na wakati wowote kuanzia leo atamwagiza Waziri wa Kilimo aende kulitazama bonde hilo kuona namna linavyoweza kutumika kwa kilimo.

Ameagiza mamlaka za mkoa huo zisiwabughudhi wafugaji ambao tayari wana mifugo katika bonde hilo, lakini wasiruhusu mifugo mingine kuingia.

Lowassa aliyasema hayo alipozungumza na wakazi wa kata ya Msinda wilayani Sumbawanga mkoani Rukwa, ikiwa ni sehemu ya ziara yake ya siku nne iliyoanza Jumanne wiki hii.

Aliwaeleza wakazi wa eneo hilo lililopo chini ya mlima Muze, kuwa bonde lao ni zuri, lina rutuba ya kutosha na zao lolote linaweza kustawi hapo, hivyo lazima litumike kwa kilimo chenye tija.

Kwa mujibu wa Lowassa, endapo bonde hilo litatumika vizuri kwa ajili ya kilimo linaweza kuulisha mkoa huo wote, Iringa na Mbeya hivyo haoni sababu ya kutolitumia kikamilifu.

Lowassa alitoa changamoto kwa Mbunge wa Kwela, Chrisant Mzindakaya kutumia uzoefu, umaarufu na uwezo wake wa ujasiriamali kuona namna bonde hilo linavyoweza kutumika kwa ukamilifu kwa kilimo cha kisasa.

Alisema bonde hilo lina maji ya kutosha, hivyo kila kitu kinastawi hivyo akamuagiza pia Mzindakaya na viongozi wengine wa eneo hilo wapitie mpango wa Taifa wa kuendeleza kilimo kuona namna wanavyoweza kulitumia kwa ukamilifu kuongeza tija katika kilimo.

Kabla ya kuzungumza na wananchi hao, Waziri Mkuu alifungua josho la mifugo la kijiji cha Mfinga lililojengwa kwa gharama ya Sh milioni 17.

Katibu wa Chama cha Ushirika cha Msingi cha wafugaji na wazalishaji mali wa Mfinga, Nathani Kisusi, alimweleza Waziri Mkuu kuwa josho hilo limejengwa kuunga mkono jitihada za serikali za kuwaletea wananchi maisha bora na kuongeza kipato kupitia sekta ya mifugo.

Lengo kuu la ujenzi wa josho la Mfinga ni kuzuia vifo vya mifugo vinavyosababishwa na magonjwa yanayoenezwa na kupe. Asilimia 75 ya vifo vya ndama katika kata ya Mpito na Mfinga vinasababishwa na magonjwa yanayoenezwa na kupe, alisema Kisusi.

Wanaushirika hao waliishukuru serikali kwa kuwapatia dawa ya kuogeshea mifugo ya ruzuku, lakini walisema bei bado ni kubwa kwa wafugaji walio wengi kwa kuwa lita moja ya dawa hiyo wanauziwa kwa Sh 34,500.

Source: HabariLeo

'Top Down management approach' inaweza kufanya kazi kama inatekelezeka ipasavyo. Lasivyo inapotumika katika mfumo wa jamii kimakosa makosa huonekana kama 'jamii hiyo ni ya kijeshi' au darasa fulani hivi kwenye shule yenye msimamo wa udikteta.

Viongozi wanapokurupuka au kujiandaa na kutoa maonyo au kukemea fikra na matendo wasiyoafiki au yasiyo afikika katika jamii zao ni bora wafanye hivyo kistaarab na kiuungwana kwa kuonyesha mifano bora na mbinu za kutatua matatizo hayo. Kukemea au kuamuru tu hakutoshi. Kwani wao pia kama wananchi na watu tuliowapatia dhamana kwa kutuomba kuwapigia kura au kuwachagua ili kutuongoza, tunaweza pia kuwakemea pale tunapoona mahitaji yetu muhimu hayatimiliki mwaka nenda rudi.

Yaani pale tunapoona ahadi za hospitali, mashule na walimu hazitimiliki. Ahadi za mabarabara zinazidi kusogezwa mbele na chaguzi zinapokuja wanatuahidi yale yale tena... Hapo basi tunabidi kuwakemea kama vile wao watukemeavyo, na ndipo 'top down' management approach inapogeuka kuwa 'bottom up' ghafla... labda ujiulize, katika mfumo uliojijenga wa top-down, je hili linakubalika?! Hapa ngoja tu nirudie tena usemi wa wahenga wetu kuwa, 'mkuki kwa nguruwe...'

Amtaka Waziri ashughulikie matatizo sekondari Kantalamba

HabariLeo; Saturday,November 24, 2007 @00:03

WAZIRI Mkuu, Edward Lowassa, juzi alimwamuru Naibu Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Ludovick Mwananzila, asishiriki kwenye ziara aliyoifanya jana asubuhi mjini Sumbawanga, aende katika shule ya sekondari ya Kantalamba kushughulikia matatizo kati ya walimu na wanafunzi wa shule hiyo.

Alitoa agizo hilo katika uwanja wa Nelson Mandela mjini Sumbawanga baada ya mmoja ya wanafunzi wa Kantalamba kumweleza kuwa wanafunzi wa kidato cha tano na sita hawana mwalimu hata mmoja, hivyo wanachofanya ni kuseremua yaani kukariri tu.

Mwanafunzi huyo, Prosper Kanyombo pia alimweleza Lowassa kuwa wanalishwa chakula kibaya, hivyo kuathiri afya zao.

Waziri Mkuu alimwita Mkuu wa Shule hiyo atoe maelezo, lakini hakuwapo uwanjani hapo hivyo akamtaka Mwananzila ajibu tuhuma hizo hapo hapo uwanjani, hali iliyosababisha wananchi waliokuwapo uwanjani hapo kushangilia wakiwamo wanafunzi wa shule hiyo.

Mwananzila alikiri kuwapo kwa upungufu wa walimu katika shule hiyo, lakini akasema kuna walimu sita wa vidato vya tano na sita kati ya walimu 39 waliopo shulemi hapo.

Alisema walimu ni wachache kwa kuwa baadhi ya wanaopangiwa kufundisha Rukwa huenda katika mikoa mingine na kwamba, mfuko wa kutoa hamasa kwa watumishi uitwao Mfuko wa Mwalimu Nyerere umesaidia kupunguza ukubwa wa tatizo hilo.

Naibu Waziri alikiri pia kwa wanafunzi hao wamekuwa wakila chakula kibaya kwa kuwa ndicho kilichokuwa kikipatikana kwa kuwa waliokuwa wakipeleka chakula katika shule hiyo na shule nyingine walikuwa hawajalipwa fedha zao.

Mwananzila alisema Oktoba 10 mwaka huu serikali ilianza kuwalipa wafanyabiashara hao, hivyo wanafunzi hao wataanza kupata chakula kizuri.

Alimuagiza mkuu wa shule hiyo akae na walimu na wanafunzi wakubaliane chakula gani wanapenda kula ili wasome vizuri.

Source: HabariLeo.


Nimechoka nimechoka nimechoka, kwani naamini kabisa kuwa Tanzania yetu si nchi yenye vilaza wote, pamoja na kuwa baadhi yetu wanaweza kuwa. Tanzania yetu si nchi ya viongozi wenye imla na kukurupuka kwani baadhi ya viongozi wetu wanaonyesha umaridadi, utanashati na uwajibikaji unaozingatia kanuni zote na maadili ya uongozi.

Tatizo, kukaa kwetu kimya na upole wetu, muungano na undugu wetu, amani na utulivu wetu unafanywa uwe chombo cha kutuangusha badala ya kuwa nyenzo madhubuti ili kutuhamasisha na kutuendeleza. Kibaya zaidi ni kuwa, mfumo wa maisha yetu, kama vile mazingira ya kijamii, uchumi, sheria na siasa zetu umejijengea mizizi na kutufanya sisi sote tuamini kuwa hatuwezi kubadilika na kuleta mapinduzi ya kifikra na vitendo katika kuiendeleza nchi yetu. Kingine kilichojiotea mizizi na cha kusikitisha ni kuwa kuhoji viongozi wetu ni kukosa maadili na kukiuka tamaduni zetu.

MUNGU IBARIKI NCHI YETU TANZANIA NA BARA LETU AFRIKA. AMINA!

SteveD.
 
Na skendo zinazidi kulipuka na kujirudia, haziishi, sasa Kiwira na Mchuchuma...

Picha kwa hisani ya haki-hakingowi blog.

SteveD.
 
SteveD:

Hapana ndugu yangu, waTanzania wote sio vilaza. Ni swala la mda tu, sote inabidi tuwe na subira kidogo, na tuendelee kuelimishana ipasavyo.

Elimu inayofaa hasa wakati huu tukiendelea mbele ni ya kujua na kuyatambua maneno matamu ya kisiasa, hasa wakati wa chaguzi, na nyakati kama hizi za ufisadi unaolenga kutufunika macho tusione yanayotendeka.

NI MHIMU SANA WAANZE KUJIFUNZA KUULIZA MASWALI MAGUMU NA KUSISITIZA WAPEWE MAJIBU BILA YA KUMJALI HUYO ANAYEULIZWA ANACHO CHEO GANI.

Nadhani yule kijana wa Sekondari kule Ukerewe ni mfano mzuri. Ni mhimu tumuige.
 
Ni kweli kabisa, siyo wote vilaza nakubaliana na hilo na nililisema hapo mwisho. Hata viongozi wetu, wapo ambao wanatenda kazi kama jinsi ipasavyo.

Kalamu, mfano wako wa huyo kijana aliyeuliza swali ni mzuri sana.. nami hivi sasa nasubiria kusoma report ya tume mpya kutoka wizara ya Afya iliyopelekea watu wawili kufanyiwa upasuaji tofauti, na mwingine kufariki (RIP), katika kuangalia ngazi za uzembe zilizopo...

SteveD.
 
SteveD,

Hofu yangu ni kuwa je, hawa 'watawala' wetu wana masikio ya kusikia na macho ya kuona? wana hata chembe ya tafakari? Huyu EL nilidhani semina ya ngurdoto imemsaidia walau kujua namna y akuwaheshimu wananchi na viongozi wenzake lakini naona bado naye 'amekariri' uongozi wa kidikteta kama huo

Katika hili, mapambano ya kifikra bado yana safari ndefu kuzaa matunda!
 
Matatizo ya Tanzania ni kama uzi uliojiviriga viriga. Inatakiwa ufundi mkubwa kuufumua na kuuweka uzi huo katika hali ya kuweza kutumika tena.

Viongozi wa Tanzania wanatoka miongoni mwa watanzania. Ni kioo cha watanzania. Je jamii ya kitanzania ni ya watu wa aina gani? Well, naweza kusema wengi wetu tuna ugonjwa wa utumwa wa kifikra. Viongozi/watawala wakati wa ukoloni waliishi maisha tofauti na wanaowatala. Waliishi kadiri ya standard ya wanaowawakilisha....nchi za kikoloni.

Waliokamata dola baada ya wakoloni wameshindwa kufuta au kubadili utumwa huu wa kimtazamo. Nyerere alijitahidi kiasi kuondoa aina hii ya utumwa. Lakini alizungukwa na wanafiki, waliofurahia maisha ya juu tofauti na walalahoi.

Haiingii akilini kumuona waziri au kiongozi mwingine wa juu akiwa ndani ya gari la kifahari kwenda kutembelea wananchi ambao wengine hata viatu hawana, mlo wa siku kuupata ni songombingo, kula nyama mara moja kwa miezi 2 au zaidi. Kiongozi huyo huyo kama atakuwa na ratiba ya kula lunch katika kijiji kimoja, atatayarishiwa chakula bora ambacho familia nyingi hukipata sikukuu tu za Christmas au Eid. Huo ndio utumwa wa kifikra.

Dawa yake ni kuelimishana tu. Pole pole tutaona mwanga kwenye tanuru.
 
SteveD,

Hofu yangu ni kuwa je, hawa 'watawala' wetu wana masikio ya kusikia na macho ya kuona? wana hata chembe ya tafakari? Huyu EL nilidhani semina ya ngurdoto imemsaidia walau kujua namna y akuwaheshimu wananchi na viongozi wenzake lakini naona bado naye 'amekariri' uongozi wa kidikteta kama huo

Katika hili, mapambano ya kifikra bado yana safari ndefu kuzaa matunda!

Nakulilia... haswaaaaa, umemenena hapo. Unajua mtoto wa shule anafundishwa mbinu zote za kusoma na kuelewa anachokisoma, kisha anakuwa mbunifu na anayetafakari kile alichokisoma ili kuendeleza jamii kwa kugundua mbinu mpya au kuendeleza zilizopo lakini katika hali iliyo maradufu.

Tatizo la viongozi wetu WENGI, ni kuwa kuna semina kibao wanahudhuria, lakini tatitizo ni kuwa wanaenda 'kukariri' badala ya kuelewa!

Kuna pahala ambapo kukariri kunakubalika, lakini si katika kila jambo. Mengine yanahitaji 'kutafuna', 'kumeza' kisha 'kuyatumia tumboni' kurutubisha uhai wetu badala ya 'kuyacheua tu'.

SteveD.
 
Wazee hongera sana kwa kuonyesha uchungu mlio nao juu ya nchi yetu. Lakini kama rafiki alivyosema hapa, ni kwamba Mabadiliko ya nchi yetu yanahitaji kusukumwa na sisi wenyewe. Watanzani tulishabatizwa majina kwamba ni wazuri wa siasa za mdomoni lakini utendaji hakuna.

Kinachohitajika hapa ni kuibana serikali pale inapoonekana kumekuwa na issue na si kwa media tu bali hata matendo. Kwa mafano suala Muhimbili, litatia kinyaa. Tume iliyochunguza suala waziri wa afya ameikataa report mpaka amemuamua kuunda tume nyingine. Sasa vitu kama hivyo some serius reactions should be arleady taken kwa watuhumiwa wote, na si kusimamishwa tu bali kuwekwa rumande wakati uchunguzi ukifanyika. Unaposimamisha kazi kwa muda unawapa muda wa kuinterrupt uchunguzi.

Sisi wenyewe tubadilike, tufanye mambo kwa vitendo si siasa za mdomo tu.
 
Invincible:
Mimi sina tatizo na ukarimu wa kweli kabisa walio nao waTanzania, hasa walioko huko vijijini. Hii ni jadi yetu, ingawaje sasa imepindishwa na kuwa aina ya rushwa kwa huyo waziri mwenye shangingi anayetembelea kijijini. Matarajio sasa yamekuwa ni kuwa, labda kigogo huyo akisharudi huko atokako, nae atawakumbuka kwa ukarimu wao (isomeke - anayekumbukwa ni kiongozi hapo kijijini aliyepiga kelele zaidi, ili na yeye afaidike kibinafsi na wala sio kama kijiji).

Je, ingekuwaje patokee waziri au kiongozi anayeamua kujaza shangingi lake vifaa vya ujenzi wa shule pale kijijini bila ya kusubiri yeye ndie apewe chakula? Hata katika tamaduni zetu, mgeni huleta neema (zawadi n.k.) na yeye hukarimiwa bila kujali alicholeta.
 
Kalamu
Duniani hapa ukarimu ni sifa njema. Ukarimu huu wetu umezidi kipimo. Ni kwa hasara yetu kwa kweli. Hivi mtu anapata 'kwashiakor', kwa sababu tu chakula bora anakitunza hadi atakapopata mgeni? Tuonyeshe ukarimu kwa yale yaliyo ndani ya uwezo wetu wa kila siku, na sio vinginevyo. Ndivyo jamii nyingi zinavyofanya. Ukarimu kwa hasara yako, ndio nini hii?

Tulisifiwa pia kwamba tumekuwa wakarimu kwenye mikataba ya madini. Could that be partly a result of this kind of African/Tanzanian generosity?

Halafu suala la gari la kifahari nina maana ya tofauti kubwa mno ya maisha kati ya viongozi na wananchi. Gari la kifahari libebe tena vifaa vya ujenzi?

Naamini bado tatizo la msingi ni mental slavery. Tunamtumikia bwana mkubwa. Na anayepata cheo anataka atumikiwe kama bwana mkubwa. Na Mkapa alikuwa living example wa mental slavery. Amewatumikia wazungu zaidi kuliko wananchi wake.
 
SteveD said:
NATAMANI KUONA NCHI YENYE MABARABARA BORA, NCHI YENYE RELI BORA, WANANCHI WALIOJAA MATUMAINI, HOSPITALI NA SHULE ZILIZO MARIDADI. NATAMANI KUONA JAMII YA WATU WAWAJIBIKAJI, NCHI YENYE WAFANYABIASHARA, WAKULIMA, WATAALAMU NA VIONGOZI WACHAPAKAZI, WAKUBWA KWA WADOGO WOTE WANAOFATA KANUNI NA SHERIA KATIKA MAZINGIRA YAO. JAMII YENYE MASHAUKU NA KUULIZA MASWALI KUJUA UKWELI, JAMII INAYOJIBIWA IKIULIZA, JAMII YENYE WATU WABUNIFU NA WATU WAJASIRI LAKINI PIA WATU WEMA NA WAUNGWANA.
Kwanza ni muhimu kufahamu jinsi viongozi na wananchi wenyewe wanavyofikiria. Unajua kama watatimiza lolote hapo juu basi tutakuwa tumetoka ktk fungu la kupewa misaada yaani sisi sii maskini tena.
Pili, wanafikiria kwamba uchumi wetu unazidi kujengeka kama alivyo maskini yaani kila anavyoonekana hoi ndio riziki inavyozidi..

Hata Utalii wanaamini bado ni mbuga na wanyama kwa hiyo kama utatengeneza barababara nzuri,hospital n.k utakuwa umeharibu picha ya mbuga na sii ajabu watalii wakaacha kuja. Ile hali ya asili ndio inayovutia watalii wakiona Masai na Mang'ati ktk mavazi yao na madawa ya miti shamba hiyo ndio Tanzania wanayotaka watalii kuiona. Hivyo hivyo ktk taasisi nyinginezo zote mawazo yetu ni kusaidiwa kwanza na how tutaweza kupata misaada hiyo?

Tatu, na mwisho ni kwamba wao ndio watawala wa nyumba hii ya maskini na kamwe ombaomba hawezi kuamini kuwa mwanaye anaweza kutoka ktk curse hii ya Umaskini.... kwa hiyo Principal za maisha ya maskini na ombaomba haziwezi kubadilika kwa kufikiria nje ya umaskini huo. ndio maana kila unapouliza swali kiongozi wetu jibu lao la kwanza huanza na - Sisi maskini, nchi yetu maskini kwa hiyo... blaa blaaa blaaaa!

Point zao zote hujengwa within the closet la Umaskini! ndio maana nasema labda kizazi hiki kipya na sijui kitakuja lini maanake huyu JK mwenyewe nilifikiria he belongs to this generation!...
 
Point zao zote hujengwa within the closet la Umaskini! ndio maana nasema labda kizazi hiki kipya na sijui kitakuja lini maanake huyu JK mwenyewe nilifikiria he belongs to this generation!...

Mkandara, shukrani, maneno mazito hayo kama kawaida...

Kuhusu kizazi 'hiki' ni kuwa kipo, ila kama inapita miaka kama 7 mingine bila kuwa hakijaamka, basi itatutumia vizazi vingine viwili au vitatu kuamka. Namaanisha kuwa, hii nguvu ya kuamsha watu ingelianza kama miaka 10 iliyopita na ingekuwa inawezekana kama hivi sasa kutokana na mfumuko wa teknolojia ya mawasiliano, basi leo hii tungelikuwa tunaweza kupima hatua tuliyopiga katika kukiwezesha kizazi hiki kujua kuwa maisha na fikra tulizonazo hivi sasa zinaweza epukika na kuwa na fikra endelevu zaidi.

Miaka 10 iliyopita maandishi yako hapo juu nisingeweza kuyaona katika makala iliyochapishwa au inayosikika bila kukujua wewe. Lakini hivi sasa, tunaweza kuunganika kirahisi. Hebu fikiria wewe mwenyewe, nikiamini kuwa wewe ni mzoefu katika kujadili mazingira yetu na ya uongozi nchini; je, mawazo yako yalikuwa yanaweza kuwafikia watu zaidi ya 10 miaka 10 iliyopita pale unapo yatoa?! Situmaini, labda kama ulikuwa unayaweka kwenye magazeti yetu. Lakini hivi sasa, uzoefu wako na mawazo yako yote unayoweza kuyaandika kwenye mtandao, yananifikia mimi na wengine. Hapo basi kama mimi ni mpenda maendeleo, nitayatafakari na kuyatumia ipasavyo kwa kuyatawanya zaidi au vinginevyo.

Hivyo basi, kizazi ni hiki. Tukitumikie kwa moyo wote. Teknolojia iko nyuma yetu kutusukuma na kutuwezesha.

SteveD.
 
Naweza kukubaliana kwa kiasi fulani kwamba Jamii yetu ni Vilaza. kama wapo wasiovilaza basi ni wachache sana kiasi wanamezwa na vilaza wengi.

Wakati fulani hufikiri labda vilaza ni wale ambao kwa bahati mbaya hawakupata bahati ya kuingia darasani lakini imekuwa ni kinyume chake, wote wasomi na wasio wasomi tumebaki kuwa vilaza.

Tunalo tatizo kubwa la msingi (ignorance), karibu kila mtu amekuwa ignorant kwa nafasi yake, iwe ofisini, shuleni, shambani vijiweni na kwingineko. inawezekana tukipata tiba ya ugonjwa huu tunaweza tukasogea kwa kiasi.

Wakati mimi nawaza kwamba ili tusonge mbele tunahitaji Bunge balanced kwa mfano. kwa maana kwamba wasomi wetu wangeliangalia hili kwa mtazamo wa kitaifa hivyo kujigawa kwa makusudi kwenye vyama vya siasa. kinachotokea kila anayetaka ubunge anakimbilia CCM why? ignorance, Wananchi nao kwa upande wao wanatumbukia kwenye shimo hilo hilo 'ignorance'

Vijana wanapiga kelele weee, ikifika wakati wa uchaguzi hawajiandikishi, lakini wanataka viongozi wapya, nani awachagulie 'ignorance'

Viongozi wa CCM nao wakiona upinzani unapata nguvu kidogo, haoo na mapesa yao kuwarubuni viongozi wanaonekana wana nguvu wajiunge ccm, why? 'ignorance' Wote tumeoza hakuna watu wenye mapenzi ya kweli na nchi yetu.
 
SteveD,

Nakuhakikishia kuwa mimi binafsi siyo Kilaza ila najuta kuwa nina ndugu zangu wengi sana ambao ni vilaza. Hata hivyo pole pole sasa nao wameanza kujinasua kutoka makucha hayo ya ukilaza.

Ndugu zangu wamekuwa wakidai kuwa hawaoni mtu mweingine wa kumpa uongozi kwa hiyo wanampa fisadi yule yule; sijawahi kuelewa maana yao kufanya uamuzi wa aina hii. Namna nyingine ya kumfunza fisadi ni kumnyima kula hata kwa kumpa nafasi fisadi mwingine lakini siyo yule yule.
 
Saharavoice,

IGNORANCE!...Hizo nondo mjomba nondo!...nimekupata safii toka ktk FM 93.5..

Je, hili neno ndio hasa linalofany tuvune VILAZA?

SteveD,
Shukran mkuu wangu ndio maana tupo hapa na tutaendelea kuchangia yetu mawili matatu kwa ajili yenu vijana mtakao tupa malezi sisi tukisha anza kutembea na mikongojo, ndio tumaini lililobakia.

Unajua katika fikiria zangu hasa ktk swala la kujikwamua nadhani kweli hili neno ignorance limebeba uzito mkubwa zaidi ya kila kitu. hata ukitazam pande zote mbili za shilingi bado majibu yanatokana na hili neno ignorance!...Saharavoice kama alikuwa kichwani mwangu vileeee!

Kwa mfano hivi sasa Tanzania nzima na hasa Africa yote tunalilia DEMOKRASIA. Viongozi wote na wananchi neno kubwa limekuwa DEMOKRASIA lakini wakati huo huo tumeshindwa kuangalia hii demokrasia hupatikana vipi...why?.

Yote inatokana na Ignorance, na ngoma hii nzito sana haijali kabisa elimu ya mtu. Tumeshindwa kabisa kufikiria kuwa, haiwezekani hata Kidogo nchi kuwa na demokrasia ya kweli ikiwa nchi hiyo INATAWALIWA. Reality na ukweli umesimamama kuwa Tanzania na nchi nyingi za kiafrika zinatawaliwa! Nchi zetu zina watawala hazina viongozi na kama utafikiria kwa undani utagundua kuwa hakuna kitu RULE of LAW. Yaani inavyotakiwa kua ni Rais ama serikali wao ni viongozi wanaojenga Leadership kuonmgoza nchi na sheria (Rule of Law) ndio hutawala nchi. Lakini kwetu sivyo, mtawala (rais na serikali yake) ndiye mwenye mamlaka na sheria zote na hatuthubutu kuwanyooshea kidole ama kuwakosoa kama vile majumbani mwetu mzee akitoa shuzi.

Ni Mila chafu ambayo tumeirithi kutoka ktk Utumwa ama tamaduni zetu wenyewe, kiasi kwamba ignorance tuliitazama kwa yule mtenda maovu tu bila kufahamu kuwa victim naye anaposhindwa kusimamia haki yake basi naye ni Ignorant. Kama mila za majumbani mwetu, wanawake (wake zetu) wasingeweza pata haki zao kama wasingeweza simama na kupigania haki hizo KIFIKRA. Siku zote kwa mwanamme wa kiafrika ndoa ilikuwa na maana kuwa mwananume ndiye huoa na mke ni mali yake na yeye ndiye mtawala wa nyumba. Anaruhusiwa kumburuza mkewe na watoto atakavyo na mke hana sauti kabisa na hata dini zilipoingia bado tulishindwa kutafsiri maana hasa za aya zinazohusu mahusiano kati ya mume na Mke. Neno KUONGOZA kwetu sisi lina maana moja tu nayo ni KUTAWALA kwa hiyo tuliweza kulijengea lingo dhidi ya hata aya za dini..

Tulishindwa kuelewa kuwa mwanamme alipewa madaraka ya kuongoza familia (nyumba na sio kuwa Mtawala wa nyumba hiyo na kwamba mwanamke ana nafasi sawa na yeye nisehemu kubwa ya familia hiyo akija na mazuri yake na mapungufu yake kama alivyo mwanamme. Ndio maana kwetu sisi mwanaume alikuwa hakosei jambo na hata nmama zetu walikubali udhaifu huo kutokana na kuwa ignorance hadi pale kizazi kipya kiliposimama na kusema NO WAY!...changes zikafuata lakini ndio hivyo kuna wanaodai kuwa changes hizo zimetoa uhuru mkubwa kwa wananwake kiasi kwamba mwanaume hawezi KUONGOZA tena familia na ndio maana ndoa zinavunjika ovyo ovyo. Tunarudi kule kule kuwa ndoa za babu zetu zilidumu zaidi kwa sababu baba zetu walikuwa WATAWALA through ignorance na mama zetu walikubali unyonge huo wa kutawaliwa (ignorance) kwa hiyo picha zikaiva.

Kutokana na mfano huo hapo juu nina imani kubwa kuwa hata sisi AMANI na UTULIVU Uliopo Tanzania inatokana na Ignorance yetu wenyewe. Viongozi na wananchi wake, sisi wananchi tumekubali kuburuzwa na viongozi wetu kama walivyokubali mama zetu kuburuzwa ktk ndoa zao.

Tanzania tumeendeleza na kuikumbatia ile mila ya kutawaliwa na kama wasemavyo CCM wao ndio wameleta UTULIVU na AMANI nchini naweza kubali hilo kwa mfano mkubwa wa hizo ndoa za wazazi wetu kwani CCM ndiye mume ndani ya nyumba hii Tanzania, na kupitia ignorance zake anajiona mtawala na mwenye kujenga taifa lenye AMANI wakati huo huo sisi wananchi tunasema sio CCM waliojenga amani na utulivu nchini isipokuwa sisi wenyewe kutokana na ignorance yetu ya kupuuza kutawaliwa..Ndoa yetu imeiva...

Duh! nimesema mengi ya kutosha kwa leo! nadhani ipo haja kubwa ya kuandika kitabu.

Pamoja nayote haya nadhani swala kubwa hapa ni IGNORANCE!...
 
Mkandara shukrani sana,

Kama ulivyosema hapo juu unaweza kuandika kitabu chenye kurasa nyingi kuhusu ugonjwa huu ignorance. umaskini wetu, ufisadi wetu na maradhi yetu yametokana na huyu ignorance. Hivi inakuwaje mtu uitwe fisadi na bado unajisikia ni fahali kama kwamba ufisadi ni kisifa cha jina lako kama vile kuitwa Mheshimiwa, Dr, mwalimu, Prof na mengineyo 'ignorance'

Inakuwaje mtaalamu wetu uliyesomeshwa kwa pesa za kodi za wananchi maskini kabisa. unatengeneza mikataba yenye kuliangamiza Taifa lako mwenyewe? 'ignorance' (Nimeamini Kweli ******** huibomoa nyumba yake kwa mikono yake mwenyewe)

Ni kwa vipi Waziri mkuu unaagiza (kwa mfano) bonde la ziwa Rukwa litumike kwa kilimo cha umwagiliaji bila kutafuta kwanza ufumbuzi wa tatizo sugu la mkoa huo 'Barabara'? Je miaka yote Rukwa imekuwa haizalishi ziada ya chakula lakini kutokana na ubovu wa barabara mazao yao yamekuwa yakiozea ndani au kuuzwa kwa bei isiyolingana na gharama za uzalishaji? Hata wakilitumia hilo bonde watayatoaje mazao yao huko kuyafikisha kwenye soko lenye faida?'ignorance'

Je hivi kweli hakuna viongozi wenye ujasiri na wanaoumizwa na ufisadi ndani ya serikali yetu ambao kwa ujumla wao wangemeguka kutoka mzimu CCM na kujiunga upinzani tuwe na political balance katika nchi yetu kama tunavyoshuhudia kwa majirani zetu Kenya, Malawi na hata Zambia? Mbona Mwalimu JK aliwahi kusema kwamba upinzani wa kweli utatoka ccm? ina maana kweli hakuna wasomi ndani ya ccm wanaweza kutafsiri kwa mapana sentensi hiyo?

Hivi kweli hatuna watu ndani ya ccm ambao hata wakigombea ubunge kupitia upinzani watapita kutokana na ama umaarufu wao au uadilifu wao kwa wapiga kura wao? kitu gani watapoteza? au ni Uwaziri? mbona wapo wasio Mawaziri hata sasa na wamebakia kuwa wabunge wanaoburuzwa na Waziri mkuu pasipo matakwa yao? 'ignorance'

Mkandara, tuendelee kumjadili huyu mdudu huenda tukapata ufumbuzi wa Tatizo letu.
 
SteveD:
Instincts za kila kiumbe ni 'self-preservation' kwanza kabla ya mengine yote. Tuachane na haya mambo ya 'ignorance' wala nini; kwa maana definition yake itatupeleka kwenye ubishi usiokuwa na mwisho hapa.

Jawabu unalo kabisa SteveD, katika sentensi yako hii: " Hivi kweli hatuna watu ndani ya ccm ambao hata wakigombea ubunge kupitia upinzani watapita kutokana na ama umaarufu wao au uadilifu wao kwa wapiga kura wao?" Jibu ni kwamba watu hao wapo sana, na wengi mno; lakini sikubali kuwa ni 'ignorance' yao ndio inayowafanya wasichukue hatua hiyo, bali ni 'self-preservation' kwa kujua hatari zinazoambatana na uamzi wa namna hiyo.

SteveD: Ninaamini kabisa, katika hali ya 'utawala' huu tulionao sasa hivi, Kikwete asingekuwa na nafasi nyingine tena ifikapo hapo 2010, kama pangekuwepo na msindani aliyejitoa mhanga toka humo humo CCM kupitia upinzani. Lakini hali inavyoendelea sasa hivi ni dhahiri kwamba watu wataendelea kumchagua Kikwete na wabunge walewale, kwa kukosa ujasiri wa viongozi waliomo ccm wanaoonekana kuwa na sifa zinazokubalika na wananchi.

Tuchukulie mfano huu: Salim Ahmed Salim, au hata Prof. Mwandosya angeamua kuwa mambo yaliyomo ccm wakati huu hayafai, na akaamua kujiunga na, tuseme CHADEMA, na hao akina Mbowe wawakubali na kuwapa hadhi wanzostahili; hili lingewezesha kuwepo na uwezekano mkubwa wa kumwondoa Kikwete na mafisadi wenzake kuliko kumtegemea Mbowe aifanye kazi hiyo, ambayo najua na pengine hata yeye mwenyewe anajua kuwa haiwezi.

Kwa bahati mbaya, ni viongozi kama hao, kwa sababu za kulinda maslahi? yao binafsi wanashindwa kujitoa kulitetea taifa.

Hiyo 2010, wengine tunaanza kukata shauri la kutopiga kura kabisa. Tuiteni 'ignorant' lakini hatuoni mwanga popote katika hali iliyopo sasa hivi.
 
Mheshimiwa Kalamu,

Sote tunazungumza Lugha moja ingawa tunatofautiana namna ya kulipa jina hili tatizo letu la msingi. mimi nimeona kwamba ignorance ndiyo mama wa hayo mabaya tunayoshuhudia na hata huo ubinafsi unatokana na hiyo Ignorance yetu.

Kuhusu kumeguka. wazo langu si mtu mmoja kujitoa ccm, bali jopo la viongozi wanaokerwa na ufisadi kumeguka kutoka ccm na kuunda upinzani wenye nguvu. Mwaka 1995 tulishuhudia Mrema akimeguka peke yake na haikusaidia sana kwenye kukuza demokrasia kwa sababu hatukupata wabunge wengi kutoka upinzani. na ndivyo inavyoweza kutokea pia kama aidha Salim, au Mwandosya peke yake ameguka kutoka ccm ili kushindana na Kikwete. tunahitaji jopo siyo mtu mmoja.
 
Saharavoice:

Nakubaliana nawe kuhusu 'kumeguka kundi', badala ya mtu mmoja mmoja.

Lakini pia ni busara tusiichukulie hali ya 1995 kuwa halisi ya hali ya 2010; kuna tofauti kubwa sana, na wananchi wanaijua vizuri sasa.

Pengine ni kwa vile mambo mengi yanayofanyika ndani ya vyama vya ushindani, wengi tusiohusika hatuyajui, lakini ingekuwa ni jambo zuri sana kama wakati huu, 2007 tukielekea 2008 wangekuwa tayari wamekwishaanza mipangilio ya 2010. Kwa mfano, hata kuwatambua wabunge wa ccm wanaoweza kushambuliwa na kushindwa. Kama mbunge amekaa bungeni miaka 10, 15, au 20 rekodi yake ipo wazi kabisa, ni kwa nini msianze kuifanyia kazi?

Kwanza wabunge watarajiwa wakati huu wangekuwa ndio wanajifahamisha kwa wananchi mmoja mmoja, badala ya kusubiri zima moto ya kampeni ya mwezi mmoja au miwili hapo 2010. Kwani ni kitu gani kinachowazuia akina Kitila kuanza sasa?

Haina ulazima wa mpaka Slaa na Zitto wafike huko vijijini ndipo wananchi waelewe mambo yasiyofaa yanayofanywa na CCM.
 
Kalamu, Saharavoice, Mkandara

This is interesting discussion!

1. May be tulinganishe Tz na majirani- Kenya, Malawi na hata Zambia! Ina maanishisha Wtz hatuna UJASIRI kuamua? Au maslahi binafsi mbele kwanza? Ni kitu gani kinawafanya Viongozi shupavu ndani ya CCM kukubali/kukuaa tu kimya na yanayoendelea? Angalia hapo Kenya mambo ni tofauti!

Are we afraid of changes? Kuna kitu/mbegu Mwal. aliiweka ya woga? Kuna rafiki yangu mmo0ja tena toka Ghana aliniambia Watz we are not as agressive and mobile as other Africans kama Ghanians, Kenyans, Ugandans etc. hata international vacancies zikitokes Mtz hachangamkii- yeye akiwa na kazi yake tu ya laki 3 kwa mwezi inamtosha! Nimeangalia naona kama kuna ukweli- wenzangu mnasemaje? Na jawabu lake ni nini? It is more than Ignorance!

2. Je upinzani ni jawabu la matatizo yetu ya sasa? Mbowe, Lipumba, Mbatia sii Watz wale wale? Au ni tofauti? Tuangalie senario za Zambia, Malawi, Ghana na Kenya- are they better off today kwa kuwa tu kuna upinzani madarakani?
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom