Candid Scope
JF-Expert Member
- Nov 8, 2010
- 11,883
- 6,884
- YAKATAA SHERIA YA KUZUIA NDOA YA WAKE WENGI NA USHOGA
SERIKALI ya Tanzania imeyakataa rasmi mapendekezo manne yaliyotolewa na Baraza la Umoja wa Mataifa la Haki za Binadamu likiwamo lile lililotaka kuzuiwa kwa haki ya kuoa wanawake wengi. Naibu Mwanasheria Mkuu wa Serikali, George Masaju, alisema hayo mjini hapa jana alipozungumza na waandishi wa habari mara baada ya ufunguzi wa mkutano uliojadili vipengele 53 vya haki za binadamu kama vilivyopendekezwa mbele ya Baraza la Umoja wa Mataifa la Haki za Binadamu.
Aliyataja mapendekezo mengine yaliyokataliwa kati ya 153 yaliyopendekezwa kuwa ni pamoja na lile lililotaka Tanzania kuwa na sheria inayoruhusu ndoa za jinsia moja (ushoga) kupiga marufuku ulipaji wa mahari na kuruhusu tohara kwa wasichana ambalo lilikwisha kukataliwa tangu mwaka 1998.
Masaju alisema katika mkutano uliofanyika Geneva, Uswisi mwezi Oktoba, mwaka huu Tanzania ilitakiwa kukubaliana na mapendekezo hayo, lakini iliyakataa kwa kuwa hayaendani na mila na deturi za Kiafrika na zaidi ingekuwa ni kuingilia uhuru wa mtu. Alisema katika mkutano huo ujumbe wa Tanzania uliridhia mapendekezo 96 kati ya 153, ambayo nayo yatapelekwa kwa wananchi kwa ajili ya majadiliano ili kupata majibu ya kisera yatakayopelekwa mbele ya baraza hilo baadae.
Pamoja na kukataa mapendekezo hayo, lakini serikali imesema kuwa haitaweza kufuta adhabu ya kifo kwa sasa kama ilivyoombwa na Watanzania wengi. Masaju alisema kuwa suala hilo ni zito na litaamuliwa tu hadi pale litakapojadiliwa kwa kina na wananchi wote hususan katika mchakato wa uundwaji wa Katiba mpya ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Tanzania daima