Tanzania yatia aibu huko Olympic

Mkuu ili mwanamichezo wa kada yoyote ashiriki Olympics ni hadi afikie viwango vya kwenda huko...

Riadha, masumbwi na siku za karibuni kuogelea ndio yamekuwa mashindano makuu ambayo Tanzania imekuwa ikitoa wawakilishi...

Kuna mahali nilisoma, Olimpiki ya mwaka huu tutakuwa na wawakilishi wachache sababu hatukuweza kupeleka watu wa masumbwi kwenye qualifications (nadhani Covid ndio kikwazo)...

Hivyo nafasi pekee zilizosalia ni riadha ndio hizo nafasi tatu na kuogelea (kulikuwa na mabwana wadogo wawili sijui kama walifuzu wale)
 
Picha hizi mbili zimepigwa jana tarehe 23 Julai 2021 wakati wa tukio la ufunguzi wa michezo ya Olimpiki jijini Tokyo, Japan.

Ki-utaratibu, kila nchi iliyopeleka wawakilishi inatajwa halafu wawakilishi wanapita mbele ya umati wakiwa na bendera ya taifa lao. Kutakuwa na jumla ya matukio 339, kwa aina za michezo 33, kwa namna 46

Picha ya juu ni tukio baada ya Tanzania kutajwa. Wawakilishi wa Tanzania ni watatu tu, lakini hawakuwepo. Hapa alionekana mtu mmoja mwenye asili ya Asia akipeperusha bendera ya Tanzania kama mwakilishi wa nchi yetu.
Picha ya chini ni tukio baada ya Kenya kutajwa.

Jumla ya wanamichezo 11,091 kutoka nchi 206 duniani watashindana kupata medali za dhahabu, fedha au shaba. Zipo nchi zimepeleka wanamichezo 100+, 200+, 400+ hadi 600+

Tanzania, nchi yenye watu takribani milioni 60, na asilimia zaidi ya 90 wapo chini ya miaka 35, umri wa michezo, imepeleka wawakilishi watatiu, ambao hawajaonekana wakati nchi yao ikitajwa.

Vijana wamebaki ndani ya nchi yao wanacheza ndondo, kubeti, singeri na kuuza karanga. Viongozi wao hawajali! Maneno mengi ya kutia matumaini yanasemwa majukwaani, vijana wanakubali bila kufikiri, na akili ya kudai hawana. Wamefungwa akili, wanaamini Mungu ndiye aliyewapangia kuwa kama walivyo, siku yao itakuja... miaka mia ijayo.

Ni nani mwenye akili ya kupunguza tatizo la ajira kwa vijana kwa kuboresha sekta ya michezo na kuiunganisha nchi na jumuia za michezo za kimataifa? Hakuna. Kuna wizara ya michezo? Ipoipo tu.

Tuendelee na masiasa yetu ya kuumizana, ndicho tunachoweza.View attachment 1866543View attachment 1866544
Watadai hawana hela?! Mpaka tozo za miamala zikubaliwe..
 
  • Kicheko
Reactions: BAK
Nilikuwa najiuliza watanzania wako wapi kwenye hii olympic kumbe wameenda watatu na hawajulikani walipo. Aibu
Namna ya kuwapata wawakilishi inawezekana ndio tatizo lilipoanzia:
1.Mashindano ya kuwapata wachezaji ,ingehusisha ngazi za wilaya, mikoa hadi Kitaifa.
2.Unaweza kukuta Taarifa ya mashindano ya Olyimpiki haikushirikisha wadau kwa kupanga,kuandaa na kuwaibua washiriki wenye kutimiza vigezo vya ushiriki mashindano husika.
3.Hivi viongozi wa michezo,mmeshindwa hata kuiga kwa jirani(Kenya,Ethiopia na wengine);mfumo wao wa usimamizi na wanafanyaje hadi kuwa na wanamichezo wengi.
4.Waziri wa michezo hapa kuna haja ya kuongeza nguvu ya ufuatiliaji na sera ya michezo kuangaliwa upya.
 
Picha hizi mbili zimepigwa jana tarehe 23 Julai 2021 wakati wa tukio la ufunguzi wa michezo ya Olimpiki jijini Tokyo, Japan.

Ki-utaratibu, kila nchi iliyopeleka wawakilishi inatajwa halafu wawakilishi wanapita mbele ya umati wakiwa na bendera ya taifa lao. Kutakuwa na jumla ya matukio 339, kwa aina za michezo 33, kwa namna 46

Picha ya juu ni tukio baada ya Tanzania kutajwa. Wawakilishi wa Tanzania ni watatu tu, lakini hawakuwepo. Hapa alionekana mtu mmoja mwenye asili ya Asia akipeperusha bendera ya Tanzania kama mwakilishi wa nchi yetu.
Picha ya chini ni tukio baada ya Kenya kutajwa.

Jumla ya wanamichezo 11,091 kutoka nchi 206 duniani watashindana kupata medali za dhahabu, fedha au shaba. Zipo nchi zimepeleka wanamichezo 100+, 200+, 400+ hadi 600+

Tanzania, nchi yenye watu takribani milioni 60, na asilimia zaidi ya 90 wapo chini ya miaka 35, umri wa michezo, imepeleka wawakilishi watatiu, ambao hawajaonekana wakati nchi yao ikitajwa.

Vijana wamebaki ndani ya nchi yao wanacheza ndondo, kubeti, singeri na kuuza karanga. Viongozi wao hawajali! Maneno mengi ya kutia matumaini yanasemwa majukwaani, vijana wanakubali bila kufikiri, na akili ya kudai hawana. Wamefungwa akili, wanaamini Mungu ndiye aliyewapangia kuwa kama walivyo, siku yao itakuja... miaka mia ijayo.

Ni nani mwenye akili ya kupunguza tatizo la ajira kwa vijana kwa kuboresha sekta ya michezo na kuiunganisha nchi na jumuia za michezo za kimataifa? Hakuna. Kuna wizara ya michezo? Ipoipo tu.

Tuendelee na masiasa yetu ya kuumizana, ndicho tunachoweza.View attachment 1866543View attachment 1866544
Huyo nu bongo zozo,anaiwakilisha tanzania

Sent from my SM-N960F using JamiiForums mobile app
 
Taifa la watu karibia milioni 60 tumewakilishwa na watu watatu Olympic?!

Nashauri tukapimwe mkojo.
Hv Kuna ulazima gani wakushiriki haya mashindano ikiwa maandalizi ni finyu,si ni Bora kutokushiriki au Kuna ulazima kila nch kushiriki?
 
Hakuna tunachokiweza sisi zaidi yakupiga mdomo nakutishiana kwakutumia mamlaka na vyombo vya dola.Kuanzia raia mmoja mmoja hadi viongozi wakubwa tunachokiweza kwa uhakika ni kuongea ila sio mambo ya kutumia akili au ushindani wowote.Kamwe usitegemee jambo lolote la maana nalakujivunia toka kwa huyu mtu anayetoka kwenye hii ardhi.Na tatizo linaanzia kwa aina ya viongozi tulionao.
 
Picha hizi mbili zimepigwa jana tarehe 23 Julai 2021 wakati wa tukio la ufunguzi wa michezo ya Olimpiki jijini Tokyo, Japan.

Ki-utaratibu, kila nchi iliyopeleka wawakilishi inatajwa halafu wawakilishi wanapita mbele ya umati wakiwa na bendera ya taifa lao. Kutakuwa na jumla ya matukio 339, kwa aina za michezo 33, kwa namna 46

Picha ya juu ni tukio baada ya Tanzania kutajwa. Wawakilishi wa Tanzania ni watatu tu, lakini hawakuwepo. Hapa alionekana mtu mmoja mwenye asili ya Asia akipeperusha bendera ya Tanzania kama mwakilishi wa nchi yetu.
Picha ya chini ni tukio baada ya Kenya kutajwa.

Jumla ya wanamichezo 11,091 kutoka nchi 206 duniani watashindana kupata medali za dhahabu, fedha au shaba. Zipo nchi zimepeleka wanamichezo 100+, 200+, 400+ hadi 600+

Tanzania, nchi yenye watu takribani milioni 60, na asilimia zaidi ya 90 wapo chini ya miaka 35, umri wa michezo, imepeleka wawakilishi watatiu, ambao hawajaonekana wakati nchi yao ikitajwa.

Vijana wamebaki ndani ya nchi yao wanacheza ndondo, kubeti, singeri na kuuza karanga. Viongozi wao hawajali! Maneno mengi ya kutia matumaini yanasemwa majukwaani, vijana wanakubali bila kufikiri, na akili ya kudai hawana. Wamefungwa akili, wanaamini Mungu ndiye aliyewapangia kuwa kama walivyo, siku yao itakuja... miaka mia ijayo.

Ni nani mwenye akili ya kupunguza tatizo la ajira kwa vijana kwa kuboresha sekta ya michezo na kuiunganisha nchi na jumuia za michezo za kimataifa? Hakuna. Kuna wizara ya michezo? Ipoipo tu.

Tuendelee na masiasa yetu ya kuumizana, ndicho tunachoweza.View attachment 1866543View attachment 1866544
Nimeumia sana kwa tukio hilo mkuu The Genius ,lakini nimeumia sana zaidi kwa hayo maandishi yako mkuu.
Umeandika ukweli mtupu.
 
Back
Top Bottom