Halisi
JF-Expert Member
- Jan 16, 2007
- 2,802
- 613
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
*
Tanzania imeshinda tuzo kwa kutekeleza vizuri malengo ya Elimu katika Malengo ya Maendeleo ya Milenia ya Umoja wa Mataifa yanayotakiwa yakamilishwe mwaka 2015.*
Tuzo hiyo ilipokokelewa rasmi jana na Waziri Mkuu Mizengo Pinda kwenye sherehe ya Tuzo za Malengo ya Milenia kwa mwaka 2010, katika ukumbi wa Hoteli ya Waldorf Astoria jana (Jumapili Sept. 19, 2010) mjini New York, Marekani.
*
Akipokea tuzo hiyo, Waziri Mkuu alisema tuzo hiyo itaipa moyo Tanzania kufanikiwa katika malengo yote ya Milenia ifikapo mwaka 2015.
*
Ni kama mafuta ya kulainisha katika injini, alisema huku akishangiliwa na mamia waliohudhuria tafrija hiyo.
*
Tanzania imefanya vizuri katika Lengo la Elimu la kuhakikisha Watoto wote wanaandikishwa shuleni, na kufikia Asilimia 95 mpaka sasa.*
Malawi nayo imepata tuzo kwa kufanikiwa kuondoa njaa na kuwafanya wananchi wawe na chakula cha kutosha. Rais Bingu wa Mutharika alipokea tuzo ya Malawi.*
Tuzo ya Utekelezaji wa Malengo ya Milenia hutolewa na Kamati ya Tuzo, ambayo ni Taasisi isiyo ya kibiashara yenye madhumini ya
*kuunga mkono jitihada za utekelezaji wa Malengo hayo.
*
Mapema, Waziri Mkuu Pinda alikutana kwa mazungumzo ya kawaida na Naibu Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Mhe. Dk. Asha-Rose Migiro na baadaye Mwakilishi wa Umoja wa Afrika katika Umoja wa Mataifa, Mhe. Amina Salum Ali.
*
Mhe. Pinda yuko New York, kwa niaba ya Rais Kikwete, kuhudhuria Mkutano wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa na Mkutano Mkuu wa kujadili utekelezaji wa Malengo ya Maendeleo ya Milenia.
(mwisho)
Imetolewa na:
********* Ofisi ya Waziri Mkuu,
********* S.L.P. 3021,
********* DAR ES SALAAM
Jumatatu Sept. 20, 2010
*
*
Tanzania imeshinda tuzo kwa kutekeleza vizuri malengo ya Elimu katika Malengo ya Maendeleo ya Milenia ya Umoja wa Mataifa yanayotakiwa yakamilishwe mwaka 2015.*
Tuzo hiyo ilipokokelewa rasmi jana na Waziri Mkuu Mizengo Pinda kwenye sherehe ya Tuzo za Malengo ya Milenia kwa mwaka 2010, katika ukumbi wa Hoteli ya Waldorf Astoria jana (Jumapili Sept. 19, 2010) mjini New York, Marekani.
*
Akipokea tuzo hiyo, Waziri Mkuu alisema tuzo hiyo itaipa moyo Tanzania kufanikiwa katika malengo yote ya Milenia ifikapo mwaka 2015.
*
Ni kama mafuta ya kulainisha katika injini, alisema huku akishangiliwa na mamia waliohudhuria tafrija hiyo.
*
Tanzania imefanya vizuri katika Lengo la Elimu la kuhakikisha Watoto wote wanaandikishwa shuleni, na kufikia Asilimia 95 mpaka sasa.*
Malawi nayo imepata tuzo kwa kufanikiwa kuondoa njaa na kuwafanya wananchi wawe na chakula cha kutosha. Rais Bingu wa Mutharika alipokea tuzo ya Malawi.*
Tuzo ya Utekelezaji wa Malengo ya Milenia hutolewa na Kamati ya Tuzo, ambayo ni Taasisi isiyo ya kibiashara yenye madhumini ya
*kuunga mkono jitihada za utekelezaji wa Malengo hayo.
*
Mapema, Waziri Mkuu Pinda alikutana kwa mazungumzo ya kawaida na Naibu Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Mhe. Dk. Asha-Rose Migiro na baadaye Mwakilishi wa Umoja wa Afrika katika Umoja wa Mataifa, Mhe. Amina Salum Ali.
*
Mhe. Pinda yuko New York, kwa niaba ya Rais Kikwete, kuhudhuria Mkutano wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa na Mkutano Mkuu wa kujadili utekelezaji wa Malengo ya Maendeleo ya Milenia.
(mwisho)
Imetolewa na:
********* Ofisi ya Waziri Mkuu,
********* S.L.P. 3021,
********* DAR ES SALAAM
Jumatatu Sept. 20, 2010
*