Tanzania yapinga ripoti ya UN ya Tume ya Haki za Binadamu

Quinine

JF-Expert Member
Jul 26, 2010
21,272
47,268
Waziri wa mambo ya nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Profesa Palamagamba Kabudi amesema kuwa tathimini iliyotolewa hailingani na uhalisia wa hali ilivyo Tanzania.

Tume ya Haki za Binadamu ya Umoja wa Mataifa imetoa taarifa juu ya haki za binadamu maeneo mbalimbali Duniani na kuonesha wasiwasi wake juu ya hali ya Tanzania.

Ripoti yenyewe hii hapa.

https://www.state.gov/wp-content/uploads/2020/03/TANZANIA-2019-HUMAN-RIGHTS-REPORT.pdf

Report in summary;

In 2017 Mwananchi Communication journalist Azory Gwanda disappeared in Kibiti District in Pwani Region while reporting on unexplained killings in the area and remained missing.

On May 4, Mdude Nyagali, a critic of President Magufuli, was kidnapped in Mbozi, Songwe, by armed masked men.
On July 29, an investigative journalist and government critic, Erick Kabendera, was arrested by plainclothes police officers who did not inform him of the charges.

Political Prisoners and Detainees

Several opposition politicians and individuals critical of the government were arrested or detained during the year, were usually charged with sedition, incitement, or unlawful assembly. For example, two opposition members of parliament, Freeman Mbowe and Esther Matiko of CHADEMA, served four months in jail after the court arbitrarily revoked their bail in November 2018.

On July 19, three students from Kampala International University in Tanzania were sentenced on counts of distributing pictures through WhatsApp groups showing President Magufuli wearing a hijab. The students were sentenced to four years in prison.

On April 24, the Kisutu Resident Magistrates Court continued with the criminal case against opposition MP Zitto Kabwe. The case alleges that Zitto made several seditious remarks against the TPF, accusing it of killing more than 100 civilians in Kigoma.

Freedom of Peaceful Assembly.

The government restricted freedom of peaceful assembly and association, including through bans decreed by authorities but not supported by law. The ruling CCM is the only party that may legally conduct public rallies.

Opposition political parties continued to be harassed and detained by law enforcement and have unsuccessfully sought redress in the courts. For example, on May 27, the former minister for tourism and natural resources Lazaro Nyalandu and two opposition members from CHADEMA were arrested in Itagi Ward in Sigida during a closed-door meeting.

In June the speaker removed opposition CHADEMA MP Tundu Lissu for absenteeism and failing to submit required disclosure statements in a timely manner. Lissu survived an assassination attempt in 2017 and since then has been abroad for medical care.

On October 16, the Court of Appeal overturned a May High Court of Dar es Salaam decision to prohibit district executive directors from supervising elections. The district executive directors are presidentially appointed to act as the secretary of district councils, and many are active members of the ruling CCM party.

In March 2018, police arrested nine top CHADEMA leaders and charged them with unlawful assembly and disobeying an order to disperse after demonstrating with supporters to demand the issuance of credentials for party polling agents on the eve of a February 2018 by-election.

======

Pro. Palamagamba Kabudi amesema kuwa wamepokea kwa mshangao mkubwa sana na wanaamini kama Kamishna wa wa umoja wa kimataifa wa za haki za binadamu Mishel Bashlet angekuwa Tanzania sasa basi asingetoa taarifa hiyo au asingeandika tathmini hiyo.

Anasema wamechukua hatua ya kuhakikisha kwamba leo balozi wa Tanzania katika wa umoja wa kimataifa ofisi ya Geniva anawasilisha majibu yetu rasmi kuhusu taarifa waliyoitoa.

Amesema hali halisi ya Tanzania hailingani na taarifa waliyoitoa na kwa kuwa sasa wapo kwenye uchaguzi mkuu na wana wagombea 17 na hakuna aliyezuiliwa kufanya kampeni wote wanafanya mikutano yao sehemu mbalimbali za nchi kwa ratiba ambayo imepangwa na tume ya uchaguzi na mikutano inahudhuriwa na wananchi wengi kwa wagombea wote hivyo hali halisi hailingani na kilichosemwa kwenye taarifa hiyo.

Amesema hakuna aliebanwa kwa kuwa hata wale wanaotukana wanatukana kadri wanavyoweza na wala hakuna aliechukuliwa hatua yoyote kwa kuwa wanajua hiki ndio kipindi cha wagombewa kusikilizwa ili wananchi watoe maamuzi yao hapo octoba.

Amesema kuwa kampeni za uchaguzi za mwaka huu ni tofauti na chaguzi zilizopita tangu kuingia kwa vyama vingi kwa kuwa uchaguzi wa mwaka huu umekuwa wa amani, umetulia kabisa na kila mgombea uraisi anasema anachotaka kusema na hatmae wananchi wafanye maamzi yao.

Ameendelea kusema kuwa sio tabia wala ada ya watanzania kupuuza kauli ya mtu yoyote amesema watanzania hupokea yote mabaya , ya uongo ya uzushi na kwa kuwa ndio hulka yao kupoea yote

Lakini ukisoma hiyo taarifa nzima kuna kitu kinataka kuoneshwa kwa dunia lakini kwa sasa Magufuli tangu aingie madarakani amefanya maendeleo makubwa hakuna anayenyoosha kidole kwa Magufuli kuhusu ubadhilifu wala rushwa, madawa ya kulevya hakuna anayenyoosha kidole amesema mambo hayo ndio yalikuwa yakipigiwa kelele na mataia na vyama vya upinzani na sasa ndani ya miaka mitano malalamiko yote Magufuli kayaondoa na kuyatatua.

Amesema kuwa sasa wanatafuta namnanyingine ya kumkamata, amedai kuwa Kiongozi wa kiafrika akifanikiwa wakashindwa kumkamata kwenye rushwa na ubadhilifu wanaanza kumtafuta kwenye demokrasia na haki za binadamu.

Amesema ilani ya chama cha Mapinduzi sura ya sita inazungumzia haki za binadamu na maendeleo na amesema Tanzania imeajiri mtu kwa ajili ya kutoa msaada wa kisheria kwa watu wasio na uwezo kwa makosa ya jinai na kesi za dahawa lengo ni kulinda haki za binadamu na kuhahakisha haki za kila mmoja zinalindwa na kuheshimiwa.

Sheria ya vyama vya habari ambyo imepitishwa Tanzania amesema imeangalia uhuru wa vyombo vya habari na maslahi ya wanahabari ikiwa na maana ya kulinda maslahi yao na haki zao kama watumishi.

Amesema kuwa hakuna taasisi isiyo ya kiserikali ambayo imefutwa na hao amabao fedha zao zimezuiwa amesema wametunga sheria kuhusu uwazi na uwajibikaji kuhusu fedha, wapo katika kipindi kigumu sana cha utakatishaji wa fedha amesema taasisi nyingine zipo kwenye uchunguzi na muda wa kujirekebisha hivyo hakuna taasisis yoyote iliyofutwa.

Amesema wanadai mahakama haziko huru lakini mahakama ziko huru na hao ambao wanadhani haki zao zimevunjwa basi waende mahakani wakapate haki zao.
 
Waziri wa mambo ya nje Prof Kabudi amesema ripoti ya hali ya haki za binadamu nchini Tanzania iliyotolewa na UN haina uhalisia wowote.

Kabudi amemtaka balozi wetu pale UN kuwafafanulia jinsi mambo yalivyo mazuri hapa nchini hapo barazani Umoja wa Mataifa.
Source BBC

Maendeleo hayana vyama!
 
Waziri wa mambo ya nje Prof Kabudi amesema ripoti ya hali ya haki za binadamu nchini Tanzania iliyotolewa na UN haina uhalisia wowote.

Kabudi amemtaka balozi wetu pale UN kuwafafanulia jinsi mambo yalivyo mazuri hapa nchini hapo barazani Umoja wa Mataifa.
Source BBC

Maendeleo hayana vyama!
Ipo wapi Tanzania ya Nyerere. Unatawala hautaki kukosolewa haya kama ni baba wa familia ukigoma changamoto ndani ya nyumba utatembeza vichapo kwa mke na watoto hatimaye jirani watajua.
 
Kwa yanayoendelea kwa akina Nusrat Henje,unategemea status ya haki za binadamu itakuwa vizuri?

Wakituambia tumeingia uchumi wa kati,tunawatangaza kila mahali na kukubaliana nao haraka sana!Sasa subiri watuambie ukweli mchungu,lahaula mishipa inasimama kupinga tu!

Kwanini Kabudi asiende kuomba report ili aangalie vigezo vilivyotumika na serikali ichukue hatua kurekebisha hayo?

Wakati mwingine hizi report zitusaidie kuangalia ni wapi tumeteleza!Kama hii ya haki za binadamu ni kwa manufaa ya watanzania ikiwa mambo yatarekebishwa!

Sema tu kwasababu wengi wanaotaabika ni wapinzani ndio maana report hizo zinapuuzwa na watawala!

Lakini pia taasisi za haki za binadamu zinapitia katika tanuru la moto,nyingine zimefungiwa account zao ili zishindwe kujiendesha!Hapo sio bure,ni kujaribu kufukia uovu unaoendelea nchini!

Shame!
 
7 Reactions
Reply
Back
Top Bottom