Tanzania yapata Mkopo wa Dola Mil 278 kutoka Benki ya Dunia

Ktk mfumo wa kibepari lazima awepo mnyonyaji na mnyonywaji. Tajiri na maskini. Hali tulio nayo ulimwengu wa tatu imetengenezwa na hao mabeberu ya dunia. Ukoloni mamboleo ndio unatamalaki sasa.


Jesus is Lord
Hata baada ya "Kujitawala" sisi wenyewe, bado tuendelee tu kulaumu mfumo? Haiwezekani tukasema sisi tunataka kufanya mambo tofauti kidogo tuonavyo inafaa sisi wenyewe?

Ninajua jibulako mkuu, usihangaike kunijibu hilo swali nililouliza hapo.

Ngoja nitumie muda kidogo kutumia hoja yako hii, nami kuweka ninachoamini juu ya hali yetu hii tuliyomo.

Binafsi ninaamini lawama hasa inaanzia kwetu sisi wenyewe na viongozi wetu wanaotuongoza katika awamu mbalimbali, na hasa hasa hizi awamu za miaka hii ya karibuni.

Tunashindwa hata kufanya mambo madogo madogo yaliyomo katika uwezo wetu, kubadili hali zetu, na badala yake tunasubiri mikopo kama hii, inayojadiliwa hapa.

Wananchi wengi wanaoishi ndani ya nchi yetu sasa hivi ni zao la uhuru wa nchi yetu, wengi wamesoma shule zilizoanzishwa na sisi wenyewe, lakini zikashindwa kuwapa uwezo wa kutumia akili ya kutumia nyezo zilizo katika uwezo wao kubadili mazingira yao. Hata vyoo vya mashimo, inakuwa ni tatizo kwetu, kweli?

Zahanati na vituo vya afya vimejengwa huko vijijini, lakini hatuna uwezo wa kuvifanya vifanye kazi kwa ufanisi. Hatujiulizi inakuwaje?

Kilimo chetu kwa sehemu kubwa ni kilekile alichotuachia mkoloni! Mkulima ambaye amesoma kwenye shule tulizoziendesha sisi wenyewe, hajabadilika, miaka sitini? Tunasubiri mikopo,kama hii, na inapopopatikana, hatujui inakopitia?
Hapo mwanzo, baada ya uhuru, tulisema kukosa watu wetu wenye elimu na utaalam katika mambo mbalimbali ilikuwa ni kikwazo kwetu.
Watu wakasomeshwa, tena kwa wingi na kwa gharama kubwa. Leo hii sidhani kuna eneo ambalo hatuna watu walilolisomea ndani ya nchi hii, lakini huoni kazi za hawa watu, sana sana itakulazimu uende ndani ya CCM, na utawakuta wamejazana huko, wakifanya yao yanayowafaa wao wenyewe, na siyo kunufaisha taifa.

Viongozi wetu sasa wameamua, kwamba sisi hatuwezi kuleta maendeleo katika nchi hii, kwa hiyo njia sahihi na bora iliyopo, ni kuagiza watu toka nje, waje watuletee maendeleo!

Hakuna kiongozi anayetaka kufanya kazi na wananchi hawa, kuwatia moyo na kuwahimiza wajiletee maendeleo ya kweli. Wananchi nao sasa wanawasikiliza viongozi wao, wakisubiri waletewe maendeleo, huku raslimali za nchi yao zikizolewa kama takataka!

Sasa acha tusubiri maendeleo, miaka sitini mingine inayofuata toka sasa! Sijui kama bado utakuwa upo kuyafaidi hayo maendeleo, au vipi mkuu 'BloodofJesus'?
 
Kuna wakati unatamani tuwakabidhi nchi watu wanaoweza kutuletea maendeleo. Sie abaki rais tu kama nembo lakini mambo ya uongozi, utawala na mipango ya maendeleo na utekelezaji wapewe watu wengine, sie tuwalipe kamisheni ya hiyo kazi.

Ukiangalia gharama zinatumika Kwa bunge, viongozi na kuendesha serikali ni mzigo Kwa wananchi na tija haipo kiviile.

Mikopo tutapewa lakini Mara nyingi inaishia kutafunwa na wachache huku deni la taifa likiongezeka.

Nnachokiona Kwa Sasa ninitahidi kustaafu na kuwaachia chochote wanangu. Kupata rais atakaeiletea maendeleo hii nchi na ikabadilika, ni zaidi ya miaka 30 ijayo.
 
Kuna wakati unatamani tuwakabidhi nchi watu wanaoweza kutuletea maendeleo. Sie abaki rais tu kama nembo lakini mambo ya uongozi, utawala na mipango ya maendeleo na utekelezaji wapewe watu wengine, sie tuwalipe kamisheni ya hiyo kazi.

Ukiangalia gharama zinatumika Kwa bunge, viongozi na kuendesha serikali ni mzigo Kwa wananchi na tija haipo kiviile.

Mikopo tutapewa lakini Mara nyingi inaishia kutafunwa na wachache huku deni la taifa likiongezeka.

Nnachokiona Kwa Sasa ninitahidi kustaafu na kuwaachia chochote wanangu. Kupata rais atakaeiletea maendeleo hii nchi na ikabadilika, ni zaidi ya miaka 30 ijayo.
Bora ya Samia mara 100000 kuliko yule sadist wenu aliyekuwa anakopa kimyakimya ...na kuhonga wapinzani wamuunge mkono
 
Tanzania imepata Mkopo kwaajili ya miundombinu na huduma bora kupitia mkopo Jumuiya ya Maendeleo ya Kimataifa (IDA*) wa dola za Kimarekani milioni 278 ulioidhinishwa tarehe 13 Jun 2022 na Benki ya Dunia.

====

Tanzania: Seven Million Urban Residents to Access Improved Infrastructure and Services

WASHINGTON, June 13, 2022—At least seven million residents in Tanzania’s secondary cities will benefit from strengthened urban management and access to better infrastructure and services through a new International Development Association (IDA*) credit of $278 million approved today by the World Bank.

“Tanzanian cities are increasingly at risk of climate change, particularly due to projected changes in rainfall patterns which, when coupled with poor development controls and environmental degradation, will increase flooding,” said Mara Warwick, World Bank Country Director for Tanzania, Malawi, Zambia, and Zimbabwe. “This investment directly responds to these vulnerabilities by including climate change adaptation as a cross-cutting issue in its design. It also supports connectivity and access to markets through road infrastructure, bus stop improvements and public space upgrades to reduce travel times and costs, and safety improvements.”

Tanzania’s urban population is expected to increase from 34% in 2018 to 49% by 2040, with the highest growth rates occurring in the country’s secondary and tertiary cities. “Urban areas are critical for Tanzania’s economy and for poverty reduction, however institutional systems and infrastructure have not kept pace with rapid urbanization,” added Ms. Warwick.

The Tanzania Cities Transforming Infrastructure and Competitiveness project (TACTIC) will address these gaps by providing support to key areas of urban management in participating cities, including municipal finance, urban planning, resilience and green development, improved service delivery, and local economic development in addition to infrastructure investments. Through these activities, TACTIC is expected to directly benefit a total of over seven million people through strengthened urban management performance, and among them five million people through improved basic infrastructure and services. This will include the urban poor and vulnerable population who will benefit from increased access to urban infrastructure, basic services, economic opportunities, and reduced risks from climate impacts. At the national level, the project will also strengthen institutional capacity of central ministries.

“Rapid urbanization and increased population density have contributed to urban sprawl and low-density development in Tanzania’s cities, with poor connectivity between people, industries, and markets. The risk of climate-related disasters also runs high,” said David Mason, World Bank Urban Specialist and Task Team Leader. “TACTIC will contribute to harnessing urbanization to promote economic growth and job creation; strengthening public accountability and financial efficiency in delivering services; and improving the efficiency and attractiveness of public investments to crowd-in private investments.”

TACTIC is coordinating with other projects funded by the government and various development partners including the European Union, the Danish International Development Agency, the Nordic Development Fund, the French Development Agency, the Credit Institute for Reconstruction, the German Corporation for International Development, and the United Nations Human Settlement Program. It has benefited from technical assistance activities funded by the Foreign Commonwealth and Development Office of the United Kingdom.

* The World Bank’s International Development Association (IDA), established in 1960, helps the world’s poorest countries by providing grants and low to zero-interest loans for projects and programs that boost economic growth, reduce poverty, and improve poor people’s lives. IDA is one of the largest sources of assistance for the world’s 74 poorest countries, 39 of which are in Africa. Resources from IDA bring positive change to the 1.3 billion people who live in IDA countries. Since 1960, IDA has provided $458 billion to 114 countries. Annual commitments have averaged about $29 billion over the last three years (FY19-FY21), with about 70 percent going to Africa. Learn more online: IDA.worldbank.org. #IDAworks
sasa tunaenda kushuhudia ujenzi wa bonde la msimbazi ikiwa ni pamoja na ujenzi wa flyover pale jangwani
 
Hata baada ya "Kujitawala" sisi wenyewe, bado tuendelee tu kulaumu mfumo? Haiwezekani tukasema sisi tunataka kufanya mambo tofauti kidogo tuonavyo inafaa sisi wenyewe?

Ninajua jibulako mkuu, usihangaike kunijibu hilo swali nililouliza hapo.

Ngoja nitumie muda kidogo kutumia hoja yako hii, nami kuweka ninachoamini juu ya hali yetu hii tuliyomo.

Binafsi ninaamini lawama hasa inaanzia kwetu sisi wenyewe na viongozi wetu wanaotuongoza katika awamu mbalimbali, na hasa hasa hizi awamu za miaka hii ya karibuni.

Tunashindwa hata kufanya mambo madogo madogo yaliyomo katika uwezo wetu, kubadili hali zetu, na badala yake tunasubiri mikopo kama hii, inayojadiliwa hapa.

Wananchi wengi wanaoishi ndani ya nchi yetu sasa hivi ni zao la uhuru wa nchi yetu, wengi wamesoma shule zilizoanzishwa na sisi wenyewe, lakini zikashindwa kuwapa uwezo wa kutumia akili ya kutumia nyezo zilizo katika uwezo wao kubadili mazingira yao. Hata vyoo vya mashimo, inakuwa ni tatizo kwetu, kweli?

Zahanati na vituo vya afya vimejengwa huko vijijini, lakini hatuna uwezo wa kuvifanya vifanye kazi kwa ufanisi. Hatujiulizi inakuwaje?

Kilimo chetu kwa sehemu kubwa ni kilekile alichotuachia mkoloni! Mkulima ambaye amesoma kwenye shule tulizoziendesha sisi wenyewe, hajabadilika, miaka sitini? Tunasubiri mikopo,kama hii, na inapopopatikana, hatujui inakopitia?
Hapo mwanzo, baada ya uhuru, tulisema kukosa watu wetu wenye elimu na utaalam katika mambo mbalimbali ilikuwa ni kikwazo kwetu.
Watu wakasomeshwa, tena kwa wingi na kwa gharama kubwa. Leo hii sidhani kuna eneo ambalo hatuna watu walilolisomea ndani ya nchi hii, lakini huoni kazi za hawa watu, sana sana itakulazimu uende ndani ya CCM, na utawakuta wamejazana huko, wakifanya yao yanayowafaa wao wenyewe, na siyo kunufaisha taifa.

Viongozi wetu sasa wameamua, kwamba sisi hatuwezi kuleta maendeleo katika nchi hii, kwa hiyo njia sahihi na bora iliyopo, ni kuagiza watu toka nje, waje watuletee maendeleo!

Hakuna kiongozi anayetaka kufanya kazi na wananchi hawa, kuwatia moyo na kuwahimiza wajiletee maendeleo ya kweli. Wananchi nao sasa wanawasikiliza viongozi wao, wakisubiri waletewe maendeleo, huku raslimali za nchi yao zikizolewa kama takataka!

Sasa acha tusubiri maendeleo, miaka sitini mingine inayofuata toka sasa! Sijui kama bado utakuwa upo kuyafaidi hayo maendeleo, au vipi mkuu 'BloodofJesus'?
Mfumo wa elimu yetu umekaa hovyo, haumwandai mtanzania kujitegemea kimaarifa, asipoajiriwa amekwama. Na once anapoajiriwa anawaza kuiba tu yaani kujinufaisha kibinafsi. Mtu anaitwa msomi lakini ni kwa kukariri ideas za hao hao wazungu, najua unajua kuwa huwa tunasoma kufaulu mitihani.

Unaonaje unalima mazao malighafi ambayo huwezi kuitumia. Hadi uwaombe hao hao wazungu wanunue, wasiponunua umekwama. Na wananunua kwa bei wanayokupangia.

Una mali ndani ya ardhi yako madini na vito vya thamani huwezi kuchimba hadi uwaombe hao hao wazungu waje wachimbe!

Unalazimishwa uishi watakavyo ukijidai kujitenga nao wakikupiga "vikwazo" athari zake zinakuwa dhahiri. Kumbuka kilichowatokea nchi ya Zimbabwe kipindi kile cha Mugabe kwenye ishu ya wakulima wa kizungu nchini mwake.

Ukiona tunawakopa, ujue tokea karne nyingi walishajua kuwa tutafika muda ambao lazima tutawakopa tu. "the situation that we are experiencing now is a created one by those people over there"

Nakumbuka wimbo wa mtu mmoja unasema: "the world is not my home"


Jesus is Savior
 
Bora ya Samia mara 100000 kuliko yule sadist wenu aliyekuwa anakopa kimyakimya ...na kuhonga wapinzani wamuunge mkono

Kwanza kabisa jifunze kujikita kwenye hoja acha mambo ya kufikiria unachowaza wewe ndivyo kilivyo, hiyo kauli "sadist wenu" inaingiaje hapa? Unajua mie nipo upande upi?

Tukirudi kwenye hoja, hakuna unafuu wowote. Ndio maana nikasema tungekabidhi tu haya mambo nchi iendeshwe kama kampuni Kwa kuzingatia KPI, tungekua mbali sana.
 
Kukopa kwa mwafrika imekuwa sifa kutwa kutangaza kwenye magazeti

Wenzetu wanaandika maendeleo yao sisi tunajisifia kukopa halafu hatuoni hiyo mikopo imesaidia nini

Deni la Taifa linapaa ila watu bado wanauza maji kwa ndoo mpaka mikoani ambapo leo tungekuwa na mabomba ya maji kila kaya

Miaka ya 70 mitaani kulikuwa na maji ya bure kutoka idara ya maji
Hiyo mikopo wacha waibe tu
 
Kukopa kwa mwafrika imekuwa sifa kutwa kutangaza kwenye magazeti

Wenzetu wanaandika maendeleo yao sisi tunajisifia kukopa halafu hatuoni hiyo mikopo imesaidia nini

Deni la Taifa linapaa ila watu bado wanauza maji kwa ndoo mpaka mikoani ambapo leo tungekuwa na mabomba ya maji kila kaya

Miaka ya 70 mitaani kulikuwa na maji ya bure kutoka idara ya maji
Hiyo mikopo wacha waibe tu
Wewe hapo kwako hata kisima cha laki 2 umechimba?
 
Wachimbaji gani hawana hamu hao?yaani umekaa nyuma ya keyboard unaanza kuharisha....tuna vijana wa hovyo Sana nchi hii
Mkuu, ukweli unauma, inabudi uuzoee!!

Kwenye machimbo huko kuna vilio, wanatimuliwa tuu huko ili waheshi miwa.... Waji milk she wao aisee, huyo mtu anaitwa Ro 1, mtamkoma
 
4 Reactions
Reply
Back
Top Bottom