MIMI BABA YENU
JF-Expert Member
- Mar 1, 2019
- 295
- 679
Wataalamu wa Nguvu za Atomiki kutoka nchi 46 za Afrika wamekutana Arusha kujadili utekelezaji miradi ya matumizi salama ya Sayansi na Teknolojia ya nyuklia katika nchi zao
Ni Mkutano wa kimataifa wa waratibu wa miradi ya Sayansi na Teknolojia ya Nyuklia kutoka nchi 46 wanachama wa Shirika la Kimataifa la Nguvu za Atomiki ( IAEA )
Naibu Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, William Ole Nasha amesema wamekutana kuweka mikakati ya matumizi sahihi ya Atomiki
Nchi za Afrika zimepata manufaa makubwa katika matumizi ya Atomiki hususani Tanzania ambayo imepata Tsh bilioni 9 zinazotekeleza miradi mbalimbali ikiwemo ya ununuzi wa vifaa tiba vya kuchunguza Saratani katika Hospitali ya Ocean Road jijini Dar es Salaam na Bugando jijini Mwanza
Aidha, wanaendelea kupata mafunzo mbalimbali ya jinsi ya kudhibiti mionzi isilete madhara
Pamoja na hayo Serikali ya Tanzania kupitia Tume ya Nguvu za Atomiki Tanzania (TAEC) imefanikiwa kuimarisha usimamizi na udhibiti wa matumizi ya Teknolojia ya Nyuklia nchini.
Hayo yamesemwa na Naibu Waziri wa Elimu, Sayansi na Tekenolojia Mheshimiwa William Ole Nasha wakati wa ufunguzi wa mkutano huo
Ni Mkutano wa kimataifa wa waratibu wa miradi ya Sayansi na Teknolojia ya Nyuklia kutoka nchi 46 wanachama wa Shirika la Kimataifa la Nguvu za Atomiki ( IAEA )
Naibu Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, William Ole Nasha amesema wamekutana kuweka mikakati ya matumizi sahihi ya Atomiki
Nchi za Afrika zimepata manufaa makubwa katika matumizi ya Atomiki hususani Tanzania ambayo imepata Tsh bilioni 9 zinazotekeleza miradi mbalimbali ikiwemo ya ununuzi wa vifaa tiba vya kuchunguza Saratani katika Hospitali ya Ocean Road jijini Dar es Salaam na Bugando jijini Mwanza
Aidha, wanaendelea kupata mafunzo mbalimbali ya jinsi ya kudhibiti mionzi isilete madhara
Pamoja na hayo Serikali ya Tanzania kupitia Tume ya Nguvu za Atomiki Tanzania (TAEC) imefanikiwa kuimarisha usimamizi na udhibiti wa matumizi ya Teknolojia ya Nyuklia nchini.
Hayo yamesemwa na Naibu Waziri wa Elimu, Sayansi na Tekenolojia Mheshimiwa William Ole Nasha wakati wa ufunguzi wa mkutano huo