Synthesizer
JF-Expert Member
- Feb 15, 2010
- 11,143
- 18,774
Juzi hapa kulikuwa na habari katika IPP Media kwamba mwaka 2010 waliandika kuwakandia Wa-Afika Kusini kutuwekea masharti magumu ya visa kwenda bondeni wakati tuliwasaidia sana katika suala la kupigania uhuru wa nchi yao. Baada ya taarifa hiyo ya gazetini, Afrika Kusini walitoa suala la visa, na sasa Watanzania wanaruhusiwa kwenda bondeni bila visa.
Sasa kimbembe ni kwamba, Tanzania imegoma kuwaondolea visa Waafrika kusini kuja Tanzania, kwa kisingizio kwamba wao wanafaidika kuja Tanzania kuliko sisi Watanzania kwenda bondeni. Ukweli ni kwamba serikali ya Tanzania wanajua ubalozi wa Tanzania pale Pretoria bila hela ya visa za Waafrika kusini utakuwa kama mtoto yatima omba omba.
Msishangae Afrika Kusini wakirudisha visa tena kwenda bondeni, kwa msimamo huu wa Tanzania kwa kile kinaitwa "reciprocal arrangement".
Sasa kimbembe ni kwamba, Tanzania imegoma kuwaondolea visa Waafrika kusini kuja Tanzania, kwa kisingizio kwamba wao wanafaidika kuja Tanzania kuliko sisi Watanzania kwenda bondeni. Ukweli ni kwamba serikali ya Tanzania wanajua ubalozi wa Tanzania pale Pretoria bila hela ya visa za Waafrika kusini utakuwa kama mtoto yatima omba omba.
Msishangae Afrika Kusini wakirudisha visa tena kwenda bondeni, kwa msimamo huu wa Tanzania kwa kile kinaitwa "reciprocal arrangement".