Tanzania yafuzu kombe la Dunia mchezo wa soka kwa wenye ulemavu

Roving Journalist

JF Roving Journalist
Apr 18, 2017
2,746
11,876
Na. John Mapepele

Waziri mwenye dhamana ya Michezo nchini. Mhe, Innocent Bashungwa leo Disemba 1, 2021 amewaongoza watanzania kuishangilia Timu ya Tanzania (Tembo Warriors) ambayo imefuzu na kuwa timu ya kwanza miongoni mwa timu nne zinazoingia nusu fainali ya Soka ya Bara la Afrika kwa wenye ulemavu (CANAF 2021) na hivyo kupata tiketi ya kushiriki Mashindano ya Dunia ya mchezo huo yatakayofanyika nchini Uturuki 2022 baada ya kuichapa timu ya Cameroon mabao 5-0.

Timu ya Tanzania ambayo katika kipindi chote cha maandalizi imesimamiwa na Kamati Maalum ya Kitaifa chini ya Katibu Mkuu wa Utamaduni, Sanaa na Michezo, Dkt. Hassani Abbasi ilianza vizuri kutokana hamasa iliyotolewa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Mhe, Samia Suluhu Hasan.

Katika mechi zote za mashindano haya Tanzania imepoteza mechi moja tu ya Uganda mbayo ilifungwa goli 1-0, ambapo Tembo iliifunga timu ya Morocco 2-1 na Sierra Leone ambapo tembo ilishinda goli 1-0.

Akizungumza na Waandishi wa Habari mara baada ya mechi hii, Mhe. Bashungwa amewahakikishia kwamba Serikali itaendelea kuiisaidia timu hiyo ili iendelee kufanya vizuri maandalizi ya Kombe la Dunia.

Aidha, Dkt Abbasi amesema kwa kuwa safari ya kuelekea kombe la dunia imekamilika kazi iliyobaki ni kuhakikisha kuwa kombe linabaki Tanzania.

Magoli mawili ya Tanzania yamefungwa na Alfan Kyanga dakika ya 2 na 15 , Ramadhan Chomole dakika ya 18, na Frank Ngailo dakika ya 36 na 44.

Mchezo huo pia umeshuhudiwa na Rais wa Mashindano hayo duniani Mateus Wildack.

PICHA_0006_8T5A1706.jpg
PICHA_0005_8T5A1700.jpg
PICHA_0003_8T5A1735.jpg
PICHA_0002_8T5A1742.jpg
PICHA_0000_8T5A1757.jpg
8T5A1670_0008_Background.jpg
PICHA_0001_8T5A1743.jpg
8T5A1670_0007_8T5A1669.jpg
8T5A1670_0006_8T5A1653.jpg
8T5A1670_0002_8T5A1684.jpg
8T5A1670_0000_8T5A1677.jpg
8T5A1670_0004_8T5A1655.jpg
8T5A1670_0001_8T5A1661.jpg
8T5A1670_0005_8T5A1657.jpg
 
Hongera sana,
Na tunataraji kuwaona hao hao uturuki sio kutuongezea sijui mtoto wa mjomba au shangazi
Hatutaki aisee hao hao ndio waende uturuki
 
Na. John Mapepele

Waziri mwenye dhamana ya Michezo nchini. Mhe, Innocent Bashungwa leo Disemba 1, 2021 amewaongoza watanzania kuishangilia Timu ya Tanzania (Tembo Warriors) ambayo imefuzu na kuwa timu ya kwanza miongoni mwa timu nne zinazoingia nusu fainali ya Soka ya Bara la Afrika kwa wenye ulemavu (CANAF 2021) na hivyo kupata tiketi ya kushiriki Mashindano ya Dunia ya mchezo huo yatakayofanyika nchini Uturuki 2022 baada ya kuichapa timu ya Cameroon mabao 5-0.

Timu ya Tanzania ambayo katika kipindi chote cha maandalizi imesimamiwa na Kamati Maalum ya Kitaifa chini ya Katibu Mkuu wa Utamaduni, Sanaa na Michezo, Dkt. Hassani Abbasi ilianza vizuri kutokana hamasa iliyotolewa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Mhe, Samia Suluhu Hasan.

Katika mechi zote za mashindano haya Tanzania imepoteza mechi moja tu ya Uganda mbayo ilifungwa goli 1-0, ambapo Tembo iliifunga timu ya Morocco 2-1 na Sierra Leone ambapo tembo ilishinda goli 1-0.

Akizungumza na Waandishi wa Habari mara baada ya mechi hii, Mhe. Bashungwa amewahakikishia kwamba Serikali itaendelea kuiisaidia timu hiyo ili iendelee kufanya vizuri maandalizi ya Kombe la Dunia.

Aidha, Dkt Abbasi amesema kwa kuwa safari ya kuelekea kombe la dunia imekamilika kazi iliyobaki ni kuhakikisha kuwa kombe linabaki Tanzania.

Magoli mawili ya Tanzania yamefungwa na Alfan Kyanga dakika ya 2 na 15 , Ramadhan Chomole dakika ya 18, na Frank Ngailo dakika ya 36 na 44.

Mchezo huo pia umeshuhudiwa na Rais wa Mashindano hayo duniani Mateus Wildack.

View attachment 2029283View attachment 2029284View attachment 2029285View attachment 2029286View attachment 2029287View attachment 2029288View attachment 2029289View attachment 2029290View attachment 2029291View attachment 2029292View attachment 2029293View attachment 2029294View attachment 2029295View attachment 2029296
Kama tayari wanasiasa wameshatia mikono yao tayari walishatiwa najisi hawatashinda tena.

Hata taifa stars ingeweza kufuzu kwenda hatua ya mtoano lakini wanasiasa walipotia mkono wangu nilisema hapa timu itafungwa na Congo.
 
Hongera sana,
Na tunataraji kuwaona hao hao uturuki sio kutuongezea sijui mtoto wa mjomba au shangazi
Hatutaki aisee hao hao ndio waende uturuki
Daaah kweli aiseee, maana hawachelewi hawa viongozi kuongeza watt wa shangaz
 
Halafu wenye uelewa na viungo vyote wanaishia kukimbia ovyo uwanjani wakiogopa injuary wasirudi kwenye vilabu vyao na makovu
Shame on
Natania tuu
 
2 Reactions
Reply
Back
Top Bottom