Tanzania ya sasa ni kama ngombe aliyekatwa kichwa!

Revolutionary

JF-Expert Member
Jan 7, 2011
456
86
Kwa mtazamo wangu tena finyu hiki ndio kipindi ambacho uongozi wa nchi umefeli kabisa.

The president kama kichwa cha nchi can't hold things together! Nabaki najiuliza "what is the president for?"

nchi inaparaganyika into pieces, viongozi wamekuwa ndio wapotoshaji wasiolete umoja na amani na kuelewana baina ya watanzania,...

Viongozi wanafitini, wanapandikiza mipasuko na chuki ndani ya jamii, vongozi ndio wanaovuruga nchi igawanyike vipande vipande kiislamu na kikristu,kitajiri na kimaskini,kielimu na kiumbumbumbu,kitumwa na kibwana,kijamii,kikabila,kisiasa,kimaslahi, kimtazamo na mengine mengi ya kusikitisha.

Kazi ya viongozi ni kufanya watu wa tofauti hizi waweze kukaa pamoja kwa amani na kuheshimiana (kama baba wa taifa alivyoweza kufanya the miracles of times)

kila kona mambo ya kusikitisha yanaendelea, raia wanauawa na askari (zao lake ni chuki), wanafunzi wanagoma huku na kule hadi mkuu wa wilaya anaweka chini ya ulizi wa wanafunzi gari inatolewa upepo! (kweli Tanzania hii hii ninayoijua mimi??) Huku nako raia wanataka makabidhiwe askari aliyeua wadeal nae wenyewe (kwa haraka haraka nafikiri hawana imani na mfumo wa utoaji haki na inasikitisha)

Hawa wanataka nchi iongozwe kidini wale wanakwiba nchi! Tunalipishwa madeni kama ya dowans wananchi hatuelewi nini kinaendelea! Na kadhalika na kadhalika.


Kinachoendelea ni fitna tupu, kinyume kabisa na maana na kazi ya kiongozi ya uongozi!.

Nchi inakosa mwelekeo kabisa, shetani anafanye kazi yake kweli.

Tanzania ya sasa ni kama ngombe aliyekatwa kichwa!
 
Wewe, can't you see that we are in a vibrant, truely democratic and transparent african world and our leaders are acting in the best interest of every one?, both in the east and in the west, in the south and in the north, who cherishes freedom, justice and human dignity? Kingómbe n'gome ndo vibrant, and true democracy. teh teh :thinking:
 
Ujakosea kabisaa! yaani ulichonena ni ukweli mtupu!.
CCM na mtandao wake wako tayari kuivuruga nchi hii
kulikowao kuachia madaraka. yaani hawana akili kabisa.
Kila kukicha wanahibua mapropaganda ya kuigawa nchi.
Ila oneday yes na yote yatakwisha kwa rekhema za mungu!
 
Ulichosema ni sahihi kabisa, kama ng'ombe hana kichwa unategemea nini? haoni aendako, akili haipo ............ ni kweli hata sijui tunakoelekea, tunasubiri kujibamiza sehemu, na matokeo yake sijui yatakuwaje. Tuombe Mungu atunusuru na hali hii, pamoja na hivyo inabidi tutafute jinsi ya kuondokana na hali hii kwa maana Mungu umsaidia anayejisaidia. Watanzania tuamke.
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom