Getang'wan
JF-Expert Member
- Apr 9, 2015
- 3,075
- 3,413
Paragraph ya mwisho ni nzito sanatumuombe mwenyezi Mungu ampe hekima na busara mama yetu atuongoza kwa haki..
Mama akichukua mazuri ya JK na mazuri ya JPM akatuongoza basi nchi itapiga hatua haraka.. JK alikuwa na akili na mtazamo wa dunia ya sasa inavyotaka kufikia kwenye maendeleo, JPM alikuwa ni msimamizi na muangalizi mzuri kwenye rasimali na utendaji.. Mama akichukua vyote akavitumia kama silaha tutakwenda mbele...
Tatizo la CCM ni makundi, haya makundi ndio yanaweza kuwa kikwazo kwa mama, makundi yameota mizizi mpaka taasisi nyeti na kila kukicha yanaibuka makundi mapya..Ni wakati sasa wa viongozi wa haya makundi kuweka maslahi ya Taifa mbele na kuachana na minyukano yao...