Tanzania Vision 2025 vs Kenya Vision 2030: Mizengo Pinda upo?



john-komba.jpg

Ingekuwa ni kenya huyu mbunge asingechaguliwa tena na wananchi wake
 
Last edited by a moderator:
hani tuna kila sababu ya kujilinganisha na Kenya.... kutetea vision iliyo blind ni kujipofua permanently
 
ndugu yangu wewe ita vyovyote vile plan mchakato mipango ,,lakini kinachotakiwa ni uhalisia nikupe mfano watalii asilimia kubwa wanatua kenya wanatalii kwanza halafu ndio wanaingia tz angalia idadi ya ndege toka duniani ni ngapi kwa siku halafu linganisha na jk air port ,,angalia mauwa yote ya arusha na moshi yana pitia nrb kwenda ulaya..
Wamenunua ndege ya kubebe tani 120 inasafiri zaidi ya mara tatu kwenda ulaya kupeleka mauwa tu...viwanja vipya international kisumu taveta na kule tarakea vyote hivyo wametubana sisi tumelala..bandari wanapanua mombasa na lam wanajenga kubwa wao wanabenki na shoping mall huku kwetu sisi hatuna hata blue band zinatoka kwao mimi huwa napenda kwenda mombasa likizo huduma na mandhari ni nzuri kuliko kwetu si zungumzii ushabiki ni uhalisia

mkuu sio hivyo tu kenya waka mbali mfano kwa siku ndege zinazotoka kenya kwenda dubai ni nne sisi tuna moja tu ambayo ni emirates na wala haijai
 
Watanzania hawana sababu ya kujilinganisha na masikini, ukifikia lengo la kuona upeo wako ni Kenya basi ujue umefilisika kwa kila hali. Watanzania wapo katika level nyingine na katu hawawezi kujilinganisha na manyang'au. Tunajaribu kuwafikia wale walio kwenye the real 21st century.


Nadhani sii vyema kuwaita majina ya ajabu bila sababu za msingi.
Wakenya wataendelea kuwa juu coz huwa wanatafakari mambo kwa kina kabla ya maamuzi.
Wakenya hawakukimbilia siasa za ujamaa kwakuwa hawkuona future ktk hiyo, sisi tulikurupuka tumeshindwa then twawaona wao ndo wachawi.

Hebu tafakari hivi wajuwa hadi sasa bado soko kubwa la Tanzanite lipo kenya.........si tunaipeleka wenyewe? serikali imeshndwa kuwekeza mitaji ktk mashine za kukatia madini hayo hapa nchini..................

Hebu tafakari hadi sasa mtalii anayekuja kupanda ml Knjaro sehemu kubwa kabisa ya fedha ya matumizi yake inabaki kenya.........hilo linafahamika miaka nenda rudi................je ni tatizo la wakenya?

Acha matusi acha uvivu wa kufikiri..............................jamaa wapo juu na watakuwa hvyo kwa miaka mingi ijayo kwani kwa siasa zetu tumelelewa kidhaifu sana na tumepumbazwa....na kubaki walalamikaji tuuuuuuuuuuuuuuuuuuuu..
 
MUNGU yupo ndio final say ju mstakabari wa tanzania mungu wetu ndio ataamua hatma ya ccm kuwepo madarakani, mimi nipo ngorongoro viongozi wanaiba mali kila kukicha huyo ndugai ni fisadi wa kutisha na cheo chake cha makamo mwenyekiti wa bodi ya mamlaka ya ngorongoro asilima kubwa wakazi wa ngorongoro na vitongoji vyake wanategeme vyakura kutoka kenya Naroku tuwekwisha Tufanye mabadiliko watanzania bila woga C CM itatuzika ilipotufikisha imetosha ndugu zangu naandika nikiwa na machungu kuona leo hii 4bilion kwenye mfuko binafsi. Sijajua huyu kagashek kaja huku kutafuta nini ama kuchukua bahasha yake kwa mwalabu kule loliondo gate.
 
Hapo kuna vitu viwili tofauti:
1.Vision
2.Plan na programu

Kenya wamejaribu kutoa kwa ufupi plan yao kulingana na vision, lakini Tanzania wametoa doc yenye vision kwa ujumla lakini malengo kama hayo utayapata kwenye national plan na development programu ambazo wizara mbalimbali zilikuwa zinaandaa, sina uhakika zimefikia wapi ila ya miaka mitano mitano utaipata ambazo zinatekeleza hiyo vision.

Hata hivyo, kuna vitu ambazo nchi kama nchi imeshaanza kutekeleza kama suala la special economic zone, miji ya kitalii na kibiashara ipo kwenye plan labda utekelezaji tu unatakiwa kuanza.

Hiyo doc ni jinsi ya kuiwasilisha tu. Inaaminika vitu vingi wabongo tunavianzisha katika maandishi na vinakubalika sana na wenzetu wajanja wanakopy na kuanza kuvifanyia kazi. Hivyo, basi hakuna jipya ambalo wakenya wameliandika hapo ambalo halipo katika plan na development programme zetu.


mkukuta na five years development plans ambazo zote ni porojo tu....
 
hani tuna kila sababu ya kujilinganisha na Kenya.... kutetea vision iliyo blind ni kujipofua permanently



iyo vision 2025 yenyewe ya tanzania haina jipya....kila kitu kilikuwa kwenye arusha declaration, tena azimio la arusha lilifanyanya poa kuliko ata iyo vision ya wa-magharibi
 
Ya tanzania iko very generic na inaonekana imeandikwa na mtoto wa darasa la 5


Says alot about haya matatizo tuliyonayo

na mbaya zaidi hatupendi self criticisms mfano ni namna tunavyojadili na kupanga hoja zetu
 
mimi nimeingia Kenya mara nyingi sana tukifanya ulinganifu angalau kwa kulisha macho :cool2::cool2: utagundua kwetu maneno ni mengi kuliko utendaji,Kwa rasilimali tunawazidi ila ukiangalia mikataba ya kichina tuliyowekea saini na Wachina basi,utaona ni kazi kweli kweli kuwafikia Wakenya,Otherwise TZ tunahitaji kiongozi Dikteta mwenye kuzitumia Rasilimali ipasavyo kuleta maendeleo kwa UMMA hapo Majirani zetu watatuheshimu.:hail::hail:
 
Kenya walijua hawana rasilimali nyingi hivyo wakaamua kufañya kazi kwa nguvu na akili kubwa
Mtaji wa masikini ni nguvu Zake
 
Back
Top Bottom