Tanzania tunawezaje/tufanye nini ili kufaidika na ukuaji wa uchumi wa China?

Red Giant

JF-Expert Member
Mar 9, 2012
15,658
20,889
Ni hao wakuu. Wandugu uchumi wa China na ukuaji wake ni jambo la kuogopesha sana kwa ukubwa wake. Miaka michache ijayo China itaongoza kiuchumi karibu kwenye kila sekta. Kwa huo uchumi mkubwa China amekuwa mtumiaji mkubwa wa malighafi duniani . Pia ukuwaji huo umetengeneza mamilioni ya matajiri wenye njaa ya kutumia. Kwahiyo China ni mtumiaji mkubwa sana wa malighafi na anaenda kuwa mtumiaji mkubwa wa consumer goods. Iliwabidi Mercedes wajenge kiwanda China baada ya kuzidiwa na mahitaji.

Zamani uchumi wa China ulishikwa na makampuni ya serikali lakini leo zaidi ya 60% ya uchumi unashikwa na sekta binafsi. Makampuni mengi binafsi ya China hayajawekeza nje ya China. Makampuni ya serikali ndiyo yametoka kuwekeza kwenye malighafi. Ndani ya China kuna competition ya hatarl. Kwa kila kampuni moja inayofanikiwa basi kuna maelfu yamekufa. Kwahiyo haya makampuni yana njaa sana ya kuwekeza nje maana licha ya competition pia mishahara inapanda kwa kasi. Mampuni mengi yameanza kuoperate Vietnam na Indonesia. Kuja Afrika CEO mmoja alisema miundombinu(Barabara, bandari, umeme) ni mibovu na kuwa tuna poor work ethics.

Tufanye nini ili tufaidike na soko la mamilioni ya matajiri wa China? Tufanye nini tufaidike na makampuni ya China yenye njaa ya kuoperate nje ya China?
Tufanye nini kufaidika na ukuaji wa uchumi wa China?
 
Ni hao wakuu. Wandugu uchumi wa China na ukuaji wake ni jambo la kuogopesha sana kwa ukubwa wake. Miaka michache ijayo China itaongoza kiuchumi karibu kwenye kila sekta. Kwa huo uchumi mkubwa China amekuwa mtumiaji mkubwa wa malighafi duniani . Pia ukuwaji huo umetengeneza mamilioni ya matajiri wenye njaa ya kutumia. Kwahiyo China ni mtumiaji mkubwa sana wa malighafi na anaenda kuwa mtumiaji mkubwa wa consumer goods. Iliwabidi Mercedes wajenge kiwanda China baada ya kuzidiwa na mahitaji.

Zamani uchumi wa China ulishikwa na makampuni ya serikali
lakini leo zaidi ya 60% ya uchumi unashikwa na sekta binafsi. Makampuni mengi binafsi ya China hayajawekeza nje ya China. Makampuni ya serikali ndiyo yametoka kuwekeza kwenye malighafi. Ndani ya China kuna competition ya hatarl. Kwa kila kampuni moja inayofanikiwa basi kuna maelfu yamekufa. Kwahiyo haya makampuni yana njaa sana ya kuwekeza nje maana licha ya competition pia mishahara inapanda kwa kasi. Mampuni mengi yameanza kuoperate Vietnam na Indonesia. Kuja Afrika CEO mmoja alisema miundombinu(Barabara, bandari, umeme) ni mibovu na kuwa tuna poor work ethics.

Tufanye nini ili tufaidike na soko la mamilioni ya matajiri wa China? Tufanye nini tufaidike na makampuni ya China yenye njaa ya kuoperate nje ya China?
Tufanye nini kufaidika na ukuaji wa uchumi wa China?

Hapo penye boldi ndipo penye siri ya mafanikio ya China. Wanaimba Kijamaa, Wanacheza Kibepari. Labda ndipo pa kuwaiga.

Soko la China? Naomba kufahamishwa bidhaa tatu tu za Tanzania ambazo zimekosa soko la ndani, na ambalo soko la China likipatikana litakuwa ni ufumbuzi.
 
Hapo penye boldi ndipo penye siri ya mafanikio ya China. Wanaimba Kijamaa, Wanacheza Kibepari. Labda ndipo pa kuwaiga.

Soko la China? Naomba kufahamishwa bidhaa tatu tu za Tanzania ambazo zimekosa soko la ndani, na ambalo soko la China likipatikana litakuwa ni ufumbuzi.
Bidhaa ni nyingi sana mkuu. Tuanze na utalii leo tunapata wateja 1.2m na lengo letu tufike 10m. Wachina leo wana helaa na wanasafiri sana kutalii. Mfano tungekuwa na hoteli za 'kichina'tungeongeza sana wateja.
Kuna kahawa, watanzania wengi hatumudu kunywa kahawa, hata wachina zamani hawakumudu lakini leo ni wanwaji wakubwa. Tungekaanga na kuwauzia. Pia watanzania wengi hatuwezi mudu viatu vipya vya ngozi lakini tuna ngozi kibao. Tutengeneze tuwauzie wachina. List ni ndefu na uzuri hwa wachina hawajali sana brand kama wamagharibi.
 
Back
Top Bottom