Tanzania tunamuhitaji Rais wa aina gani 2025?

Ali Mafuruki ana uzoefu gani kwenye siasa mpaka sasa? maana kuwa rais sio kujua biashara tu.. huyo Cyril ni mfanyabiashara lakini alikuwa kwenye siasa tangia kitambo sana
 
Habarini za Asubuhi wanabodi..

Uzi huu niuandika baada ya kusikiliza kupindi cha Straight Talk Afrika cha Shaka. Jana walikuwa wanaongelea siasa za Afrika Kusini na Cyril Ramaphosa. Binafsi sikuwa namjua Cyril vizuri mpaka alipokwaa madaraka kutoka kwa Zuma. Hapo ndipo nilishawishika kutafuta na kuusoma wasifu wake. Ukiacha mengine mengi, he is a purely businessman.

Tanzania tuna mipango na matazamio mengi mbeleni, tunaitaka Tanzania ya viwanda na ifikapo 2025 tunatazamiwa kuwa nchi yenye uchumi wa kati (Second world country).

Binafsi siamini kama hawa walioko madarakani sasahivi watatufikisha kwenye hata moja kati ya hayo mawili. Kufika huko hatuhitaji kauli za kibabe, sera zisizoeleweka za kuwakandamiza wawekezaji, kujifungia ndani tukiwasubiri mpaka wao waje.

Serikali yetu ya sasa labda inafanya mazuri kwenye baadhi ya mambo ambayo kiukweli ni machache na yanahesabika. Serikali ya sasa imejaa wanataaluma ambao kiukweli hawana background yeyote kiuongozi hasahasa kibiashara zaidi ya kuwa wakufunzi tu.

Mambo mengi yanakwama, viwanda tulivyohaidiwa hatuvioni vinavyofunguliwa vingi kama sio vyote vilikuwa initiated wakati wa Kikwete, wakati huo ilikuwa rahisi kushawishi wawekezaji sababu purchasing power ilikuwepo, hali ya fedha kwenye mzunguko ilikuwa nzuri. Ila sasa, ni wenyewe tu ndio wanajua wanachofanya.

Tukirudi kwenye mada kuu, Je, kwa hapa tulipo na huu mkwamo tunaoupitia bila shaka kwanza tunahitaji Rais msomi lakini pia Rais ambaye amebobea kwenye masuala ya kibiashara.

Hapa haraka lilinijia jina la ALI MAFURUKI. Kwa kiasi kikubwa naona Mtanzania huyu anaweza kutupeleka kule tunakotaka kwenda. Huyu amekulia kwenye buashara na anajua biashara haitaki ubabe, biashara yeyote duniani inataka NEGOTIATIONS, biashara haitaki two faced people. Kwamba leo tunaongea hiki alafu kesho tunageuka.

Kwa mtizamo wako; nani unaona atafaa kuwa mrithi wa JPM?
Mbona unaongelea 2025 wakati Kuna Uchaguzi 2020???
 
Salama!
Watanzania waulize hawapendi nini, hapo utapata majibu hata page 30 lakini ukiwauliza wanapenda nini hautakaa upate majibu yaliyosahihi.

Ni kama wewe mwandishi ulivyosema hapo kwamba tumejifungia ndani kusubiri wawekezaji waje badala ya kuwafwata huko waliko. Miaka mitano nyuma ninyi wenyewe mlikuwa mnalalamika hapa kwamba rais kikwete anasafiri sana mara oh hatulii nyumbani mpaka kumbatiza majina ya ajabu mzee yule.

Leo hii tunakiongozi ambaye anafanya mnayoyataka ninyi watanzania lakini bado mnalalama kwamba rais anajifungia ndani hatafuti wawekezaji. Ndugu ukiwa na mali yako unaiuza mteja hawezi kukupangia bei na majira ya kuiuza hiyo mali. kama utaruhusu mteja apange bei na majira ya kununua hiyo mali yako basi andika umeumia na maumivu yake hautayaona leo ila baadae sana.

Maendeleo tuliokuwa tunayalilia kila siku yana gharama yake mkuu, maendeleo hayaji kama ghafla bin vuu. Ili tufikie hayo maendeleo ni lazima tutoke jasho, tule sana mboga za majani, tushone viraka vya kutosha ili kufikia dhumuni kuu ambalo ni maendeleo. Viwanda vingi sana vinajengwa mkoa wa pwani hasa bagamoyo na kwingineko, tembea uone nchi inavyobadirika. Huwezi kuona mabadiriko ya nchi ukiwa umekaa sehemu moja, waulize ambao wako pembezoni mwa nchi watakwambia Tanzania wanaionaje?.

Hii purchasing power unayoizungumzia hapa mkuu ni ipi? ni purchasing power kwa serikali au kwa raia? kama ni kwa raia , ndiyo raia tulikuwa na pesa nyingi sana mikononi ambazo hazikuwa zetu, tulikuwa na pesa chafu kwenye mzunguko na ndiyo maana tulikuwa tunaishi maisha ya "ibiza" ndani ya Tanzania.

Huyu rais tuliye naye anania na dhamira ya kweli na taifa hili tumuunge mkono na siyo kumbeza. Maendeleo ni gharama na ili ufike ni sharti ulipie

Shukrani!

Umuunge mkono mtu asiekua na vision?
 
Samahani sana naona uko kichama zaidi, mimi siyo mwanapropaganda hivyo usiwe na jazba tujadili maslahi ya nchi.
tulikokuwa tumefikia tulimhitaji sana mtu wa namna hii.
Kipi kikubwa alichokifanya? Au tumpe muda?

Binafsi ninampongeza kwenye miundombinu pekee.. Mpaka 2025 nadhani tutakuwa na barabara nzuri za rami kila kijiji.. Lakini kwa mengine mengi anafeli, hatuwezi kufikia nchi ya uchumi wa kati kwa idadi ya barabara tu.. Kuna mengi ya kufanya
 
Kwanza sio 2025 ni 2027,pili kuna kila dalili mzee baba akabakia ulingoni hiyo 2027 kuelekea 2034

Ni vyema mkafikiria mtakabiliana vp na hii hali kama hamtakubaliana nayo na hivi ndo mambo yalivyo wala msijaribu kutumia njia nyepesi ya kutatua tatizo kwa ku assume ya kwamba halipo....
Mkuu achana na story za vijiweni.. hata JK alishutumiwa kutaka kujiongezea muda. Hilo haliwezekani nchini kwetu
 
Mkuu achana na story za vijiweni.. hata JK alishutumiwa kutaka kujiongezea muda. Hilo haliwezekani nchini kwetu
Tangu lini kijana wa kitanzani akawa na utamaduni wa kujadili mambo kama haya vijiweni??
Hakuna kijiwe chenye upeo wa kujua na kupambanua hayo mambo siku hizi ,vijiwe vyote siku hizi vimejaa story za Diamond na Zari,Kusaga na Ruge,Gigy money na mimba,shilole na Uchebe,Okwi na Boko na story zingine zinazohusu ugumu wa maisha

....just jaribu kusoma vitabu then soma system ya uongozi ya huu utawala utagundua hilo jambo haliepukiki ndugu,watz wengi hawaamini hilo kama linaweza tokea ni kwasababu tu wana vichwa vigumu kuusoma mchezo..
 
Kwahiyo pesa chafu imeondoka? Kama imeondoka na serikali inalijua hilo imepima impact yake? Wamefanya nini kuongeza mzunguko wa pesa mtaani? Hiyo pesa chafu ilikuwa pia inafanya biashara na serikali inapata kodi yake. Baada ya kuiondoa biashara ikoje? Wananchi wanakopesheka? Mabenki yamestahimili hicho kishindo?

Mwenye nia ya dhati anaua, anakandamiza wengine? Asikilizi ushauri, ana pesa za kununua wapinzani na kurudia chaguzi ila za kuwalipa wastaafu hana? Huyo ndiye mwenye nia ya dhati?

Viwanda unavyoongelea vya Pwani vilianza kujengwa tangia awamu ya JK. Yeye kaleta kiwanda gani cha maana?
Unaongea usichokijua.
Kuna kampuni nazijua hazikufanya ukaguzi wa hesabu(Auditing) kwa zaidi ya miaka miwili kinyume na sheria zinavyotaka.

Na zilikuwa hazipeleki hesabu za marejesho ya kodi ya ongezeko la thamani au VAT. ( I mean they did not file VAT returns) na kuzituma TRA.

Zilikuwa zinasuasua kulipa Corporate Tax za limited companies.

Kilichokuwa kinafanyika ni kuwapoza tu wafanyakazi wa TRA kitu kidogo kama milioni 3 au 4 kwa kuchelewesha au kutowachukulua kabisa hatua kutikana na kidi wanazodaiwa zinazoanzia milioni 150.

Jiulize hapo serikali inapoteza 150M kwa ajili ya mtumishi wake anavuta 5M na kisha analipwa stahiki zake kibao zinazofikia 4M au zaidi ni faida hiyo kwa taifa?

Hizo 145M anazobakiwa nazo mfanyabiashara ndio ulikuwa unaona vurugu huku mitaani na maendeleo kwa taifa kama miundombinu na madawa au elimu bora hakuna kwa hao masikini(walaji) ambao wametozwa kodi.

Bank kama CRDB zilikuwa jeuri hazikopeshi watu wa chini. Zinakopesha taasisi kubwa na matajiri ili maafisa wa bank wanaowezesha mkopo upite wapate 10% yao. Mwisho wa siku mikopo halipiki kwa wakati na kupelekea majanga kama ya bank ya wanawake.
Ilikuwa deal kutajatisha fedha za serikali. Sasa waone CRDB wapo kwenye list yenye hali tete wakati hawa walisifiwa sana. Lakini NMB iliyokumbatia wanyonge hadi sasa hawajayumba sana labda pesa za mikopo ya waliotumbuliwa vyeti feki ndio zitawasumbua kidogo.

Ule mfumo Kikwetwe ulikuwa unatajirisha wachache na kuifilisi nchi. Ni uchumi bandia ulikuwa unafaida kwa nchi za magharibi na China waliojipenyeza kwetu.

Mkuu hayo madudu machache nasema kitu nilichokishuhudia kwenye corporate business companies. Na bado nipo nashuhudia huku mitaani wanavyoshindwa sasa kujiendesha na kudhibiti nidhamu yao ya matumizi huku wakilipa madeni ya nyuma.

Hali mbaya ya sasa kifedha huku mtaani sio kosa la Magufuli bali ni la watangulizi wake na yeye anapojaribu kutuepusha yasitukute ya Cyprus, Ugiriki na kwingineko tunamrushia lawama za bure.
 
Kipi kikubwa alichokifanya? Au tumpe muda?

Binafsi ninampongeza kwenye miundombinu pekee.. Mpaka 2025 nadhani tutakuwa na barabara nzuri za rami kila kijiji.. Lakini kwa mengine mengi anafeli, hatuwezi kufikia nchi ya uchumi wa kati kwa idadi ya barabara tu.. Kuna mengi ya kufanya

Mi naamini kila mtu huwa na Malengo yake, kwa wiki, mwezi na mwaka. Na katika hayo malengo yake kuna yenye kipaumbele zaidi.
Ili tuweze kuwa na uchumi wa viwanda nilazima tuwe na nishati ya umeme ya uhakika ( rejea hotuba ya Obama ubungo) nadhani unajua nini kinaendelea kuhusu hili la umeme, kuna mradi unaitwa Rufiji Hydro Power Plant (RHPP).

Miundo mbinu kama ulivyosifia hapo juu nadhani sina haja ya kulizungumzia hilo.

Naomba tuwe na subira na kumwamini, kuna mambo mazuri naamini atafanya na yataacha alama kwenye jamii ya kitanzania ambayo kizazi kijacho kitajivunia mara baada ya sisi (kucheck out.)

Dhana ya upinzani siyo kukosoa kila jambo ambalo serikali inafanya au kusonya mbele ya camera HAPANA.

Kwa navyofahamu upinzani ni kuipa serikali changamoto kwa hoja zilizoshiba, kuishauri serikali kwenye maamuzi yake ndani ya bunge na si kuitisha maandamano yasiyokuwa na tija kwa umma.

Ukiwa Mtanzania jisikie furaha na kujisifu kwenye kadamnasi kuwa na rais jembe na mpambanaji kama JPM.
 
kila nikikaa na kufikiria kuwa kuna namna ya mkulu kudumu kwenye kiti,mwili unakufa ganzi kabisa,kiukweli graduates tulioanza maisha enzi za huu utawala,tunakwama saana.
 
Umuunge mkono mtu asiekua na vision?

Mtu asiyekuwa na vision ni marehemu tu, ila binadamu yeyeto ana vision. Watanzania sijui tunakula vyakula gani siku hizi mpaka tunasahau haraka kiasi hiki!

Ndugu rejea ufunguzi wa kampeini za ccm pale jangwani 2015, nenda YouTube tizama na sikiliza.
 
Mtu asiyekuwa na vision ni marehemu tu, ila binadamu yeyeto ana vision. Watanzania sijui tunakula vyakula gani siku hizi mpaka tunasahau haraka kiasi hiki!

Ndugu rejea ufunguzi wa kampeini za ccm pale jangwani 2015, nenda YouTube tizama na sikiliza.

Zile ni porojo zisizokua na mbele wala nyuma, hauwezi kusikiliza maneno ya mtu anaeomba kura ukayatilia maanani.
 
Zile ni porojo zisizokua na mbele wala nyuma, hauwezi kusikiliza maneno ya mtu anaeomba kura ukayatilia maanani.

Porojo ambazo huwa hazitiliwi maanani ni zile zitolewazo mtu akiwa juu ya kifua.

Awamu hii ya tano ina dhamira ya kweli na wakwamishaji nadhani unaona wanachofanywa. Tuunge juhudi za mhe Rais na sikubeza kila kitu.
 
Porojo ambazo huwa hazitiliwi maanani ni zile zitolewazo mtu akiwa juu ya kifua.

Awamu hii ya tano ina dhamira ya kweli na wakwamishaji nadhani unaona wanachofanywa. Tuunge juhudi za mhe Rais na sikubeza kila kitu.

Nimuunge kwa lipi la maana alikofanya mpaka sasa?
 
Tangu lini kijana wa kitanzani akawa na utamaduni wa kujadili mambo kama haya vijiweni??
Hakuna kijiwe chenye upeo wa kujua na kupambanua hayo mambo siku hizi ,vijiwe vyote siku hizi vimejaa story za Diamond na Zari,Kusaga na Ruge,Gigy money na mimba,shilole na Uchebe,Okwi na Boko na story zingine zinazohusu ugumu wa maisha

....just jaribu kusoma vitabu then soma system ya uongozi ya huu utawala utagundua hilo jambo haliepukiki ndugu,watz wengi hawaamini hilo kama linaweza tokea ni kwasababu tu wana vichwa vigumu kuusoma mchezo..
Wewe umeuona mchezo unaoendelea na umeuelewa vizuri. Huu utaratibu wa kuwanunua wabunge wa upinzani unanionyesha kuna lengo kubwa kabisa mbele. Hii ni njama kubwa dhidi ya watanzania, wanatafuta mbili ya tatu ya wabunge wa bara ili wabadilishe katiba na kuweka kipengele cha kubadilisha mhula wa utawala. Kama rais atatusamehe, ataongezea kipindi kiwe miaka 7 kama Mhe. Juma Nkamia alivyotaka. Na watataka hiki kipindi cha miaka mitano kisihesabike. Kama hili litafaulu inawezekana utawala wa sasa kutawala miaka 19, hadi 20134.
 
Habarini za Asubuhi wanabodi..

Uzi huu niuandika baada ya kusikiliza kupindi cha Straight Talk Afrika cha Shaka. Jana walikuwa wanaongelea siasa za Afrika Kusini na Cyril Ramaphosa. Binafsi sikuwa namjua Cyril vizuri mpaka alipokwaa madaraka kutoka kwa Zuma. Hapo ndipo nilishawishika kutafuta na kuusoma wasifu wake. Ukiacha mengine mengi, he is a purely businessman.

Tanzania tuna mipango na matazamio mengi mbeleni, tunaitaka Tanzania ya viwanda na ifikapo 2025 tunatazamiwa kuwa nchi yenye uchumi wa kati (Second world country).

Binafsi siamini kama hawa walioko madarakani sasahivi watatufikisha kwenye hata moja kati ya hayo mawili. Kufika huko hatuhitaji kauli za kibabe, sera zisizoeleweka za kuwakandamiza wawekezaji, kujifungia ndani tukiwasubiri mpaka wao waje.

Serikali yetu ya sasa labda inafanya mazuri kwenye baadhi ya mambo ambayo kiukweli ni machache na yanahesabika. Serikali ya sasa imejaa wanataaluma ambao kiukweli hawana background yeyote kiuongozi hasahasa kibiashara zaidi ya kuwa wakufunzi tu.

Mambo mengi yanakwama, viwanda tulivyohaidiwa hatuvioni vinavyofunguliwa vingi kama sio vyote vilikuwa initiated wakati wa Kikwete, wakati huo ilikuwa rahisi kushawishi wawekezaji sababu purchasing power ilikuwepo, hali ya fedha kwenye mzunguko ilikuwa nzuri. Ila sasa, ni wenyewe tu ndio wanajua wanachofanya.

Tukirudi kwenye mada kuu, Je, kwa hapa tulipo na huu mkwamo tunaoupitia bila shaka kwanza tunahitaji Rais msomi lakini pia Rais ambaye amebobea kwenye masuala ya kibiashara.

Hapa haraka lilinijia jina la ALI MAFURUKI. Kwa kiasi kikubwa naona Mtanzania huyu anaweza kutupeleka kule tunakotaka kwenda. Huyu amekulia kwenye buashara na anajua biashara haitaki ubabe, biashara yeyote duniani inataka NEGOTIATIONS, biashara haitaki two faced people. Kwamba leo tunaongea hiki alafu kesho tunageuka.

Kwa mtizamo wako; nani unaona atafaa kuwa mrithi wa JPM?
Kiongozi wa Taifa tunayemtaka antakiwa kuwa na uwezo mkubwa kabisa kwa nyanja mbalimbali, sio biashara tu, sio ukali tu, sio uaminifu tu. Mambo mengi, yanahitajika, lakini jambo kubwa kabisa anatakiwa mtiifu kwa katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
 
1.Rais ambayo atakubali kupitishwa kwa Katiba mpya.
2.ambaye askari wa jeshi lake hawatapiga risasi ya plastiki juu hewani ikarudi chini ikakata kona ikaingia kwenye gari na kuua mtu.
3.ambaye Atafanya matajiri waishi kama malaika na masikini wawe matajiri
4.ambaye ataifanya kuwa nchi ya uchunguzi umekamilika kutoka katika nchi ya uchunguzi bado unaendelea.
5.atayekubali kukosolewa kama kikwete, ukimsema sana anakuita ikulu.
6.atakaye pandisha thamani ya sarafu yetu kama mkapa
7.atayeruhusu watu kufanya siasa na biashara kisheria kama mwinyi
8.atakayepambana na madawa ya kulevya kama magufuli.
 
3 Reactions
Reply
Back
Top Bottom