Tanzania, Tunaenda wapi jamani?

Hizi ndo sifa zilizitawala Tanzania yetu
  1. Viongozi ni wezi sana kupita maelezo, kila mtu anaiba kutokana na nafasi yake
  2. Viongozi ni wababe sana na wanajichukulia sheria mikononi wanavyotaka,
  3. Hajira Hakuna, na kila kukicha zilizokuwepo zinatoweka
  4. wanaotafuta Riziki mitaani wanapigwa tu na migambo bila kujali kuwa hakuna njia ya kupata pesa ya kujikimu.
  5. Mwizi ni yule anayeiba maembe kariakoo, na anayeiba kwa kutumia bunduki, ila wanaoiba kwa kuwasomesha viongozi juu, na kuingia mikataba mibovu sio wezi hao,
  6. Uraisi umekuwa ni mahala pa kutajirikia baada ya kuwasaidia wananchi na kunyanyua maisha

Na mengineyo mengi, sasa ebu tuangalie hapa tunaenda wapi


Tanzania tunaelekea walikoelekea wananchi wote katika nchi nyingine za Afrika - A failed state - kwa sababu waafrika ndivyo tulivyo kila sehemu kuanzia Jamaica hadi lesotho!
 
Tunafanya nini kulinusuru Taifa letu, maana sisi hapa JF tunaifanya kazi kweli kweli, lakini bado about 80% ya watanzania hawana access na JF
Tua strategy please za kuwafikia wadanganyika na kuwaondoa kwenye wimbi hilo

BabaH,

JF inapitisha habari ambazo magazeti ya nyumbani yanaziona moto kuziandika haraka. Zikishapozwa makali kidogo - magazeti yanachukua na kuzifikisha kwa wananchi - multiplier effect inakuja na hatimaye hiyo asilimia 80 itafikiwa one of these days
 
Mpendwa,asilimia ya watu wanaojua nini kinaendelea ktk taifa letu ni sawa na asilimia ya watanzania wanaopata huduma ya umeme,sembuse kazi nzuri ya JF? 99% ya Watz hawajui.Shimo tutakaloingia ni kubwa na refu sana.Fikiria mpaka mjumbe wa shina anagombea ili ale 10% ya viwanja vya uswahilini,hagongi mhuri wa serikali ya mtaa mpaka kitu kidogo. Nina imani thabiti kuwa mapinduzi yaja ambayo yatageuza kila jiwe.
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom