Pascal Mayalla
Platinum Member
- Sep 22, 2008
- 50,441
- 113,450
Wanabodi,
wale wenye access angalieni Star TV, kipindi cha Jicho Letu Ndani ya Habari kinachorushwa live na Star TV, kila siku za Jumamosi asubuhi, leo Mtangazaji Mahiri, Leonard Mapuli yuko na Mkurugenzi Mtendaji wa Umoja wa Press Clubs, UTPC, Aboubakar Karsan, anamwaga nondo za kufa mtu, kwanza kwa kuwaita baadhi ya viongozi ni "Vichwa Maji".
Aboubakar Karsan, anasema Tanzania tuna sheria nzuri inayotoa uhuru mkubwa wa habari tatizo ni Tanzania hatuna Media zenye uwezo wa kuutumia ipasavyo uhuru tulionao, amesema Tanzania tuna media iliyojaa uoga katokana na kuwaogopa viongozi vichwa maji!.
Karsan anasema, media ya Tanzania, ingeutumia vizuri na kikamilifu uhuru tulionao, Tanzania tungekuwa mbali sana kimaendeleo, kwa sababu vitendo vya rushwa, uhujumu, ufisadi, ubadhirifu na madudu yote yanayoibuliwa kwenye ziara za Mhe. Rais, vingeibuliwa kabla na serious media na sio kusubiri hadi rais afanye ziara ndipo madudu yaibuliwe.
Aboubakar Karsan, anasema ile kauli ya rais, John Pombe Joseph Magufuli kuvionya vyombo vya habari kuwa "Watch out, you are not that free", ilitolewa kwa nia njema, kuwaasa media kuwa hakuna uhuru usio mipaka, na kila haki inaadamana na wajibu. Kupitia kauli hii, baadhi ya wasaidizi wa rais wakiwemo mawaziri, wakuu wa mikoa na wakuu wa wilaya, ambao amewaita "vichwa maji", wakaitafsiri vibaya kauli hiyo, na kuanza kuvibinya vyombo vya habari na kuwabinya waandishi wa habari, ikiwemo kuvifungia vyombo vya habari na kuviadhibu.
Karsan anasema, haungi mkono fungia fungia ya vyombo vyombo vya habari yakiwemo magazeti ni kuwanyima haki haki wananchi wanaotegemea media hiyo kupata habari, ameshauri zitumike adhabu mbadala.
Karsan anasema, uhuru wa kweli wa habari, uanzie ndani ya vyombo vyenyewe vya habari, kwa wamiliki wa vyombo vya habari, kuwalipa vizuri waandishi wao, wawape haki zote za msingi za wanahabari, ikiwemo vitendea kazi bora, mazingira bora ya Kazi, bima ya afya, kinga maalum kwa waandishi wa habari za kiuchunguzi. Baada ya waandishi kupata haki zao na stahiki zao newsroom ndipo sasa tukatafute hiyo haki nje ya newsroom kwa kusisitiza sheria, taratibu, na kanuni zifuatwe.
Karsan anasema kuna waandishi wa kweli wa habari, na wanaharakati wa kihabari, kazi za uandishi wa habari, sio uanaharakapti za kihabari, ila amekiri kwenye media kuna sera za media za kihabari na media za ki propaganda na za kiharakati, akatolea mfano gazeti la Uhuru, tangu usajili wake ni gazeti la propaganda ya Chama cha Mapinduzi, hivyo likiandika propaganda yoyote ndiko kutimiza wajibu wake. Lakini vyombo vya kawaida vya habari, vinatakiwa kuwa impartial kwa kuripoti balanced news. Amelaani magazeti huru kujigeuza vyombo vya propaganda za vyama Fulani akatolea mfano gazeti la Tanzania Daima ni gazeti huru, likifanya propaganda ya Chadema, ni kinyume cha sera ya gazeti hilo.
Hitimisho.
Karsan anasisitiza, Tanzania tuna Uhuru mkubwa wa habari kwa mujibu wa sheria, unakwamishwa na viongozi vichwa maji, na media zenye uoga, hivyo amesisitiza media tutimize wajibu wetu bila uoga kwa mujibu wa sheria, tukiacha uoga, tutaisaidia sana serikali, tutaisaidia jamii na kulisaidia Taifa.
Asanteni kufuatilia.
Paskali
wale wenye access angalieni Star TV, kipindi cha Jicho Letu Ndani ya Habari kinachorushwa live na Star TV, kila siku za Jumamosi asubuhi, leo Mtangazaji Mahiri, Leonard Mapuli yuko na Mkurugenzi Mtendaji wa Umoja wa Press Clubs, UTPC, Aboubakar Karsan, anamwaga nondo za kufa mtu, kwanza kwa kuwaita baadhi ya viongozi ni "Vichwa Maji".
Aboubakar Karsan, anasema Tanzania tuna sheria nzuri inayotoa uhuru mkubwa wa habari tatizo ni Tanzania hatuna Media zenye uwezo wa kuutumia ipasavyo uhuru tulionao, amesema Tanzania tuna media iliyojaa uoga katokana na kuwaogopa viongozi vichwa maji!.
Karsan anasema, media ya Tanzania, ingeutumia vizuri na kikamilifu uhuru tulionao, Tanzania tungekuwa mbali sana kimaendeleo, kwa sababu vitendo vya rushwa, uhujumu, ufisadi, ubadhirifu na madudu yote yanayoibuliwa kwenye ziara za Mhe. Rais, vingeibuliwa kabla na serious media na sio kusubiri hadi rais afanye ziara ndipo madudu yaibuliwe.
Aboubakar Karsan, anasema ile kauli ya rais, John Pombe Joseph Magufuli kuvionya vyombo vya habari kuwa "Watch out, you are not that free", ilitolewa kwa nia njema, kuwaasa media kuwa hakuna uhuru usio mipaka, na kila haki inaadamana na wajibu. Kupitia kauli hii, baadhi ya wasaidizi wa rais wakiwemo mawaziri, wakuu wa mikoa na wakuu wa wilaya, ambao amewaita "vichwa maji", wakaitafsiri vibaya kauli hiyo, na kuanza kuvibinya vyombo vya habari na kuwabinya waandishi wa habari, ikiwemo kuvifungia vyombo vya habari na kuviadhibu.
Karsan anasema, haungi mkono fungia fungia ya vyombo vyombo vya habari yakiwemo magazeti ni kuwanyima haki haki wananchi wanaotegemea media hiyo kupata habari, ameshauri zitumike adhabu mbadala.
Karsan anasema, uhuru wa kweli wa habari, uanzie ndani ya vyombo vyenyewe vya habari, kwa wamiliki wa vyombo vya habari, kuwalipa vizuri waandishi wao, wawape haki zote za msingi za wanahabari, ikiwemo vitendea kazi bora, mazingira bora ya Kazi, bima ya afya, kinga maalum kwa waandishi wa habari za kiuchunguzi. Baada ya waandishi kupata haki zao na stahiki zao newsroom ndipo sasa tukatafute hiyo haki nje ya newsroom kwa kusisitiza sheria, taratibu, na kanuni zifuatwe.
Karsan anasema kuna waandishi wa kweli wa habari, na wanaharakati wa kihabari, kazi za uandishi wa habari, sio uanaharakapti za kihabari, ila amekiri kwenye media kuna sera za media za kihabari na media za ki propaganda na za kiharakati, akatolea mfano gazeti la Uhuru, tangu usajili wake ni gazeti la propaganda ya Chama cha Mapinduzi, hivyo likiandika propaganda yoyote ndiko kutimiza wajibu wake. Lakini vyombo vya kawaida vya habari, vinatakiwa kuwa impartial kwa kuripoti balanced news. Amelaani magazeti huru kujigeuza vyombo vya propaganda za vyama Fulani akatolea mfano gazeti la Tanzania Daima ni gazeti huru, likifanya propaganda ya Chadema, ni kinyume cha sera ya gazeti hilo.
Hitimisho.
Karsan anasisitiza, Tanzania tuna Uhuru mkubwa wa habari kwa mujibu wa sheria, unakwamishwa na viongozi vichwa maji, na media zenye uoga, hivyo amesisitiza media tutimize wajibu wetu bila uoga kwa mujibu wa sheria, tukiacha uoga, tutaisaidia sana serikali, tutaisaidia jamii na kulisaidia Taifa.
Asanteni kufuatilia.
Paskali