kimboka one
JF-Expert Member
- Jan 23, 2010
- 734
- 85
Ndugu zangu wanajamvi,niwape pole sana kwa misiba yote miwili ya viongozi wetu iliyotukumba hivi karibuni.
Nametakafakari sana mwenendo na mwelekeo wa siasa za Tanzania kwa kupitia katiba na ilani ya vyama vyote hususani vile vilivyoweka wagombea uchaguzi uliopita,pamoja na kuangalia mwelekeo ya vyama hivyo.
kadhalika nimetazama mtazamo wa jamii na mahitaji ya watanzania wasasa,nasisitiza watanzania wasasa. watanzania wameamka sana na kuashiria kutengana na mawazo ya kikoloni tulioishi nayo kwa muda mrefu,watanzania wanataka sasa wapate chama kinacholingana na watanzania wa leo,kwani vyama vilivyopo vinamtazamo ile ile wa kikoloni ya kunyunya na kunufaisha wachache na mbaya zaidi ni vikundi vya watu wanaosaka utajiri na umaarufu kwa udi na uvumba.
lengo langu kuja na hoja hii ni kutaka kukumbusha wadau hili tufikiri namna ya kupata chama kipya hasa baada ya katiba mpya.
chama ambacho kitaweka wazi namna ambavyo chama kitaepusha serikali yake na mafisadi na watu wavivu kwa mkakati sahihi na wakudumu.
aidha kupitia katiba ya chama hicho kibainishe sifa za viongozi watakao ongoza serikali yake na hapa turejee kwenye azimio la arusha na kuchukua zile sifa kama zilivyo,ni imani yangu watanzania wenye uwezo na sifa hizo wapo,mfano kiongozi wa chama asiwe mfanyabihashara,asiwe na mali nyingi na hili linapimika tu,kama azimio la arusha lilitaja nyumba leo tutaje sifa hizo kama vile asiwe na nyuma zaidi ya moja,asiwe na magari zaidi ya mawili na hapa watoto,mke au wake na ndugu wa karibu wanausika katika kuhakiki mali za viongozi,kwa uchache ndiyo njia ya kuziba ombwa hili.wewe unawazaje?
Nametakafakari sana mwenendo na mwelekeo wa siasa za Tanzania kwa kupitia katiba na ilani ya vyama vyote hususani vile vilivyoweka wagombea uchaguzi uliopita,pamoja na kuangalia mwelekeo ya vyama hivyo.
kadhalika nimetazama mtazamo wa jamii na mahitaji ya watanzania wasasa,nasisitiza watanzania wasasa. watanzania wameamka sana na kuashiria kutengana na mawazo ya kikoloni tulioishi nayo kwa muda mrefu,watanzania wanataka sasa wapate chama kinacholingana na watanzania wa leo,kwani vyama vilivyopo vinamtazamo ile ile wa kikoloni ya kunyunya na kunufaisha wachache na mbaya zaidi ni vikundi vya watu wanaosaka utajiri na umaarufu kwa udi na uvumba.
lengo langu kuja na hoja hii ni kutaka kukumbusha wadau hili tufikiri namna ya kupata chama kipya hasa baada ya katiba mpya.
chama ambacho kitaweka wazi namna ambavyo chama kitaepusha serikali yake na mafisadi na watu wavivu kwa mkakati sahihi na wakudumu.
aidha kupitia katiba ya chama hicho kibainishe sifa za viongozi watakao ongoza serikali yake na hapa turejee kwenye azimio la arusha na kuchukua zile sifa kama zilivyo,ni imani yangu watanzania wenye uwezo na sifa hizo wapo,mfano kiongozi wa chama asiwe mfanyabihashara,asiwe na mali nyingi na hili linapimika tu,kama azimio la arusha lilitaja nyumba leo tutaje sifa hizo kama vile asiwe na nyuma zaidi ya moja,asiwe na magari zaidi ya mawili na hapa watoto,mke au wake na ndugu wa karibu wanausika katika kuhakiki mali za viongozi,kwa uchache ndiyo njia ya kuziba ombwa hili.wewe unawazaje?