TANZANIA (taifa stars) vs CAMEROON !!!

Mtaalam

JF-Expert Member
Oct 1, 2007
1,369
233
kipute ndo hichooo chakaribia bandugu na wa cameroon washatua darisalama tayari kwa mpambano
 
Kocha Marcio Maximo asema Cameroon wanaheshimu Taifa Stars

KOCHA wa Taifa Stars, Marcio Maximo amesema kuwasili kwa Cameroon siku nne kabla ya mechi ni kuonyesha ni jinsi gani wanaivyoheshimu timu yake.

Stars itapambana na Cameroon kwenye mchezo wa kutafuta tiketi ya kucheza Fainali za Kombe la Dunia na Mataifa ya Afrika zitakazofanyika kwenye Uwanja Mpya wa Taifa jijini, Dar es Salaam Jumamosi.

Akizungumza na Mwananchi jijini wiki hii, Maximo alisema ni vizuri kuwa timu hiyo ya Cameroon imekuja mapema kwa kuwa wameonyesha dhahiri kuwa wanaohofia Stars.


Alisema sasa kila timu inaogopa kukutana na Stars na ndivyo walivyoonyesha Cameroon kwani wamekuja mapema ili kuisoma Stars na hii inaonyesha kabisa kuwa wanaohofia timu hiyo.

''Wamekuja mapema ili kuonyesha dhahiri kuwa wanatujali na kutuheshimu na hii ni picha kuwa sasa timu yetu ni bora na inaogopeka tutakwenda uwanjani kama mbogo Jumamosi, hatuna hofu yoyote ingawa hatupewi nafasi, lakini mashabiki wataona uwanjani,'' alisema.

Na Phillip Nkini
gazeti la Mwananchi
 
nmekutana na hiyo habari gazeti la mwananchi hadi nkajisikia kuanzisha thread bandugu...i think the coach anaongea sanaa ndo tatizo lake n at the end ikifka jumamosi jioni sijui atatoa visingizio gani..

if ni sie tumezoea ujinga wetu wa kwenda kwenye mechi za kimataifa siku moja au mbili kabla ni sie na ujinga wetu ila timu nzuri hufika siku tatu au zaidi kabla kuzoea hali ya hewa n stuffs!!i wish ningekua huko ufisadini nijionee mpambano huu jamani wadau wa tz muwe mwatuhabarisha wakati huo tasafalini
 
1375.jpg

Aisee hivi huyu jamaa ana miaka mingapi?....ataweza mikikimikiki ya Etoo fils?
 
kuja siku nne kabla jamaa wamekuja tour tu hiyo game ni matokeo katika safari yao,mana wakitoka hapa wanenda kisiwani kabisa Mauritius!!!!
 
Maximo kweli msanii, yaani Cameroun kuja mapema ni kuiogopa Stars? he must be joking.

Hana habari kuwa safari yao hii pia ni ya kujipumzisha wakitoka Dar wanaenda mbuga za wanyama kustarehe
 
I think our boys need to approach this game as their world cup final, they have nothing to lose in this game. Ukicheza vizuri kwenye games kama hizi unajiwekea mazingira mazuri kupata soko ulaya, miracles do happen ie Chelsea V Barnsley, FA Cup 1/4 final 08, remember that?
 
I think our boys need to approach this game as their world cup final, they have nothing to lose in this game. Ukicheza vizuri kwenye games kama hizi unajiwekea mazingira mazuri kupata soko ulaya, miracles do happen ie Chelsea V Barnsley, FA Cup 1/4 final 08, remember that?

kana,those things kama sijui barnsley na chelsea au na liverpool do happen kwa zile timu zinazocheza mpira...sio butu butua from no where mpira udunde nyavuni kama maximo atakavyo kutujaza ujinga sie!
 
kuja siku nne kabla jamaa wamekuja tour tu hiyo game ni matokeo katika safari yao,mana wakitoka hapa wanenda kisiwani kabisa Mauritius!!!!

heheh looh kumbe ndio maana wakaanza onekana madukani etc...loh wamekuja tour kufanya shopping na kisha wakimaliza wanaondoka!!
wadau mlioko bongo tupeni habari majamaa hawajaenda na ngorongoro kucheki wanyama au zenji kula raha kabsaa?!!maana i doubt hata mazoezi kama wanafanya!
 
kana,those things kama sijui barnsley na chelsea au na liverpool do happen kwa zile timu zinazocheza mpira...sio butu butua from no where mpira udunde nyavuni kama maximo atakavyo kutujaza ujinga sie!

Ama kweli wapundaka wafadhilaka ... maximo mbona anajitahidi
 
Ama kweli wapundaka wafadhilaka ... maximo mbona anajitahidi

sijakataa kuwa anajitahidi ila nisichotaka ni hicho cha kutujaza ujinga kila siku hadi nw anadirikia ropoka kuwa cameroon yatuogopa!!!kwa mpira upi tulionao??!!!!
 
Habari nilizozipata leo toka bongo ni kwamba wachezaji wa cameroon wamekuwa wakionekana viwanja mbalimbali wakijivinjari na machangu, haswa Etoo ambaye amekuwa akigombaniwa na dada zetu kama mpira wa kona kila anapotia mguu! Huu ni ushahidi wa yale yaliyosemwa na captain wao Rigobert Song kwamba wamekuja mapema ili wapumzike! Vijana wetu nahisi wana nafasi, lets wait tuone hiyo kesho itakuwaje.
 
Habari nilizozipata leo toka bongo ni kwamba wachezaji wa cameroon wamekuwa wakionekana viwanja mbalimbali wakijivinjari na machangu, haswa Etoo ambaye amekuwa akigombaniwa na dada zetu kama mpira wa kona kila anapotia mguu! Huu ni ushahidi wa yale yaliyosemwa na captain wao Rigobert Song kwamba wamekuja mapema ili wapumzike! Vijana wetu nahisi wana nafasi, lets wait tuone hiyo kesho itakuwaje.

Sikia KKN pale hata akina Etoo wakilala Jolly club wakaamkia uwanjani hata draw hatupati.Kesho kichapo tu tusijipe hope za kinamna au mpaka tutoke damu ndio itajulikana Stars mahututi?
 
Habari nilizozipata leo toka bongo ni kwamba wachezaji wa cameroon wamekuwa wakionekana viwanja mbalimbali wakijivinjari na machangu, haswa Etoo ambaye amekuwa akigombaniwa na dada zetu kama mpira wa kona kila anapotia mguu! Huu ni ushahidi wa yale yaliyosemwa na captain wao Rigobert Song kwamba wamekuja mapema ili wapumzike! Vijana wetu nahisi wana nafasi, lets wait tuone hiyo kesho itakuwaje.

sio tu wamekuja kupumzika bali wanawaonyesha kiasi gani wanatudharau..yaan so far nimeona picha chache za mazoezi..nyingi ni za shopping na matanuzi!!alafu nabado watatufunga wakati sie kutwa mazoezini!
 
jamani kuna aliyeuliza humu je kuna namna twaweza jionea huu mpambano kupitia internet wajimini???wataalam tupeni dataz basiiiii au muwe mwatuhabarisha kila litokealo uwanjani aiseeee!!
 
nmekuta bbc huko squad letu ndo hilooo mwee angalau dakika kumi zimepita hatujafungwaa!!!

1 Ivo MAPUNDA (GK)
2 Salum SWED
4 Athuman IDDY
5 Shaban NDITI
7 Danny MRWANDA
8 Mrisho NGASA
9 Geofrey BONY
13 Nadir HAROUB
14 Shadrack NSAJIGWA
16 Nizar KHALFAN
17 Amir MAFTAH
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom