Tanzania sasa hivi ndiyo nchi ngumu kufanya biashara

Major

JF-Expert Member
Dec 20, 2007
1,865
2,439
Ukiondoa Sudani ya kusini, Ktk Africa yote Tanzania ndiyo nchi yenye mazingira na uchumi duni kuliko Nchi yoyote Africa. Hali hii, inaifanya Tanzania kuwa Sehemu hatari kabisa kufanya biashara ktk Africa.

Tusipobadilika haraka, Nina Imani baada ya Mwaka mmoja kuazia sasa, hayo makusanyo ya kodi yatashuka kwa Zaidi ya 60%.. Na tuombe Mungu uchaguzi wa Kenya uvurugike ili pasiwe na Amani mwezi wa August lakini Kama uchaguzi wa kenya utakuwa wa amani, Mhh! Kuna hatari mapato ya Tz yakashuka kwa zaidi ya 70%.
Tatizo kubwa linaloitafuna Nchi kwa sasa ni Ubaguzi. Na hii dhambi inayofanywa na viongozi wetu ni mbaya kuliko zote. Tukiendelea kuvumilia hali hii bila kuipigia kelele, matokeo yatakuwa mabaya sana.kuna tetesi kwamba TBL wana mpango wa kupunguza wafanyakazi zaidi ya 600. Na hii inatokana na hali mbaya ya mauzo. Coca pia, makampuni mengi yanataka kufungasha.

Ukiteuliwa na wananchi ili uwaongoze, basi jua kwamba unafanya kazi ya Mungu, kitendo ya Cha viongozi wetu wakuu kuwa double standard, ni hatari sana. Ki tendo cha kiongozi kuwa Rafiki wa Asiyekuwa Rafiki wa wananchi au mtu mwenye Roho mbaya chuki na husda, ni hatari sana kwa Mustakabali wa Nchi hii,

Ni Maajabu sana. Ktk Taifa changa na masikini Kama hili, basi kila mtu aliyekuwa na Kipato, basi huyu mtu anaitwa. mpiga Dili, kana kwamba Tanzania mtu Akiwa tajiri ni dhambi. Halafu maneno hayo yanatamkwa na Viongozi ambao tuna Amini wana Akili timamu, na wanatamka ktk Majukwaa au ktk mikutano muhimu ya Kitaifa. Binafsi mpaka sasa sijamuona kiongozi yeyote Ambaye yuko Serious kulisongesha hili Taifa,

Tukishakuchagua kuwa kiongozi wetu jua ni lazima utende haki. Uwe na busara na hekima. Ubaguzi kwako uwe Mwiko. Maana kiongozi aliyechaguliwa lazima ajitambue kuwa haongozi familia Bali anawangoza Watanzani ambao ni Zaidi ya milioni 50
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom