Ghazwat
JF-Expert Member
- Oct 4, 2015
- 23,718
- 66,262
Patashika ya Ligi Kuu Tanzania kuendelea leo Mei 16, 2019 kwa Bingwa wa Nchi Simba SC, Mnyama Mkali Mwituni, Lunyasi kwa kuwakaribisha Mtibwa Sugar, WakataMiwa kunako uwanja wa Uhuru jijini Dar es salam.
Mchezo huu wa leo miongoni mwa michezo ya ukingoni kuelekea kumalizika kwa msimu wa 2018/2019, TPL, unategemewa kuwa mkali na wakusisimua kwa muda wote wa dakika tisini, hasa ukizingatia matokeo yaliyopita kutoridhisha kwa pande zote zinazokutana, ambapo Simba SC imetoka kugawana alama kwa kwenda sare ya bila kufungana na Azam FC huku Mtibwa Sugar wakiambulia kipigo cha 1-0 na Coastal Union.
Je Simba SC watarekebisha makosa na kuondoka na ushindi na kurudi kileleni ama watapokea Surprise kutoka kwa Mtibwa Sugar? tusubiri mwisho wa mchezo..! Usikose Ukaambiwa na kumbuka kabumbu hili murua litakuwa Mubashara Azam Sports 2 kuanzia saa 10: 00 jioni.
Wakati wowote mpira utaanza uwanja wa Uhuru.
Naaaaaaam mpira umeanza TPL
Simba SC 0-0 Mtibwa Sugar
10' Simba wanafanya shambulizi kuelekea Mtibwa, lakini Kado golikipa anaokoa.
15' Mtibwa Sugar wanajaribu kwenda mbele kutafuta bao nguvu yao ni chache mbele.
20' Simba wanakosa nafasi ya wazi kabisa kwa washambuliaji Okwi na Kagere.
25' Uwanja unachezwa upande wa Mtibwa Sugar, lakíni Simba hawajafanikiwa kupata bao..!
Hatari lango la Simba...Dickson Daudi anapiga nje na kuwa goal kick
30' Simba wanapata kona, ambayo haijaza matunda
Simba SC 0-0 Mtibwa Sugar
32' Gooooooaaaal Simba wanaandika bao kwanza kupitia kwa John Bocco baada ya kupokea krosi ya Maddie Kagere
Simba SC 1-0 Mtibwa Sugar
35' Mtibwa wagong pasi ndefu ambazo zinaokolewa na walinzi wa Simba
La la la la kwa mara nyingine tena Simba wanakosa bao la wazi...kupitia kwa Kagere ilikuwa gonga safi kwa washambuliaji wa Simba
Mpambano ni wa upande mmoja hakika kutokana mpira kuchezwa Sana eneo la Mtibwa
40' Simba SC 1-0 Mtibwa Sugar
Ni faulo kuelekea Simba, inapigwa na Kibaya lakini unatoka nje..! Na kuwa goal kick..!
45+3' kuelekea kuwa mapumziko TPL
Naaam mpira ni mapumziko ambapo Simba wanatoka wakiwa mbele kwa bao la kutangulia kupitia kwaJohn Bocco kunako dakika ya 32
Kipindi cha pili cha lala salama kimeanza uwanja wa Uhuru jijini Dar es, Salaam
47' Goooooooaal gooooaaal Chama anaandika la pili baada ya kuwahi mpira uliopotezwa na mabeki wa Mtibwa Sugar
Simba SC 2-0 Mtibwa Sugar
50' Simba wameanza kwa mashambuliza ya nguvu sana, ambapo Mtibwa
56' Okwiiiiiiiiii gooooooooooooaal
Emmanuel Okwi anaipatia Simba bao la tatu.
Simba SC 3-0 Mtibwa Sugar
60' Anatoka John Bocco anaingia Mzamir Yasin upande wa Simba SC..!
Wakati huohuo Mtibwa wanamuingiza Ismail kuongeza nguvu
65' Ni piga nikupige upande wa Mtibwa Sugar ambapo Simba wapo mbele.
68' Kihimbwa anapiga shuti lakini golikipa Manula anatokea na kuruka juu na kudaka bila wasiwasi
70' Simba SC wako mbele kwa bao 3 na dhahir Mtibwa Sugar wana wakati mgumu kusawazisha
73' Adam Salamba anaingia kuchukua nafasi ya Maddie Kagere
74' Saleh anakwenda mbele na kupiga shuti ambalo halikuzaa matunda upande wa Mtibwa
80' Salamba anapiga Krosi lakini mabeki wa Mtibwa Sugar wanaokoa
83' Anatoka Niyonzima anaingia Dilunga..! Upande wa Simba na Anatoka Kihimbwa anaingia Juma Luzio kwa Mtibwa Sugar
85' Chama chamaaaa anampigia Salamba lakini Salamba anapiga shuti golikipa Kado anatokea na kudaka.
88' Simba SC 3-0 Mtibwa Sugar
Makarani anafanyiwa madhambi, ni free kick kuelekea Simba...
Dhahir kabisa hakuna mipango ya kuweza kupata bao kwa Mtibwa Sugar
90+3' kuelekea kumalizika kwa mpambano huu wa TPL
Naaaaaaaaam mpira umekwisha Uwanja wa Uhuru ambapo Simba wanaibuka na ushindi wa mabao matatu bila majibu kwa mabao ya John Bocco 32' na Chama 47' Okwi 56.
Simba SC 3 -0 Mtibwa Sugar
Mchezo huu wa leo miongoni mwa michezo ya ukingoni kuelekea kumalizika kwa msimu wa 2018/2019, TPL, unategemewa kuwa mkali na wakusisimua kwa muda wote wa dakika tisini, hasa ukizingatia matokeo yaliyopita kutoridhisha kwa pande zote zinazokutana, ambapo Simba SC imetoka kugawana alama kwa kwenda sare ya bila kufungana na Azam FC huku Mtibwa Sugar wakiambulia kipigo cha 1-0 na Coastal Union.
Je Simba SC watarekebisha makosa na kuondoka na ushindi na kurudi kileleni ama watapokea Surprise kutoka kwa Mtibwa Sugar? tusubiri mwisho wa mchezo..! Usikose Ukaambiwa na kumbuka kabumbu hili murua litakuwa Mubashara Azam Sports 2 kuanzia saa 10: 00 jioni.
Wakati wowote mpira utaanza uwanja wa Uhuru.
Naaaaaaam mpira umeanza TPL
Simba SC 0-0 Mtibwa Sugar
10' Simba wanafanya shambulizi kuelekea Mtibwa, lakini Kado golikipa anaokoa.
15' Mtibwa Sugar wanajaribu kwenda mbele kutafuta bao nguvu yao ni chache mbele.
20' Simba wanakosa nafasi ya wazi kabisa kwa washambuliaji Okwi na Kagere.
25' Uwanja unachezwa upande wa Mtibwa Sugar, lakíni Simba hawajafanikiwa kupata bao..!
Hatari lango la Simba...Dickson Daudi anapiga nje na kuwa goal kick
30' Simba wanapata kona, ambayo haijaza matunda
Simba SC 0-0 Mtibwa Sugar
32' Gooooooaaaal Simba wanaandika bao kwanza kupitia kwa John Bocco baada ya kupokea krosi ya Maddie Kagere
Simba SC 1-0 Mtibwa Sugar
35' Mtibwa wagong pasi ndefu ambazo zinaokolewa na walinzi wa Simba
La la la la kwa mara nyingine tena Simba wanakosa bao la wazi...kupitia kwa Kagere ilikuwa gonga safi kwa washambuliaji wa Simba
Mpambano ni wa upande mmoja hakika kutokana mpira kuchezwa Sana eneo la Mtibwa
40' Simba SC 1-0 Mtibwa Sugar
Ni faulo kuelekea Simba, inapigwa na Kibaya lakini unatoka nje..! Na kuwa goal kick..!
45+3' kuelekea kuwa mapumziko TPL
Naaam mpira ni mapumziko ambapo Simba wanatoka wakiwa mbele kwa bao la kutangulia kupitia kwaJohn Bocco kunako dakika ya 32
Kipindi cha pili cha lala salama kimeanza uwanja wa Uhuru jijini Dar es, Salaam
47' Goooooooaal gooooaaal Chama anaandika la pili baada ya kuwahi mpira uliopotezwa na mabeki wa Mtibwa Sugar
Simba SC 2-0 Mtibwa Sugar
50' Simba wameanza kwa mashambuliza ya nguvu sana, ambapo Mtibwa
56' Okwiiiiiiiiii gooooooooooooaal
Emmanuel Okwi anaipatia Simba bao la tatu.
Simba SC 3-0 Mtibwa Sugar
60' Anatoka John Bocco anaingia Mzamir Yasin upande wa Simba SC..!
Wakati huohuo Mtibwa wanamuingiza Ismail kuongeza nguvu
65' Ni piga nikupige upande wa Mtibwa Sugar ambapo Simba wapo mbele.
68' Kihimbwa anapiga shuti lakini golikipa Manula anatokea na kuruka juu na kudaka bila wasiwasi
70' Simba SC wako mbele kwa bao 3 na dhahir Mtibwa Sugar wana wakati mgumu kusawazisha
73' Adam Salamba anaingia kuchukua nafasi ya Maddie Kagere
74' Saleh anakwenda mbele na kupiga shuti ambalo halikuzaa matunda upande wa Mtibwa
80' Salamba anapiga Krosi lakini mabeki wa Mtibwa Sugar wanaokoa
83' Anatoka Niyonzima anaingia Dilunga..! Upande wa Simba na Anatoka Kihimbwa anaingia Juma Luzio kwa Mtibwa Sugar
85' Chama chamaaaa anampigia Salamba lakini Salamba anapiga shuti golikipa Kado anatokea na kudaka.
88' Simba SC 3-0 Mtibwa Sugar
Makarani anafanyiwa madhambi, ni free kick kuelekea Simba...
Dhahir kabisa hakuna mipango ya kuweza kupata bao kwa Mtibwa Sugar
90+3' kuelekea kumalizika kwa mpambano huu wa TPL
Naaaaaaaaam mpira umekwisha Uwanja wa Uhuru ambapo Simba wanaibuka na ushindi wa mabao matatu bila majibu kwa mabao ya John Bocco 32' na Chama 47' Okwi 56.
Simba SC 3 -0 Mtibwa Sugar