Informer
JF-Expert Member
- Jul 29, 2006
- 1,582
- 6,627
Pato la Taifa kwa robo mwaka ya pili ya mwaka huu limekua kwa kwa asilimia 6.9, ikilinganishwa na asilimia 7.0 mwaka jana, ambapo thamani halisi ya pato hilo ni Sh. 4,730709, ikilinganishwa na Sh. 4,426,905 mwaka jana.
Ripoti hiyo ilitolewa na Mkurugenzi wa Takwimu za Uchumi wa Ofisi ya Taifa ya Takwimu, Maurice Oyuke, jana jijini Dar es Salaam, alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari kuhusu ripoti ya pato la Taifa kwa robo ya pili ya mwezi Aprili na Juni, 2012.
Oyuke alisema kuwa pato katika kilimo limekua kwa asilimia 5.2 ikilinganishwa na asilimia 5.9 kwa robo pili ya mwaka jana na kwamba ongezeko hilo limetokana na mvua za kutosha pia na juhudi za serikali katika uboreshaji wa masuala ya kilimo.
Aliongeza shughuli za madini limekua kwa asilimia 1.0 ikilinganishwa kwa asilimia 5.6 mwaka jana kutokana na kupungua kwa kasi ya ukuaji baada ya ikufungwa kwa muda mgodi wa dhahabu wa Geita ili kupisha ukarabati wa mitambo.
Kwa upande wa uvuvi, alisema pato limekua kwa asilimia 4.0 kutoka asilimia 0.3 ya mwaka jana kutokana na ongezeko la uvunmaji wa samaki kwa ajili ya soko la ndani na nje.
Kwa upande wa viwanda, alisema pato limekua kwa asilimia 8.2 ikilindanishwa kwa asilimia 8.5 mwaka jana. Alisema kiwango hicho kimefikiwa kutokana na upatikanaji wa umeme.
Kuhusu umeme, gesi na maji, Oyuke alisema pato limekua kwa asilimia 5.6 ikilinganishwa kwa asilimia 10.3 ya mwaka jana kutokana na kupungua uzalishaji wa umeme katika kipindi hicho.
Katika sekta za chukuzi na mawasiliano, alisema patolimekua kwa asilimia 5.2 ikilinganishwa na asilimia 16.6 mwaka jana na kwamba hali hiyo imetokana na matumizi ya simu, usafilishaji wa abaria na mazigo. Pato la huduma ya fedha limekua kwa asilimia 14.1 ikilinganishwa kwa asilimia 10.0 mwaka jana kutokana na kuongezeka kwa amana na mikopo.
CHANZO: NIPASHE | Oktoba 04, 2012
Ripoti hiyo ilitolewa na Mkurugenzi wa Takwimu za Uchumi wa Ofisi ya Taifa ya Takwimu, Maurice Oyuke, jana jijini Dar es Salaam, alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari kuhusu ripoti ya pato la Taifa kwa robo ya pili ya mwezi Aprili na Juni, 2012.
Oyuke alisema kuwa pato katika kilimo limekua kwa asilimia 5.2 ikilinganishwa na asilimia 5.9 kwa robo pili ya mwaka jana na kwamba ongezeko hilo limetokana na mvua za kutosha pia na juhudi za serikali katika uboreshaji wa masuala ya kilimo.
Aliongeza shughuli za madini limekua kwa asilimia 1.0 ikilinganishwa kwa asilimia 5.6 mwaka jana kutokana na kupungua kwa kasi ya ukuaji baada ya ikufungwa kwa muda mgodi wa dhahabu wa Geita ili kupisha ukarabati wa mitambo.
Kwa upande wa uvuvi, alisema pato limekua kwa asilimia 4.0 kutoka asilimia 0.3 ya mwaka jana kutokana na ongezeko la uvunmaji wa samaki kwa ajili ya soko la ndani na nje.
Kwa upande wa viwanda, alisema pato limekua kwa asilimia 8.2 ikilindanishwa kwa asilimia 8.5 mwaka jana. Alisema kiwango hicho kimefikiwa kutokana na upatikanaji wa umeme.
Kuhusu umeme, gesi na maji, Oyuke alisema pato limekua kwa asilimia 5.6 ikilinganishwa kwa asilimia 10.3 ya mwaka jana kutokana na kupungua uzalishaji wa umeme katika kipindi hicho.
Katika sekta za chukuzi na mawasiliano, alisema patolimekua kwa asilimia 5.2 ikilinganishwa na asilimia 16.6 mwaka jana na kwamba hali hiyo imetokana na matumizi ya simu, usafilishaji wa abaria na mazigo. Pato la huduma ya fedha limekua kwa asilimia 14.1 ikilinganishwa kwa asilimia 10.0 mwaka jana kutokana na kuongezeka kwa amana na mikopo.
CHANZO: NIPASHE | Oktoba 04, 2012