Tanzania nzima inaweza msahau Hayati Magufuli ila sio Tabora

Wewe ndio unaropoka mkuu,

Tanzania iliweka mpango, ifikapo 2025, ifikie Uchumi wa kati wa Chini, mwaka 2020 Tanzania ikafikia uchumi wa kati wa chini.

Mipango ni kitu kimoja, kutekeleza mipango ni kitu kingine.

Kupanga ni rahisi sana ila kutekeleza ni kazi inayohitaji kujitoa sadaka.

Nadhani utaacha uropokaji baada ya hapa.
Kwa hiyo uliamini takwimu za kupika na taarifa za magumashi kuwa Tanzania imeingia uchumi wa kati? Kwa nini usijishughulishe kidogo kutafuta ukweli wa takwimu, taarifa na maarifa?

Hivi unajua kuwa dikteta Adolf Hitler alifanya "maendeleo" makubwa sana Ujerumani miaka ya 1930 kuliko haya ya dikteta uchwara mnayoyaimbia? Sasa kama kupeleka huduma rahisi kama maji (ambao ni ushahidi mwingine wa ubovu na ufisadi wa CCM kwa miaka yote), angefanya maendeleo ya kweli si mngemwabudu? Lakini kwa nini Hitler anatajwa kuwa miongoni mwa watawala na watu waovu katika historia ya ulimwengu huu.....kama vile Nimrod, Antioch, Nero, Julius Cesar na wenzao? Katika nchi inayojitambua, yenye utawala wa Sheria, kupeleka maji ni kazi ya Diwani au Mbunge, na haitopigiwa mwingi.

Tambua: Juhudi au harakati zozote za kujaribu kumsafisha au kumsifia hayati Magufuli tayari zimeshindwa na zitaendelea kushindwa maradufu kila uchao, maana uongo hauwezi kuushinda ukweli, na dhuluma haiwezi kuishinda haki, NEVER!
Mapambio yenu yataendelea kumfifisha na kumfedhesha hayati Magu, yaani hata mje na gia gani au hadithi za namna gani; ukweli unabaki kuwa hayati Magufuli alikuwa rais na mtu alikuwa mwovu, katili na mbovu katika historia ya Tanganyika na Tanzania.
 
Kwa hiyo uliamini takwimu za kupika na taarifa za magumashi kuwa Tanzania imeingia uchumi wa kati? Kwa nini usijishughulishe kidogo kutafuta ukweli wa takwimu, taarifa na maarifa?

Hivi unajua kuwa dikteta Adolf Hitler alifanya "maendeleo" makubwa sana Ujerumani miaka ya 1930 kuliko haya ya dikteta uchwara mnayoyaimbia? Sasa kama kupeleka huduma rahisi kama maji (ambao ni ushahidi mwingine wa ubovu na ufisadi wa CCM kwa miaka yote), angefanya maendeleo ya kweli si mngemwabudu? Lakini kwa nini Hitler anatajwa kuwa miongoni mwa watawala na watu waovu katika historia ya ulimwengu huu.....kama vile Nimrod, Antioch, Nero, Julius Cesar na wenzao? Katika nchi inayojitambua, yenye utawala wa Sheria, kupeleka maji ni kazi ya Diwani au Mbunge, na haitopigiwa mwingi.

Tambua: Juhudi au harakati zozote za kujaribu kumsafisha au kumsifia hayati Magufuli tayari zimeshindwa na zitaendelea kushindwa maradufu kila uchao, maana uongo hauwezi kuushinda ukweli, na dhuluma haiwezi kuishinda haki, NEVER!
Mapambio yenu yataendelea kumfifisha na kumfedhesha hayati Magu, yaani hata mje na gia gani au hadithi za namna gani; ukweli unabaki kuwa hayati Magufuli alikuwa rais na mtu alikuwa mwovu, katili na mbovu katika historia ya Tanganyika na Tanzania.
Mnaweza nishinda kwa kubwajaja hapa JF ila barabara, umeme, meli za kisasa, bandali, reli, bwawa la Nyerere vinaongea.
 
Mkuu Nebuchadinezzer, kila Rais ailyepata kuiongoza nchi yetu ana mazuri yake kutokana na fursa na changamoto za wakati alizokutana nazo. Nyerere hakuwa na wataalamu wa kutosha wala hakuchimba madini mengi isipokuwa almasi lakini aliweza kufanya mazuri yake.

Baada ya uchumi kuvurugwa na vita vya Kagera na anguko la ukomonisti duniani, Mzee Mwinyi bado aliweza kusimama imara kwa nafasi yake kwa kukubaliana na sera za uchumi huria.

Mzee Mkapa na Mzee Kikwete walinufaika sana na sera za uchumi huria. Mbali ya kubinafsishwa na kuuzwa kwa makampuni ya umma, bado marais hawa ndio waliweza kunufaika na fursa na faida zitokanazo na uchimbaji wa gesi na madini. Hapa ndipo nchi ilipoanza kupata uwezo wa kuendeleza miundombinu mingi iliyokuwa katika "blue prints" za awamu zilizopita.

Magufuli amekuta kila kitu kipo sawa, alikuta nchi ina fedha na pia inakopesheka na kwa kweli alikopa na kukomba kila kitu Aliendeleza tu yale yaliyokuwa yamepangwa kufanyika. Tatizo lake kubwa alitaka kwa makusudi kufunika yaliyofanywa na wenzake, na alifanya hivyo kwa ajili kiki na kupenda sifa ambazo hakustahili kuzipata.

Nchi yetu nikiifananisha na nyumba, ujenzi wake ulianza hata kabla ya Tanganyika na Zanzibar kuwa nchi huru. Nathubutu kusema wale machifu wa awali ndiyo walianza kujenga msingi wa nyumba yetu ijapokuwa historia haiwasemi kwa uwazi.

Kwa upande wa Nyerere aliifikisha katika lenta na kupandisha kozi kadhaa juu yake. Mzee Mwinyi aliweka mbao za kupaua, Mzee Mkapa alipaua nyumba, Kikwete alianza kazi ya "finishing" ambayo iliendelezwa na Magufuli na hata sasa inaendelezwa na Mama SSH.

Je! Sasa ni kwa nini Magufuli pekee atambulike ndiye aliyeijenga nyumba Tanzania na wala si mtu mwingine!? Lazima kuna tatizo kubwa sehemu fulani.
Huu ni upotoshaji wa hali ya juu. Kama hujui kitu ni bora ukae kimya usizungumze kwa hisia zako kwasbbu ya chuki.
 
We unafikiri watu wa Kimara watamsahau

Pia kule Bukoba walipatwa Janga la tetemeko he watamsahau?

Kule Lindi fedha zao za Korosho unafikiri watamsahau
 
Huu ni upotoshaji wa hali ya juu. Kama hujui kitu ni bora ukae kimya usizungumze kwa hisia zako kwasbbu ya chuki.
Mkuu, kama unathibitisha mimi sijui kitu ni bora ukaweka ubaoni hicho kitu mbadala ambacho wewe binafsi unahisi kinakosekana katika bandiko langu. Nasimama ili kukubali ukweli wa kukosolewa kupitia hoja makini, uwanja ni wako kwa hilo
 
Nimefika Tabora ndugu zangu, nimelia sana baada ya kukumbuka kuwa JPM hayupo tena duniani.

Magufuli, Magufuli, Magufuli, nimekuita mara tatu, najua hunisikii, ila Mungu atakulipa siku ya ufufuo. Ni miaka 60 tangu tupate uhuru, mkoa wa Tabora ulisahaulika sana...hasahasa kwenye huduma muhimu za kijamii.

Awamu zote kabla ya JPM zilipita,bila kuwaletea wana Tabora maji safi na salama. JPM aliwahi kusema, ukiomba mkopo ili upeleke huduma ya maji Tabora, wahisani wanakataa.... JPM aliamua kutumia hela anayokusanya (Kodi) kupeleka maji katika mkoa mkubwa wenye historia iliyotukuka.

Kilichoniliza sio JPM kufa, wala kuleta maji Tabora. Kilichoniliza, kuna bibi mmoja, aliniomba hela 2,000...nikasita kumpatia maana anaonekana ni mlevi. Mimi msabato, ni makosa kumpatia mtu hela akanunue kitu kitakachomuangamiza.

Nikamuuliza ya nini 2000, akanambia "Mjukuu wangu, hii naenda kulipia mkopo wa bomba la maji" Nilishituka, ikabidi nimuite dogo mmoja, alikuwa anapita, nikamuuliza kama kuna mikopo ya hivyo.

Dogo akanambia baada ya maji kufika wilaya ya nzega kipindi cha JPM, changamoto ilikuwa wananchi wengi hawakuwa na uwezo wa kuvuta mabomba ya maji kutoka ziwa Viktoria. Serikali ya wanyonge, kupitia rais Magufuli akatoa order, kila asiyenauwezo wa kuvuta bomba la maji, atakopeshwa, atakuwa analipa 2000 kila wiki mpaka itakapo timia 40,000.

Bibi yule nilimpa 2000. Sasa leo Napita zangu mitaa ile yule bibi ananiletea risti inayodhibitisha kalipia maji. Nilishangaa sana. Nilimpa 20,000 ili akalipe deni lote. Baada ya kufika, napolalaga, nilianza kulia baada ya kukumbuka kuwa JPM hayupo tena duniani.

Tabora nayoifahamu mimi, leo ndoo mbili shilingi 50? Miaka 60 bila maji, Magufuli akaleta maji.

AsanteMagufuli- Kweli vizuri havidumu
Upuuzu mtupu! Magufuli atakumbukwa na misukule yake tu aliyoiacha kama mtoa mada. Hayo maji aliyopeleka Tabora yako wapi?
 
Magufuli anachukiwa na watu wachache sana hapa duniani, niamini mimi bro. Fanya research mkuu. Wanaomchukia ni kikundi cha watu wachache sana ambao wako JF, twitter na Ufipa basi.
Watanzania hawajawahi kuwa na chuki dhidi ya marehemu yeyote yule.

Ukibisha hudhuria misiba mingi uwezavyo.
 
Alimuua nani kwenye familia yako?
Alimuua Ben Saanane, Azory Gwanda, na wale aliokuwa anawatupa kwenye viroba baharini.

Mwendazake aliua na wakazi 340 wa wilaya za Mkuranga, Kibiti na Rufiji
 
Nimefika Tabora ndugu zangu, nimelia sana baada ya kukumbuka kuwa JPM hayupo tena duniani.

Magufuli, Magufuli, Magufuli, nimekuita mara tatu, najua hunisikii, ila Mungu atakulipa siku ya ufufuo. Ni miaka 60 tangu tupate uhuru, mkoa wa Tabora ulisahaulika sana...hasahasa kwenye huduma muhimu za kijamii.

Awamu zote kabla ya JPM zilipita,bila kuwaletea wana Tabora maji safi na salama. JPM aliwahi kusema, ukiomba mkopo ili upeleke huduma ya maji Tabora, wahisani wanakataa.... JPM aliamua kutumia hela anayokusanya (Kodi) kupeleka maji katika mkoa mkubwa wenye historia iliyotukuka.

Kilichoniliza sio JPM kufa, wala kuleta maji Tabora. Kilichoniliza, kuna bibi mmoja, aliniomba hela 2,000...nikasita kumpatia maana anaonekana ni mlevi. Mimi msabato, ni makosa kumpatia mtu hela akanunue kitu kitakachomuangamiza.

Nikamuuliza ya nini 2000, akanambia "Mjukuu wangu, hii naenda kulipia mkopo wa bomba la maji" Nilishituka, ikabidi nimuite dogo mmoja, alikuwa anapita, nikamuuliza kama kuna mikopo ya hivyo.

Dogo akanambia baada ya maji kufika wilaya ya nzega kipindi cha JPM, changamoto ilikuwa wananchi wengi hawakuwa na uwezo wa kuvuta mabomba ya maji kutoka ziwa Viktoria. Serikali ya wanyonge, kupitia rais Magufuli akatoa order, kila asiyenauwezo wa kuvuta bomba la maji, atakopeshwa, atakuwa analipa 2000 kila wiki mpaka itakapo timia 40,000.

Bibi yule nilimpa 2000. Sasa leo Napita zangu mitaa ile yule bibi ananiletea risti inayodhibitisha kalipia maji. Nilishangaa sana. Nilimpa 20,000 ili akalipe deni lote. Baada ya kufika, napolalaga, nilianza kulia baada ya kukumbuka kuwa JPM hayupo tena duniani.

Tabora nayoifahamu mimi, leo ndoo mbili shilingi 50? Miaka 60 bila maji, Magufuli akaleta maji.

AsanteMagufuli- Kweli vizuri havidumu
Unalia kila mara, wewe unawaza kwa muda mchache sana. Pole
 
Upo sahihi mkuu,
Rais haleti maji ila kodi za wananchi zinaleta maji.

JPM alikubali kutukanwa na kuambiwa anachukua kodi kwa nguvu ili apate hela ya kupeleka maji Tabora.

Kukusanya kodi kwa wafanyabiashara waliozoea kusamehewa na kukwepa kodi sio mchezo mkuu.

Si unajua kuna baadhi ya wafanyabiashara walihamishia biashara zao nje ya nchi ili kukwepa kodi? Akiwepo tajiri Freeman Mbowe wa Moshi?

Miaka yote ya uhuru, kodi imekusanywa, Tabora ni miongoni mwa mikoa inayotoa mapato makubwa sana, mbona maji hayakuwepo?
Yaani dunia ya wajinga ni kubwa klk ya werevu, zaidi ya miaka sitini ya uhuru kuna nchi watu wake wanawaza bomba la maji. Na kuyapata ni pongezi kwa aliekucheleweshea
 
Ishukuru CCM kwa kukufanya Masikini, na kukupa Elimu ndogo, ikakunyima exposure basi unaridhika na mambo madogo
Ndio maana yule jamaa alisema mnataka mpewe mimba nyinyina wake zenu ndipo muone kitukimefanyika.

Sasa wewe mjinga, unategemea serikali ikufanyie nini mpaka usuuzike, zaidi ya kukutoa bikra ya nyuma!!!
 
Tuipende na kuijenga nchi yetu kwa pamoja na umoja. Tusimsifu kiongozi anayetimiza wajibu wake kupita kiasi.
 
Hivi Rais ndio analeta sehemu maji?

Haya mambo ndio yanatufanya tushinikize katiba mpya

"UGATUZI" watu wapate maendeleo wanayoyataka kwa kupanga wenyewe sio kupangiwa na yeyote

Maana watu ndio walipa kodi sio mtu anaamka kisa yeye ni Rais anajenga uwanja wa ndege kwao na Hifadhi ya wanyama

Hivi wananchi wa Chato kipaumbele chao ni Uwanja wa ndege na Mbuga ya wanyama?
wewe ni mjinga na mpumbavu sana
 
Acha uzwazwa Rais asiposimamia kitu hakuna kitakachofanyika
Hivi Rais ndio analeta sehemu maji?

Haya mambo ndio yanatufanya tushinikize katiba mpya

"UGATUZI" watu wapate maendeleo wanayoyataka kwa kupanga wenyewe sio kupangiwa na yeyote

Maana watu ndio walipa kodi sio mtu anaamka kisa yeye ni Rais anajenga uwanja wa ndege kwao na Hifadhi ya wanyama

Hivi wananchi wa Chato kipaumbele chao ni Uwanja wa ndege na Mbuga ya wanyama?
 
Mipango ipo mingi tu tatizo utekelezaji.Ngosha aliwapiga BAO la kisigino kwa kuwa yeye alikuwa man of action.Mtamchukia lakini pengo hamtaliziba.Jamaa atabaki juu kama timu ya Italy.Mtasubiri sana
Yaani unamaanisha yule mwehu jambazi!
 
Back
Top Bottom