Amani Msumari
JF-Expert Member
- Aug 21, 2016
- 1,830
- 976
Wakuu, naomba nipendekeze kwenu kuwa vijana nao wapate nafasi ya kukutana na Rais Magufuli.
Awali ya yote napenda kuweka wazi kuwa mimi ni mwanachama wa CCM lakini mkutano huu hautahusu mambo ya chama bali mustakabali wa Tanzania kwa muono (perspective) ya vijana.
Pia natambua kuwa tuko kwenye mchakato wa uchaguzi lakini naamini Rais Magufuli ataibuka kidedea kutokana na upepo wa kampeni unavyoonekana hasa ukizangatia kazi alizozifanya.
Nataka nianze mchakato huu ili kusudi kwamba baadae uchaguzi ukishapita basi vijana nao kama yalivyopita makundi mengine nao wapate nafasi ya kuzungumza na Magufuli Kama Rais wao na baba hasa ukizangatia umri wake na umri wa vijana.
Ninaamini wapo vijana wenye uwezo mkubwa wa kiakili, maarifa, uzoefu na wenye mawazo chanya ambayo yatapata nafasi ya moja kwa moja kusikiwa na mkuu wa nchi. Tunaweza kuratibu mawazo hayo na kuhakikisha tunakuwa na ajenda za kueleweka ambazo zitajaa ushauri kwa Rais wetu.
Tunaweza kuorodhesha kero mbalimbali zinazotukabili kama vijana na kupendekeza masuluhisho yake mbele ya Rais. Binafsi naona Kama jambo hili linaweza kuwa la maana sana. Tafadhali toeni ushauri wenu ili tuweke nyama kwenye hili wazo halafu tuanze mikakati kwa pamoja.
Amani Msumari.
Tanga.
Awali ya yote napenda kuweka wazi kuwa mimi ni mwanachama wa CCM lakini mkutano huu hautahusu mambo ya chama bali mustakabali wa Tanzania kwa muono (perspective) ya vijana.
Pia natambua kuwa tuko kwenye mchakato wa uchaguzi lakini naamini Rais Magufuli ataibuka kidedea kutokana na upepo wa kampeni unavyoonekana hasa ukizangatia kazi alizozifanya.
Nataka nianze mchakato huu ili kusudi kwamba baadae uchaguzi ukishapita basi vijana nao kama yalivyopita makundi mengine nao wapate nafasi ya kuzungumza na Magufuli Kama Rais wao na baba hasa ukizangatia umri wake na umri wa vijana.
Ninaamini wapo vijana wenye uwezo mkubwa wa kiakili, maarifa, uzoefu na wenye mawazo chanya ambayo yatapata nafasi ya moja kwa moja kusikiwa na mkuu wa nchi. Tunaweza kuratibu mawazo hayo na kuhakikisha tunakuwa na ajenda za kueleweka ambazo zitajaa ushauri kwa Rais wetu.
Tunaweza kuorodhesha kero mbalimbali zinazotukabili kama vijana na kupendekeza masuluhisho yake mbele ya Rais. Binafsi naona Kama jambo hili linaweza kuwa la maana sana. Tafadhali toeni ushauri wenu ili tuweke nyama kwenye hili wazo halafu tuanze mikakati kwa pamoja.
Amani Msumari.
Tanga.