Tanzania ni tishio kwa kitu gani kwa nchi za africa mashariki?

Uganga, Tanzania mnatisha kwa uganga. Kenya kila eneo kuna mabango ya kupromote waganga toka sumbawanga, inaonekana mme specialize on this. Kenya pia wanatisha kwa utapeli, its not a good thing but I guess we are being honest here.
Kumbe Kenya mnatisha kwa kuwatumia waganga. It is an issue of Demand vs Supply:)
 
Hivi una akili kweli? Inamaanisha wachina hawana akili kisa hawajui kingereza katika ufundishaji wao? Kujua kingereza sio point ya kuangalia level ya elimu. Chunguza rank za elimu haziangalii lugha. Kila lugha ni bora hapa duniani. Angalia vitu kama idadi ya wanaojua kusoma na kuandika, idadi ya taasisi na maeneo husika ya kutoa elimu na hata sylabus ilivyo. Hongera Watanzania kwa kukitunza kiswahili na kukipa kipaumbele.
Sijawahi kuwa katika moja ya nchi za Afrika mashariki na kusikia raia wa nchi hizo wanatuogopa kwa vitu gani hasa.&lt;br /&gt;<br />
Sisi tunawagopa wakenya katika nyanja nyingi mfano elimu yao inatutisha balaa hasa jinsi wanavyoweza kuongea kiingereza kuzidi wabongo, kwa sababu wabongo kipimo chao cha elimu ni uwezo wa kuongea kiingereza.&lt;br /&gt;<br />
&lt;br /&gt;<br />
Wakenya pia wanatisha kwa ujanja wa kibiashara na wamekuwa wakijipatie mapato mengi kutokana na rasilimali zetu kama mlima kilimanjaro na Tanzanite hata babu wa Loliondo.&lt;br /&gt;<br />
&lt;br /&gt;<br />
Ukija kwa waganda, pia wanatutisha kwenye elimu na ujanja kiaina. Je sisi tunatisha kwa lipi?
&lt;br /&gt;<br />
&lt;br /&gt;
 
Kweli kabisa
Mi nadhani tunatisha zaidi kwenye sanaa hasa filamu kiukweli kwa afrika mashariki kifilamu tumekuja juu na ni tasnia inayokuja kwa kasi sana ukienda rwanda burundi uganda na hata kenya kwenyewe wanaisoma namba ingawa ndio kwaaaanza tumeanza
<br />
<br />
 
Jamani kiukweli...wanawake wa Tanzania ni wazuri Afrika mashariki. Yaani ni noma!
 
Tunatisha kwa kupenda starehe uliko kazi. kujiremba, usista duu,usharobaro, pamba kali lakini tunalala kwnye maboksi.
 
Sijawahi kuwa katika moja ya nchi za Afrika mashariki na kusikia raia wa nchi hizo wanatuogopa kwa vitu gani hasa.
Sisi tunawagopa wakenya katika nyanja nyingi mfano elimu yao inatutisha balaa hasa jinsi wanavyoweza kuongea kiingereza kuzidi wabongo, kwa sababu wabongo kipimo chao cha elimu ni uwezo wa kuongea kiingereza.

Wakenya pia wanatisha kwa ujanja wa kibiashara na wamekuwa wakijipatie mapato mengi kutokana na rasilimali zetu kama mlima kilimanjaro na Tanzanite hata babu wa Loliondo.

Ukija kwa waganda, pia wanatutisha kwenye elimu na ujanja kiaina. Je sisi tunatisha kwa lipi?

Living beyond our means
 
Sijui kwa nini watanzania wengi tunakuwa kama hatujiamini. Nimewahi kwa nyakati tofauti kufanya kazi na wakenya na wa uganda. Hawana cha ajabu na mambo mengine mimi ndio niliwaelekeza wao. Vua uoga wako na jiamini kwa kila unachokifanya. Hata wao kuna mambo mengi huwa hawajiamini na huwa wanatusifia sisi. Remember: Fear is nothing more than a monster you have created yourself,a negative stream of conciousness.
 
ni kweli.., ila mkuu bado najiuliza sana hilo.., mi nimekutana na watu wa nchi mbalimbali .., wasouth, nigeria., botswana., zimbabwe..etc cha kushangaza bado wanajua mt. kilimanjaro ipo Kenya.., ikabidi nipate kazi kidogo ya kuwaelimisha.., bahati nzuri kulikuwa na wakenya nashukuru na wao walinisaidia kusema upo TZ. napata wasiwasi kwamba bado watu wengi duniani wanajua upo Kenya.
 
itajulikana tu kuweni na subra ingawa upande wa sanaa tayari tume-take over
 
Seriously kwa Kenya na nchi zingine za EA tunawazidi kwa less tribalism. Kwa kweli pamoja na uozo uliojaa nchi hii bado tumejitahidi sana kwa kutokuwa na ukabila coz nackia huko Kenya utakuta wizara moja imejaa watu wa kabila moja 2, kitu ambacho kwa Tz hakipo.. Kenya hawatatushinda kwa hili . never!
 
Back
Top Bottom