Deogratias Mutungi
Senior Member
- Oct 1, 2019
- 136
- 178
Salaam wana JF,
Nianze andiko hili fupi kwa kusema Tanzania ni taifa imara kwa misingi ya siasa, uchumi, utamaduni na utawala bora, Tanzania kama yalivyo mataifa mengine ulimwengu tunayo misingi na taratibu za ndani za kuendesha shughuli zetu za kiutawala kulingana serikali iliyopo madarakani, Aidha Tanzania tunayo aina ya demokrasia yetu tunayoiishi katika kuendesha mambo yetu ya ndani.
Pia Tanzania kwa sasa tunaye kiongozi mwenye misimamo isiyoyumbishwa na mamluki kutoka aidha nje au ndani ya taifa letu, ni wazi kuwa Chuki kutoka mataifa makubwa zinaanzia hapa "kwenye dhana ya misimamo ya Mkuu wa nchi"
Viongozi wengi wa Afrika, Asia na Amerika ya mwambao wa Kaskazini Kusini wamechukiwa na kuwa maadui wa mataifa ya Ulaya na Marekani kwa sababu ya misimamo yao ya uzalendo kwa mataifa wanayoyaongoza, Kwa bahati mbaya mataifa haya yamekuwa na wasaliti wa ndani wanaoshiriki kuhujumu mataifa yao kwa maslahi yao binafsi, hata hiyo historia inaonyesha wasaliti ndani ya bara la Afrika wamekuwepo tangu karne ya kumi, Kwahiyo usaliti si jambo geni kwa Afrika.
Watanzania Juzi walipokea taarifa ya kamati ya Bunge la Ulaya wakihoji baadhi ya mambo, wapo waliofurahi na kushangilia mitandaoni kana kwamba wao si wananufaika na misaada ya walipa kodi wa Ulaya, Ukweli ni kwamba Mimi na wewe kwa kujua au kwa kutokujua tumekuwa wananufaika wa kodi ya wazungu kwa muda mrefu, Swali ni je wote wanaofurahia hoja iliyotolewa bungeni Juzi wanajitambua au hawajitambui kwamba na wao ni sehemu ya wanufaika ya kile kinachohojiwa?
Pengine nitajibiwa kwa mapana yake, Hata hivyo hoja ya Bunge ya EU inajibiwa kwa hoja, kwa sababu ni hoja ambayo imeibuliwa na upande wa pili una nafasi ya kujibu kwa mapana yake, Watanzania Kilichoongelewa juzi ni hoja na wala sio maazimio ya bunge aidha ni Hoja za kamati mojawapo kati ya kamati nyingi zinazounda bunge hilo, Rai yangu nikutanguliza uzalendo mbele na si Upotoshaji usio kuwa na Tija kwa taifa letu na vizazi vyetu vya sasa na hapo badae, Tuache ushabiki wenye kubomoa badala yake tuwe na ushabiki wenye kujenga taifa letu.
Nianze andiko hili fupi kwa kusema Tanzania ni taifa imara kwa misingi ya siasa, uchumi, utamaduni na utawala bora, Tanzania kama yalivyo mataifa mengine ulimwengu tunayo misingi na taratibu za ndani za kuendesha shughuli zetu za kiutawala kulingana serikali iliyopo madarakani, Aidha Tanzania tunayo aina ya demokrasia yetu tunayoiishi katika kuendesha mambo yetu ya ndani.
Pia Tanzania kwa sasa tunaye kiongozi mwenye misimamo isiyoyumbishwa na mamluki kutoka aidha nje au ndani ya taifa letu, ni wazi kuwa Chuki kutoka mataifa makubwa zinaanzia hapa "kwenye dhana ya misimamo ya Mkuu wa nchi"
Viongozi wengi wa Afrika, Asia na Amerika ya mwambao wa Kaskazini Kusini wamechukiwa na kuwa maadui wa mataifa ya Ulaya na Marekani kwa sababu ya misimamo yao ya uzalendo kwa mataifa wanayoyaongoza, Kwa bahati mbaya mataifa haya yamekuwa na wasaliti wa ndani wanaoshiriki kuhujumu mataifa yao kwa maslahi yao binafsi, hata hiyo historia inaonyesha wasaliti ndani ya bara la Afrika wamekuwepo tangu karne ya kumi, Kwahiyo usaliti si jambo geni kwa Afrika.
Watanzania Juzi walipokea taarifa ya kamati ya Bunge la Ulaya wakihoji baadhi ya mambo, wapo waliofurahi na kushangilia mitandaoni kana kwamba wao si wananufaika na misaada ya walipa kodi wa Ulaya, Ukweli ni kwamba Mimi na wewe kwa kujua au kwa kutokujua tumekuwa wananufaika wa kodi ya wazungu kwa muda mrefu, Swali ni je wote wanaofurahia hoja iliyotolewa bungeni Juzi wanajitambua au hawajitambui kwamba na wao ni sehemu ya wanufaika ya kile kinachohojiwa?
Pengine nitajibiwa kwa mapana yake, Hata hivyo hoja ya Bunge ya EU inajibiwa kwa hoja, kwa sababu ni hoja ambayo imeibuliwa na upande wa pili una nafasi ya kujibu kwa mapana yake, Watanzania Kilichoongelewa juzi ni hoja na wala sio maazimio ya bunge aidha ni Hoja za kamati mojawapo kati ya kamati nyingi zinazounda bunge hilo, Rai yangu nikutanguliza uzalendo mbele na si Upotoshaji usio kuwa na Tija kwa taifa letu na vizazi vyetu vya sasa na hapo badae, Tuache ushabiki wenye kubomoa badala yake tuwe na ushabiki wenye kujenga taifa letu.