Buchanan
JF-Expert Member
- May 19, 2009
- 13,199
- 1,969
Jamani tuache utani, watanzania ni watu "wazuri" na nchi yao pia ni nzuri sana! Kwa nini?
1. Mbunge akiona hajafanya chochote ndani ya kipindi cha miaka 4 anarudi mwaka wa tano na kuwaahidi kwamba atafanya makubwa, watanzania kwa jinsi walivyo "wazuri" wanampa kura.
2. Rais alitoa ahadi nyingi sana na kama angezitekeleza Tanzania ingekuwa nchi inayotiririka "asali na maziwa,"lakini mimi sina uhakika kama ametekeleza hata moja, mwaka huu mwezi Oktoba Rais akiomba kura utashangaa watanzania walivyo "wazuri" watampa kura!
3. Wageni toka nje wanakuja nchini kwetu wanachota vijisenti kupitia mikataba mibovu, watanzania walivyo "wazuri" wananung'unika siku mbili tatu, kisha mkubwa wao anawaahidi kuunda Litume la kupitia mikataba mibovu. Mkubwa akiona watanzania "wazuri" wameshatulia basi anaweka likarabrasha kwenye shelf!
4. Mkubwa akisoma hotuba Bungeni kwamba eti kuna wezi wamerudisha vijisenti walivyoiba bila kuwataja wezi wenyewe! Watanzania "wazuri" walinung'unika kichini chini lakini wakaahidiwa kwamba vijisenti hivyo vitawekwa kwenye Benki yao ya Raslimali bila hata kuridhiwa na Bunge! Watanzania "wazuri" wakaridhika na mpaka sasa haijulikani kwamba vijisenti hivyo viliwekwa huko na kama wakulima walifaidika au la! Hata kama ikitokea walifaidika, wezi wasio na majina walifanywa nini?
5. Ama kweli Tanzania ni nchi "nzuri," ndio maana hata Rwanda, Burundi, Uganda na Kenya wanakomalia sana Jumuiya ya Afrika Mashariki (yaani kuwa nchi moja) kwa sababu wanajua "uzuri" wa Tanzania na Watanzania!
6...........................
7..........................
8..........................
Mungu Ibariki Tanzania, Mungu Wabariki Watanzania!
1. Mbunge akiona hajafanya chochote ndani ya kipindi cha miaka 4 anarudi mwaka wa tano na kuwaahidi kwamba atafanya makubwa, watanzania kwa jinsi walivyo "wazuri" wanampa kura.
2. Rais alitoa ahadi nyingi sana na kama angezitekeleza Tanzania ingekuwa nchi inayotiririka "asali na maziwa,"lakini mimi sina uhakika kama ametekeleza hata moja, mwaka huu mwezi Oktoba Rais akiomba kura utashangaa watanzania walivyo "wazuri" watampa kura!
3. Wageni toka nje wanakuja nchini kwetu wanachota vijisenti kupitia mikataba mibovu, watanzania walivyo "wazuri" wananung'unika siku mbili tatu, kisha mkubwa wao anawaahidi kuunda Litume la kupitia mikataba mibovu. Mkubwa akiona watanzania "wazuri" wameshatulia basi anaweka likarabrasha kwenye shelf!
4. Mkubwa akisoma hotuba Bungeni kwamba eti kuna wezi wamerudisha vijisenti walivyoiba bila kuwataja wezi wenyewe! Watanzania "wazuri" walinung'unika kichini chini lakini wakaahidiwa kwamba vijisenti hivyo vitawekwa kwenye Benki yao ya Raslimali bila hata kuridhiwa na Bunge! Watanzania "wazuri" wakaridhika na mpaka sasa haijulikani kwamba vijisenti hivyo viliwekwa huko na kama wakulima walifaidika au la! Hata kama ikitokea walifaidika, wezi wasio na majina walifanywa nini?
5. Ama kweli Tanzania ni nchi "nzuri," ndio maana hata Rwanda, Burundi, Uganda na Kenya wanakomalia sana Jumuiya ya Afrika Mashariki (yaani kuwa nchi moja) kwa sababu wanajua "uzuri" wa Tanzania na Watanzania!
6...........................
7..........................
8..........................
Mungu Ibariki Tanzania, Mungu Wabariki Watanzania!