11. Tunambiwa na JK kwamba ana mpango kabambe wa kujenga fly-overs Dar ili kupunguza foleni, wakati barabara zilizopo tu ni mbovu na finyu. Badala ya kumwambia akarabati na kupanua kwanza zilizopo, tunampigia makofi na kumpa kura tena 2010.
12. Tunajengewa shule za sekondari za Kata zilizotoa wanafunzi 65,000 wenye divisheni ZIRO kisha serikali inaripoti UNDP kwamba school enrolment imepanda, bila kuzingatia wanafunzi hao wanapata elimu gani na katika mazingira yepi....!
13.Anatokea kiongozi mwingine anawafananisha watanzania na mbuzi eti hata wakila majani poa tu ilimradi rada inunuliwe na watanzania walivyopoa wanasema sawa baba kwani kuwa mbuzi,kondoo etc kitu gani...kesho akiomba kura watampa aendelee kuwaita mbuzi wao poa tu...
15. Bunge lina hairishwa kirahisirahisi tu eti kamati azija jiridhisha kuwa ripoti zimekamilika, walikuwa wapi miaka yote mbona kila kikao ni hivi?
Naibu spika anasema muda auta ongezwa kwahiyo hizo ripoti azina nafasi tena tusubiri kikao kijacho cha bunge
Jamani tuache utani, watanzania ni watu "wazuri" na nchi yao pia ni nzuri sana! Kwa nini?
1. Mbunge akiona hajafanya chochote ndani ya kipindi cha miaka 4 anarudi mwaka wa tano na kuwaahidi kwamba atafanya makubwa, watanzania kwa jinsi walivyo "wazuri" wanampa kura.
2. Rais alitoa ahadi nyingi sana na kama angezitekeleza Tanzania ingekuwa nchi inayotiririka "asali na maziwa,"lakini mimi sina uhakika kama ametekeleza hata moja, mwaka huu mwezi Oktoba Rais akiomba kura utashangaa watanzania walivyo "wazuri" watampa kura!
3. Wageni toka nje wanakuja nchini kwetu wanachota vijisenti kupitia mikataba mibovu, watanzania walivyo "wazuri" wananung'unika siku mbili tatu, kisha mkubwa wao anawaahidi kuunda Litume la kupitia mikataba mibovu. Mkubwa akiona watanzania "wazuri" wameshatulia basi anaweka likarabrasha kwenye shelf!
4. Mkubwa akisoma hotuba Bungeni kwamba eti kuna wezi wamerudisha vijisenti walivyoiba bila kuwataja wezi wenyewe! Watanzania "wazuri" walinung'unika kichini chini lakini wakaahidiwa kwamba vijisenti hivyo vitawekwa kwenye Benki yao ya Raslimali bila hata kuridhiwa na Bunge! Watanzania "wazuri" wakaridhika na mpaka sasa haijulikani kwamba vijisenti hivyo viliwekwa huko na kama wakulima walifaidika au la! Hata kama ikitokea walifaidika, wezi wasio na majina walifanywa nini?
5. Ama kweli Tanzania ni nchi "nzuri," ndio maana hata Rwanda, Burundi, Uganda na Kenya wanakomalia sana Jumuiya ya Afrika Mashariki (yaani kuwa nchi moja) kwa sababu wanajua "uzuri" wa Tanzania na Watanzania!
6...........................
7..........................
8..........................
Mungu Ibariki Tanzania, Mungu Wabariki Watanzania!