Tanzania ni laana au viongozi?

Mkombozi

JF-Expert Member
Feb 19, 2008
805
425
Ninaangalia taarifa ya habari ya ITV,Libya imeendelea sana.Miundombinu safi,maji n.k.Libya ipo kwenye jangwa ila Tanzania licha ya rasilimali zote bado tunasuasua.Nimeumia sana.Jiji la Dar tu linawashinda viongozi,Je ni laana au ni viongozi?
 
Yaani umeniwahi mtu wangu! na mimi nilikuwa naandaa posti kama yako.
Hivi imagene nchi kama Egipty na Libya ni jangwa la kufa mtu kila kona,lakini
wanaumeme kibao na maji ya kumwaga kila pembe ya nchi zao. Cha kushangaza
hapa kwetu pamoja na vianzilishi vyote hivyo vya nishati tulivyokuwanavyo.
Yaani aibu tupu
 
Ninaangalia taarifa ya habari ya ITV,Libya imeendelea sana.Miundombinu safi,maji n.k.Libya ipo kwenye jangwa ila Tanzania licha ya rasilimali zote bado tunasuasua.Nimeumia sana.Jiji la Dar tu linawashinda viongozi,Je ni laana au ni viongozi?

Walishatuambia "nchi haina rasilimali!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!" hivi waseme mara ngapi ndipo tujue:

Wamesahau wakati tunasoma walituimbisha "ili tuendelee tunahitaji mambo manne "WATU, ARDHI, SIASA SAFI na UONGOZI BORA" hapo hapakuwa pakitajwa RASILIMALI kwa sababu zilikuwapo... sasa sijui zimeenda wapi baada ya miaka michache tu :embarrassed: (yaani wanatuaminisha "hakuna madini, hakuna mbuga za wanyama, hakuna samaki, ardhi yetu haina tija, bandari yetu iko kama pambo.. na.. na... na.... na.... wizi mtupu!
hapana sio laana TUMIROGWA
 
Libya wana petro-dollar wewe... Nyie uchumi wenu wa kuuza korosho, viazi, mchele, dhahabu na bongo fleva... Sio kwamba hatuna raslimali, lakini mafuta is a game changer... subiri uone Kampala baada ya miaka 10. Mafuta ogopa, yanaendesha uchumi wa dunia. Pamba na korosho hamna kitu..
 
Libya wana petro-dollar wewe... Nyie uchumi wenu wa kuuza korosho, viazi, mchele, dhahabu na bongo fleva... Sio kwamba hatuna raslimali, lakini mafuta is a game changer... subiri uone Kampala baada ya miaka 10. Mafuta ogopa, yanaendesha uchumi wa dunia. Pamba na korosho hamna kitu..
Mbona Nigeria wana mafuta lakini ni choka mbaya?
 
Rasilimali tunazo za kutosha mkuu, ndo maana hata katika bendera yetu tuna rangi ya njano denoting rasilimali, tatizo kubwa tulilonalo ni utatu wa nafsi za viongozi wetu, yaani (I, Me and My self) nafsi zake hizo tatu zikishiba ndo afanye kazi aliyokabidhiwa. Simply naweza kusema tatizo letu ni ukosefu wa utawala bora
 
Rasilimali tunazo za kutosha mkuu, ndo maana hata katika bendera yetu tuna rangi ya njano denoting rasilimali, tatizo kubwa tulilonalo ni utatu wa nafsi za viongozi wetu, yaani (I, Me and My self) nafsi zake hizo tatu zikishiba ndo afanye kazi aliyokabidhiwa. Simply naweza kusema tatizo letu ni ukosefu wa utawala bora

Rasilimali bila ingenuity ni good for nothing.
 
Libya wana petro-dollar wewe... Nyie uchumi wenu wa kuuza korosho, viazi, mchele, dhahabu na bongo fleva... Sio kwamba hatuna raslimali, lakini mafuta is a game changer... subiri uone Kampala baada ya miaka 10. Mafuta ogopa, yanaendesha uchumi wa dunia. Pamba na korosho hamna kitu..

Nigeria hadi wamezalisha waasi wenye uchungu na mafuta huko Niger Delta.
Upuuzi wa viongozi wa Tz nikukimbilia kuuza kila kitu eti uwekezaji. Mwishowe wanamiliki mali yetu na wanapata tax holiday.
Na mie nimeangalia Libya. Watawala wetu hawana uzalendo na sisi tunatatizo la utii na ukondoo. Angalia swala la Dowans, tumefanya nin wananchi baada ya kupata habari?
 
Kiini cha matatizo makubwa kwa maendeleo ya Tanzania ni viongozi na si laana; kama ni laana basi ni y akuwachagua greedy leaders; hakuna lingine. Hakuna mipango ya kumwendeleza common person, whatever little we we have is used extravagantly by leaders you live spendthrift lives, yaani viongozi wetu hawangaike nini wakati wao wanaishi maisha as if they are not in Tanzania, they live even better than some people in the developed countries, they determine their own salaries and benefits, they squander what belong to the people, hivi hatuoni hata hiyo extreme difference between common man and the leaders and their business allies? Jamani hata sisi tunaruhusu maana ndio tunaopigania kwa hali n amali ili kuwarudisha madarakani those who rip us so much, tutamaka lini, tutaendelea tu kulalama umaskini umaskini wakati na sisi tuna-authorize? Tujifikirie na kufikiria vizazi vyetu vijavyo, kama wataishi katika umaskini somehow na sisi tume-contribute....what legacy are we leaving behind for our children and our children's children?
 
Ninaangalia taarifa ya habari ya ITV,Libya imeendelea sana.Miundombinu safi,maji n.k.Libya ipo kwenye jangwa ila Tanzania licha ya rasilimali zote bado tunasuasua.Nimeumia sana.Jiji la Dar tu linawashinda viongozi,Je ni laana au ni viongozi?


Kama hali ndiyo hii kuna haja gani ya kuexperience socialism? Bora udikteta kama kule kwa kamanda gaddafi.

Tatizo la viongozi wa bongo ni kwamba wao wanatanguliza maslahi yao badala ya taifa. Hakuna mwenye fikra chanya, wote hasi tupu. Hebu 2015 tumpe Slaa hii nchi kama hatujawa kama libya sijui.
 
Kiini cha matatizo makubwa kwa maendeleo ya Tanzania ni viongozi na si laana; kama ni laana basi ni y akuwachagua greedy leaders; hakuna lingine. Hakuna mipango ya kumwendeleza common person, whatever little we we have is used extravagantly by leaders you live spendthrift lives, yaani viongozi wetu hawangaike nini wakati wao wanaishi maisha as if they are not in Tanzania, they live even better than some people in the developed countries, they determine their own salaries and benefits, they squander what belong to the people, hivi hatuoni hata hiyo extreme difference between common man and the leaders and their business allies? Jamani hata sisi tunaruhusu maana ndio tunaopigania kwa hali n amali ili kuwarudisha madarakani those who rip us so much, tutamaka lini, tutaendelea tu kulalama umaskini umaskini wakati na sisi tuna-authorize? Tujifikirie na kufikiria vizazi vyetu vijavyo, kama wataishi katika umaskini somehow na sisi tume-contribute....what legacy are we leaving behind for our children and our children's children?

Sasa kwa nini kila mwaka wa uchaguzi wanachaguliwa viongozi wale wale ambao kwa kweli kazi waifanyayo hata haonekani.
 
Rasilimali bila ingenuity ni good for nothing.

Na hiki ndicho kitakuwa kifo chetu waafrika, wakati wenzetu wanashikilia zaidi kuwa na akili za ku control vitu, kiasi hata sisi wenye rasilimali tunapangiwa bei nao, wenye dhahabu tunawaita wao watuchimbie, sis tunaishia kukodolea macho rasilimali.

Kuna balozi mmoja nafikiri wa Ujerumani yule nchini Tanzania, kuna siku ilibidi aweke diplomasia pembeni na kuwapa wabongo kitu na boksi, akawaambia kuna siku rasilimali zenu zitaisha hizi, inabidi muanze kujipanga kuunda uchumi ulio complex zaidi kuliko kutegemea rasilimali tu.

Bei za rasilimali kiujumla zimekuwa zikishuka kwa miaka 30 iliyopita, kuna siku wenzetu wataweza kutengeneza kila rasilimali yetu tunayoringia kwenye lab, sijui tutauza nini.
 
Na hiki ndicho kitakuwa kifo chetu waafrika, wakati wenzetu wanashikilia zaidi kuwa na akili za ku control vitu, kiasi hata sisi wenye rasilimali tunapangiwa bei nao, wenye dhahabu tunawaita wao watuchimbie, sis tunaishia kukodolea macho rasilimali.

Kuna balozi mmoja nafikiri wa Ujerumani yule nchini Tanzania, kuna siku ilibidi aweke diplomasia pembeni na kuwapa wabongo kitu na boksi, akawaambia kuna siku rasilimali zenu zitaisha hizi, inabidi muanze kujipanga kuunda uchumi ulio complex zaidi kuliko kutegemea rasilimali tu.

Bei za rasilimali kiujumla zimekuwa zikishuka kwa miaka 30 iliyopita, kuna siku wenzetu wataweza kutengeneza kila rasilimali yetu tunayoringia kwenye lab, sijui tutauza nini.

I'm glad you see it that way kwa sababu mimi nimeuimba sana huu wimbo tokea bcstimes.com lakini ni wachache sana wanaonielewa.
 
Mbona Nigeria wana mafuta lakini ni choka mbaya?
Je kanchi kama Rwanda? Tazameni kanavyokwenda mbio. huwezi amini Kigali ya leo kama ndio iliyosambaratishwa na vita! Ukija baadhi ya maeneo ya Dar ndipo unaweza kudhani ile vita ya kule ilipiganwa! Rasilimali hatuna!!! Kweli nakubali Tanzania hakuna rasilimali, ila WANASIASA WA TANZANIA WANAZO RASILIMALI BINAFSI... Hivi mbona huwa hawazitangazi mali zao wanachoogopa ni nini? Vijisenti au?
 
Libya wana petro-dollar wewe... Nyie uchumi wenu wa kuuza korosho, viazi, mchele, dhahabu na bongo fleva... Sio kwamba hatuna raslimali, lakini mafuta is a game changer... subiri uone Kampala baada ya miaka 10. Mafuta ogopa, yanaendesha uchumi wa dunia. Pamba na korosho hamna kitu..


I oppose u somehow u skipped something, petrodollars is not enough itself for development, it can cause even worst ever
situation in the country na ushahidi upo, eg NIGER DELTA IN NIGERIA, iraq, so kitu kikubwa sana hapa ni GOOD GOVERNANCE, THEN NDIO IJE RESOURCES kama mafuta, madini, wanyama pori ( tourism), fishing, bandari, mazao ya kilimo, viwanda vya ndani nk, narudia UONGOZI BORA, UONGOZI BORA UONGOZI BORA maana ukisema once watu hawaelewi,
ww shahidi na uchafu mwingi which is evidence of poor governance.
 
There can be no real individual freedom in the presence of economic insecurity.
 
Libya wana petro-dollar wewe... Nyie uchumi wenu wa kuuza korosho, viazi, mchele, dhahabu na bongo fleva... Sio kwamba hatuna raslimali, lakini mafuta is a game changer... subiri uone Kampala baada ya miaka 10. Mafuta ogopa, yanaendesha uchumi wa dunia. Pamba na korosho hamna kitu..

Nigeria wanamafuta,Angola wanamafuta na bado taabu tupu ,johansberg ilijengwa kwa dhahabu sisi tunadhabu bado mukichwa hakuna akili ya kuendelea eeh bana jaribu kuwa mkweli viongozi wetu ni vilaza full stop
 
Nigeria wanamafuta,Angola wanamafuta na bado taabu tupu ,johansberg ilijengwa kwa dhahabu sisi tunadhabu bado mukichwa hakuna akili ya kuendelea eeh bana jaribu kuwa mkweli viongozi wetu ni vilaza full stop

Viongozi wetu wanatoka miongoni mwetu sisi wenyewe na ni sisi wenyewe ndiyo tunawapa hiyo dhamana ya kutuongoza. Kwa hiyo viongozi wetu wanaakisi jamii nzima waiongozayo. Sasa kwa kufuata mantiki hiyo utaona kuwa viongozi wetu kama ni vilaza basi na sisi ni vilaza vile vile.
 
Kichwa cha thread tu kinatuonyesha tatizo linaanza wapi, hata kwa wanaonuia kuubana uongozi.

Wewe mtu enzi hii ya sayansi na teknolojia bado unaamini kuna laana tu ?

Laana ni nini ? Inatumia media gani kuwa transmitted ? Inapatikana kwenye frequencies zipi? Inaambukizwa kwa vijidudu kama bacteria na virus au inapatikanaje ?
 

Similar Discussions

0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom