Herbalist Dr MziziMkavu
JF-Expert Member
- Feb 3, 2009
- 42,314
- 33,108
Tanzania inaongoza kwa kutoa misamaha mikubwa zaidi ya kodi ikilinganishwa na nchi nyingine za Afrika Mashariki pamoja na bajeti yake kuwa tegemezi kwa misaada ya nje kwa zaidi ya asilimia 30.
Taarifa hiyo ilitolewa jana jijini Dar es Salaam na Rose Aiko, mchambuzi wa utafiti toka Uwazi (Pata
picha kamili) alipokuwa akiwasilisha muhtasari wa utafiti uliofanywa na taasisi isiyo ya kiserikali ya Uwazi-Twaweza kuhusiana na misamaha ya kodi Tanzania.
Aiko alisema kiwango cha misamaha ya kodi inayotolewa Tanzania ni kikubwa ukilinganisha na misamaha inayotolewa na nchi za Uganda na Kenya.
Hapa kwetu, kati ya miaka ya 2005/06 na 2007/08, misamaha ya kodi ilikadiriwa kuwa wastani wa asilimia 3.9 ya pato la taifa. Mwaka 2008/09, ilikuwa asilimia 2.8 na mwaka 2009/10 asilimia 2.3, alisema.
Aiko alieleza wakati hali iko hivyo nchini, misamaha ya kodi katika kipindi chote hicho kwa Kenya ilikuwa ni asilimia moja ya pato la Taifa na kwa Uganda ilikuwa ni asilimia 0.4.
Alisema ukiachilia mbali Uganda ambayo inatoa misamaha kwa kiwango cha chini kabisa, kama
Tanzania ingerekebisha viwango vya misamaha ya kodi ili kulingana na kiwango kilichofikiwa na Kenya, zaidi ya Sh. bilioni 600 zingeokolewa kwa mwaka 2007/08 peke yake.
Aidha, Aiko alisema ukubwa wa kiwango cha misamaha inayotolewa unaweza kuelezwa kwa
kulinganisha na malengo ya ukusanyaji wa mapato ya kodi ambayo Tanzania inashindwa kuyafikia.
Mwaka 2008/09 na 2009/10, Serikali haikutimiza lengo lake la kukusanya mapato kwa wastani wa Sh. bilioni 453 kila mwaka. Katika kipindi hicho hicho, misamaha ya kodi iliyotolewa ilifikia wastani wa Sh. bilioni 724 kwa mwaka, alisema. Alisema kama misamaha ya kodi ingetolewa katika kiwango
kinachofanana na kiwango cha misamaha ya kodi inayotolewa Kenya, Sh. bilioni 484 zingeokolewa mwaka 2008/9 na Sh. bilioni 302 mwaka 2009/10.
Kwa maneno mengine, upungufu katika ukusanyaji wa mapato ungepunguzwa kwa kiasi kikubwa, alifafanua.
Kadhalika, Aiko alieleza kuwa wawekezaji wakubwa wa kimataifa nchini wananufaika zaidi na misamaha ya kodi kuliko makundi mengine yanayopata misamaha hiyo.
Alisema makampuni hayo ni yale yenye vyeti vya kupatiwa motisha vinavyotolewa chini ya sheria ya uwekezaji Tanzania na sheria ya kuendeleza na kulinda uwekezaji Zanzibar, ambayo yanapata misamaha inayofikia asilimia 45.12.
Kundi linalofuata ni la walipaji kodi ya Ongezeko la Thamani (VAT) chini ya vifungu namba 220,223 na 224 ambalo linapata misamaha ya asilimia 24.22 na kundi la tatu ni la makampuni ya madini, chini ya Sheria ya Madini, alisema Aiko.
Akijibu swali la NIPASHE lililohusu sababu za kufanya utafiti kama huu na kuutoa siku chache kabla ya uchaguzi, Mkurugenzi Mkuu wa Twaweza, Rakesh Rajani, alisema wao kama taasisi hawafungwi na muda wa kueleza walichonacho.
Sisi kama taasisi tunafanya tafiti nyingi. Tuliona umuhimu wa kufanya tafiti za misamaha ya kodi ili wananchi waone kama kutolewa kwa misamaha hiyo kuna ulazima kwa nchi inayokabiliwa na changamoto ya kukusanya fedha za kutosha kugharimia bajeti yake, alisema.
Alisema utafiti wao umetumia takwimu za ripoti ya mapato kutoka Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) na wameyatoa matokeo ya utafiti huo sasa ili Watanzania waelewe kuhusiana na rasilimali zao na wakapige kura wakiwa na ufahamu huo.
CHANZO: NIPASHE
Taarifa hiyo ilitolewa jana jijini Dar es Salaam na Rose Aiko, mchambuzi wa utafiti toka Uwazi (Pata
picha kamili) alipokuwa akiwasilisha muhtasari wa utafiti uliofanywa na taasisi isiyo ya kiserikali ya Uwazi-Twaweza kuhusiana na misamaha ya kodi Tanzania.
Aiko alisema kiwango cha misamaha ya kodi inayotolewa Tanzania ni kikubwa ukilinganisha na misamaha inayotolewa na nchi za Uganda na Kenya.
Hapa kwetu, kati ya miaka ya 2005/06 na 2007/08, misamaha ya kodi ilikadiriwa kuwa wastani wa asilimia 3.9 ya pato la taifa. Mwaka 2008/09, ilikuwa asilimia 2.8 na mwaka 2009/10 asilimia 2.3, alisema.
Aiko alieleza wakati hali iko hivyo nchini, misamaha ya kodi katika kipindi chote hicho kwa Kenya ilikuwa ni asilimia moja ya pato la Taifa na kwa Uganda ilikuwa ni asilimia 0.4.
Alisema ukiachilia mbali Uganda ambayo inatoa misamaha kwa kiwango cha chini kabisa, kama
Tanzania ingerekebisha viwango vya misamaha ya kodi ili kulingana na kiwango kilichofikiwa na Kenya, zaidi ya Sh. bilioni 600 zingeokolewa kwa mwaka 2007/08 peke yake.
Aidha, Aiko alisema ukubwa wa kiwango cha misamaha inayotolewa unaweza kuelezwa kwa
kulinganisha na malengo ya ukusanyaji wa mapato ya kodi ambayo Tanzania inashindwa kuyafikia.
Mwaka 2008/09 na 2009/10, Serikali haikutimiza lengo lake la kukusanya mapato kwa wastani wa Sh. bilioni 453 kila mwaka. Katika kipindi hicho hicho, misamaha ya kodi iliyotolewa ilifikia wastani wa Sh. bilioni 724 kwa mwaka, alisema. Alisema kama misamaha ya kodi ingetolewa katika kiwango
kinachofanana na kiwango cha misamaha ya kodi inayotolewa Kenya, Sh. bilioni 484 zingeokolewa mwaka 2008/9 na Sh. bilioni 302 mwaka 2009/10.
Kwa maneno mengine, upungufu katika ukusanyaji wa mapato ungepunguzwa kwa kiasi kikubwa, alifafanua.
Kadhalika, Aiko alieleza kuwa wawekezaji wakubwa wa kimataifa nchini wananufaika zaidi na misamaha ya kodi kuliko makundi mengine yanayopata misamaha hiyo.
Alisema makampuni hayo ni yale yenye vyeti vya kupatiwa motisha vinavyotolewa chini ya sheria ya uwekezaji Tanzania na sheria ya kuendeleza na kulinda uwekezaji Zanzibar, ambayo yanapata misamaha inayofikia asilimia 45.12.
Kundi linalofuata ni la walipaji kodi ya Ongezeko la Thamani (VAT) chini ya vifungu namba 220,223 na 224 ambalo linapata misamaha ya asilimia 24.22 na kundi la tatu ni la makampuni ya madini, chini ya Sheria ya Madini, alisema Aiko.
Akijibu swali la NIPASHE lililohusu sababu za kufanya utafiti kama huu na kuutoa siku chache kabla ya uchaguzi, Mkurugenzi Mkuu wa Twaweza, Rakesh Rajani, alisema wao kama taasisi hawafungwi na muda wa kueleza walichonacho.
Sisi kama taasisi tunafanya tafiti nyingi. Tuliona umuhimu wa kufanya tafiti za misamaha ya kodi ili wananchi waone kama kutolewa kwa misamaha hiyo kuna ulazima kwa nchi inayokabiliwa na changamoto ya kukusanya fedha za kutosha kugharimia bajeti yake, alisema.
Alisema utafiti wao umetumia takwimu za ripoti ya mapato kutoka Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) na wameyatoa matokeo ya utafiti huo sasa ili Watanzania waelewe kuhusiana na rasilimali zao na wakapige kura wakiwa na ufahamu huo.
CHANZO: NIPASHE