‘Tanzania ni bora duniani kwa umeme wa nguvu ya upepo’

Rutashubanyuma

JF-Expert Member
Sep 24, 2010
219,470
911,173
‘Tanzania ni bora duniani kwa umeme wa nguvu ya upepo’
Tuesday, 18 January 2011 21:40

Leon Bahati
WATAALAMU wa nishati toka nchini Norway wamefanya utafiti na kubaini kwamba Tanzania ni miongoni mwa nchi chache duniani ambazo zina mazingira bora zaidi ya kuzalisha umeme wa nguvu ya upepo.

Katika hali hiyo, wakaitaka serikali ianze kufanya maandalizi ya kuwekeza kwenye miradi ya uzalishaji wa umeme wa nguvu ya upepo ili kutatua tatizo sugu la nishati hiyo nchini.

Matokeo ya utafiti huo ni habari njema kwa Watanzania ambao kwa zaidi ya mwezi mmoja sasa wamekuwa wakikabiliwa na makali ya mgawo wa umeme, huku Shirika la Umeme Tanzania (Taesco) likiongeza gharama za nishati hiyo kwa asilimia 18. Mgawo wa umeme ni kama tatizo sugu nchini kwani limedumu kwa zaidi ya miaka mitano likijitokeza kwa vipindi na nyakati tofauti.

Mwishoni mwa mwaka jana Shirika la Maendeleo la Taifa (NDC), lilingia ubia na Kampuni ya Power Pool East Africa kuzalisha umeme wa upepo mkoani Singida utakaogharimu zaidi ya Sh180 bilioni.

Naibu Waziri wa Viwanda, Biashara na Masoko, Lazaro Nyalandu, alisema tayari makubaliano yamesainiwa na NDC na kwamba, serikali itakuwa ikimiliki asilimia 51 ya hisa na nyingine zitakuwa za mwekezaji.

Nyalandu alisema mradi huo utakuwa wa gharama nafuu katika uzalishaji utaingizwa kwenye gridi ya taifa na kwamba, kwa kuanzia zitazalishwa megawati 50 na baadaye zitaongezwa kulingana na uwezo wa wabia hao.

Kwa upande wao wataalamu kutoka nchini Norway jana waliwasilisha kwa serikali ripoti inayoonyesha nia yao ya kuwekeza kwenye mradi wa kuzalisha umeme wa nguvu ya upepo eneo la Makambako, mkoani Iringa kupitia kampuni ya Sino Tan ambayo imekusudia kuzalisha megawati 100.

Akizungumza kwa niaba ya wataalamu wenzake, Meneja wa Kampuni ya Norsk Vind Energy ya Norway, Torstein Ekern alisema Tanzania ina mazingira bora zaid ya uwekezaji katika eneo hilo ikilinganishwa na nchi kama Urusi na Bulgaria ambako pia wamewekeza.

“Tumewekeza sehemu mbalimbali duniani kama vile Urusi na Bulgaria lakini utafiti inaonyesha mradi wa Tanzani ndio utakaokuwa bora zaidi,” alisema Ekern.

Kuhusu namna utafiti huo ulivyoendesha, Mwenyekiti wa Kampuni ya Sino Tan, Alex Lema alisema waliuanza mwaka 2003 wilaya ya Same kwa miaka mitatu na baadaye kwa miaka sita Makambako.

Akasema wameamua kuwekeza Makambako kwa sababu wamebaini kuwa upepo wa kutosha kwa uzalishaji unavuma kwa mwaka mzima na kipindi cha kiangazi ambacho mara nyingi ni wakati Tanzania inakuwa na tatizo la umeme, ndipo unakuwa na kasi kubwa zaidi.

“Kwa hiyo unaweza kuona kile kipindi cha ukame, ambacho mabwawa yetu yanayotuzalishia umeme yanakuwa yamekauka na kusababisha tukose umeme, ndicho ambacho mradi wetu unaweza kuzalisha zaidi kwa sababu nguvu ya upepe unakuwa mkubwa,” alisema Lema.

Sino Tan iliwasilisha ripoti hiyo kwa serikali ili ipate kibali cha kuzalisha umeme huo mapema iwezekanavyo.

Iwapo serikali itakubali ombi lao, Lema alisema hatua inayofuata ni kufanya mazungumzo na Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco) pamoja na Mamlaka ya Kudhibiti Huduma za Nishati na Maji (Ewura) ili kuingia mkataba wa kununua megawati 100 za umeme watakaozalisha.
 
Iuf you believe this then you are doomed and you will believe anything............................................Nchi zote duniani hususani Afrika zina upepo wa kutosha na hakuna sababu ya kuikuza sana Tanzania kama ilivyobainishwa hapa.....................
 
Wasikimbilie kusaini mikataba,waisome kwanza ilikuepuka yaliyotokea kwa dowans ,richmond,iptl na ya zakia meghji kusema alidanganywa kumbe kusoma na kutafsiri sheria inahitaji elimu na ujuzi wakutosha.watumike wanasheria wazalendo sio kina nimrod mkono.itatusaidia sana kwani umeme wa upepo hauhitaji malighafi kama mafuta yenye gharama nyingi.
 
Wasikimbilie kusaini mikataba,waisome kwanza ilikuepuka yaliyotokea kwa dowans ,richmond,iptl na ya zakia meghji kusema alidanganywa kumbe kusoma na kutafsiri sheria inahitaji elimu na ujuzi wakutosha.watumike wanasheria wazalendo sio kina nimrod mkono.itatusaidia sana kwani umeme wa upepo hauhitaji malighafi kama mafuta yenye gharama nyingi.


Umenena vyema hawakawii kutupauka mbele ya safari!
 
Iuf you believe this then you are doomed and you will believe anything............................................Nchi zote duniani hususani Afrika zina upepo wa kutosha na hakuna sababu ya kuikuza sana Tanzania kama ilivyobainishwa hapa.....................

imagine ni nchi bora kwa umeme wa upuepo then wana taka kuzalisha megawat 50- 100 this is a joke, nilitegemea watazalisha 10,000mW
 
Huu ni uongop mwingine unaotungwa ili tuipende nchi yeti huku wengine wakiifaidi. .Kwa Africa Tanzania haimo. Haya ndio yale mambo ya zamani Tanzania inaongoza kwa kila kitu duniani. Uongo mtupu!
Nchi bora kwa wind power hizi hapa
Where's the best place for wind power? | eBoom Contributor


Most Windy Areas in the World

SUBMITTED BY ANUMAKONDA ON SAT, 2010-07-24 17:38.

Argentina experiences high winds in the Mountains and according to one estimate the Wind power potential is 500,000 MW.Argentina has one of the best regions of wind characteristics, it is The Patagonia. Its name comes from the marks that the Indian's feet made on soil when Magallanes saw them during one stop of his travel around the world. The meteorological average wind speed in this region is from 5 to 10 m/s approximately at 10 m height .The meteorological wind power at 10m height of Patagonia is about 200,000 MW. Wind behavior is quite special in Patagonia: low average wind speed correspond to places where wind is very seasonal (spring and summer), as Comahue Region (Neuquén – Rio Negro ), but with strong gusts of wind from 30 to 47 m/s. According to Global Energy Network Research Institute," This wind map shows that the best winds in Africa are found in the north of the continent and to its extreme east, west and south. Considering that wind energy technology will continue to improve, it would be appropriate to begin any efforts to put in place a wind power deployment strategy with the African countries that have the best wind resource. Based on the wind map and taking into account certain aspects relating to the climatological and meteorological data, 15 African countries can be identified as having the best wind resource in Africa: Southern Africa (South Africa, Lesotho, Madagascar and Mauritius); East Africa (Djibouti, Eritrea, Seychelles and Somalia); North Africa (Algeria, Egypt, Morocco and Tunisia); West Africa (Cape Verde and Mauritania). This list will also include Chad, in central Africa, whose wind power potential derives from its topographical features". Sri Lanka is another country which has excellent Wind Regime. "NREL (National Renewable Energy Laboratory, USA) estimates that there are nearly 5000 km2 of windy areas with good-to-excellent wind resource potential in Sri Lanka after accounting for excluded lands such as national parks and reserves and archaeological and cultural sites. About 4100 km2 of the total windy area is land and about 700 km2 is lagoon. The windy land represents about 6% of the total land area (65,600 km2) of Sri Lanka. Using a conservative assumption of 5 MW per km2, this windy land could support almost 20,000 MW of potential installed capacity. If the windy lagoons are included, the total wind potential increases to approximately 24,000 MW. If areas with moderate wind resource potential are considered, the estimated total windy land area increases to approximately 10,000 km2, or almost 15% of the total land area of Sri Lanka. This amount of windy land could support more than 50,000 MW of installed capacity". At the end of 2009, worldwide nameplate capacity of wind-powered generators was 159.2 gigawatts (GW). Energy production was 340 TWh, which is about 2% of worldwide electricity usage; and is growing rapidly, having doubled in the past three years. Several countries have achieved relatively high levels of wind power penetration (with large governmental subsidies), such as 20% of stationary electricity production in Denmark, 14% in Portugal and Spain, 11% in Republic of Ireland, and 8% in Germany in 2009. As of May 2009, 80 countries around the world are using wind power on a commercial basis. There are now many thousands of wind turbines operating, with a total nameplate capacity of 157,899 MW of which wind power in Europe accounts for 48% (2009). World wind generation capacity more than quadrupled between 2000 and 2006, doubling about every three years. 81% of wind power installations are in the US and Europe. The share of the top five countries in terms of new installations fell from 71% in 2004 to 62% in 2006, but climbed to 73% by 2008 as those countries - the United States, Germany, Spain, China, and India - have seen substantial capacity growth in the past two years . By 2010, the World Wind Energy Association expects 160 GW of capacity to be installed worldwide, up from 73.9 GW at the end of 2006, implying an anticipated net growth rate of more than 21% per year. Wind accounts for nearly one-fifth of electricity generated in Denmark - the highest percentage of any country - and it is tenth in the world in total wind power generation. Denmark is prominent in the manufacturing and use of wind turbines, with a commitment made in the 1970s to eventually produce half of the country's power by wind. In recent years, the US has added substantial amounts of wind power generation capacity, growing from just over 6 GW at the end of 2004 to over 35 GW at the end of 2009. The U.S. is currently the world's leader in wind power generation capacity. The country as a whole generates just 2.4% of its electrical power from wind, but several states generate substantial amounts of wind power. Texas is the state with the largest amount of generation capacity with 9,410 MW installed .This would have ranked it sixth in the world if Texas was a separate country. Iowa is the state with the highest percentage of wind generation, at 14.2% in 2009. California was one of the incubators of the modern wind power industry, and led the U.S. in installed capacity for many years. As of mid-2010, fourteen U.S. states had wind power generation capacities in excess of 1000 MW. U.S. Department of Energy studies have concluded that wind from the Great Plains states of Texas, Kansas, and North Dakota could provide enough electricity to power the entire nation, and that offshore wind farms could do the same job.. China had originally set a generating target of 30,000 MW by 2020 from renewable energy sources, but reached 22,500 MW by end of 2009 and could easily surpass 30,000 MW by end of 2010. Indigenous wind power could generate up to 253,000 MW. A Chinese renewable energy law was adopted in November 2004, following the World Wind Energy Conference organized by the Chinese and the World Wind Energy Association. By 2008, wind power was growing faster in China than the government had planned, and indeed faster in percentage terms than in any other large country, having more than doubled each year since 2005. Policymakers doubled their wind power prediction for 2010, after the wind industry reached the original goal of 5 GW three years ahead of schedule. Current trends suggest an actual installed capacity near 20 GW by 2010, with China shortly thereafter pursuing the United States for the world wind power lead. India ranks 5th in the world with a total wind power capacity of 10,925 MW in 2009, or 3% of all electricity produced in India. Mexico recently opened La Venta II wind power project as a step toward reducing Mexico's consumption of fossil fuels. The 88 MW project is the first of its kind in Mexico, and will provide 13 percent of the electricity needs of the state of Oaxaca. By 2012 the project will have a capacity of 3,500 MW. In May 2010, Sempra Energy announced it would build a wind farm in Baja California, with a capacity of at least 1,000 MW, at a cost of $5.5 billion.. Another growing market is Brazil, with a wind potential of 143 GW. Theoretical potential – World: Wind power available in the atmosphere is much greater than current world energy consumption. The most comprehensive study As of 2005[95] found the potential of wind power on land and near-shore to be 72 TW, equivalent to 54,000 MToE (million tons of oil equivalent) per year, or over five times the world's current energy use in all forms. The potential takes into account only locations with mean annual wind speeds ≥ 6.9 m/s at 80 m. The study assumes six 1.5 megawatt, 77 m diameter turbines per square kilometer on roughly 13% of the total global land area (though that land would also be available for other compatible uses such as farming). The authors acknowledge that many practical barriers would need to be overcome to reach this theoretical capacity. The practical limit to exploitation of wind power will be set by economic and environmental factors, since the resource available is far larger than any practical means to develop it (Source: Wikipedia) Dr.A.Jagadeesh Nellore(AP), India
 
Back
Top Bottom