Rutashubanyuma
JF-Expert Member
- Sep 24, 2010
- 219,470
- 911,173
Tanzania ni bora duniani kwa umeme wa nguvu ya upepo
Tuesday, 18 January 2011 21:40
Leon Bahati
WATAALAMU wa nishati toka nchini Norway wamefanya utafiti na kubaini kwamba Tanzania ni miongoni mwa nchi chache duniani ambazo zina mazingira bora zaidi ya kuzalisha umeme wa nguvu ya upepo.
Katika hali hiyo, wakaitaka serikali ianze kufanya maandalizi ya kuwekeza kwenye miradi ya uzalishaji wa umeme wa nguvu ya upepo ili kutatua tatizo sugu la nishati hiyo nchini.
Matokeo ya utafiti huo ni habari njema kwa Watanzania ambao kwa zaidi ya mwezi mmoja sasa wamekuwa wakikabiliwa na makali ya mgawo wa umeme, huku Shirika la Umeme Tanzania (Taesco) likiongeza gharama za nishati hiyo kwa asilimia 18. Mgawo wa umeme ni kama tatizo sugu nchini kwani limedumu kwa zaidi ya miaka mitano likijitokeza kwa vipindi na nyakati tofauti.
Mwishoni mwa mwaka jana Shirika la Maendeleo la Taifa (NDC), lilingia ubia na Kampuni ya Power Pool East Africa kuzalisha umeme wa upepo mkoani Singida utakaogharimu zaidi ya Sh180 bilioni.
Naibu Waziri wa Viwanda, Biashara na Masoko, Lazaro Nyalandu, alisema tayari makubaliano yamesainiwa na NDC na kwamba, serikali itakuwa ikimiliki asilimia 51 ya hisa na nyingine zitakuwa za mwekezaji.
Nyalandu alisema mradi huo utakuwa wa gharama nafuu katika uzalishaji utaingizwa kwenye gridi ya taifa na kwamba, kwa kuanzia zitazalishwa megawati 50 na baadaye zitaongezwa kulingana na uwezo wa wabia hao.
Kwa upande wao wataalamu kutoka nchini Norway jana waliwasilisha kwa serikali ripoti inayoonyesha nia yao ya kuwekeza kwenye mradi wa kuzalisha umeme wa nguvu ya upepo eneo la Makambako, mkoani Iringa kupitia kampuni ya Sino Tan ambayo imekusudia kuzalisha megawati 100.
Akizungumza kwa niaba ya wataalamu wenzake, Meneja wa Kampuni ya Norsk Vind Energy ya Norway, Torstein Ekern alisema Tanzania ina mazingira bora zaid ya uwekezaji katika eneo hilo ikilinganishwa na nchi kama Urusi na Bulgaria ambako pia wamewekeza.
Tumewekeza sehemu mbalimbali duniani kama vile Urusi na Bulgaria lakini utafiti inaonyesha mradi wa Tanzani ndio utakaokuwa bora zaidi, alisema Ekern.
Kuhusu namna utafiti huo ulivyoendesha, Mwenyekiti wa Kampuni ya Sino Tan, Alex Lema alisema waliuanza mwaka 2003 wilaya ya Same kwa miaka mitatu na baadaye kwa miaka sita Makambako.
Akasema wameamua kuwekeza Makambako kwa sababu wamebaini kuwa upepo wa kutosha kwa uzalishaji unavuma kwa mwaka mzima na kipindi cha kiangazi ambacho mara nyingi ni wakati Tanzania inakuwa na tatizo la umeme, ndipo unakuwa na kasi kubwa zaidi.
Kwa hiyo unaweza kuona kile kipindi cha ukame, ambacho mabwawa yetu yanayotuzalishia umeme yanakuwa yamekauka na kusababisha tukose umeme, ndicho ambacho mradi wetu unaweza kuzalisha zaidi kwa sababu nguvu ya upepe unakuwa mkubwa, alisema Lema.
Sino Tan iliwasilisha ripoti hiyo kwa serikali ili ipate kibali cha kuzalisha umeme huo mapema iwezekanavyo.
Iwapo serikali itakubali ombi lao, Lema alisema hatua inayofuata ni kufanya mazungumzo na Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco) pamoja na Mamlaka ya Kudhibiti Huduma za Nishati na Maji (Ewura) ili kuingia mkataba wa kununua megawati 100 za umeme watakaozalisha.
Tuesday, 18 January 2011 21:40
Leon Bahati
WATAALAMU wa nishati toka nchini Norway wamefanya utafiti na kubaini kwamba Tanzania ni miongoni mwa nchi chache duniani ambazo zina mazingira bora zaidi ya kuzalisha umeme wa nguvu ya upepo.
Katika hali hiyo, wakaitaka serikali ianze kufanya maandalizi ya kuwekeza kwenye miradi ya uzalishaji wa umeme wa nguvu ya upepo ili kutatua tatizo sugu la nishati hiyo nchini.
Matokeo ya utafiti huo ni habari njema kwa Watanzania ambao kwa zaidi ya mwezi mmoja sasa wamekuwa wakikabiliwa na makali ya mgawo wa umeme, huku Shirika la Umeme Tanzania (Taesco) likiongeza gharama za nishati hiyo kwa asilimia 18. Mgawo wa umeme ni kama tatizo sugu nchini kwani limedumu kwa zaidi ya miaka mitano likijitokeza kwa vipindi na nyakati tofauti.
Mwishoni mwa mwaka jana Shirika la Maendeleo la Taifa (NDC), lilingia ubia na Kampuni ya Power Pool East Africa kuzalisha umeme wa upepo mkoani Singida utakaogharimu zaidi ya Sh180 bilioni.
Naibu Waziri wa Viwanda, Biashara na Masoko, Lazaro Nyalandu, alisema tayari makubaliano yamesainiwa na NDC na kwamba, serikali itakuwa ikimiliki asilimia 51 ya hisa na nyingine zitakuwa za mwekezaji.
Nyalandu alisema mradi huo utakuwa wa gharama nafuu katika uzalishaji utaingizwa kwenye gridi ya taifa na kwamba, kwa kuanzia zitazalishwa megawati 50 na baadaye zitaongezwa kulingana na uwezo wa wabia hao.
Kwa upande wao wataalamu kutoka nchini Norway jana waliwasilisha kwa serikali ripoti inayoonyesha nia yao ya kuwekeza kwenye mradi wa kuzalisha umeme wa nguvu ya upepo eneo la Makambako, mkoani Iringa kupitia kampuni ya Sino Tan ambayo imekusudia kuzalisha megawati 100.
Akizungumza kwa niaba ya wataalamu wenzake, Meneja wa Kampuni ya Norsk Vind Energy ya Norway, Torstein Ekern alisema Tanzania ina mazingira bora zaid ya uwekezaji katika eneo hilo ikilinganishwa na nchi kama Urusi na Bulgaria ambako pia wamewekeza.
Tumewekeza sehemu mbalimbali duniani kama vile Urusi na Bulgaria lakini utafiti inaonyesha mradi wa Tanzani ndio utakaokuwa bora zaidi, alisema Ekern.
Kuhusu namna utafiti huo ulivyoendesha, Mwenyekiti wa Kampuni ya Sino Tan, Alex Lema alisema waliuanza mwaka 2003 wilaya ya Same kwa miaka mitatu na baadaye kwa miaka sita Makambako.
Akasema wameamua kuwekeza Makambako kwa sababu wamebaini kuwa upepo wa kutosha kwa uzalishaji unavuma kwa mwaka mzima na kipindi cha kiangazi ambacho mara nyingi ni wakati Tanzania inakuwa na tatizo la umeme, ndipo unakuwa na kasi kubwa zaidi.
Kwa hiyo unaweza kuona kile kipindi cha ukame, ambacho mabwawa yetu yanayotuzalishia umeme yanakuwa yamekauka na kusababisha tukose umeme, ndicho ambacho mradi wetu unaweza kuzalisha zaidi kwa sababu nguvu ya upepe unakuwa mkubwa, alisema Lema.
Sino Tan iliwasilisha ripoti hiyo kwa serikali ili ipate kibali cha kuzalisha umeme huo mapema iwezekanavyo.
Iwapo serikali itakubali ombi lao, Lema alisema hatua inayofuata ni kufanya mazungumzo na Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco) pamoja na Mamlaka ya Kudhibiti Huduma za Nishati na Maji (Ewura) ili kuingia mkataba wa kununua megawati 100 za umeme watakaozalisha.