Tanzania na Watanzania tunahitaji Uhuru, Ukombozi au Mapinduzi?

Yericko Nyerere

JF-Expert Member
Dec 22, 2010
16,977
20,244
Kunatafsiri tata ya tafakuri dhidi ya hitaji muhimu la Tanzania na watanzania wa leo na wakesho!

Hebu tujiulize watanzania tunajua tunachokihitaji ktk uwanda waleo tuliopo na tuuendeao?

Ni watanzania wangapi wanajua kwa ufasaha tafsiri ya Uhuru,Ukombozi au Mapinduzi?

Tujadili kwa mafaa ya kizazi hiki na kijacho!
 
Unachanganya madude. Kwanini wachina wana uhuru?

Uhuru upi? Uhuru unatafsiri nyingi hasa unaposimama ktk tuko husika!

China ni nchi huru na watu wake wapo huru,

Lakini china ilaumiwa na jumuiya za kimaghari kwa usimamiaji wa katiba na sheria za nchi hiyo yenye wakwasi wengi
 
Uhuru upi? Uhuru unatafsiri nyingi hasa unaposimama ktk tuko husika!

China ni nchi huru na watu wake wapo huru,

Lakini china ilaumiwa na jumuiya za kimaghari kwa usimamiaji wa katiba na sheria za nchi hiyo yenye wakwasi wengi

Kumbe unazijua tafsiri nyingi za uhuru? Katika hizo tafsiri kuna moja au mbili zitakazoonyesha tupo. Sasa tatizo lipo wapo?
 
Tatizo ni watanzania tunahitaji lipi kati ya Uhuri,Ukombozi na Mapinduzi?

Hivyo vitu vilishafanyiwa kazi miaka 50 iliyopita. Matatizo yaliyobaki ni kupambana na maradhi, umasikini na ujinga. Chagua kimoja wapo hapo na pambana nacho. Mtoto wako anatambana na kingine na mjukuu waku anamalizia kazi.

Unataka kurudia mambo aliyofanya Nyerere miaka 50 iliyopita, huko mwezini tutakwenda lini?
 
Hivyo vitu vilishafanyiwa kazi miaka 50 iliyopita. Matatizo yaliyobaki ni kupambana na maradhi, umasikini na ujinga. Chagua kimoja wapo hapo na pambana nacho. Mtoto wako anatambana na kingine na mjukuu waku anamalizia kazi.

Unataka kurudia mambo aliyofanya Nyerere miaka 50 iliyopita, huko mwezini tutakwenda lini?

bado ufisadi,uzalendo na haki.
 
mi naona tunahitaji zaidi mapinduzi na ukombozi wa fikra, kwa vile uhuru wa ndani ya nchi tunao tayari. labda uwe unaongelea uhuru wa kimahusisno kati ya nchi yetu na zingine huko duniani.
 
mi naona tunahitaji zaidi mapinduzi na ukombozi wa fikra, kwa vile uhuru wa ndani ya nchi tunao tayari. labda uwe unaongelea uhuru wa kimahusisno kati ya nchi yetu na zingine huko duniani.

Hivi kuna tofauto kati ya kwenda shule na mapinduzi na ukombozi wa fikra?
 
Uhuru: Nje ya ugandamizaji, hofu na magonjwa, njaa, kuishi bila wasiwasi wa kesho,

Ukombozi ni kumfungua mtu aliyefungwa na kumweka huru.

Mapinduzi ni kubadili mfumo mzima uwe wa ki fikra na kiutawala na kubadilisha jamii kuwa mpya kabisa.
 
Hivi kuna tofauto kati ya kwenda shule na mapinduzi na ukombozi wa fikra?

tofauti ipo
unaweza ukaenda shule lakini ukawa hujakomboka kifikra, unaweza ukaenda shule na ukashindwa kufanya mapinduzi vilevile japo shule inaweza kuwasaidia baadhi kukomboka kifikra na kusababisha mapinduzi.
hata ukimsoma karl marx utaona middle class ndio huleta mapinduzi, hao sio wale wenye phd after all hao wenye elimu za juu sana huwa wameridhika kuwategemea kuleta mapinduzi ni shida kidogo.
 
na pia ukumbuke kuwa shule yenyewe unayoisema ni ipi hii hii iliyoletwa na tabaka tawala na kukuchagulia cha kusoma ili uendeleze mfumo wa kuwa chini yao na kutawaliwa?

ukombozi wa fikra ni zaidi ya kusoma hesabu, historia, geografia, political science, engineering, law and many others ni zaidi ya hayo niliyoyataja.
watu wengi wamesoma lakini hawajakomboka kifikra wamefungwa bado na fikra pandikizi ya kile walichooneshwa kama mwanga.
ukombozi wa fikra ni uhuru wa kutafakari na kuyaona mambo katika kweli yenyewe.
 
tofauti ipo
unaweza ukaenda shule lakini ukawa hujakomboka kifikra, unaweza ukaenda shule na ukashindwa kufanya mapinduzi vilevile japo shule inaweza kuwasaidia baadhi kukomboka kifikra na kusababisha mapinduzi.
hata ukimsoma karl marx utaona middle class ndio huleta mapinduzi, hao sio wale wenye phd after all hao wenye elimu za juu sana huwa wameridhika kuwategemea kuleta mapinduzi ni shida kidogo.


IL;

Tofauti inakuja kwa sababu watoto wanahudhuria shule lakini hawasomi. Watu wanakwenda makazini lakini hawafanyikazi. Lakini tungekuwa na moyo ya kufanya vile tunavyopanga japo kwa 75% basi huu mjadala usingekuwepo.

Uwezi kupiga risasi bila kulenga shabaha na utegemee kupata targets zako. Wafundishe vizuri wanafunzi na baadaye uwape uhuru wa kufikiri na kuongea, watakushangaza na jinsi wanavyotumia elimu yao.

Ukombozi wa fikra mnaosema hapa ni branding ya slogans za miaka ya nyuma zilizopita. Hakuna tofauti kati ya kufuta ujinga na ukombozi wa fikra.

Usiku mwema.

Z-10
 
IL;

Tofauti inakuja kwa sababu watoto wanahudhuria shule lakini hawasomi. Watu wanakwenda makazini lakini hawafanyikazi. Lakini tungekuwa na moyo ya kufanya vile tunavyopanga japo kwa 75% basi huu mjadala usingekuwepo.

Uwezi kupiga risasi bila kulenga shabaha na utegemee kupata targets zako. Wafundishe vizuri wanafunzi na baadaye uwape uhuru wa kufikiri na kuongea, watakushangaza na jinsi wanavyotumia elimu yao.

Ukombozi wa fikra mnaosema hapa ni branding ya slogans za miaka ya nyuma zilizopita. Hakuna tofauti kati ya kufuta ujinga na ukombozi wa fikra.

Usiku mwema.

Z-10

mkuu zakumi naomba kupingana na wewe
si kweli kila aendae na kusoma akawa amefunguka kifikra, nakukatalia kwa sababu hata akisoma vp akaelewa kama anachosoma chenyewe kimelenga kumfunga ama hakijawa katika lengo la kumfungua hata apate A kila siku anaweza kabisa akawa amefungwa kifikra. hajafunguka kifikra.
ni aina gani aya elimu mtu huyo anayopata ndio hapa tunachosema.
kufanya kazi au kutofanya kazi ni jambo jingine la mjadala lakini suluhu yake ni mapinduzi. sijui unanipata.

ni sawa na kusema si kila aliyeenda shule ameelimika. sawa kabisa na kusema si kila aliyesoma amefunguka kifikra.
jitu limekremisha miformula tu ya shuleni cheti kizuri lakini uwezo wake wa kufikiri juu ya mambo mbalimbali ya maisha na suluhu zake ni mtihani kwake. hawa utasemaje kiongozi wangu.
 
mkuu zakumi naomba kupingana na wewe
si kweli kila aendae na kusoma akawa amefunguka kifikra, nakukatalia kwa sababu hata akisoma vp akaelewa kama anachosoma chenyewe kimelenga kumfunga ama hakijawa katika lengo la kumfungua hata apate A kila siku anaweza kabisa akawa amefungwa kifikra. hajafunguka kifikra.
ni aina gani aya elimu mtu huyo anayopata ndio hapa tunachosema.
kufanya kazi au kutofanya kazi ni jambo jingine la mjadala lakini suluhu yake ni mapinduzi. sijui unanipata.

ni sawa na kusema si kila aliyeenda shule ameelimika. sawa kabisa na kusema si kila aliyesoma amefunguka kifikra.
jitu limekremisha miformula tu ya shuleni cheti kizuri lakini uwezo wake wa kufikiri juu ya mambo mbalimbali ya maisha na suluhu zake ni mtihani kwake. hawa utasemaje kiongozi wangu.

Bibi Chuma;

Kiswahili lugha yangu ya pili kama kiingereza. Labda ukunielewa katika posti yangu ya mwisho kabla ya hii. Nimesema ukimfundisha mtu vizuri na kumpa uhuru atafanya mambo mengi sana na kustaajabisha kwa jinsi anavyotumia akili zake. Shule nyingi za Tanzania ni vituo vya kulelea watoto lakini hakuna mafundisho.

Tukirudi kwenye posti yako, watu wana krem formula sio kwa sababu wanapenda kufanya hivyo. Ukiwa na waalimu wazuri hakuna mtu atakayepoteza muda kukrem. Hivyo hakuna sababu ya kuomba mapinduzi ya kielimu wakati huna walimu wa kufundisha. Yakitokea mapinduzi ya kifikra leo, viongozi wa mapinduzi hayo watakimbilia kazi za ofisini na kuwaachia waalimu hawahawa kufundisha.

Chuo cha kwanza kujengwa na wananchi Tanzania kilikuwa ni chuo cha kivukoni (July 1961). Chuo ambacho kilikuwa na lengo kukukomboa kifikra. Miaka zaidi ya 50 leo watu bado mnataka ukombozi mwingine. Something must be wrong.
 
Bibi Chuma;

Kiswahili lugha yangu ya pili kama kiingereza. Labda ukunielewa katika posti yangu ya mwisho kabla ya hii. Nimesema ukimfundisha mtu vizuri na kumpa uhuru atafanya mambo mengi sana na kustaajabisha kwa jinsi anavyotumia akili zake. Shule nyingi za Tanzania ni vituo vya kulelea watoto lakini hakuna mafundisho.

Tukirudi kwenye posti yako, watu wana krem formula sio kwa sababu wanapenda kufanya hivyo. Ukiwa na waalimu wazuri hakuna mtu atakayepoteza muda kukrem. Hivyo hakuna sababu ya kuomba mapinduzi ya kielimu wakati huna walimu wa kufundisha. Yakitokea mapinduzi ya kifikra leo, viongozi wa mapinduzi hayo watakimbilia kazi za ofisini na kuwaachia waalimu hawahawa kufundisha.

Chuo cha kwanza kujengwa na wananchi Tanzania kilikuwa ni chuo cha kivukoni (July 1961). Chuo ambacho kilikuwa na lengo kukukomboa kifikra. Miaka zaidi ya 50 leo watu bado mnataka ukombozi mwingine. Something must be wrong.


unaona sasa mkuu zakumi, chuo hicho kilitoa ukombozi wa kifikra au kiliwajenga watu kuwa na mtazamo fulani?
sijui unapata ninachokusudia kusema. kwa hiyo watu wale waliohudhuria chuo hicho ndio wamekomboka kifikra?
labda tujiulize fikra zipi tunazozizungumzia hapa?
wale walilelewa kuheshimu tabaka la wakati huo tawala. walifungwa kwa namna nyingine hamna tofauti sana na hadithi ya kivuli kinaishi ya bi kilembwe
 
1 Reactions
Reply
Back
Top Bottom