Tanzania na siasa

The Infamous

JF-Expert Member
May 11, 2009
731
121
Tanzania yangu ya kesho sielewi itakuwa vipi, kama ya leo inautupu wa mwongozo, siasa imepewa asilimia 80 kama ndio mfumo wa kuongoza na kuendesha nchi, mfumo wa sheria, uwajibikaji na utawala bora umemezwa na wanasiasa, ya jana sio ya leo wala ya leo sio ya kesho, je barabara hii ya siasa ambayo viongozi wetu kama sio watawala wanatupitisha katika kuiongoza nchi yetu ni salama? nayaona machozi ya mjukuu wangu akililia amani kwani watawaliwa wameshika silaha za jadi wanaitaka haki yao.

Tanzania iliyochukua siasa wazungu wanaita politics kama mfumo wa uendeshaji nchi itatufikisha mwisho wa safari?

furaha kuzaliwa Tanzania.
 
Itafika wakati wananchi watakuwa wanaomba wabunge wao au hata madiwanu wao wafariki ili zifanyike chaguzi ndogo wapate neema. Unaweza kutafiti pesa iliyotengwa kwa igunga kwa ajili ya maendeleo ya elimu, afya, bara barabara ni kiasi gani? Usihangae ukauta pesa hyo haitfautini sana na gharama ya uchaguzi mdogo.

Hapa jf penyenwe kuna wasomi kibao lakini siasa ndio jukwaa kubwa. Ni kweli siasa ndio chanzo cha matatizo mengi ya nchi hii lakini siasa sio suluisho la hata 20% ya matatizo ya nchi hii. Kwa hiyo mimi kama mtaka mabadilio sitashangaa chama nje ya CCM kikichukua nchi kichashindwa kuleta mabadiliko ya kweli . Vyama vya siasa vinataka mabadiliko ya kisiasa lakini kuna vyama vingine vina ongoza halmashauri na majiji. Je wamefanya nini tofauti na ccm kitendaji ukiondoa tofauti za siasa.

Kwa hiyo hata uchumi wetu ni siasa. Ukisikia maneno kama

  • kilimo kwanza ni asilimia 10 ya sera utendaji na utekelezaji ni kweli ni kilimo kwanza 90% ni siasa. Na mafanikio yanapimwa kisiasa., Utekeleaji na utendaji unapelekwa kisiasa
  • Kilimo ni uti wa mgongo sio kweli Tanzania Siasa ndi uti wa mgongo. Ni sbaabu hiyo hata wataalamu mbali mbali wanaacha kazi na fani zao vyuo vikuu na tasisi nyingine kwenda kuwa wanasiasa. Ingependeza watu waache fani za waende kuwa mafisa elimu wa mkoa, waganga wauu wa mikoo, maafisa kilimo wa mikoa.
 
Back
Top Bottom