The Infamous
JF-Expert Member
- May 11, 2009
- 731
- 121
Tanzania yangu ya kesho sielewi itakuwa vipi, kama ya leo inautupu wa mwongozo, siasa imepewa asilimia 80 kama ndio mfumo wa kuongoza na kuendesha nchi, mfumo wa sheria, uwajibikaji na utawala bora umemezwa na wanasiasa, ya jana sio ya leo wala ya leo sio ya kesho, je barabara hii ya siasa ambayo viongozi wetu kama sio watawala wanatupitisha katika kuiongoza nchi yetu ni salama? nayaona machozi ya mjukuu wangu akililia amani kwani watawaliwa wameshika silaha za jadi wanaitaka haki yao.
Tanzania iliyochukua siasa wazungu wanaita politics kama mfumo wa uendeshaji nchi itatufikisha mwisho wa safari?
furaha kuzaliwa Tanzania.
Tanzania iliyochukua siasa wazungu wanaita politics kama mfumo wa uendeshaji nchi itatufikisha mwisho wa safari?
furaha kuzaliwa Tanzania.