Tanzania na Sheria: Rais Mwinyi Aliua Wengi Zaidi!

The Khoisan

JF-Expert Member
Jun 5, 2007
15,382
12,969
Awamu ya Mzee Mwinyi iliongoza kwa kunyonga

2008-01-30 17:28:15
Na Job Ndomba, Dodoma

Serikali ya awamu ya pili iliyokuwa ikiongozwa na Ali Hassan Mwinyi almaarufu kama Mzee Ruksa ndiyo inayoongoza kwa kutekeleza adhabu ya kunyonga watu.

Naibu Waziri wa Sheria na Katiba Bw. Mathias Chikawe ameliambia Bunge mapema leo asubuhi kuwa watu tangu nchi hii ipate uhuru jumla ya watu 82 wamenyongwa.

Amesema kati ya watu hao, kumi walinyongwa katika kipindi cha awamu ya kwanza, iliyokuwa ikiongozwa na Baba wa Taifa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere.

Akasema watu 72 walinyongwa awamu ya pili ya Mzee Ruksa, huku katika awamu ya tatu na ya nne hakuna mtu aliyenyongwa hadi sasa.

Naibu Waziri huyo amesisitiza kuwa adhabu ya kifo kwa Tanzania bado ni adhabu halali na inaendelea kutumika.

Hata hivyo amesema Serikali imepanua wigo wa maoni ya wananchi kwa kuiagiza Tume ya kurekebisha sheria kuanza mchakato na hatimaye kupata maoni ya wananchi kama adhabu hiyo inastahili kuendelea kuwepo kwenye vitabu vya sheria vya Tanzania ama la.

Amesema mchakato huo ukikamilika na kupata maoni ya wananchi, Serikali iko tayari kusikia maoni hayo na hata kuleta muswada bungeni wa kuiondoa sheria hiyo.

Bw. Chikawe ametoa maelezo hayo wakati akijibu swali la Mbunge wa Sumve Mheshimiwa Richard Ndasa, CCM, aliyetaka kujua idadi ya watu waliokwishanyongwa chini ya adhabu hiyo na awamu ipi ya Serikali iliyotekeleza ipasavyo adhabu hiyo.

SOURCE: Alasiri
 
Hapa kuna utata mkubwa. Wakati Nyerere anaondoka mwaka 1985 alipata nafasi ya kuzungumza katika hotuba yake ya kuagana, nadhani alikuwa na maafisa wa Magereza.

Alisema kati ya mambo magumu ambayo Rais anaweza kufanya na yamo ndani ya wajibu wake ni kutoa uamuzi wa kutekeleza hukumu ya kunyongwa.

Akasema kuwa ndani ya miaka yake zaidi ya 20 kama Rais aliruhusu watu wawili tu wanyongwe. Kuna yule aliyemuua Dr. Kleruu na mtu mwingine (sikumbuki jina lake mara moja).

Sasa leo tunaambiwa watu kumi walinyongwa wakati wa utawala wa Mwalimu, kuna mtu anatakiwa kutuambia ni kina nani hao na kwa makosa gani? Yawezekana tukapata majibu ya kina Kassim Hanga...
 
wanajichanganya wenyewe.. watuambie hao watu 10 walionyongwa wakati wa Utawala wa Mwalimu ni kina nani?
 
Kikubwa these days CCM wanawasingizia watu walio kufa kiasi kwamba we cannot recheck with Mwalimu. Mwinyi yupo anaweza kuulizwa juu ya data hizi ku clarify .
 
wanajichanganya wenyewe.. watuambie hao watu 10 walionyongwa wakati wa Utawala wa Mwalimu ni kina nani?

Kuna mama yule alikuwa nurse Muhimbili na alimkata kata mke mwenza. Nilikuwa
shuleni, nafikiri ulikuwa wakati wa Mwalimu, ingawaje inawezekana pia ilikuwa mwanzoni mwa Mwinyi.

Ilikuwa case ya kusikitisha sana. Sikumbuki majina, bwana alikuwa daktari Muhimbili.
 
wengi walihukumiwa kunyongwa. Sasa sina uhakika kama wanaohukumiwa katika mahakama za kijeshi (kama aliyemuua mjomba wangu) hukumu zao za kunyongwa nazo ni lazima zipate baraka za Rais (theoretically yes) au ndiyo jeshi likisema unanyongwa ndiyo unanyongwa?
 
Kuna mama yule alikuwa nurse Muhimbili na alimkata kata mke mwenza. Nilikuwa
shuleni, nafikiri ulikuwa wakati wa Mwalimu, ingawaje inawezekana pia ilikuwa mwanzoni mwa Mwinyi.

Ilikuwa case ya kusikitisha sana. Sikumbuki majina, bwana alikuwa daktari Muhimbili.

Mtanzania,

Ilikuwa ni kesi ya kusikitisha sana.

Yule mama alieua anaitwa Happiness Senzota na mama alieuawa anaitwa Agnes.

Mume wa marehemu alieuawa alikuwa anafahamika kama dokta Haule.

Lile tukio lilikuwa ni la kusikitisha sana ukizingatia kwamba mmoja wa watoto wa marehemu Agnes, alikuwa ni "classmate" wangu na sitakuja kusahau maishani.
 
Mtanzania,

Ilikuwa ni kesi ya kusikitisha sana.

Yule mama alieua anaitwa Happiness Senzota na mama alieuawa anaitwa Agnes.

Mume wa marehemu alieuawa alikuwa anafahamika kama dokta Haule.

Lile tukio lilikuwa ni la kusikitisha sana ukizingatia kwamba mmoja wa watoto wa marehemu Agnes, alikuwa ni "classmate" wangu na sitakuja kusahau maishani.

Kuna mmoja alikuwa anaitwa Asha Mkwizu sijui ni yupi kati ya wale wakina mama wawili. Afu hayo yote yalikuwa ni matokeo ya ndoa academia!
 
Hivi kwa nini AHM mkono wake ulikuwa mwepesi kuliko wa JKN na BWM? Any reasons?

72 ni wengi sana for 10 years out of 82 tangu tuwe huru!
 
Adhabu ya kifo iwekwe tuisome kwa umakini Ikoje...naona bado ina mapungufu mengi tu...Bado haioni mzinifu alieoa au kuolewa kama ni kosa la JINAI....hawaioni hio kama Mapinduzi ya Serikali ya MTU...ila mtu akijaribu kutaka kupindua serikali ya UFISADI basi hucheleweshwi utanyongwa na kuburuzwa barabarani watu wakuone....Just a Challenge....

back to Case Halisi ya Makosa ya Kunyongwa. Kwa Uoni wangu ikiwa ushahidi upo wa 100% kuwa mtu XYZ anastahili kunyongwa basi anyongwe...Unless apate msahamaha wa ndugu aliemuua au kulipa fidia...bloody money...

Ikiwa haikuthibitika, Kumnyonga mtu bado itakuwa ni kumuonea. kwakuwa mie si mwanasheria kujua kwanini ili happen zaid kwa mwinyi kuliko wengine sina elim nalo...niwasilikize wengine.
 
Sasa hao ambao huhukumiwa kunyongwa na Raisi asitie sahihi- hukaa tu gerezani kusubiri au hii hugeuka Life Sentence?
 
Hivi kwa nini AHM mkono wake ulikuwa mwepesi kuliko wa JKN na BWM? Any reasons?

72 ni wengi sana for 10 years out of 82 tangu tuwe huru!

Naweza kutoa layman guess; Moja inawekana wale wote waliohukumiwa kipindi cha JKN, mzee AHM aliambiwa aite mkono adhabu zitekelezwe.

Pili inawezekana wale wote waliomaster mind na kutekeleza kifo cha Sokoine walipatiwa hukumu AHM akiwa madarakani so akaitekeleza immediately.

Njaa iliyoikumba nchi 1980s ilifanya magereza kuiingia gharama kubwa so ikabidi mzee aanguke signature kupunguza wafungwa na kupunguza ghrama kwa serikali

Hiyo gues yangu tu waiting for serious and concrete reasons
 
Njaa iliyoikumba nchi 1980s ilifanya magereza kuiingia gharama kubwa so ikabidi mzee aanguke signature kupunguza wafungwa na kupunguza ghrama kwa serikali

Hiyo gues yangu tu waiting for serious and concrete reasons

Mzee Bowbow heshima kubwa kwako. Hiyo guess yako imenishanganza sana, sidhani kama kunyonga watu 72 kungepunguza gharama zozote kwenye magereza, punguzo lake ni negligible.
Lakini inawezekana kabisa kuwa utekelezaji wa kesi nyingi zenye hukumu ya kunyongwa sio instant, huwa inasubiriwa ipite muda kidogo ili kusubiri kama kutakuwa na evidence inayoweza kumnusuru mhukumiwa. Lakini ikumbukwe pia kipindi cha Mwinyi ndio kipindi watu walianza kuona gap kubwa kati ya matajiri na maskini na ni kipindi ambacho mambo emngi mabaya yalianza kutokea, kutokana na sera za ruksa, kwa hiyo unaweza kusema ni combination ya mengi ndio ilifanya hiyo namba iwe kubwa, lakini itakuwa unfair tukibebesha lawama jina la Mwinyi.
Vilevile kipindi cha Mkapa hatuwezi kusema hakukuwa na makosa ya namna hiyo, inawezekana Ben alikuwa muoga, au alitaka rais anayefuata ndiyo afanye ambayo yeye hakutaka kufanya.
 
mkjj mkulima na rangi ya kijani ndio rangi ya mkulima na rangi ya uhai.

nnajua unatuma ujumbe kuwa ww na kijani dam dam
 
Niseme mapema kuwa mimi napinga hukumu ya kifo kwa nguvu zangu zote. Ni sheria ya kidhalimu. Hukumu hii hata siku moja haiwezi kutekelezwa kwa haki. Ni wale wasionacho ndio siku zote wanatolewa kafara. Wangapi wamembapikiwa kesi? Mimi na wajua waliosota keko kwa kubambikiwa kesi na wenye nazo. Hiyo haki iko wapi? Huyo mama mnaemzungumzia nadhani aliachiwa kwa msamaha wa Rais. Brother Dito aliyeua hadharani anapeta. Mtoto mdogo wa miaka 16 yuko lupango ameshitakiwa kwa kesi ya murder ambapo hukumu yake ni kifo. Hata huko marekani ambako wana CSI wameshtuka na sasa hivi wanaiangalia upya. Jimbo la New Jersey limeifutilia mbali. Kuna mmoja amependekeza kuwa hata wazinifu nao tuwanyonge!!! Wanaobaka watoto wadogo je? Wanaouza madawa ya kulevya je? Wote hawa ni waovu. Ukweli ni kuwa hii hukumu haizuii maovu ama sivyo Texas kungekuwa ahera. Mimi naamini kabisa hukumu hii haina nafasi katika jamii yeyote inayojiona ni ya kiungwana. Ukiongezea kuwa sisi tunawanyonga kwa kamba. Kama walivyomfanyia Saddam Hussein. Pendekezo langu ni hili: Kwa kuwa tunaipenda hii hukumu, ifanywe hadharani. Waandishi wa habari (pamoja na wa TV)waalikwe siku ya mtu kunyongwa. Majina ya wale walio kwenye death row yatangazwe na sababu zilizowafikisha hapo. Na tarehe na siku ya kutekeleza hiyo hukumu itangazwe. Namna hii tutaona jinsi tunavyowaua wenzetu wasiokubalika na jamii. Pasiwe na usiri, tutembee kifua mbele kwamba hatuna mchezo sie, kamba kamba tu. Mungu atunusuru wote.

Mods: Naomba mihamishie kwenye jukwaa la siasa. Hili suala ni zito mno. Halistahili kuwa kwenye vibweka vya wakubwa.
 
Data zinatia shaka.Kama kuna majina yatajwe.Kuna mtu mwingine mbali na Kassim Hanga kwa jina Othman Shariff ambaye alikuwa mjumbe wetu UN.
 
Kassim Hanga??
Kweli mkjj una data za kutosha.....


No. siyo Kassim Hanga. Kuna yule Mzungu mmoja alimuweka mkewe kwenye gari halafu akaisukuma kwenye milima huko kusini na mkewe akafa na yule bwana akadanganya kuwa kapata ajali na akaenda kudai Insurence akalipwa pesa nyingi sana.Nasikia Mwalimu aliita mpaka Scotland Yard kufanya uchunguzi na yule mzungu alibainika na alinyongwa.Ni wakati tu tumepata Uhuru. Je, mpo hapo? Kwa hiyo Mwalimu alisaini watu wawili tu wanyongwe na siyo kumi.Mafisadi wanampakazia bwana.au watupe orodha ya hawo kumi basi.
 
Back
Top Bottom