WOWOWO
JF-Expert Member
- Aug 3, 2011
- 590
- 430
Wana Bodi kwa kawaida katika taifa lolote lazima kuwe na mijadala yenye afya ambayo hutumika kama dira ya kuleta mabadiliko na maboresho katika masuala mbalimbali yahusuyo jamii na taifa kwa upana wake.
Moja ya sekta ambayo inapaswa kuongoza kwa kuibua mijadala ni vyombo vya habari kupitia kuandaa vipindi vya mijadala na kuarika watu weledi (Naomba tuwaite Opinion Leaders/Makers) ambao wataongozwa na Mwandishi aliyebobea katika uchokonozi na kuwafanya wageni wake (Opinion Leaders) waweze kutoa michango ambayo itakuwa guideline katika issues mbalimbai zinazoibuka katika jamii yetu.
Niweke wazi kabisa kwamba opinion leaders ni aina ya watu waliobobea kwenye masuala mbalimbali katika jamii ambao kwa kawaida kunapotokea issue yoyote burning katika jamii basi vyombo vya habari na kila mtanzania anakuwa very curious kusikia nini watasema na kwa maana hiyo kuwa kama dira ya jambo lililoibuka.
Faida za Opinion Leaders katika jamii ni nyingi sana lakini baadhi ni pamoja na kukuza kisima cha fikra katika jamii, kuwa dira ya mijadala ya kitaifa, kusaidia kupatikana kwa fikra za kulisogeza taifa letu mbele, kuset agenda mbalimbali za kitaifa na kubwa zaidi kuwafanya wananchi kuwa na uelewa wa kina, misimamo na baadaye maamuzi sahihi katika issues mbalimbali za kitaifa.
Hata hivyo, pamoja na umuhimu huo wa Opion Leaders katika kujenga afya ya mijadala, Taifa letu linakosa tunu hiyo muhimu kwa maendeleo. Vyombo vya habari vimekosa programu zenye kuibua mijadala na fikra nzito na baadhi vimebaki kuwa mawakala si tu wa kuzima mijadala bali pia kuiharibu jamii ili isiwe na uwezo wa kushiriki mijadala hiyo.
Naomba niazime mifano ya vipindi kama This Week in Perspective (TBC), Kipima Joto (ITV), Tuongee Asubuhi (Star TV), Je Tutafika? (Channel 10), General on Monday (Channel 10), Hamza Kasongo Hour (Channel 10), Medani za Siasa (Star TV) na vingine ambavyo nimevisahau, vimekaaje? Vinasaidia kweli katika kuibua mijadala na kuset agenda za Taifa? Vinakidhi kweli haja? Jibu ni hapana.
Binafsi naviona kama si tu vimeshindwa kufikia viwango lakini pia hata vile vilivyokuwa vimejaribu kuchomoza hasa vile vya Je Tutafika cha Makwaiya wa Kuhenga, Kipima Joto cha ITV na Tuongee Asubuhi cha Star TV vimeporomoka ghafla na kupoteza mvuto kabisa.Kwa ujumla hatuwezi kuvitegemea kwa uhuru, uwazi, weledi na bila kuegemea upande wowote katika kuibua na kujadili issues nzito za kitaifa
Hata hivyo, kuna maswali ya kujiuliza hapa.Je huenda vipindi hivyo vimekosa mvuto kutokana na ombwe la Opinion leaders? Au waandaaji wa vipindi wanakosa mbinu na weledi? Lakini swali lingine inawezekanaje waandaaji hawa wa vipindi waka brach na kuhost wageni (Opion leaders) kutoka almost kila nyanja? Wanaweza kumudu kila taaluma?
Ukweli mchungu ni kuwa kama Taifa TUNA OMBWE LA OPION LEADERS/MAKERS ndiyo maana kwa muda mrefu tumekosa ajenda za kitaifa, mijadala yenye afya na kujenga na mara nyingi tumekuwa ni wa kushangilia matukio na yanapopita tunasahau kila kitu.
Naomba nitaje baadhi ya mijadala ya hivi karibuni tu ambayo naamini imekufa kutokana na ombwe tulilonalo la Opinion Leaders/Makers na vyombo vyetu vya habari kushindwa kukidhi haja..Ripoti ya Brig. Ngwilizi kuhusu Wabunge kupokea Rushwa, Tundu Lissu na Majaji bandia nchini, Sakata la Meno ya Tembo kukamatwa Hong Kong, Uchaguzi wa kimafia wa Meya wa Ilemela, Kashfa ya Polisi na Makuruta feki nk. nk.
Unaweza ukafikiria tu; hivi ni wasomi gani tulionao kwa sasa ambao wanaweza kujadili issues za kitaifa kwa weledi, uwazi, umakini na bila kubebwa na unazi/itikadi? Ukweli ni kwamba idadi ni finyu sana na ya kukatisha tamaa. Wengi wao wamekuwa waingiza mikono kwenye makoti ya wakubwa na kwa maana hiyo mambo mengi mazito yanapeperuka kama upepo na hakuna anayejali wala kuyashikia kidedea.
Kazi hii ya Opinion Leaders sasa imebebwa na Wanasiasa, kila siku utakumbana na Dkt.Bana, Dkt.Kitila Mkumbo, Dkt.Slaa, Kinana, Nape, Zitto, Mangula, Mnyika, Mbowe, JK, Shibuda, Lema, Kafulila nk.nk.Hatuna mijadala ya kiweledi na elekezi.Tumekufa ganzi. Hata akina Prof. Shivji (ambaye kwa sasa ndiyo naona yuko impartial) hawas
Moja ya sekta ambayo inapaswa kuongoza kwa kuibua mijadala ni vyombo vya habari kupitia kuandaa vipindi vya mijadala na kuarika watu weledi (Naomba tuwaite Opinion Leaders/Makers) ambao wataongozwa na Mwandishi aliyebobea katika uchokonozi na kuwafanya wageni wake (Opinion Leaders) waweze kutoa michango ambayo itakuwa guideline katika issues mbalimbai zinazoibuka katika jamii yetu.
Niweke wazi kabisa kwamba opinion leaders ni aina ya watu waliobobea kwenye masuala mbalimbali katika jamii ambao kwa kawaida kunapotokea issue yoyote burning katika jamii basi vyombo vya habari na kila mtanzania anakuwa very curious kusikia nini watasema na kwa maana hiyo kuwa kama dira ya jambo lililoibuka.
Faida za Opinion Leaders katika jamii ni nyingi sana lakini baadhi ni pamoja na kukuza kisima cha fikra katika jamii, kuwa dira ya mijadala ya kitaifa, kusaidia kupatikana kwa fikra za kulisogeza taifa letu mbele, kuset agenda mbalimbali za kitaifa na kubwa zaidi kuwafanya wananchi kuwa na uelewa wa kina, misimamo na baadaye maamuzi sahihi katika issues mbalimbali za kitaifa.
Hata hivyo, pamoja na umuhimu huo wa Opion Leaders katika kujenga afya ya mijadala, Taifa letu linakosa tunu hiyo muhimu kwa maendeleo. Vyombo vya habari vimekosa programu zenye kuibua mijadala na fikra nzito na baadhi vimebaki kuwa mawakala si tu wa kuzima mijadala bali pia kuiharibu jamii ili isiwe na uwezo wa kushiriki mijadala hiyo.
Naomba niazime mifano ya vipindi kama This Week in Perspective (TBC), Kipima Joto (ITV), Tuongee Asubuhi (Star TV), Je Tutafika? (Channel 10), General on Monday (Channel 10), Hamza Kasongo Hour (Channel 10), Medani za Siasa (Star TV) na vingine ambavyo nimevisahau, vimekaaje? Vinasaidia kweli katika kuibua mijadala na kuset agenda za Taifa? Vinakidhi kweli haja? Jibu ni hapana.
Binafsi naviona kama si tu vimeshindwa kufikia viwango lakini pia hata vile vilivyokuwa vimejaribu kuchomoza hasa vile vya Je Tutafika cha Makwaiya wa Kuhenga, Kipima Joto cha ITV na Tuongee Asubuhi cha Star TV vimeporomoka ghafla na kupoteza mvuto kabisa.Kwa ujumla hatuwezi kuvitegemea kwa uhuru, uwazi, weledi na bila kuegemea upande wowote katika kuibua na kujadili issues nzito za kitaifa
Hata hivyo, kuna maswali ya kujiuliza hapa.Je huenda vipindi hivyo vimekosa mvuto kutokana na ombwe la Opinion leaders? Au waandaaji wa vipindi wanakosa mbinu na weledi? Lakini swali lingine inawezekanaje waandaaji hawa wa vipindi waka brach na kuhost wageni (Opion leaders) kutoka almost kila nyanja? Wanaweza kumudu kila taaluma?
Ukweli mchungu ni kuwa kama Taifa TUNA OMBWE LA OPION LEADERS/MAKERS ndiyo maana kwa muda mrefu tumekosa ajenda za kitaifa, mijadala yenye afya na kujenga na mara nyingi tumekuwa ni wa kushangilia matukio na yanapopita tunasahau kila kitu.
Naomba nitaje baadhi ya mijadala ya hivi karibuni tu ambayo naamini imekufa kutokana na ombwe tulilonalo la Opinion Leaders/Makers na vyombo vyetu vya habari kushindwa kukidhi haja..Ripoti ya Brig. Ngwilizi kuhusu Wabunge kupokea Rushwa, Tundu Lissu na Majaji bandia nchini, Sakata la Meno ya Tembo kukamatwa Hong Kong, Uchaguzi wa kimafia wa Meya wa Ilemela, Kashfa ya Polisi na Makuruta feki nk. nk.
Unaweza ukafikiria tu; hivi ni wasomi gani tulionao kwa sasa ambao wanaweza kujadili issues za kitaifa kwa weledi, uwazi, umakini na bila kubebwa na unazi/itikadi? Ukweli ni kwamba idadi ni finyu sana na ya kukatisha tamaa. Wengi wao wamekuwa waingiza mikono kwenye makoti ya wakubwa na kwa maana hiyo mambo mengi mazito yanapeperuka kama upepo na hakuna anayejali wala kuyashikia kidedea.
Kazi hii ya Opinion Leaders sasa imebebwa na Wanasiasa, kila siku utakumbana na Dkt.Bana, Dkt.Kitila Mkumbo, Dkt.Slaa, Kinana, Nape, Zitto, Mangula, Mnyika, Mbowe, JK, Shibuda, Lema, Kafulila nk.nk.Hatuna mijadala ya kiweledi na elekezi.Tumekufa ganzi. Hata akina Prof. Shivji (ambaye kwa sasa ndiyo naona yuko impartial) hawas