Tanzania na Burundi kujenga reli ya thamani ya $900m

Kasomi

JF-Expert Member
Sep 3, 2014
11,036
20,337
Burundi na Tanzania zimetia saini mkataba wa $900m kujenga njia ya reli itakayounganisha nchi hizo mbili jirani, tovuti ya Citizen imeripoti.

Reli ya 282km ya standard gauge itaanzia Uvinza mkoani Kigoma nchini Tanzania hadi Gitega, mji mkuu wa kisiasa wa Burundi, ripoti ilisema.

Waziri wa Mipango na Fedha wa Tanzania Mwigulu Nchemba alisema nchi hizo mbili "zitatafuta maeneo ambayo tunaweza kupata fedha za kufadhili mradi huo".

Inatarajiwa kuwa reli hiyo itaunganisha bandari ya Dar es Salaam na nchi kadhaa jirani zisizo na bandari, zikiwemo DR Congo na Rwanda.

Inaweza kusaidia kupunguza gharama za usafirishaji mizigo mkoani humo kwa asilimia 40, Mwananchi ilisema.

Tanzania inalenga kujenga mtandao wa reli wa kilomita 2,561 kwa matumaini ya kukuza biashara Afrika Mashariki na Kati.
 
Kama vipi kila nchi ijenge reli yake mpaka mpakani. Na kusiwepo na ubia wa aina yoyote ile ili kuepukana na mkanganyiko usio wa lazima siku za baadaye kama huu tunao ushuhudia hivi sasa kwenye reli ya TAZARA.
 
Mbona serikali ya TZ haina Mpango wa kujenga SGR kwenda Kigoma?.

Sasa hiyo SGR ya Uvinza - Gitega itauunganishwa vipi na bandari ya DSM?
 
Kama vipi kila nchi ijenge reli yake mpaka mpakani. Na kusiwepo na ubia wa aina yoyote ile ili kuepukana na mkanganyiko usio wa lazima siku za baadaye kama huu tunao ushuhudia hivi sasa kwenye reli ya TAZARA.
Hata TAZARA kila nchi iligharimia upande wake, ila mkataba unataka uendeshaji uwe wa pamoja na kwa mujibu wa mkataba Zambia ndiyo itakuwa inatoa Mkurugenzi Mkuu na Tanzania kutoa Naibu Mkurugenzi Mkuu.
 
Mbona serikali ya TZ haina Mpango wa kujenga SGR kwenda Kigoma?.

Sasa hiyo SGR ya Uvinza - Gitega itauunganishwa vipi na bandari ya DSM?
Huenda watajenga ni swala la muda ngoja tusubiri
 
Back
Top Bottom