Tanzania, Malawi, ICJ na Ramani mpya!

Hute

JF-Expert Member
Nov 25, 2010
6,537
6,458
JAMANI, malawi wanataka watz tu pull out the new map inayoonyesha mpaka wa nchi hizi upande wa kaskazini unapitia katikati mwa ziwa. hivi malawi ni nani hata atulazimishe watz kufutilia mbali ramani hiyo? halafu, mbona sijamsikia membe akiwaambia kuwa SISI HATUWEZI KUONDOA MAP HIYO KWASABABU NDIO RAMANI YETU SISI WATZ. who cares cama wakiamua kukubaliana na usuluhishi au kama wakiamua kuchuniane tu? nani ana hasara zaidi kati yetu sisi watz na malawi? si wao?

PILI, Malawi wanataka watz na wao tukubaliane kulipeleka suala hili ICJ. tatizo ni kwamba, tukienda ICJ kulingana na nilivyoona mkataba na hoja zingine wanazotoa malawi, given the fact that uingereza ndio wenye interest ya mafuta na gas mle, kuna uwezekano tukapigwa changa la macho na kupigwa chini kabisa. once the judgement has been delivered, watz hatutakuwa na mahali popote pa kushika na mataifa yote watatutaka sisi tuheshimu maamuzi ya mahakama. SASA, NAOMBA SERIKALI YETU ISIKUBALI SUALA HILI LIENDE ICJ. kwanini? kwasababu tukienda kule tutapigwa chini.

FAIDA YAKE NI KWAMBA, ICJ haiwezi kulipokea na kuendesha shauri hadi nchi zote mbili zikubaliane, kama nchi moja ikikataa kwamba hatutaki suala letu lije hapa, basi ICJ hawana nguvu ya jurisdiction. yaani ile mahakama ya ICJ ni kama ya ku volunteer tu hapa mwanzo kabla hamjafika, ila mkifika tu mkawapa power, basi mnatakiwa kuiheshimu. kuipa mahakama ile power ni kukubaliana pande zote mbili. ukiangalia kwasasaivi, malawi wanasema kuwa, wangependa suala hili liende ICJ lakini tz hatutaki, hivyo hakuna jurisdiction pale ICJ..naomba tushika msimamo huu huu. ajabu ni kwamba, nilimsikia membe akisema kuwa, anawahakikishia watz kuwa atalilinda ziwa, tutaipeleka malawi ICJ na tutashinda kesh, tutawashinda malawi..tusilongwe bwana membe, wewe wala usitake twende huko..tung'ang'anie hapahapa kusuluhishana kwa kupitia wasuluhishi, tukishindwa twende kwenye vita tuzipige....atakayeshinda basi ni bwana wa mwingine. na ninajua nchi za ulaya haziwezi kukubali tupigane lazima watamleta msuluhishi prudent tu na kumaliza suala hili. watz tusikubali ziwa hili liende. AU LA, BASI TUUCHUNE TU ASIWEPO MTU YEYOTE ATAKAYECHIMBA MAFUTA WALA GAS, hapo kama wao watakubali haya....wakitaka kuchimba basi wasiguse eneo letu. na, wanajeshi wa tz mkiona boat au ndege au mvuvi yeyote analeta pua yake upande wa tz, safisheni kabisa ili kuleta discipline...watz tusije dharaulika.
 
Umeelewa tofauti mkuu,

Kwanza malawi si mwanachama wa ICJ hvyo haina nguvu za kulfikisha suala hili mezani pa ICJ,

Pili elewa kuwa mkataba wa Helgooland ni BATILI hivyo hautambuliwi na UN kisheria,

Mwenye mamlaka ya kulipeka suala hili ICJ ni Tanzania na si vinginevyo.

Kuwa na ramani mpya hakuzuii majadiliano ya kidiplomasia kusonga, kumbuka kuwa kuna hatua mbili muhimu bado hatujazifikia ili tulifikishe suala hilo ICJ

1) Sisi wawili kukaa na kuafikiana kama ndugu

2) Msuluhishi nje yetu,

3) Tanzania kuamua kulifikisha ICJ

4) Nguvu ya kijeshi iikibidi japo hilo halipewi nafasi sana!

Bado meza ya majadiliano ya kidiplomasia ipo, na ipo ya kutosha, propaganda za kisiasa na kimaslahi tusiziruhusu kwa pande zote zituvuruge
 
Umeelewa tofauti mkuu,

Kwanza malawi si mwanachama wa ICJ hvyo haina nguvu za kulfikisha suala hili mezani pa ICJ,

Pili elewa kuwa mkataba wa Helgooland ni BATILI hivyo hautambuliwi na UN kisheria,

Mwenye mamlaka ya kulipeka suala hili ICJ ni Tanzania na si vinginevyo.

Kuwa na ramani mpya hakuzuii majadiliano ya kidiplomasia kusonga, kumbuka kuwa kuna hatua mbili muhimu bado hatujazifikia ili tulifikishe suala hilo ICJ

1) Sisi wawili kukaa na kuafikiana kama ndugu

2) Msuluhishi nje yetu,

3) Tanzania kuamua kulifikisha ICJ

4) Nguvu ya kijeshi iikibidi japo hilo halipewi nafasi sana!

Bado meza ya majadiliano ya kidiplomasia ipo, na ipo ya kutosha, propaganda za kisiasa na kimaslahi tusiziruhusu kwa pande zote zituvuruge
Mkuu na wewe umeelewa tofauti sana
1/Malawi ndio inayotambua uhalali wa ICJ na sio tanzania.
But Tanzania ndio wanaoweza kirahisi kuwafikisha Malawi kwenye mahakama hii!!!

2/Bado zipo sheria za umoja wa mataifa zinazopelekea nchi mwanachama kufikishwa ICJ hata kama hajaridhia mkataba wa kuundwa kwa ICJ.

3/Heligoland treaty ni mkataba halali wa kihistoria na kimataifa, unatambuliwa na kuheshimiwa duniani kote, hata Tanzania tuna utambua, kuukubali na kuuthamini sana.
 
Dont worry,Chissano anakuja kusuluhisha mkuu. Tena huyu atakuwa na experience ya jinsi mpaka upande wa MSUMBIJI ulivyogawiwa nusu kwa nusu. Wasipomsikiliza mzee huyu wakaendelea na ubishi hapo ndipo itabidi tuwachape watie adabu!:target:
 
Mkuu na wewe umeelewa tofauti sana
1/Malawi ndio inayotambua uhalali wa ICJ na sio tanzania.
But Tanzania ndio wanaoweza kirahisi kuwafikisha Malawi kwenye mahakama hii!!!

2/Bado zipo sheria za umoja wa mataifa zinazopelekea nchi mwanachama kufikishwa ICJ hata kama hajaridhia mkataba wa kuundwa kwa ICJ.

3/Heligoland treaty ni mkataba halali wa kihistoria na kimataifa, unatambuliwa na kuheshimiwa duniani kote, hata Tanzania tuna utambua, kuukubali na kuuthamini sana.

ndg yangu TZ si mwanachama wa ICJ there is no way anaweza kupelekwa huko! Unlec km amevnja principles za jus cogence! Pili,important note! Wakat wa heligoland treaty Tz was a proctrate chn ya muingereza,malawi lilikuwa koloni la muingereza,muingereza alichofanya nikujimegea maeneo atakavyo mana hakuwa na mpinzani upande wa Tanganyika, laiti mjeruman nae angekuwepo asingekubal eneo lake limegwe kiasi kile! So mkataba wa heligoland nautreat km void contract kwa 7bu party nyngne(tanganyika) haukuwa na competent party ktk mugawanyo! Mi nadhani wafanye mediation,wakishndwa Waiombe UN iwatengenezee special tribunal ambayo arbitrators watatoka mataifa tofauti! Tofauti na hapo ndg zangu ni ngv itakuja ktmika!
 
Mimi kawaida sipendi vita lakini kwa swala hili la wamalawi wakizidi inabidi wafundishwe adabu nzuri.
 
Dont worry,Chissano anakuja kusuluhisha mkuu. Tena huyu atakuwa na experience ya jinsi mpaka upande wa MSUMBIJI ulivyogawiwa nusu kwa nusu. Wasipomsikiliza mzee huyu wakaendelea na ubishi hapo ndipo itabidi tuwachape watie adabu!:target:
Mkuu usisahau kuwa maafikiano ya Msumbiji na Malawi yalifanyika miaka ya 1960s nafikiri wakati huo Msumbiji ikiongozwa na Samora Mashelli na Malawi ikiongozwa na Kamuzu Banda kama sikosei.

Pia mkataba ule uliitaka Msumbiji kutoa eneo lake lenye rutuba na milima kwa malawi ili nao wapate sehemu ya ziwa Nyasa(Sehemu ya Maji tu lakini sio na visiwa vilivyomo ndani yake!!!)

Sasa sisi watanzania tutakuwa tayari kiasi gani kupoteza ardhi yetu ili tupate sehemu ya ziwa Nyasa kama Msumbiji?
 
Mimi kawaida sipendi vita lakini kwa swala hili la wamalawi wakizidi inabidi wafundishwe adabu nzuri.
Mkuu usisahau kuwa vita inaweza kutufundisha adabu hata sisi.

Hivyo tukiamua vita tuwe tayari kwa lolote katika hayo.
 
hivi tukiingia vitani na malawi nani atapata hasara zaidi kama si tz. Isiwe kwamba malawi atapigwa sana, kwanini isemwe hivyo? kwanini isiwe tz?
 
Wabongo wanavyopiga mkwara wa vita utadhani msuli wanao kweli, vita vya siku hizi unaweza dhani unapigana na Malawi kumbe mijitu inaweza tokea mbali na midege na kulipuwa nchi yote angalia waasi katika nchi za kiarabu wanavyowekea biti serikali za na mpaka kuzing'oa kwa backup kutoka ng'ambo si unajua Malawi ni nchi yao na ni soko letu na pia soko kubwa kwa SA sasa kichafueni muuone mziki wake si ndio maana wanakaza.
 
maadam ziwa lina mafuta na gesi sioni namna gani mgogoro wa mpaka unaweza kutatuliwa kwa mazungumzo tena huku watafiti pamoja na malawi wakijua upande wa Tanzania ndio wenye mafuta na gesi nyingi zaidi, hapa suluhisho ni military option tulinde mipaka yetu sio njia nyingine yoyote!
 
Wabongo wanavyopiga mkwara wa vita utadhani msuli wanao kweli, vita vya siku hizi unaweza dhani unapigana na Malawi kumbe mijitu inaweza tokea mbali na midege na kulipuwa nchi yote angalia waasi katika nchi za kiarabu wanavyowekea biti serikali za na mpaka kuzing'oa kwa backup kutoka ng'ambo si unajua Malawi ni nchi yao na ni soko letu na pia soko kubwa kwa SA sasa kichafueni muuone mziki wake si ndio maana wanakaza.

Wacha woga wewe!! yaani wwachukue ziwa lote tukae kimya kisha kuogopa nchi zingine? hata sisi tuna marafiki wenye nguvu kijeshi kama china pia! Ila kabla ya kuangalia msaada lazima uelkewe jeshi letu lipo imara mdo kijeshi na kisaikolojia
 
Wabongo wanavyopiga mkwara wa vita utadhani msuli wanao kweli, vita vya siku hizi unaweza dhani unapigana na Malawi kumbe mijitu inaweza tokea mbali na midege na kulipuwa nchi yote angalia waasi katika nchi za kiarabu wanavyowekea biti serikali za na mpaka kuzing'oa kwa backup kutoka ng'ambo si unajua Malawi ni nchi yao na ni soko letu na pia soko kubwa kwa SA sasa kichafueni muuone mziki wake si ndio maana wanakaza.

Usiogope vita yetu itakuwa ya kikomandoo na itakuwa ya mtu na mtu. Hawajakaa sawa tuko kusini mwa nchi yao. Huku Bongo watakao bakia wajichimbie mahandaki yao watulie humo mpaka turudi. Lakini kuna haja ya kufufua JKT in full swing. Vijana wa siku hizi legelege mno.
 
JAMANI, malawi wanataka watz tu pull out the new map inayoonyesha mpaka wa nchi hizi upande wa kaskazini unapitia katikati mwa ziwa. hivi malawi ni nani hata atulazimishe watz kufutilia mbali ramani hiyo.
........hii ni ramani mpya kwa maana kwamba imeonyesha Mikoa na ama Wilaya mpya, lakini mpaka kuwa katikati ya ziwa sio suala jipya..........
 
Umeelewa tofauti mkuu,

Kwanza malawi si mwanachama wa ICJ hvyo haina nguvu za kulfikisha suala hili mezani pa ICJ,

Pili elewa kuwa mkataba wa Helgooland ni BATILI hivyo hautambuliwi na UN kisheria,

Mwenye mamlaka ya kulipeka suala hili ICJ ni Tanzania na si vinginevyo.

Kuwa na ramani mpya hakuzuii majadiliano ya kidiplomasia kusonga, kumbuka kuwa kuna hatua mbili muhimu bado hatujazifikia ili tulifikishe suala hilo ICJ

1) Sisi wawili kukaa na kuafikiana kama ndugu

2) Msuluhishi nje yetu,

3) Tanzania kuamua kulifikisha ICJ

4) Nguvu ya kijeshi iikibidi japo hilo halipewi nafasi sana!

Bado meza ya majadiliano ya kidiplomasia ipo, na ipo ya kutosha, propaganda za kisiasa na kimaslahi tusiziruhusu kwa pande zote zituvuruge
Only States are eligible to appear before the Court in contentious cases. At present, this basically means the 192 United Nations Member States.

The Court has no jurisdiction to deal with applications from individuals, non-governmental organizations, corporations or any other private entity.

However, a State may take up the case of one of its nationals and invoke against another State the wrongs which its national claims to have suffered at the hands of the latter; the dispute then becomes one between States. kwahiyo member states wa UN ndio wanaweza kupeleka suala pale, lakini both parties wanahitaji wawe na consent yao binafsi, mmmoja akikataa mwingine hawezi. hivyo watz wanatakiwa kukataa.
 
Umeelewa tofauti mkuu,

Kwanza malawi si mwanachama wa ICJ hvyo haina nguvu za kulfikisha suala hili mezani pa ICJ,

Pili elewa kuwa mkataba wa Helgooland ni BATILI hivyo hautambuliwi na UN kisheria,

Mwenye mamlaka ya kulipeka suala hili ICJ ni Tanzania na si vinginevyo.

Kuwa na ramani mpya hakuzuii majadiliano ya kidiplomasia kusonga, kumbuka kuwa kuna hatua mbili muhimu bado hatujazifikia ili tulifikishe suala hilo ICJ

1) Sisi wawili kukaa na kuafikiana kama ndugu

2) Msuluhishi nje yetu,

3) Tanzania kuamua kulifikisha ICJ

4) Nguvu ya kijeshi iikibidi japo hilo halipewi nafasi sana!

Bado meza ya majadiliano ya kidiplomasia ipo, na ipo ya kutosha, propaganda za kisiasa na kimaslahi tusiziruhusu kwa pande zote zituvuruge
usichanganye ICJ na ICC, the former deals only with states, doesn't deal with individual persons, the later deals with individual persons, hata hivyo hata ingekuwa icc bado hata kama nchi moja isingekuwa signatory wa mkataba wa roma individual ambaye ametakiwa kwa warrant of arrest angekamatwa tu kama angetembeleea nchi ambayo imesaini....ila kwa icj, hii ni mahakama ambayo iko chini ya umoja wa mataifa, hivyo unataka kusema kuwa malawi sio signatory wa mkataba wa umoja wa mataifa au tuseme malawi sio member wa UN?....
 
Mkuu usisahau kuwa maafikiano ya Msumbiji na Malawi yalifanyika miaka ya 1960s nafikiri wakati huo Msumbiji ikiongozwa na Samora Mashelli na Malawi ikiongozwa na Kamuzu Banda kama sikosei.

Pia mkataba ule uliitaka Msumbiji kutoa eneo lake lenye rutuba na milima kwa malawi ili nao wapate sehemu ya ziwa Nyasa(Sehemu ya Maji tu lakini sio na visiwa vilivyomo ndani yake!!!)

Mkuu jiulize ni kwa nini Banda huyohuyo alikataa kuongea na Tanzania lakini akaenda kuongea na kurekebisha mpaka kule Msumbiji!.Usuluhishi wetu na Malawi una utofauti kidogo kulinganisha na yale mapatano kati ya muingereza na mreno ya jinsi ya mpaka kupita ziwani. Msumbiji ilikuwa ni koloni la ureno na Malawi ilikuwa ni koloni la muingereza,hivyo watawala hao walikuwa na mandate ya kuamua on behalf of their colonies.Wakati Heligoland treaty inatengenezwa,Tanganyika haikuwa koloni la muingereza na wala uingereza haikuwa na mandate yeyote kuingia mikataba ya kimataifa on behalf of Tanganyika. Walikuwa wameambiwa na UNO-AU ya sasa- kwamba waiangalie kwa muda mpaka tupatapo uhuru Malawi yenyewe ilikuwa ni koloni lao na ndio maana waliipendelea na kuweka mpaka ufukweni. Hilo ni moja,lakini la pili ni kwamba hata treaty yenyewe ni void na absurd kwani inapingana na sheria za kimataifa za mipaka ya kwenye maji! Waingereza walijua Tanganyika haikuwa na mtawala au msemaji yeyote atakayelalamika wakati ule[kumbuka Germans walikuwa bize kuondoka na hawakuwa na interest yeyote na Tanganyika]. Ndipowalifanya ule msemo wa 'shamba la bwana heri na mbuzi wa bwana heri vyote heri' ndipo wakalipendelea koloni lao la Malawi.Duniani kote hakujawahi kuwa na mpaka[kama nchi zinatenganishwa na maji] ambao uko defined na kingo za maji! chunguza ramani zote za duniani!
 
Samora alianza kuiongoza Msumbiji mwaka1975 nchi ile ilipopata uhuru kutoka kwa Wareno.
QUOTE=Concrete;5064046]Mkuu usisahau kuwa maafikiano ya Msumbiji na Malawi yalifanyika miaka ya 1960s nafikiri wakati huo Msumbiji ikiongozwa na Samora Mashelli na Malawi ikiongozwa na Kamuzu Banda kama sikosei.

Pia mkataba ule uliitaka Msumbiji kutoa eneo lake lenye rutuba na milima kwa malawi ili nao wapate sehemu ya ziwa Nyasa(Sehemu ya Maji tu lakini sio na visiwa vilivyomo ndani yake!!!)

Sasa sisi watanzania tutakuwa tayari kiasi gani kupoteza ardhi yetu ili tupate sehemu ya ziwa Nyasa kama Msumbiji?[/QUOTE]
 
Back
Top Bottom