Tanzania Law School wamefaulu wanafunzi 23 kati ya 821 sawa na 2.8%

EINSTEIN112

JF-Expert Member
Oct 26, 2018
21,713
35,524
Kati ya wanafunzi 821 waliofanya wa kuhitimu kozi ya uwakili (stashahada ya juu ya sheria kwa vitendo) kutoka shule ya Sheria Tanzania (Law School of Tanzania), wamefaulu 23 tu ambao ni sawa na 2.8% huku 97.2% wakidaiwa kufeli.

Mwaka jana walifanya mtihani 633 wakafaulu 26 pekee sawa na 4.1%, hali iliyoibua malalamiko mengi kwa wadau wa elimu na kufanya Waziri wa Sheria na Katiba, @damasndumbaro_official kuunda Kamati ya uchunguzi.

Kamati hiyo iliyoongozwa na @harrisonmwakyembe iliwasilisha taarifa kuwa tatizo ni uwezo mdogo wa wanafunzi unaotokana na vyuo walivyosoma. Lakini matokeo ya mwaka huu yanaongeza tafakuri zaidi.

Kwanza Kamati ya Mwakyembe ililalamikiwa kuhoji walimu zaidi kuliko wanafunzi. Wanafunzi waliohojiwa ni wale tu waliopewa maelekezo na uongozi wa chuo (walipangwa). Haikufanyika rundom sampling. So inawezekana kuna matatizo mengi zaidi ya kile kilichoelezwa na Mwakyembe. Huwezi kufundisha darasa la watu 100 wakafaulu wawili tu, halafu ukajitetea eti ni uwezo mdogo wa wanafunzi. Kuna tatizo ambalo halitajwi. Uchunguzi zaidi unahitajika.!

:Malisa GJ
 

Attachments

  • FB_IMG_1682440027838.jpg
    FB_IMG_1682440027838.jpg
    54.7 KB · Views: 12
Kati ya wanafunzi 821 waliofanya wa kuhitimu kozi ya uwakili (stashahada ya juu ya sheria kwa vitendo) kutoka shule ya Sheria Tanzania (Law School of Tanzania), wamefaulu 23 tu ambao ni sawa na 2.8% huku 97.2% wakidaiwa kufeli.

Mwaka jana walifanya mtihani 633 wakafaulu 26 pekee sawa na 4.1%, hali iliyoibua malalamiko mengi kwa wadau wa elimu na kufanya Waziri wa Sheria na Katiba, @damasndumbaro_official kuunda Kamati ya uchunguzi.

Kamati hiyo iliyoongozwa na @harrisonmwakyembe iliwasilisha taarifa kuwa tatizo ni uwezo mdogo wa wanafunzi unaotokana na vyuo walivyosoma. Lakini matokeo ya mwaka huu yanaongeza tafakuri zaidi.

Kwanza Kamati ya Mwakyembe ililalamikiwa kuhoji walimu zaidi kuliko wanafunzi. Wanafunzi waliohojiwa ni wale tu waliopewa maelekezo na uongozi wa chuo (walipangwa). Haikufanyika rundom sampling. So inawezekana kuna matatizo mengi zaidi ya kile kilichoelezwa na Mwakyembe. Huwezi kufundisha darasa la watu 100 wakafaulu wawili tu, halafu ukajitetea eti ni uwezo mdogo wa wanafunzi. Kuna tatizo ambalo halitajwi. Uchunguzi zaidi unahitajika.!

:Malisa GJ
Hapo ni kwamba hata mwl naye anatatizo. Nina maana mwalimu anakuwepo darasani kumwezesha asiweza kuweza. Huwezi kusema mwanafunzi ana uwezo mdogo wakati umekabidhiwa umwezeshe
 
Sqbabu ya kufelisha hvyo watu ni nini ? Hii nchi unaweza ichapa viboko.....!! Ujinga ujinga tuuu
Nilisoma mahali jamaa aliandika uzi huko twitter sema nishascroll ushapotea.

sababu baadhi;

1.Wanafunzi kutokujua lugha kwa ufasaha.
2.Kukariri kwa vile hawaelewi maana kule lugha ni ngumu sana.
3.Kutokujibu maswali kwa ufasaha tena kwa facts maana sheria haitaki uswahili na uongo mwingi.

4.Akasema kama kawaida watu kutosoma kwa makini yaani hawaconcentrate kweny masomo kwa sana mambo ni mengi.
 
Back
Top Bottom