Tanzania Labour Law (Sheria ya Kazi Tanzania)

Nimeelewa sana mkuu sorry unaweza nisaidia majukumu ya baraza la wafanya kaz na jukumu la members wake katika halmashaur?

Nitacopy na kupaste kutoka ktk slides zangu nnazotumia ktk utoaji wa elimu ya mabaraza hayo mkuu, bahati mbaya zipo kwa kiingereza ila nadhani utaelewa.

1. To advice the management on measure to be taken to ensure that public service is delivering service with efficiency, effectiveness and higher standard in order to develop sustainable national economy.

2. To advise the management on matter relating, to the interest and welfare of public servants.

3. Advise the management on any changes on laws, rules, regulations relating to terms and conditions in the public service.

4. To advise the management of matters relating to promotion and discipline in the public service.

5. To discuss and advise on organizational plans its revenue and expenditure estimate. (mambo ya bajeti za idara, halmashauri n.k)

6. Discuss and give advice, training and staff development and

7. Enhance cooperation between workers and management in carrying out Government business


Members wanaoingia ktk baraza la wafanyakazi (kwa case ya halmashauri) ni;
1. Mkuu wa Taasisi (Mkurugenzi Mtendaji)
2. Wakuu wote wa Idara
3. Wajumbe wa kuchaguliwa mmoja mmoja kutoka kila idara
4. Wajumbe wa Halmashauri ya chama cha wafanyakazi kilichopo eneo la mwajiri.....kama kuna chama zaidi ya kimoja (manake halmashauri kuna walimu wanakuwa CWT, watumishi wa afya unakuta wapo TUGHE, watumishi wengineo unakuta wapo TALGWU) basi maana yake hapa kutakuwa na 'Master Council' na katiba yenu itakuwa imeainisha mgawango wa wajumbe watakaoingia kwenye baraza kwa uwakilishi wa kila chama cha wafanyakazi kilichopo hapo).....a representative from a 'master council'
5. Mwakilishi kutoka makao makuu ya chama cha wafanyakazi.
6. Afisa Kazi (kwa ishu za uchaguzi na uelimishaji)

Na legitimacy ya uwepo wa mabaraza ya wafanyakazi ktk taasisi za umma ni kwa mujibu wa;
  1. Presidential secular No. 1 of 1970 by J.K Nyerere – the genesis of Workers council in Tanzania. The directive to be used with observations.
  2. Public Service(Negotiating Machinery) Act No. 19 of 2003 reading with regulations of 2005
  3. Public Service Act No. 8 of 2002 reading with regulations of 2003
  4. Employment and Labour Relations Act No.6 of 2004 reading together with Rules of Codes of Good Practice GN. 42 of 2007
  5. Labour Institutions Act No. 7 of 2004 reading together with Rules of Codes of Good Practice GN.42 of 2007.
  6. United Republic of Tanzania Constitution of 1977, Article 18 (freedom of expression).
  7. ILO Conventions and Recommendations on Social Dialogues and Collective Bargaining.

  1. In Tanzania workers’ council is implemented in Public Institutions as per Public Service (Negotiating Machinery) Act No. 19 of 2003 reading with regulations of 2005. Rule 24 state that:
There shall be a workers’ council in each of the Ministry, Independent Department, Regions, Local Government Authority, Government Institutions and Executive Agencies formed in accordance with the procedures stipulated under the law providing for establishment of trade unions”. Refer section 73 of ELRA No. 6 of 2004"

NADHANI NITAKUWA NIMEJIBU VEMA SWALI LAKO MTUMISHI.
 
Wadau kuna kitu kinaitwa Gratuity,hii upewa mwajiliwa wa mkataba wa mwaka mmoja baada ya kufikia mwisho wa mkataba kabla ya Ku renew mkataba mpya . hivi hii kitu inastahiri kukatwa kodi?
 
Hivi ni section gani inazungumzia malipo baada ya mkataba kuisha? Sec 42 ya ELRC 2004 inasema severance pay ni hadi uwe terminated sasa mimi mkataba umeisha na sikuwa terminated, natambua section 42.1 inasema malipo yapo ila section 42 iko chini ya heading "other incidents of termination" naomba msaada jamank
Unapewa Gratuity 25% of total amount you accumulated during entire contract period
 
Mkuuuu!! Hapo kwenye wages me nmeshindwa kuelewa kidogo hiyo minimum wage wanayoandika 100,000 au 130,000 kwa mwezi ni mshahara wa MTU kweli kwa nyakati hizi au me ndo sielew

Maazimio ya pamoja ya Shirika la Kazi Duniani (ILO)
  • Yanahusu zaidi kanuni za kisheria ambazo zinatoa miongozo na haki katika sehemu ya kazi
  • Kwa ufupi, miongozo na haki sehemu za haki zinahusiana na;
1. Ajira za watoto: No 138/1973; 182/1999
2. Kazi za lazima: No 29/1930;105/1951
3. Ubaguzi: No.111/1958; 100/1951
4. Uhuru wa kuungana na kuingia makubaliano ya hiari ya pamoja: No.87/1948; 98/1949

Haki za mtoto S.5
  • Inazuia ajira kwa mtoto yeyote mwenye umri chini ya miaka 14
  • Mtoto mwenye umri wa miaka 14 au zaidi anaweza kuajiriwa kufanya kazi nyepesi tu,
  • Inazuia kumfanyisha mtoto kazi nyakati za usiku.
  • Ajira zinazozuliwa hapa ni pamoja na aina mbaya za ajira za mtoto kama utumwa, usafirishaji wa watoto, uwekaji rehani kwa ajili ya deni na aina zote za ajira za shuruti, biashara ya ngono na utengenezaji filamu za ngono, kuajiri watoto kwa lazima kwa shughuli za kijeshi n.k
Tazama pia Sheria ya Mtoto ya Mwaka 2009

Kazi za lazima S.6
Sheria inakataza kazi za lazima lakini inatoa nafasi kwa aina fulani za kazi za lazima kama;
  • Kazi yoyote inayotekelezwa chini ya Sheria ya Ulinzi wa Taifa ya mwaka 1966, kwa kazi ambayo ni ya kijeshi.
  • Kazi yoyote ambayo ni sehemu ya wajibu wa kawaida wa kiraia kwa raia Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
  • Kazi yoyote inayotekelezwa kwa dharura au hali ya hatari.
  • Kazi yoyote inayotolewa kwa mtu yeyote ikiwa ni matokeo ya kutiwa hatiani na mamlaka ya sheria.
Kuzuia ubaguzi sehemu ya kazi

S.7 - (1) Kila mwajiri atatakiwa kuhakikisha kwamba anaendeleza fursa sawa katika ajira na kujitahidi kuondoa ubaguzi katika sera yoyote ya ajira mazoezi kwa vitendo

(2) Mwajiri atalazimika kusajili kwa Kamishna wa Kazi, mpango wa kuendeleza fursa sawa na kutokomeza ubaguzi katika sehemu ya kazi

(3)Kamishna wa Kazi anaweza kumtaka mwajiri:-
  • Kuunda mpango wa kuendeleza fursa sawa na kutokomeza ubaguzi katika sehemu ya kazi kama inavyoelekezwa katika kifungu kidogo cha (2); na
  • Kuusajili mpango huo kwa Kamishna
  • Kutokuunda mpango huo na kuusajili ni kosa kisheria

(4) Mwajiri yeyote asifanye ubaguzi wa dhahiri au usiokuwa wa dhahiri kwa mwajiriwa, katika sera au mazoea katika moja ya sababu zifuatazo:

a)Rangi
b)Utaifa
c)Kabila au sehemu anayotoka
d)Asili
e)Uasili wa Taifa
f)Asili ya kijamii
g)Maoni ya kisiasa au kidini
h)Mwanamke au Mwanaume
i)Jinsia
j)Ujauzito
k)Kuolewa ama kutoolewa au majukumu ya familia
l)ulemavu
m)VVU/UKIMWI
n)Umri; au
o)Maisha anayoishi

HAKI KUUNGANA WAAJIRIWA

S 9 - (1) Kila mfanyakazi ana haki ya;

a)Kuunda na kujiunga na chama cha wafanyakazi.
b)Kushiriki katika kazi halali za chama cha wafanyakazi.

S 9 - (3) Mtu yeyote haruhusiwi kufanya ubaguzi kwa mfanyakazi kwa sababu huyo:-
  • Ametekeleza au alitekeleza haki yoyote chini ya Sheria hii au Sheria nyingine inayosimamiwa na Waziri.
  • Ni mwanachama au alikuwa mwanachama wa chama cha Wafanyakazi; au
  • Ameshiriki au alishiriki katika kazi halali cha chama

S 9(4) Mtu yeyote haruhusiwi kufanya ubaguzi, kwa mfanyakazi wa chama cha wafanyakazi au shirikisho kwa kukiwakilisha au kushiriki katika kazi halali za chama.

S 9(5) Mtu yeyote anayekiuka masharti ya vifungu vidogo vya (3) na (4), anatenda kosa.

S 9(6) Kwa madhumuni ya kifungu hiki;

a)“mfanyakazi” inajumuisha mwombaji wa kazi;
b)“mfanyakazi wa ngazi ya juu ya uongozi” maana yake ni mfanyakazi ambaye, kulingana na nafasi ya mfanyakazi huyo-
  1. Anatengeneza sera kwa niaba ya mwajiri; na
  2. Anaruhusiwa kuingia mikataba ya hiari kwa niaba ya mwajiri.

HAKI YA KUUNGANA WAAJIRI


S. 10 - (1) Kila mwajiri atakuwa na haki-

a)Kuunda na kujiunga na chama cha waajiri;*
b)Kushiriki katika kazi halali za chama cha waajiri,

S .10 - (2) Mtu yeyote haruhusiwi kufanya ubaguzi kwa mwajiri kwa sababu mwajiri-
  • Ametekeleza au alitekeleza haki yoyote chini ya Sheria hii au Sheria inayosimamiwa na Waziri;
  • Ni mwanachama au alikuwa mwanachama wa chama cha waajiri; au
  • Ameshiriki au alishiriki katika kazi halali za chama cha waajiri.

VIWANGO VYA AJIRA

1. Mikataba ya Ajira

a). Aina za mikataba
  1. Mkataba kwa kipindi cha muda usiotajwa (mara nyingi huitwa mkataba wa kudumu)
  2. Mkataba kwa kipindi cha muda kilichotajwa
  3. Mkataba wa kazi maalumu
Kazi maalumu - maana yake ni zile zinazotokea mara chache au za msimu ambazo sio endelevu. ( ELRA Misc. Amendment No 38 of 2015; S.4)

b). Taarifa ya maelezo ya maandishi S.15
15-(1) Mwajiri anatakiwa kumpa mfanyakazi, maelezo ya mkataba kwa maandishi kama-

i. Jina, umri, anuani ya kudumu na jinsia ya mfanyakazi
ii. Mahali alipoajiriwa
iii. Kazi yake
iv. Tarehe ya kuanza
v. Muundo na muda wa mkataba
vi. Kituo cha kazi
vii. Masaa ya kazi
viii. Ujira, njia ya ukokotoaji wake, na taarifa za mafao mengine au malipo ya vitu; na
ix. Kitu kingine kilichotajwa

(2) Kama taarifa zote zilizotajwa katika kifungu kidogo cha (1) zimeelezwa kwenye mkataba wa maandishi na mwajiri amempa mfanyakazi mkataba huo, mwajiri anaweza asitie maelezo yaliyoandikwa yaliyotajwa katika kifungu cha 14.

(3) Kama mfanyakazi haelewi maelezo yaliyoandikwa , mwajiri anatakiwa kuhakikisha kwa yanafafanuliwa kwa mfanyakazi katika hali ambayo mfanyakazi anaelewa.

(4) Pale ambapo suala lililotajwa katika kifungu kidogo cha (1) litabadilika, mwajiri atatakiwa kwa kuwasiliana na mfanyakazi, kurekebisha maelezo yaliyoandikwa ili kuendana na mabadiliko na kumtaarifu mfanyakazi mabadiliko hayo kwa maandishi.

(5) Mwajiri atatakiwa kutunza maelezo ya maandishi yaliyotajwa katika kifungu kidogo cha (1) kwa muda wa miaka mitano baada ya kusitishwa kwa ajira

(6) Ikiwa katika mwenendo wowote wa kisheria, mwajiri atashindwa kutoa mkataba wa maandishi au maelezo ya maandishi yaliyotolewa kwa mujibu wa kifungu kidogo cha (1), jukumu la kuthibitisha au kukanusha sharti la ajira linalodaiwa na lililotajwa katika kifungu kidogo cha (1) litakuwa ni la mwajiri.

(7) Masharti ya kifungu hiki hayatatumika kwa mfanyakazi ambaye anafanya kazi chini ya siku sita kwa mwezi kwa mwajiri.

2. Masaa ya Kazi

a) Masaa ya kazi – Masaa 9 kwa siku; Masaa 45 kwa wiki; na Siku 6 katika wiki yoyote

b) Si zaidi ya saa 50 ya ziada katika mzunguko wa wiki nne

c) Mwajiriwa hatatakiwa kufanya kazi zaidi ya masaa 12 kwa siku hata kama wamekubaliana hivyo (kifungu cha 19)

d) Kazi zitakazofanyika usiku kati ya saa 02:00 usiku na saa 12.00 asubuhi, Mwajiri atatakiwa kumlipa mfanyakazi angalau 5% ya mshahara wa mfanyakazi huyo kwa kila saa atakayofanya kazi usiku na kama saa anayofanya kazi ni ya ziada; 5% itakokotolewa katika kima cha saa za zaida za mfanyakazi. (Kifungu cha 20(4)).

NB:
Kazi za usiku haziruhusiwi kwa mwanamke mjamzito miezi miwili kabla ya tarehe tarajiwa ya kujifungua, au miezi miwili baada ya tarehe ya kuzaa . (Kifungu 20(2))

e) Mapumziko katika siku ya kazi
S.23 - (1): Mwajiri anatakiwa kumpa mfanyakazi ambaye amefanya kazi mfululizo kwa zaidi ya saa 5 mapumziko ya angalau dakika 60. (Break given if the job can be left unattended)

(2) Mwajiri anaweza kumtaka mfanyakazi kufanya kazi wakati wa mapumziko ikiwa tu kama kazi haiwezi kufanywa na mfanyakazi mwingine.

(3) Mwajiri hatakiwi kuwajibika kumlipa mfanyakazi katika kipindi cha mapumziko isipokuwa kama mfanyakazi anatakiwa kufanya kazi au kuwepo kwa ajili ya kazi wakati wa mapumziko


3. Ujira
a) S.26 (2): Kima cha ujira kwa saa, siku au mwezi kitatakiwa kuamuliwa kwa kufuata orodha iliyotolewa katika Jedwali la Kwanza

b). Malipo ya fedha yatakuwa katika bahasha iliyofungwa kama malipo yanafanyika kwa fedha taslimu au kwa hundi (Kifungu 27 (1)(c)); au fedha iwekwe katika akaunti ya benki ambayo mfanyakazi ameichagia mwenyewe kwa maandishi.

c). Mwajiri hatakiwi kufanya makato yoyote kwenye ujira wa mfanyakazi isipokuwa tu yale ambayo yapo kwa mujibu wa Sheria ama mfanyakazi amekubali kukatwa kuhusiana na deni.

d). Malipo yafanyike katika muda wa kazi, mahali pa kazi katika siku waliyokubaliana.


4. Likizo ya mwaka

a). Anayestahili:
Mfanyakazi mwenye miezi chini ya sita kazini hatakuwa na haki ya kupata likizo yenye malipo chini ya masharti ya sehemu hii. ELRA, see Section 29 (1)

Mfanyakazi mwenye utumishi wa chini ya miezi sita na ambaye amefanya kazi zaidi ya mara moja katika mwaka, atakuwa na haki ya kupata likizo yenye malipo chini ya masharti ya Sehemu hii kama jumla ya kipindhi alichofanya kazi kwa mwajiri huyo kinazidi miezi sita kwa mwaka huo. S.29-(1) (b)

S.30-(1) (c) “Likizo yenye malipo” maana yake ni likizo yoyote inayolipwa chini ya Sehemu hii na inayokokotolewa kwa kuangalia mshahara wa kawaida wa mfanyakazi.

S.31-(1) Likizo ya Mwaka; Mwajiri atatakiwa kutoa kwa mfanyakazia angalau siku 28 mfululizo kuhusiana na kila mzunguko wa likizo, na likizo hiyo itajumuisha siku yoyote ya sikukuu ambayo inaweza kuangukia ndani ya kipindi cha likizo

Employment and Labour Laws (Miscellaneous Amendment 2015- amends sect 31 on LEAVE

(6) Kwa makubaliano na Mfanyakazi, Mwajiri anaweza kumruhusu Mwajiriwa kumfanyia kazi katika kipindi ambacho Mfanyakazi huyo alitakiwa kuwa likizo kwa sharti kwamba mwajiriwa huyo asifanye kazi mfululizo kwa miaka miwili. (yaani unamuuzia mwajiri wako likizo yako)

(7) Mwajiri atamlipa mfanyakazi mshahara wa mwezi mmoja badala ya likizo ya mwaka ambayo mfanyakazi alitakiwa kwenda ama alitakiwa na mwajiri kumfanyia kazi badala ya kwenda likizo hiyo.


5. Likizo ya Ugonjwa (Kifungu cha 32

• siku 63 za kwanza – mshahara mzima
• siku 63 zinazofuata – nusu mshahara

Jumla ya siku 126 ambazo mfanyakazi atakuwa na haki ya likizo ya ugonjwa katika kila mzunguko wa likizo (Mzunguko wa likizo katika Sehemu hii ni miezi 36)

ED zinahesabika kama sehemu ya likizo ya ugonjwa

Likizo itatolewa kwa mfanyakazi kuwasilisha kwa mwajiri cheti cha matibabu kilichotolewa na tabibu aliyesajiliwa au tabibu mwingine yeyote anayekubalika na mwajiri, ambacho kukubalika kwake hakutakiwi kukataliwa bila sababu za msingi.

6. Likizo ya uzazi

i). Taarifa (S.33(1)) Mfanyakazi mwanamke atoe notisi kwa mwajiri kuhusiana na kusudio lake la kuchukua likizo ya uzazi angalau miezi mitatu kabla ya tarehe tarajiwa ya kujifungua na notisi hiyo italazimika kuambatana na cheti cha kitabibu.

ii). Mfanyakazi anaweza kuanza likizo ya uzazi muda wowote kutoka wiki nne kabla ya tarehe tarajiwa ya kujifungua, au tarehe ya mapema kama tabibu atathibitisha kwamba ni muhimu kwa afya ya mfanyakazi au ya mtoto wake ambaye hajazaliwa

iii). Mfanyakazi hatatakiwa kufanya kazi ndani ya wiki sita baada ya kuzaliwa kwa mtoto wake, labda tabibu awe amethibitisha kuwa anaweza kufanya hivyo. (Section 33(3)

iv). Likizo ya uzazi itakuwa siku 84 au siku 100 kama mfanyakazi atajifungua watoto zaidi ya mmoja kwa wakati mmoja. (Section 33 (6)

v). Mfanyakazi mjamzito au anayenyonyesha hataruhusiwa kufanya kazi ambazo ni hatari kwa afya yake au kwa afya ya mtoto wake., mwajiri atalazimika kumpa kazi nyingine mbadala inayofaa ikiwa inawezekana, kwa masharti na mazingira ambayo si mabaya zaidi ya masharti na mazingira yake.

vi). Mfanyakazi atakuwa na haki ya masaa hadi mawili kwa siku ya kumnyonyesha mtoto wakati wa saa za kazi.

(G.N No.47 Employment and Labour Relations (General) Regulations, 201)
"Mfanyakazi mwanamke, kwa kipindi kisichopungua miezi sita mfululizo baada ya kuisha kwa likizo ya uzazi, atatakiwa kuondoka mahali pa kazi angalau kwa masaa mawili katika wakati anaoona unafaa, kwa ajili ya kunyonyesha mtoto"

7. Likizo ya Uzazi ya baba na aina nyingine za likizo

a). Angalau siku 3 za likizo ya uzazi ya baba yenye malipo kama:
  • Likizo itachukuliwa ndani ya siku 7 tangu kuzaliwa mtoto
  • Mfanyakazi ni baba wa mtoto. (Section 34 (1)(b) and 34(1)(b)).
b)Angalau siku 4 za likizo ya malipo kwa sababu zifuatazo
  • Ugonjwa au kifo cha mtoto wa mfanyakazi
  • Kifo cha mke wa mfanyakazi, wazazi, bibi na babu, mjukuu au kitukuu
Siku 3 zilizotajwa hapo juu ni jumla ya idadi ya siku ambazo mfanyakazi ana haki bila kujali watoto wangapi wa mfanyakazi wamezaliwa ndani ya mzunguko wa likizo


NAOMBA KUWASILISHA.
 
Asante mkuu kwa ushaur wa kitaalamu Mi naomba kuuliza!

Nina Ndugu yangu alifukuzwa kazi bila utaratibu akaenda Labour kutafuta msaada,baada ya muda labour wakaandika barua ya kumruhusu arud kazin!Shirika likakataa Barua ya Labour na likampeleka mahakamani Baada ya miaka 6 hukumu ikatoka akahukumiwa miaka 2. kifungo cha nje(Hapa hakimu alimwambia usithubutu kukata rufaa)

Ni miaka 3 imepita kwa sasa yeye ni mgonjwa Anahitaji kupata stahiki zake kwasababu utaratibu haukufuatwa wakati wa kufukuzwa kazi!Je ana uwezo wowote wa kupata stahiki zake?
 
Mkuu "formal probation" ni siku ngapi na je ni sababu zipi zinaweza kupelekea probation kuwa extended..?
 
Asante mkuu kwa ushaur wa kitaalamu Mi naomba kuuliza!
Nina Ndugu yangu alifukuzwa kazi bila utaratibu akaenda Labour kutafuta msaada,baada ya muda labour wakaandika barua ya kumruhusu arud kazin!Shirika likakataa Barua ya Labour na likampeleka mahakamani Baada ya miaka 6 hukumu ikatoka akahukumiwa miaka 2 kifungo cha nje(Hapa hakimu alimwambia usithubutu kukata rufaa)!!
Ni miaka 3 imepita kwa sasa yeye ni mgonjwa Anahitaji kupata stahiki zake kwasababu utaratibu haukufuatwa wakati wa kufukuzwa kazi!Je ana uwezo wowote wa kupata stahiki zake?

Habari!

Sheria ya Ajira na mahusiano kazini imetoa utaratibu wa kushughulikia mgogoro wa uachishwaji kazi. Kimsingi kwa suala la Termination of employment Mfanyakazi anapaswa kuwasilisha mgogoro huo mbele ya Tume ya usuluhishi na Uamuzi ndani ya siku 30 tangu alipoachishwa kazi. Ikitokea umechelewa then unatakiwa kuwasilisha mgogoro huo kwa njia ya maombi ya kuomba Tume isikilize mgogoro wako nje ya muda “condonation”. Katika maombi hayo utajaza fomu maalumu ya kuwasilisha mgogoro CMA, pamoja na fomu maalumu ya Condonation, hati kiapo na taarifa ya kufanya maombi.

Katika fomu hiyo utaeleza pamoja na mambo mengine sababu za zilizokufanya uchelewe kufungua mgogoro. (Ifahamike kwamba Tume mpaka ijiridhishe kua sababu zilizokufanya uchelewe ni za msingi ndipo maombi hayo yatakubaliwa na shauri la termination litaanza kusikilizwa)

Kimsingi inatakiwa kila siku uliyochelewa uonyeshe sababu za kuchelewa. Ilitokea kulikua na uzembe Tume itatupilia mbali maombi hayo.

Sasa inapotokea kwa wakati mmoja unashauri mahakama ingine, bado haikuzuii kufungua mgogoro wa kikazi. Mara nyingi ni vyema ufungue ukiwa ndani ya muda then ufanye maombi maalum ya kusimama ukingoja kuisha kwa kesi ingine (zinatakiwa ziwe na uhusiano unaoathiriana)

Nimeona nishare na nyinyi! Kama kuna mahali sijapagusia then Wanahaki wenzangu wataongezea
 
na sheria ikoje kuhusu mfanykazi wa uma kuwa na tattoo!?

Hilo linakuwa kosa la kimaadili mkuu (misconduct)....huyo mrejeshe kwenye ile Kanuni ya Maadili ya Utumishi wa Umma aisome aielewe vizuri. Kama ni Tatoo ambayo iko eneo la wazi la kuonekana inabidi aifute.
 
Ni swali kidogo. Mfano ulipewa mkataba mwenye gratuity baada ya miaka miwili. Ila mkataba huo kila mwaka ukiisha unasaini upya. Mwaka mmoja ukaisha vema. Mwaka wa pili unataka usaini gafla kipengele kimeondolewa. Je kuna haki yoyote muajiriwa anaweza kupata hapa?
 
unajua mkuu,watz wengi hawana muda wakusoma hiyo katiba ya ili wajue sheria na haki yao inasemaje,ndio mana wengi tunaburuzwa ktk makampuni na taasisi za umma,
 
  • Thanks
Reactions: sab
Mkuu kuna kundi la wafanyakazi waliopandishwa vyeo mwaka 2016 kwa barua kutoka katibu mkuu lkn mwaka 2018 wamepewa barua ya kusitisha upandishaji wa vyeo uliofanyika mwaka 2016 na badala yake barua imewatambua kwamba wamepanda mwaka 2017 sababu ni kwamba kipindi hicho serikali ilisimamisha upandishwaji wa vyeo kutokana na zoezi la uhakiki! hapo maswali kadhaa yameibuka je wanaweza kupewa ushauri gani wa kisheria?je,waliostaafu kabla ya barua hizi mpya wanakuwa na nafasi gani?

Je, Katibu mkuu anayo mamlaka kufuta barua aliyo itoa yeye mwenyewe na kusogeza mbele wakati watumishi hao walianza kutumikia vyeo vyao vipya mara baada ya kutunukiwa?
 
Nilikuwa nafanya kazi sector binafsi kwenye mradi wa miaka 3,mkataba kwa wafanya kazi ni mwaka mmoja then una-renew.

Mkataba wangu ulikuwa from 1st April 2017 to 31st March2018, mkataba unasema ikitokea hawata renew basi one month notice itatolewa-ila all over sudden Jana tar 29.3...wametangaza haturenew mkataba na siku ya mwisho kuwepo kazini ni tar 31...sijapewa barua...ndio nataka kwenda chukua jmos.

....sijui hii imekaaje wakuu
 
Back
Top Bottom