Tanzania Labour Law (Sheria ya Kazi Tanzania)

Msaada Kwa wajuzi wa Sheria
Niliajiriwa company flani nadhani kutokana na kutokujua Sheria au njaa zangu sula la muda wa kazi kuingia na kutoka sikuzingatia
Sasa ni kwamba nafanya kazi masaa 12 Kwa siku 6 za wiki yaani napumzika siku 1 Kwa wiki.
Nilijaribu kumdokeza mwajiri kuhusu kunilipa masaa ya ziada Ila akawa kama mbogo alie jeruhiwa.
Nataka kujua endapo nitakwenda kufungua kesi je kuna uwezekano wa kupata stahiki zangu..maana hata muda wa kuingia kazini unajulikana Ila muda wa kutoka hakuna sehemu ya sign out
Lakini Nina ushahidi wa watu wanaojua muda ninaotoka.Sina daily evidence ya muda ninaotoka labda itokee kuna kitu basi namsainisha boss namwambia weka na muda uliopokea huu mzigo
Msaada Kwa wajuzi wa
Zaidi ya contract of employment unayopewa na Mwajiri, vile vile kuna Oral Contract ambayo unasaini na Mwajiri ana saini. Kwa Sheria za Tanzania, Mfanyakazi atafanya kazi kwa masaa 40 kwa wiki sawa na masaa 8 kwa siku mara siku 5.

Kinacho endelea kati yako na Mwajiri ni huruma yako tu kufanya masaa hayo 60 kwa wiki ambayo ni ziada ya masaa 12 kwa wiki. Nakushauri;
1. Nenda kaangalie tena mkataba wako ujue ni masaa mangapi ulisaini

2. Kama hayajatajwa masaa ya kazi basi mkataba una mapunhufu. Muombe Mwajiri wako mupitie upya vipengele vya mkataba ili kipengele cha masaa kikae kisheria.

3. Nenda Ofisi ya Kazi Mkoa kaombe upewe mwogozo wa masaa ya kazi ambao utautumia kumuonyesha Mwajiri kwenye kupitia vipengele vya mkataba.

4. Akishaona unauelewa wa haki zako atachukua hatua. Ila ukienda kumshhataki Mahakamani au CMA huwezi kumshinda kwa vile huna ushahidi. Na baada ya hapo kutakuwa na kutoelewana au kuaminiana na wewe.
 
Mkuu hivi kama umefanya kazi sehemu si Chini ya miaka mitatu bila mkataba wala maandishi yoyote,ikitokea mwajiri akakufukuza kazi Hapo sheria imekaaje mkuu
 
Mkuu hivi kama umefanya kazi sehemu si Chini ya miaka mitatu bila mkataba wala maandishi yoyote,ikitokea mwajiri akakufukuza kazi Hapo sheria imekaaje mkuu
Hiyo haitatambulika popote Kama hukuwa na mkataba. Labda uwe na kitabu cha mahudhurio ya kika siku ndiyo utumie kukionyesha
 
Mkuu hivi kama umefanya kazi sehemu si Chini ya miaka mitatu bila mkataba wala maandishi yoyote,ikitokea mwajiri akakufukuza kazi Hapo sheria imekaaje mkuu
Vipi kulikua Daftari la Mahudhurio?? ( Attendance) je ulipewa emails za ofisi? Kitambulisho je? Na nyaraka zozote ambazo uliwai kusaini zipo? Unazo?

Haya yanaweza kuwa kama ushahidi mahakamani na ukashinda kesi kwa kigezo cha Oral Contract.
 
Zaidi ya contract of employment unayopewa na Mwajiri, vile vile kuna Oral Contract ambayo unasaini na Mwajiri ana saini. Kwa Sheria za Tanzania, Mfanyakazi atafanya kazi kwa masaa 40 kwa wiki sawa na masaa 8 kwa siku mara siku 5.

Kinacho endelea kati yako na Mwajiri ni huruma yako tu kufanya masaa hayo 60 kwa wiki ambayo ni ziada ya masaa 12 kwa wiki. Nakushauri;
1. Nenda kaangalie tena mkataba wako ujue ni masaa mangapi ulisaini

2. Kama hayajatajwa masaa ya kazi basi mkataba una mapunhufu. Muombe Mwajiri wako mupitie upya vipengele vya mkataba ili kipengele cha masaa kikae kisheria.

3. Nenda Ofisi ya Kazi Mkoa kaombe upewe mwogozo wa masaa ya kazi ambao utautumia kumuonyesha Mwajiri kwenye kupitia vipengele vya mkataba.

4. Akishaona unauelewa wa haki zako atachukua hatua. Ila ukienda kumshhataki Mahakamani au CMA huwezi kumshinda kwa vile huna ushahidi. Na baada ya hapo kutakuwa na kutoelewana au kuaminiana na wewe.
Mkuu,,, hv inapokea employer akavunja mkataba, kwenye termination letter hakukuwa na reason yeyote ya termination, haki za mwajiriwa ni zipi,,, na kayoka hilo mkataba uko valid kwa muda wa miez 9 ijayo!!! Je muajiriwa ana haki ya kulipwa na miez yote iliyobakia? Natanguliza shukrani kwa hili
 
Habari mkuu,,
Samahani mkuu Nina shida hapa ya kisheria naomba Sana unisaidie Kama hutojali,
Sheria ya kazi inasemaje kuhusiana na madai ya wafanyakazi ambao imepita miezi 2 ambazo Ni karibia siku 60 hawajaenda mahakamani kudai stahiki zao za malipo baada ya kukaa Muda mrefu hawajalipwa na mwajiri..????
Je wakienda mahakamani kushitaki watalipwa stahiki zao au ndo malipo hayo yamepotea hivyo...???

Sent from my CPH1923 using JamiiForums mobile app
Jazz CMA F 2 pamoja na Kapoor kwa mujibu wa kanuni ya 29 utaeleza sababu ya kuchelewa kufungua shauri, kumbuka sababu iwe ya msingi tofauti na hapo shauri litafutwa.
 
Zaidi ya contract of employment unayopewa na Mwajiri, vile vile kuna Oral Contract ambayo unasaini na Mwajiri ana saini. Kwa Sheria za Tanzania, Mfanyakazi atafanya kazi kwa masaa 40 kwa wiki sawa na masaa 8 kwa siku mara siku 5.

Kinacho endelea kati yako na Mwajiri ni huruma yako tu kufanya masaa hayo 60 kwa wiki ambayo ni ziada ya masaa 12 kwa wiki. Nakushauri;
1. Nenda kaangalie tena mkataba wako ujue ni masaa mangapi ulisaini

2. Kama hayajatajwa masaa ya kazi basi mkataba una mapunhufu. Muombe Mwajiri wako mupitie upya vipengele vya mkataba ili kipengele cha masaa kikae kisheria.

3. Nenda Ofisi ya Kazi Mkoa kaombe upewe mwogozo wa masaa ya kazi ambao utautumia kumuonyesha Mwajiri kwenye kupitia vipengele vya mkataba.

4. Akishaona unauelewa wa haki zako atachukua hatua. Ila ukienda kumshhataki Mahakamani au CMA huwezi kumshinda kwa vile huna ushahidi. Na baada ya hapo kutakuwa na kutoelewana au kuaminiana na wewe.
Mkuu masaa ya kazi kwa wiki ni 45 kwa wale wenye j'mos 5hrs
 
moja kwa moja shaurr linafutwa labda awe na sababu za msingi za kuweza kuishawishi mahakama isifute shaur hilo ASANTEE
 
Habari!.Ni taratibu zipi nifuate ili kupewa uhamisho wa muda kutoka halmashauri moja kwenda nyingine au kwenda mashirika ya umma?..
 
Mkataba wa ajira, kama ilivyo desturi kwa mikataba mingine kwa mujibu wa sheria, huzaliwa, huishi na kufa; kama ilivyo kwa binadamu na viumbe hai vingine.

Unazaliwa mara baada ya mwajiriwa na mwajiri kutia saini zao. Hapo ndipo wanapouanzisha, utekelezaji wake unapoanza kuchukua hatua na kifo ni pale tu yanapoanza kujitokeza baadhi ya mambo au masuala yanayoainishwa na sheria.

Aidha, zipo taratibu maalum za kumaliza au kuua mkataba wa ajira na hii ni katika mazingira yote, iwe kwa hiari na yale ya kumaliza kwa kulazimika kulingana na sababu mbalimbali.
Kumalizika au kukoma mkataba wa ajira kwa hiari au kufikia ukomo wa kazi kulingana na wepesi wa kutekeleza majukumu ya kazi yenyewe.

Kanuni ya 4 (1)-(7) na ya 5 (1)-(5), zote ni Kanuni za Ajira na Mahusiano Kazini, Kanuni za Utendaji Bora za Mwaka 2007, zinaeleza hakuna shida kama ilivyo kumaliza, kukoma mkataba wa ajira kwa kulazimika kutokana na sababu mbalimbali za kinidhamu.

Katika uhusiano kazini, jambo mojawapo linalomfukuza mtu kazi au kusababisha kukoma mkataba wa ajira, ni utovu wa nidhamu. Hiyo ni mojawapo, kati ya sababu za msingi zinazoweza kumfanya mwajiriwa au mfanyakazi kupoteza ajira yake.

Kimsingi, kanuni hizo zinaelekeza kuwa ni sahihi kumfukuza mfanyakazi kwa sababu za kinidhamu, lakini haimaanishi kuwa mwajiri amtafutie mwajiriwa kisa cha kuzusha au kupika, ili kumwondoa kazini.
Kinachosisitizwa hapa, ni lazima sababu hizo ziwe zimejitokeza na kuthibitika kweli na ziweze kuthibitishwa pale itakapotakiwa kufanyika hivyo.

Ujenzi wa hoja kwa kushikilia mkazo kuwa nilisikia au nahisi, zitasababisha tuhuma hizo kukosa mashiko mbele ya msuluhishi, hakimu au jaji kutegemeana na shauri lilikofika.

Kanuni ya 8 (1)(d) na 12 (1)-(5), zote za Ajira na Uhusiano Kazini na Kanuni za Utendaji Bora za mwaka 2007, sanjari na Kifungu cha 37 (2), Sheria ya Ajira na Uhusiano Kazini, 2004 Sura ya 366, zote zinasisitiza ukweli na uthibitisho wa madai yanayotolewa.

Angalizo ni kwamba, sheria inaelekeza kuwa mwajiriwa au mfanyakazi, atafukuzwa kazi mara moja, bila ya hata kupatiwa barua ya onyo kwa kosa la mara ya kwanza au “summary dismissal”.

Kwa utaratibu huo, imafanya mwajiriwa, au mfanyakazi kupoteza haki zake zote za msingi kama kiinua mgongo. Kifungu cha 42 (1)-(4) cha Sheria ya Ajira na Uhusiano Kazini ya mwaka 2004 Sura ya 366 inalifafanua hilo.

Hivyo basi, ni kosa kwa mwajiri kumfukuza mfanyakazi kwa utaratibu wa mara moja, yaani ‘summary dismissal, isipokuwa kama hilo litafanyika katika mazingira ambayo sheria inaruhusu wazi kufanya hivyo na siyo kinyume chake.
Kifungu cha 41 (1)-(7) cha Sheria ya Ajira na Uhusiano Kazini ya 2004 sura ya 366 ina ufafanuzi.

Haki ya Kusikilizwa
Kila mtu ana haki ya kusikilizwa, kabla hatua ya kisheria kuchukuliwa. Ni haki ya asili, ambayo haiwezi kuondolewa na mtu au mamlaka yoyote ile. Kwa maana hiyo, pasipo kujali ukubwa wa kosa, hata kama kosa la mwajiriwa, mhusika anapaswa kupewa nafasi ya kutoa utetezi wake.

Atajitetea na kutakiwa kuwasilisha utetezi wake, dhidi ya: “Kwanini asichukuliwe hatua za kinidhamu?” Kanuni ya 13 (1)-(13) Kanuni za Ajira na Uhusiano Kazini, 2007 inaeleza.

Ni kosa kwa mwajiri au mkuu wa kazi kumfukuza mfanyakazi, bila ya kumpatia nafasi ya kumsikiliza au kujitetea. Hii siyo hiari ya mwajiri kuamua kumpatia mwajiriwa haki husika, bali ni haki ya msingi. Hiyo ni kwa sababu, haki yenyewe ipo kwa mujibu wa sheria, hivyo utekelezaji wake ni lazima.

Haki ya Malipo Stahiki

Kifungu cha 44 (1)(a) cha Sheria ya Ajira na Mahusiano Kazini ya mwaka 2004, Sura ya 366, kinaelekeza haki za msingi alizo nazo mwajiriwa atakayefukuzwa kazi, kutokana na sababu za kinidhamu. Hiyo ni pamoja na kulipwa mshahara au ujira wake.

Mshahara utalipwa kwa kuzingatia tarehe ya mshahara wa mwisho mpaka siku ambayo mwajiriwa amefukuzwa, mathalan kama tarehe ya mwisho ya kupokea mshahara itakuwa Juni 30, 2019, kisha mhusika atafukuzwa Julai 17, 2019; pesa itakayotolewa ni kwa kuzingatia siku ambazo mhusika amefanyakazi. Yaani jumla ya siku 17 kuanzia tarehe 1 hadi 17 Julai. Inatajwa kuwa haki ya msingi, wala isipuuzwe kulinda maslahi ya pande zote mbili.

Ingia hapa ujisomee sheria ya ajira na mahusiano kazini

Sheria ya ajira na mahusiano kazini

==============

Michango ya wadau


----

----

----
Habari za majukumu wakuu. Naomba msaada juu ya haya.

1. Inakuaje kama una mkataba wa ajira, halafu baada ya siku kadhaa, mwajiri akakuongezea majukumu yaliyo nje ya makubaliano/mkataba na akakutaka kuyafanya majukumu hayo kwa lazima hata kama sio professional yako.

2. Na vipi kuhusu kulipwa allowance inapotokea mwajiriwa akafanya kazi nje muda ulio katika mkataba. {kwenye mkataba imeahinishwa kuwa muda wa ziada mwajiriwa atalipwa mara mbili ya mshahara wake wa siku ikiwa atafanya kazi nje ya muda au siku kuu. Na vile vile imetundikwa kwenye kuta kama moja ya haki ya mwajiriwa. Lakini mwajiri anadai halitambui hilo!


3. Ni jambo gani mtu anatakiwa kulifanya kama mwajiri wake anatumia lugha mbaya eneo la kazi. Lugha ya matusi na kudhalilisha mbele za watu?


*Tatizo ni kila mtu anaogopa kufanya lolote kuhusu haya kwa hofu ya kupoteza ajira.

Msaada tafadhali kadri ya siku zinavyo enda hali inakuwa mbali zaidi.
@busweru
 
Wakuu habari za muda huu.
Naombeni kufahamu Sheria inasemaje kwa mtu anayetaka kurudi kwenye Utumishi wa umma baada ya kuacha au kuachishwa kazi ? Taratibu zipoje?
 
kiufupi hakuna gharama zozote za kufungua shauri sema kunatakiwa tu ujazaji mzuri wa form za cma kuna form zinakuwa 2 moja inaelezea tatizo na utaambatanisha na mchanganuo wa madai ambao kitaalamu tunaita claim schedule yani utasema unadai kipi na kipi na jumla yake alafu form ya 2 ni hati ya wito kwa muajiri wako kuitwa mahakamani zote hizo utampelekea ili audhurie kwa wito wa mahakama na ajue anadaiwa nini hivyo na wewe utabakia na kopi
Kwa mfano sijasaini mkataba lakini vielelezo vingne vipo tofauti na mkataba kwa mfano form za ofisi zenye nembo yao,group la ofisi tuliyokuwa tunashea mambo ya kazi na miamala ya pesa waliyokuwa wananitumia hela.Je naweza kufungua kesi ya madai??
 
Ofisi za CMA zipo wapi kwa dsm au idara ya ajira ya kazi zipo wapi kwa temeke??
 
Wadau, naomba kujua sheria inasemaje juu ya mwajiri private (kampuni) ambapo mwajiriwa (wafanyakaz wote kwa ujumla hawana mikataba ya kaz) hajapewa mkataba na amefanya kaz zaid ya miaka 3.....+ overtime bila malipo yyte....wakat huo huo kikipotea chochote hata daftar mfanyakaz utalipa.......mfanyakaz anafukuzwa kiholela tu bila chochote.....je huyu mfanyakaz analindwa vp na sheria?
 
Wakuu habari za muda huu.
Naombeni kufahamu Sheria inasemaje kwa mtu anayetaka kurudi kwenye Utumishi wa umma baada ya kuacha au kuachishwa kazi ? Taratibu zipoje?
Humu hamna wanasheria au wenye uzoefu wa maswala haya?
 
Wadau, naomba kujua sheria inasemaje juu ya mwajiri private (kampuni) ambapo mwajiriwa (wafanyakaz wote kwa ujumla hawana mikataba ya kaz) hajapewa mkataba na amefanya kaz zaid ya miaka 3.....+ overtime bila malipo yyte....wakat huo huo kikipotea chochote hata daftar mfanyakaz utalipa.......mfanyakaz anafukuzwa kiholela tu bila chochote.....je huyu mfanyakaz analindwa vp na sheria?
Hawa wafanyakazi bado wapo kazini?

Kisheria hao ni wafanyakazi halali kabisa na wanastahili haki zao kama wafanyakazi wengine. Wakienda CMA ndo itawasaidia na uzuri wapo wengi
 
Wadau, naomba kujua sheria inasemaje juu ya mwajiri private (kampuni) ambapo mwajiriwa (wafanyakaz wote kwa ujumla hawana mikataba ya kaz) hajapewa mkataba na amefanya kaz zaid ya miaka 3.....+ overtime bila malipo yyte....wakat huo huo kikipotea chochote hata daftar mfanyakaz utalipa.......mfanyakaz anafukuzwa kiholela tu bila chochote.....je huyu mfanyakaz analindwa vp na sheria?
Sheria ya Tanzania ya mahusiano kazini ya 2004 na maboresho yake kwa miaka iliyofuata inatambua mwajiriwa wa zaidi ya siku 90 kama muajiriwa wa kidumu iwe kuna mkataba ulioandikwa au hakuna. Stahiki zote anazostahili mwajoriwa wa kudumu zinamhusu na huyo ikiwa ni pamoja na likizo, overtime, pension, notisi ya siki 30 ya luachishwa kazi, posho ya kuachana nk. Kama mwajiriwa husika kaweka evidence zake vizuri anaweza kudai haki zake mahakamani na anaweza kushonda kabosa
 
Back
Top Bottom