Tanzania Labour Law (Sheria ya Kazi Tanzania)

Kusimamishwa kazi bila kuchukuliwa maelezo ya awali ni sahihi kwa mjibu wa sheria za kazi...!!? Au barua yakusimamishwa kazi na kuchukuliwa maelezo kipi huanza kati ya hivyo viwili.
Kwa sekta ya Umma Sheria ya Utumishi wa Umma Na. 8 ya 2002 na Kanuni zake za 2003 zimetoa mwongozo wa kushughulikia mashauri ya Nidhamu kazini.

1. Inaweza na taarifa ya uchunguzi kuhusu suala fulani ambalo Mwajiri anadhani kuna uvunjifu wa sheria.
2. Ripoti ndiyo itaonyesha ni mfanyakazi gani anahusika na vitendo vya uvunjifu wa sheria au Kanuni za ndani
3. Mwajiri atamuandikia Mfanyakazi husika barua kwa tuhuma ambazo ana muhimu na kumpa muda wa kujieza

3. Baada ya muda inatakiwa Mfanyakazi atawasilisha maelezo ya tuhuma husika kwa Mwajiri. Kama Mwajiri ataridhika na maelezo ya mtuhumiwa basi shauri litafungwa.

4. Kama Mwajiri hajaridhika ndipo atamsimamisha kazi mfanyakazi.

5. Ataunda Kamati ya kusikiliza shauri la mfanyakazi ambalo wajumbe wake wanapaswa kuwa maofisa wenye cheo zaidi ya cheo cha mtuhumiwa.

6. Kamati itamuita mtumiwa na kumpa mashtaka mtuhumiwa na muda wa kujibu tuhuma kwa mwandishi.
 
Mkataba wa ajira, kama ilivyo desturi kwa mikataba mingine kwa mujibu wa sheria, huzaliwa, huishi na kufa; kama ilivyo kwa binadamu na viumbe hai vingine.

Unazaliwa mara baada ya mwajiriwa na mwajiri kutia saini zao. Hapo ndipo wanapouanzisha, utekelezaji wake unapoanza kuchukua hatua na kifo ni pale tu yanapoanza kujitokeza baadhi ya mambo au masuala yanayoainishwa na sheria.

Aidha, zipo taratibu maalum za kumaliza au kuua mkataba wa ajira na hii ni katika mazingira yote, iwe kwa hiari na yale ya kumaliza kwa kulazimika kulingana na sababu mbalimbali.
Kumalizika au kukoma mkataba wa ajira kwa hiari au kufikia ukomo wa kazi kulingana na wepesi wa kutekeleza majukumu ya kazi yenyewe.

Kanuni ya 4 (1)-(7) na ya 5 (1)-(5), zote ni Kanuni za Ajira na Mahusiano Kazini, Kanuni za Utendaji Bora za Mwaka 2007, zinaeleza hakuna shida kama ilivyo kumaliza, kukoma mkataba wa ajira kwa kulazimika kutokana na sababu mbalimbali za kinidhamu.

Katika uhusiano kazini, jambo mojawapo linalomfukuza mtu kazi au kusababisha kukoma mkataba wa ajira, ni utovu wa nidhamu. Hiyo ni mojawapo, kati ya sababu za msingi zinazoweza kumfanya mwajiriwa au mfanyakazi kupoteza ajira yake.

Kimsingi, kanuni hizo zinaelekeza kuwa ni sahihi kumfukuza mfanyakazi kwa sababu za kinidhamu, lakini haimaanishi kuwa mwajiri amtafutie mwajiriwa kisa cha kuzusha au kupika, ili kumwondoa kazini.
Kinachosisitizwa hapa, ni lazima sababu hizo ziwe zimejitokeza na kuthibitika kweli na ziweze kuthibitishwa pale itakapotakiwa kufanyika hivyo.

Ujenzi wa hoja kwa kushikilia mkazo kuwa nilisikia au nahisi, zitasababisha tuhuma hizo kukosa mashiko mbele ya msuluhishi, hakimu au jaji kutegemeana na shauri lilikofika.

Kanuni ya 8 (1)(d) na 12 (1)-(5), zote za Ajira na Uhusiano Kazini na Kanuni za Utendaji Bora za mwaka 2007, sanjari na Kifungu cha 37 (2), Sheria ya Ajira na Uhusiano Kazini, 2004 Sura ya 366, zote zinasisitiza ukweli na uthibitisho wa madai yanayotolewa.

Angalizo ni kwamba, sheria inaelekeza kuwa mwajiriwa au mfanyakazi, atafukuzwa kazi mara moja, bila ya hata kupatiwa barua ya onyo kwa kosa la mara ya kwanza au “summary dismissal”.

Kwa utaratibu huo, imafanya mwajiriwa, au mfanyakazi kupoteza haki zake zote za msingi kama kiinua mgongo. Kifungu cha 42 (1)-(4) cha Sheria ya Ajira na Uhusiano Kazini ya mwaka 2004 Sura ya 366 inalifafanua hilo.

Hivyo basi, ni kosa kwa mwajiri kumfukuza mfanyakazi kwa utaratibu wa mara moja, yaani ‘summary dismissal, isipokuwa kama hilo litafanyika katika mazingira ambayo sheria inaruhusu wazi kufanya hivyo na siyo kinyume chake.
Kifungu cha 41 (1)-(7) cha Sheria ya Ajira na Uhusiano Kazini ya 2004 sura ya 366 ina ufafanuzi.

Haki ya Kusikilizwa
Kila mtu ana haki ya kusikilizwa, kabla hatua ya kisheria kuchukuliwa. Ni haki ya asili, ambayo haiwezi kuondolewa na mtu au mamlaka yoyote ile. Kwa maana hiyo, pasipo kujali ukubwa wa kosa, hata kama kosa la mwajiriwa, mhusika anapaswa kupewa nafasi ya kutoa utetezi wake.

Atajitetea na kutakiwa kuwasilisha utetezi wake, dhidi ya: “Kwanini asichukuliwe hatua za kinidhamu?” Kanuni ya 13 (1)-(13) Kanuni za Ajira na Uhusiano Kazini, 2007 inaeleza.

Ni kosa kwa mwajiri au mkuu wa kazi kumfukuza mfanyakazi, bila ya kumpatia nafasi ya kumsikiliza au kujitetea. Hii siyo hiari ya mwajiri kuamua kumpatia mwajiriwa haki husika, bali ni haki ya msingi. Hiyo ni kwa sababu, haki yenyewe ipo kwa mujibu wa sheria, hivyo utekelezaji wake ni lazima.

Haki ya Malipo Stahiki

Kifungu cha 44 (1)(a) cha Sheria ya Ajira na Mahusiano Kazini ya mwaka 2004, Sura ya 366, kinaelekeza haki za msingi alizo nazo mwajiriwa atakayefukuzwa kazi, kutokana na sababu za kinidhamu. Hiyo ni pamoja na kulipwa mshahara au ujira wake.

Mshahara utalipwa kwa kuzingatia tarehe ya mshahara wa mwisho mpaka siku ambayo mwajiriwa amefukuzwa, mathalan kama tarehe ya mwisho ya kupokea mshahara itakuwa Juni 30, 2019, kisha mhusika atafukuzwa Julai 17, 2019; pesa itakayotolewa ni kwa kuzingatia siku ambazo mhusika amefanyakazi. Yaani jumla ya siku 17 kuanzia tarehe 1 hadi 17 Julai. Inatajwa kuwa haki ya msingi, wala isipuuzwe kulinda maslahi ya pande zote mbili.

Ingia hapa ujisomee sheria ya ajira na mahusiano kazini

Sheria ya ajira na mahusiano kazini

==============

Michango ya wadau


----

----

----
Naomba unitumie hizo Sheria kwa 0762904054(WhatsApp)

Sent using Jamii Forums mobile app
 
mm naomba kufahamu juu ya hii case yangu nitaweza kusolve vipi, nilipata kazi kwenye kampuni Fulani inaendeshwa na wahindi lakini ni zaidi ya miaka miwili sijapatiwa mkataba wa kudumu na hata malipo ninayoyapata hayaendani na viwango kisheria Nina bachelor degree lakini nalipwa chini ya laki 6, mshahara naweza nisiangalie sana lakini nakosa haki za msingi mfano likizo sipati, sipo kwenye mifuko ya kijamii hata Ikitokea nafukuzwa kazi sina cha kujitetea lakini kabla ya hayo yote kutokea naomba nipate darasa nini nifanye ili miaka yangu miwili ya kuwatumikia hawa watu isipotee bure, na sio kwangu tu ninawafanyakaz wenzangu pia wanatatizo kama hili.

don't waste your time on lecturing me, this is 2020

Upo mkoa gani wewe mkuu?
 
Naomba msaada wakisheria please, mnapo sainishana mkataba na mwajiri najua haya nimakubaliano kati ya mwajiri najua mwajiriwa...
Kwa mfano ndani ya mkataba kuna kipengere cha Medical Insurance, ambayo inamutaka mwajiriwa achangie 3% na mwajiri nayeye achangie 3%, mwisho wa siku mwajiri anasema ameshindwa kumuhudumia mfanyakazi kwenye huduma hiyo ya Medical Insurance wakati mkataba unaonyesha kwamba mwajiri atapata matibabu kwa mjibu wa mkataba.
Je hapa sheria inasemaje baada ya mwajiri kuvunja vifungu vya mkataba..!!?

Naomba msaada tafadhali

Kwa masuala yote ya kukiukwa vipengele vya mkataba (breach of contract agreement) kama mfano hilo ulilotaja unatakiwa kufungua shauri ktk Tume ya Usuluhishi na Uamuzi wa Migogoro ya Kikazi (tunaitwa CMA) katika mkoa uliopo/unaofanyia kazi

Kwa masuala yote uvunjifu wa sheria za kazi (breach of labour laws) mfano kufanyishwa kazi zaidi ya masaa ya kisheria bila kulipwa malipo ya ziada (overtime), kulipwa ujira ulio chini ya viwango vya kisheria, kutokupewa likizo, kubaguliwa sehem ya kazi n.k haya ya nature hii unawasilisha ktk Ofisi ya Idara ya Kazi ktk mkoa wako ulipo/unakofanyia kazi ili wayashughulikie
 
Habari wakuu!.

Naomba kujulishwa kwa mujibu wa sheria.Ni mambo gani uangaliwa kwenye fedha za kujikimu anazopewa muajiriwa mpya pindi anapo report kazini?.Na je,tofauti ya malipo ya fedha ya kujikimu kwa waajiriwa wa level moja serikalini kutofautiana uzingatia nini?.



Sent using Jamii Forums mobile app
 
mm naomba kufahamu juu ya hii case yangu nitaweza kusolve vipi, nilipata kazi kwenye kampuni Fulani inaendeshwa na wahindi lakini ni zaidi ya miaka miwili sijapatiwa mkataba wa kudumu na hata malipo ninayoyapata hayaendani na viwango kisheria Nina bachelor degree lakini nalipwa chini ya laki 6, mshahara naweza nisiangalie sana lakini nakosa haki za msingi mfano likizo sipati, sipo kwenye mifuko ya kijamii hata Ikitokea nafukuzwa kazi sina cha kujitetea lakini kabla ya hayo yote kutokea naomba nipate darasa nini nifanye ili miaka yangu miwili ya kuwatumikia hawa watu isipotee bure, na sio kwangu tu ninawafanyakaz wenzangu pia wanatatizo kama hili.

don't waste your time on lecturing me, this is 2020

Naomba uweke wazi kwenye hili hapa : zaidi ya miaka miwili sijapatiwa mkataba wa kudumu:

malipo ninayoyapata hayaendani na viwango kisheria Nina bachelor degree lakini nalipwa chini ya laki 6 hili swali kwa mujibu ya minimum wage order ya mwaka 2013 inahainisha kila sekta na kiwango cha pesa yake sasa ungesema unafanya sekta ipi ili upewe jibu je iyo pesa ni kubwa au ndogo

sipo kwenye mifuko ya kijamii hapa wanakuwa wametenda makosa 2 kwa mujibu wa sheria ya nssf ya mwaka 1997 namarejeo yake ya 2018 ni kosa kwa muajiri wa sekta binafsi kutojisajili na mfuko sasa inawezekana hajajisajili na mfuko ndio maana hata wafanyakazi wake hawachangii nssf ilo kosa la kwanza kosa la 2 kutokukulipia wewe kama mfanyakazi wao ambapo kisheria anatakiwa apigwe penati ya asilimia 10% kwa kila mchango wa kila mwezi kwa muda huo wa miaka 2

hata Ikitokea nafukuzwa kazi sina cha kujitetea kuna mamlaka husika ambazo hutatua kesi zote baina ya muajiri na muajiriwa inaitwa tume ya utatuzi na usukuhishi ( CMA) hivyo haki yako haitapotea

Nini cha kufanya kama una uhakika wa kupata kazi nyingine wafungulie shtaka mahakama ya kazi iliyopo karibu na wewe kama upo dar es salaam zimegawika kwa mkoa mfano kinondoni, ilala na temeke na utawapelekea samansi ya kesi na wito wa kuitwa mahakama ya kazi na madai yako yatakuwa kama ifuatavyo

kufanyishwa kazi bila kuwa na mkataba kwa muda wa miaka 2
kutoenda likizo kwa muda wa miaka 2
kutochangiwa kwenye mfuko wowote wa kijamii
kulipwa mshahara kima cha chini tofauti na maelekezo ya minimum wage order ya 2013 ila hii inategemea upo sekta ipi

Angalizo utakapoanza hayo mambo hakikisha unakazi nyingine ipo mkononi.
 
TUNASHUKURU SANA KWA MAELEZO YAKO, SASA NDUGU YANGU , NISAIDIE HAPA UKO KWENYE KAMPUNI BINAFISI UNAPEWA MKATABA MFANO WA MWAKA MMOJA BAADA YA MKATABA KUISHA MWAJILI ANASEMA ATAKUPATIA MKATABA MWINGINE SIKU ZINAZIDI KWENDA MPAKA LABDA MIEZI 6 AFU ANAKUJA KUKUSIMAMISHA KAZI NA ANADAI MKATABA WAKO ULIKUWA UMEISHA JE KATIKA MAZINGIRA HAYO HAKI ZAKO NI ZIPI HAPO

ipo hivi kwa mujibu wa sheria ya ajira na mahusiano kazini ya mwaka 2004 na kanuni zake za mwaka 2007 kuhusu mkataba wa muda maalumu kukoma wenyewe pale muda wake unapofika tuseme mkataba wako ulitakiwa kuisha 2020 january na ilipofika boss wako hakutoa notes ya kuonesha mkataba utakapokaribia kuisha siku 28 kabla kwamba hawatakupa mkatba mpya ikafika mwezi wa 2 wakakulipa mshahara mwezi wa 3 akakulipa mshahara hapo sheria inatambua mkataba ule umekuwa mpya yani mi miezi 12 mingine sasa akija kukuachisha kwa kigezo mkataba uliisha na muda ulikuepo kwenye mktaba kuisha na yeye kukaa kimya kosa ni lake mwenyewe na anatiwa kulipa miezi iliyobaki.
 
Kwa masuala yote ya kukiukwa vipengele vya mkataba (breach of contract agreement) kama mfano hilo ulilotaja unatakiwa kufungua shauri ktk Tume ya Usuluhishi na Uamuzi wa Migogoro ya Kikazi (tunaitwa CMA) katika mkoa uliopo/unaofanyia kazi

Kwa masuala yote uvunjifu wa sheria za kazi (breach of labour laws) mfano kufanyishwa kazi zaidi ya masaa ya kisheria bila kulipwa malipo ya ziada (overtime), kulipwa ujira ulio chini ya viwango vya kisheria, kutokupewa likizo, kubaguliwa sehem ya kazi n.k haya ya nature hii unawasilisha ktk Ofisi ya Idara ya Kazi ktk mkoa wako ulipo/unakofanyia kazi ili wayashughulikie

Safi majibu mazuri sana japo kuipata iyo haki sasa hapo ndipo ilipo changamoto
 
Per diem ndio nini?
Naomba kufahamu juu ya PER-DIEM hivi nikweli PER-DIEM inaondoa uharali wakulipwa masaa ya ziada yani (OVERTIME) Mwajiri wangu ananiambia kwamba kama ananilipa PER-DIEM hawezi kunilipa overtimes, kituo changu cha kazi ni DSM, ila kampuni imepata kazi huku Mbeya, hivyo nimeondoka sehemu yakituo changu kwa ajiri ya hii kazi na ninafanya masaa zaidi ya nane kila siku iendayo kwa Mungu bila kupumunzika, je nisasa kutokulipwa overtime kisa mwajiri ananipa PER-DIEM...!!?

Naomba kusaidiwa hapo tafadhali.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Je muajili asipo toa mkataba kwa muda wa miaka 2 then mwishon ana kufukuza kazi je yupo sahihi au ana kosa na je nikipewa mkataba siku ambayo ana nifukuzisha kazi ndipo Ni sain je nikubali au nigome msahada jaman
 
Naomba kufahamu Kuwa mfano kampuni aipeleki pesa ktk mfuko wa jamoi nssf kwa muda wa miaka miwili akuna ata sent tano na ninapo kwenda nssf Wanadai awanaditell za kuniusu Mimi Kama kweli michango yangu ina kwenda nilipo kuwa nafanyia kazi napewa salary slip ambazo zinaonesha ukatwaji wa pesa na kupelekwa kwao je endapo ikitokea gafra kampuni yangu imesepa je pesa zangu nazipataje angali nssf Wana kanusha kuwa awaja pokea pesa za michango yangu na kampuni Ina dai imepeleka pesa Nini ushauli je Mimi natakiwa kuwalipot kampuni au nssf
 
Naomba kufahamu Kuwa mfano kampuni aipeleki pesa ktk mfuko wa jamoi nssf kwa muda wa miaka miwili akuna ata sent tano na ninapo kwenda nssf Wanadai awanaditell za kuniusu Mimi Kama kweli michango yangu ina kwenda nilipo kuwa nafanyia kazi napewa salary slip ambazo zinaonesha ukatwaji wa pesa na kupelekwa kwao je endapo ikitokea gafra kampuni yangu imesepa je pesa zangu nazipataje angali nssf Wana kanusha kuwa awaja pokea pesa za michango yangu na kampuni Ina dai imepeleka pesa Nini ushauli je Mimi natakiwa kuwalipot kampuni au nssf
Kama NSSF wanatimiza majukumu yao wanapaswa wawe wamemshtaki Mwajiri wako kwa kutowasilisha michango yako kwenyebtawi lao lililo karibu na Mwajiri wako.

Kama Mwajiri kasepa itakuwa imekula kwako
 
Kama NSSF wanatimiza majukumu yao wanapaswa wawe wamemshtaki Mwajiri wako kwa kutowasilisha michango yako kwenyebtawi lao lililo karibu na Mwajiri wako.

Kama Mwajiri kasepa itakuwa imekula kwako
Kweli Ni tatizo tunapo kwenda kuwapa tarifa nssf wanasema wanalifanyia kazi miaka sasa
 
Mkataba wa ajira, kama ilivyo desturi kwa mikataba mingine kwa mujibu wa sheria, huzaliwa, huishi na kufa; kama ilivyo kwa binadamu na viumbe hai vingine.

Unazaliwa mara baada ya mwajiriwa na mwajiri kutia saini zao. Hapo ndipo wanapouanzisha, utekelezaji wake unapoanza kuchukua hatua na kifo ni pale tu yanapoanza kujitokeza baadhi ya mambo au masuala yanayoainishwa na sheria.

Aidha, zipo taratibu maalum za kumaliza au kuua mkataba wa ajira na hii ni katika mazingira yote, iwe kwa hiari na yale ya kumaliza kwa kulazimika kulingana na sababu mbalimbali.
Kumalizika au kukoma mkataba wa ajira kwa hiari au kufikia ukomo wa kazi kulingana na wepesi wa kutekeleza majukumu ya kazi yenyewe.

Kanuni ya 4 (1)-(7) na ya 5 (1)-(5), zote ni Kanuni za Ajira na Mahusiano Kazini, Kanuni za Utendaji Bora za Mwaka 2007, zinaeleza hakuna shida kama ilivyo kumaliza, kukoma mkataba wa ajira kwa kulazimika kutokana na sababu mbalimbali za kinidhamu.

Katika uhusiano kazini, jambo mojawapo linalomfukuza mtu kazi au kusababisha kukoma mkataba wa ajira, ni utovu wa nidhamu. Hiyo ni mojawapo, kati ya sababu za msingi zinazoweza kumfanya mwajiriwa au mfanyakazi kupoteza ajira yake.

Kimsingi, kanuni hizo zinaelekeza kuwa ni sahihi kumfukuza mfanyakazi kwa sababu za kinidhamu, lakini haimaanishi kuwa mwajiri amtafutie mwajiriwa kisa cha kuzusha au kupika, ili kumwondoa kazini.
Kinachosisitizwa hapa, ni lazima sababu hizo ziwe zimejitokeza na kuthibitika kweli na ziweze kuthibitishwa pale itakapotakiwa kufanyika hivyo.

Ujenzi wa hoja kwa kushikilia mkazo kuwa nilisikia au nahisi, zitasababisha tuhuma hizo kukosa mashiko mbele ya msuluhishi, hakimu au jaji kutegemeana na shauri lilikofika.

Kanuni ya 8 (1)(d) na 12 (1)-(5), zote za Ajira na Uhusiano Kazini na Kanuni za Utendaji Bora za mwaka 2007, sanjari na Kifungu cha 37 (2), Sheria ya Ajira na Uhusiano Kazini, 2004 Sura ya 366, zote zinasisitiza ukweli na uthibitisho wa madai yanayotolewa.

Angalizo ni kwamba, sheria inaelekeza kuwa mwajiriwa au mfanyakazi, atafukuzwa kazi mara moja, bila ya hata kupatiwa barua ya onyo kwa kosa la mara ya kwanza au “summary dismissal”.

Kwa utaratibu huo, imafanya mwajiriwa, au mfanyakazi kupoteza haki zake zote za msingi kama kiinua mgongo. Kifungu cha 42 (1)-(4) cha Sheria ya Ajira na Uhusiano Kazini ya mwaka 2004 Sura ya 366 inalifafanua hilo.

Hivyo basi, ni kosa kwa mwajiri kumfukuza mfanyakazi kwa utaratibu wa mara moja, yaani ‘summary dismissal, isipokuwa kama hilo litafanyika katika mazingira ambayo sheria inaruhusu wazi kufanya hivyo na siyo kinyume chake.
Kifungu cha 41 (1)-(7) cha Sheria ya Ajira na Uhusiano Kazini ya 2004 sura ya 366 ina ufafanuzi.

Haki ya Kusikilizwa
Kila mtu ana haki ya kusikilizwa, kabla hatua ya kisheria kuchukuliwa. Ni haki ya asili, ambayo haiwezi kuondolewa na mtu au mamlaka yoyote ile. Kwa maana hiyo, pasipo kujali ukubwa wa kosa, hata kama kosa la mwajiriwa, mhusika anapaswa kupewa nafasi ya kutoa utetezi wake.

Atajitetea na kutakiwa kuwasilisha utetezi wake, dhidi ya: “Kwanini asichukuliwe hatua za kinidhamu?” Kanuni ya 13 (1)-(13) Kanuni za Ajira na Uhusiano Kazini, 2007 inaeleza.

Ni kosa kwa mwajiri au mkuu wa kazi kumfukuza mfanyakazi, bila ya kumpatia nafasi ya kumsikiliza au kujitetea. Hii siyo hiari ya mwajiri kuamua kumpatia mwajiriwa haki husika, bali ni haki ya msingi. Hiyo ni kwa sababu, haki yenyewe ipo kwa mujibu wa sheria, hivyo utekelezaji wake ni lazima.

Haki ya Malipo Stahiki

Kifungu cha 44 (1)(a) cha Sheria ya Ajira na Mahusiano Kazini ya mwaka 2004, Sura ya 366, kinaelekeza haki za msingi alizo nazo mwajiriwa atakayefukuzwa kazi, kutokana na sababu za kinidhamu. Hiyo ni pamoja na kulipwa mshahara au ujira wake.

Mshahara utalipwa kwa kuzingatia tarehe ya mshahara wa mwisho mpaka siku ambayo mwajiriwa amefukuzwa, mathalan kama tarehe ya mwisho ya kupokea mshahara itakuwa Juni 30, 2019, kisha mhusika atafukuzwa Julai 17, 2019; pesa itakayotolewa ni kwa kuzingatia siku ambazo mhusika amefanyakazi. Yaani jumla ya siku 17 kuanzia tarehe 1 hadi 17 Julai. Inatajwa kuwa haki ya msingi, wala isipuuzwe kulinda maslahi ya pande zote mbili.

Ingia hapa ujisomee sheria ya ajira na mahusiano kazini

Sheria ya ajira na mahusiano kazini

==============

Michango ya wadau


----

----

----
Thanks kaka naomba msaada wako pia kwa hili. Kazin kwetu tumeambiwa kwa njia ya sim kuwa tutatumiwa form ya kusain ili kuchukua rikizo ya miezi mitatu isiyokuwa na malipo je ni haki kisheria?. Na kingine jinsi ya kukokotoa holidays endapo unahitaji kuacha kazi saraly 300 kwa mwezi
 
Na je akifanyiwa termination hakuna haki zake za msingi ukilinganisha na haki ambazo angepata akifanyiwa early retirement?
Ukishamaliza mzunguka wa likizo yako ya ugonjwa kama ulivyoainisha hapo juu, na ukawa bado haujapona kuweza kuendelea na kazi, basi mwajiri anaweza kuangalia kama una likizo za aina ingine ambazo haujachukua (mfano zile annual leave za siku 28), ikiwa nazo ulishamaliza, basi ktk good practice wewe mtakaa na mwajiri wako mshauriane aidha ustaafu mapema zaid (early retirement) ama pia anaruhusiwa kusitisha ajira yako kutokana na sababu za ugonjwa (termination on medical grounds).

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Habari wakuu

Sheria ipoje ikiwa mfanya kazi kaacha kazi baada ya kumaliza likizo lakin yupo ndani ya mkataba an vp swala NSSF kwa tajir kutoa barua na kutotoa barua no amri yake?


Sent using Jamii Forums mobile app

Sheria ya shirika la taifa la hifadhi ya jamii marejeo ya mwaka 2018, inaweka wazi kabisa itafanya malipo ya mwanachama wa aina 2
a) kuachishwa kazi maana yake ikiwemo ukomo wa mkataba au kuachishwa kwazi kwa sababu yoyote ile kwa mujibu wa sheria ya ajira na mahusiano kazini mwaka 2004 na kanuni za ajira na mahusiano kazini mwaka 2007
b) Kupunguzwa kazini

Fomu ya NSSF/UB1 inasehemu za kuweka tiki katika vipengele tajwa hapo juu ila ukiacha kazi mwenyewe NSSF haina ilo fao kwa sasa

Kumbuka: Malipo haya atalipwa tu mfanyakazi ambaye hana ujuzi ila kwa mfanyakazi mwenye ujuzi atalipwa 30% ya jumla ya michango yake ila kama ilo utaliona gumu basi utasubiri ukifika miaka 55
 
Back
Top Bottom