Stuxnet
JF-Expert Member
- Feb 12, 2011
- 10,369
- 17,935
Kwa sekta ya Umma Sheria ya Utumishi wa Umma Na. 8 ya 2002 na Kanuni zake za 2003 zimetoa mwongozo wa kushughulikia mashauri ya Nidhamu kazini.Kusimamishwa kazi bila kuchukuliwa maelezo ya awali ni sahihi kwa mjibu wa sheria za kazi...!!? Au barua yakusimamishwa kazi na kuchukuliwa maelezo kipi huanza kati ya hivyo viwili.
1. Inaweza na taarifa ya uchunguzi kuhusu suala fulani ambalo Mwajiri anadhani kuna uvunjifu wa sheria.
2. Ripoti ndiyo itaonyesha ni mfanyakazi gani anahusika na vitendo vya uvunjifu wa sheria au Kanuni za ndani
3. Mwajiri atamuandikia Mfanyakazi husika barua kwa tuhuma ambazo ana muhimu na kumpa muda wa kujieza
3. Baada ya muda inatakiwa Mfanyakazi atawasilisha maelezo ya tuhuma husika kwa Mwajiri. Kama Mwajiri ataridhika na maelezo ya mtuhumiwa basi shauri litafungwa.
4. Kama Mwajiri hajaridhika ndipo atamsimamisha kazi mfanyakazi.
5. Ataunda Kamati ya kusikiliza shauri la mfanyakazi ambalo wajumbe wake wanapaswa kuwa maofisa wenye cheo zaidi ya cheo cha mtuhumiwa.
6. Kamati itamuita mtumiwa na kumpa mashtaka mtuhumiwa na muda wa kujibu tuhuma kwa mwandishi.