Tanzania kwa nini haihamasishi mauzo ya nyama ya punda China wakati soko liko kubwa mno?

China nyama ya Punda na ngozi za punda zina soko kubwa mno .Kwa nini serikali haihamasishi ufugaji mkubwa wa punda Tanzania na kuanzisha minada ya punda?
Kuna balozi huko sijui wanafanya nini hasa. Nje kuna fursa sana za kuongeza ajira kupitia bidhaa zetu, ila ndio hivyo mabalozi wetu akina Retired General.

Mimi naamini tunahitaji majasusi wa kiuchumi, waende wakiwa na mtazamo wa kutafuta masoko ya bidhaa zetu kama Asali, Nyama ya Punda, Maua, Organic Products n.k.n.k.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kuna balozi huko sijui wanafanya nini hasa. Nje kuna fursa sana za kuongeza ajira kupitia bidhaa zetu, ila ndio hivyo mabalozi wetu akina Retired General.

Mimi naamini tunahitaji majasusi wa kiuchumi, waende wakiwa na mtazamo wa kutafuta masoko ya bidhaa zetu kama Asali, Nyama ya Punda, Maua, Organic Products n.k.n.k.

Sent using Jamii Forums mobile app
CHINA ndio wanaongoza duniani kwa majasusi wa kiuchumi kwa sasa ndio maana ukuaji uchumi wao ni tishio
 
Kuongea ni rahisi, kutekeleza ni vigumu.

Angalia waafrika tusivyojua kujipanga


Tanzania yaikalia kooni China usafirishaji wa ngozi ya punda

Hatimaye China imeanza mpango wa kuzalisha mazao ya punda katika miji yake ili kukabiliana na zuio la baadhi ya nchi za Afrika ambazo zimepiga marufuku usafirishaji wa nyama na ngozi ya punda kwenda katika nchi hiyo.


Tanzania imeungana na nchi nyingine za Afrika kama vile Uganda, Botswana, Niger, Burkina Faso, Mali, na Senegal kupiga marufuku biashara ya kuuza punda kwasababu inatishia kutoweka kwa wanyama hao ambao wanatumiwa na wakazi wengi wa bara hilo katika shughuli za kiuchumi ikiwemo kusafirisha mizigo na kulima.


Uamuzi wa kuzalisha punda wengi nchini China umefikiwa na kampuni ya Dong-E-E-Jiao ambayo inajihusisha na uagizaji wa ngozi ya punda kutoka nchi mbalimbali duniani ili kutengeneza dawa ya asili ijulikanao kama ‘ejiao’.


Akihojiwa na gazeti la Financial Times, Makamu rais wa kampuni hiyo, Liu Guangyuan amesema wanaagiza ngozi 450,000 za punda kila mwaka ambapo bei yake imepanda maradufu hadi kufikia Dola za Marekani 473 (Tsh. Milioni 1.065) kwa ngozi moja.


Kutokana na ongezeko la mahitaji ya ngozi wanapanga kufungua vituo vya uzalishaji wa mazao ya punda ili kukidhi mahitaji ya wateja wa dawa ya ‘ejiao’.


“Dong-E-E-Jiao imewekeza kwenye vituo vya uzalishaji katika majimbo 3 ya Kaskazini mwa China, ikitumia upandikizaji wa mbegu wa punda wakubwa ambao ngozi yake ni kubwa kuliko punda wa kawaida” amesema Liu na kuongeza kuwa,


“Hadi 2020 vituo vya uzalishaji vitatengeneza ngozi ya punda ya kutosha kukidhi mahitaji ya msingi”.


Amebainisha kuwa wakati wanaendelea kujenga vituo vya uzalishai, wamezigeukia nchi za Amerika ya Kusini ikiwemo Brazil, Colombia na Mexico ambazo zimefungua milango ya kuuza ngozi ya punda ili kujipatia faida kubwa.
 
wakiisha shida gani soko kama lipo hamasisha uzalishaji uongezeke watu waache kufuga kuku kondoo hata ngombe wafuge punda
Punda hawazaliani kwa wingi kama hao wanyama wengine uliowataja. Kama hao wachina wanapenda sana hao punda waje wafuge wao punda kisha wapeleke china kuuza nyama.

BTW kwa nini china hawafugi punda? Mbona kitimoto wanaongoza kwa kufuga duniani? Kwa nini hawafugi punda kama wanapenda nyama yao?
 
Angalia waafrika tusivyojua kujipanga


Tanzania yaikalia kooni China usafirishaji wa ngozi ya punda

Hatimaye China imeanza mpango wa kuzalisha mazao ya punda katika miji yake ili kukabiliana na zuio la baadhi ya nchi za Afrika ambazo zimepiga marufuku usafirishaji wa nyama na ngozi ya punda kwenda katika nchi hiyo.


Tanzania imeungana na nchi nyingine za Afrika kama vile Uganda, Botswana, Niger, Burkina Faso, Mali, na Senegal kupiga marufuku biashara ya kuuza punda kwasababu inatishia kutoweka kwa wanyama hao ambao wanatumiwa na wakazi wengi wa bara hilo katika shughuli za kiuchumi ikiwemo kusafirisha mizigo na kulima.


Uamuzi wa kuzalisha punda wengi nchini China umefikiwa na kampuni ya Dong-E-E-Jiao ambayo inajihusisha na uagizaji wa ngozi ya punda kutoka nchi mbalimbali duniani ili kutengeneza dawa ya asili ijulikanao kama ‘ejiao’.


Akihojiwa na gazeti la Financial Times, Makamu rais wa kampuni hiyo, Liu Guangyuan amesema wanaagiza ngozi 450,000 za punda kila mwaka ambapo bei yake imepanda maradufu hadi kufikia Dola za Marekani 473 (Tsh. Milioni 1.065) kwa ngozi moja.


Kutokana na ongezeko la mahitaji ya ngozi wanapanga kufungua vituo vya uzalishaji wa mazao ya punda ili kukidhi mahitaji ya wateja wa dawa ya ‘ejiao’.


“Dong-E-E-Jiao imewekeza kwenye vituo vya uzalishaji katika majimbo 3 ya Kaskazini mwa China, ikitumia upandikizaji wa mbegu wa punda wakubwa ambao ngozi yake ni kubwa kuliko punda wa kawaida” amesema Liu na kuongeza kuwa,


“Hadi 2020 vituo vya uzalishaji vitatengeneza ngozi ya punda ya kutosha kukidhi mahitaji ya msingi”.


Amebainisha kuwa wakati wanaendelea kujenga vituo vya uzalishai, wamezigeukia nchi za Amerika ya Kusini ikiwemo Brazil, Colombia na Mexico ambazo zimefungua milango ya kuuza ngozi ya punda ili kujipatia faida kubwa.
Daah, yaani hapa tumepoteza forex za kutosha, hii demand lazima ingeongeza Uzalishaji sana. Lazima Punda wangeanza kufugwa kibiashara na kuongeza ajira.

Waafrika akili zetu tunazijua wenyewe.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Inahitajika maandalizi kwenye hili... Niliwahi kufanya kazi kwenye kiwanda bucha cha punda Dodoma.. Kwa siku walikuwa wanalala punda mia tatu.. Kwa hesabu ya mwaka ni punda 100,800 Je tunao punda wa kutosha walau kwa miaka mitano tuu?
China nyama ya Punda na ngozi za punda zina soko kubwa mno. Kwa nini serikali haihamasishi ufugaji mkubwa wa punda Tanzania na kuanzisha minada ya punda?

Jr
 
BTW kwa nini china hawafugi punda? Mbona kitimoto wanaongoza kwa kufuga duniani? Kwa nini hawafugi punda kama wanapenda nyama yao?
Mtu anakuletea biashara halafu unasema kwa nini usifuge kwenu ?
mbona sisi ni wakulima wa mpunga lakini mchele tunaagiza nje pia
 
Mtu anakuletea biashara halafu unasema kwa nini usifuge kwenu ?
mbona sisi ni wakulima wa mpunga lakini mchele tunaagiza nje pia
Mbona nguruwe hawaji kununua? Huwezi kuelewa context ya swali langu ukiwa na kichwa chepesi. Biashara ya kimataifa siyo nyepesi hivyo.
 
China nyama ya Punda na ngozi za punda zina soko kubwa mno. Kwa nini serikali haihamasishi ufugaji mkubwa wa punda Tanzania na kuanzisha minada ya punda?
Kuna waziri alizuia wachina wasinunue punda Dodoma eti watanzania sio utamaduni wetu kula punda,halafu punda wanateswa,eti wataisha.Nilishangaa sana,rejeeni vyombo 2017 vya habari msiwe wasahaulifu.Yaani punda ufuge wewe mtu mmoja aje akupangie matumizi.
Hivi kubebesha punda mizigo sio mateso? Nenda njombe Kaone punda wanavyopandishwa steep slope na gunia la viazi huku kunamatope(so kujamba huko), ila kuwachinja ndo mateso,hao ndio viongozi wa kiafrika wanakula nguruwe ila punda sio utamaduni.Poor thinking!!!
 
2 Reactions
Reply
Back
Top Bottom