Tanzania kupoteza Trilioni 2 kwenye Utalii

Ingefaa waziri aweke 'komitimenti' kwamba utalii ukishuka naye cheo kinashuka mpaka kuwa 'tuwagaidi' maana vivutio vyenyewe havitangazwi vizuri kiiivyo mpaka tuwaongezee gharama nao waridhie
 
Wewe
Hujui unachoongea/unachoandika.

VAT is an indirect tax which was exempted, unlike Corporate tax.

Mtalii halipi kodi. Mtalii analipa tour company kwa package anayotaka kupitia wakala au directly.

Tour operator analipa TANAPA na NCAA (hayo ni mapato kwa serikali) kwa kila mtalii anayeingia katika mbuga na analipa kodi kutokana na faida kampuni inayopata.

Kwa hiyo kusema watalii hawalipi kodi ni kusema uongo au kuongea usichokijua.

Tour operator anauza package kwa mtalii, hapa ameuza bila VAT. Let's assume ameshauza $100 VAT excl. Sasa Gvt inasema VAT will be charged. $18 extra ambayo mtalii halipi maana ameshakulipa na kuingia mkataba na wewe. Tour company itapata loss ya hiyo $18. Fanya kwa watalii wote wanaokuja Tanzania kuanzia 01 July ambao most of them walishafanya bookings miezi na miaka nyuma.

Kampuni hizi zimeajiri Watanzania. Kampuni zinanunua vyakula kutoka kwa Watanzania. Zikipata hasara multiplier effect ni kubwa.
Wewe ndiyo aidha hujui cho chote kuhusu kodi za serikali au umeamua kupotosha kwa masilahi yako binafsi.

Kwa hiyo huo utaratibu uliokuwa unatumika kama ulivyouelezea unauona ni sahihi. Yaani mbuga ni za taifa kwa manufaa ya taifa. Halafu tunamuachia kampuni binafsi jukumu la kupokea fedha zote toka kwa watalii halafu baadaye eti akailipe TANAPA. Yaani hiyo kampuni binafsi ndiyo imekuwa mmliki wa hizo mbuga? Yaani TANAPA na TRA wamekaa tu inactively kumsubiri tour operator awaletee alichopata, wao hata data hawana. Hili haliwezi kuendelea. VAT na kodi zingine kama coperate tax lazima zote zilipwe na hawa operators na lazima wawe na mashine za EFDs. TANAPA, TRA na mamlaka mengine ya serikali kama immigration lazima sasa ziwe active ku track watalii hawa nia ya serikali kupata malipo yake stahiki.

Kisingizio eti cha multiplier effect, eti tunatoa ajira is just nonsense kwani nani ambaye hafsnyi ajira au hiyo multiplier effect? Kwanza ni vyema TANAPA yenyewe ikafanya shughuli zote zinazoendeshwa na hizo kampuni za tour operators.
 
Wewe ndiyo aidha hujui cho chote kuhusu kodi za serikali au umeamua kupotosha kwa masilahi yako binafsi.

Onyesha nilipopotosha. Usiseme mtu amepotosha bila kuonyesha alipopotosha. Kama hujui omba ueleimishwe. Hujui tofauti ya VAT na Income tax. Umeeleweshwa bure bila malipo bado unasema unapotoshwa.

Ujinga mzigo.

Kwa hiyo huo utaratibu uliokuwa unatumika kama ulivyouelezea unauona ni sahihi.

Utaratibu huo huo unatumika mpaka leo. Utaratibu huo haujabadilika. Wizara wala taasisi zake hazijabadili mfumo huo.

Kila mtalii anayeingia analipa kwa kadi kupitia wakala/kampuni ya utalii anavyoingia katika mbuga. Uliza ufundishwe. Unaonekana hujui chochote.

Umewahi kufika mbuga yotote?

Yaani mbuga ni za taifa kwa manufaa ya taifa. Halafu tunamuachia kampuni binafsi jukumu la kupokea fedha zote toka kwa watalii halafu baadaye eti akailipe TANAPA.

Wewe kweli hujui chochote.

Kampuni inalipa kwa kila mgeni inayomwingiza mbugani. Hailipi "baadae" bali inalipa pale inapoingiza mgeni mbugani. Si "baadae".

Hivyo hamna mtalii anayeingia mbugani bila kulipa. Malipo haya, kwa asilimia kubwa yanafanywa kielectroniki kwa kutumia kadi za TANAPA/NCAA. Mtalii atatoa wapi kadi hizi?

Hujui chochote afu unaropoka. Ndiyo nyie washauri wa wakubwa?

Yaani hiyo kampuni binafsi ndiyo imekuwa mmliki wa hizo mbuga?

Mbuga zinamilikiwa na Serikali. Serikali imeipa mamlaka taasisi kuziendesha. Taasisi hizi zinaingiza pesa kwa kupokea watalii. Watalii wanaletwa na makampuni binafsi. Makampuni haya yanalipa service charges zote za kuingiza watalii mbugani.

Yaani TANAPA na TRA wamekaa tu inactively kumsubiri tour operator awaletee alichopata, wao hata data hawana.

TANAPA/NCAA anapata mapato kutoka kwenye service fees ambazo ndiyo zina ongezeko la VAT. Kila mgeni anayeingia mbugani analipa kupitia kwa kampuni inayomwingiza mbugani. Hivyo TANAPA/NCAA inapata mapato yote. Tafuta mtu wa TANAPA/NCAA akufundishe maana hujui kitu.

Na bado mnasema ni kheri waje watalii watatu kuliko mia. Si mtaua hizi taasisi za Serikali? Mkiziua si mbuga zitakufa? Idiots!

Pia, TRA hawachukui kitu kwenye service fees. TRA wanadeal na kodi ya mapato among other taxes. Kampuni inapoingiza faida inalipa kodi. TRA wanafanya assessment kila mwaka. Kusema "TRA wamekaa tu" ni ujinga wa hali ya juu.

Hujui tofauti ya tax and levies collected by TANAPA/NCAA and taxes collected by TRA.

Lakini upo hapa kubishana. Jifunze kabla hujabishana.

Hili haliwezi kuendelea. VAT na kodi zingine kama coperate tax lazima zote zilipwe na hawa operators na lazima wawe na mashine za EFDs.

Ujinga mwingine unaongea. Hujui lakini unaandika tu. VAT is an indirect tax, Corporate tax is a direct tax. Kasome ujue tofauti ya hivyo viwili.

Kwa sababu serikali imeeka VAT kwenye hizo service charges, taasisi za serikali inabidi ziwe na EFD machines.

Wewe unayeuza inakubidi sasa uwe na EFD machine. NCAA/TANAPA mpaka sasa hawana EFD machines. Umeelewa?

TANAPA, TRA na mamlaka mengine ya serikali kama immigration lazima sasa ziwe active ku track watalii hawa nia ya serikali kupata malipo yake stahiki.

Immigration inarekodi za wageni walioingia kwa dhumuni la utalii. Visa fee is $50. Mtalii awe "maskini au tajiri" wote wanalipa sawa hapo. Kusema "maskini" wasije ni kuipotezea immigration mapato kupitia visa fees. Lakini mmeamua kujivika ujinga.

Pia TANAPA/NCAA wana namba zote za watalii walioingia mbugani. Kwa kila mtalii kuna form inajazwa. Hujui unachoongea. Badili ID haikufai.

Kisingizio eti cha multiplier effect, eti tunatoa ajira is just nonsense kwani nani ambaye hafsnyi ajira au hiyo multiplier effect? Kwanza ni vyema TANAPA yenyewe ikafanya shughuli zote zinazoendeshwa na hizo kampuni za tour operators.

Ungejua maana ya Utalii kuwa a major foreign currency earner ungeelewa maana ya multiplier efffect.

Unasema TANAPA ifanye shughuli zote zinazoendeshwa na tour operators? Unajua shughuli za tour operators? Kweli mmeamua kuua utalii. Ignorance is bliss. Endelea kuamini ujinga wako.
 
Hivi tunafuta wingi wa watalii wasionatija kwa taifa au watalii wachache wenye tija kwetu.
 
Tanzania tuna watalii wengi? #Manton
Pamoja na misuko suko ya Alshabab na mengineyo, Bado Kenya wanatuzidi na idadi ya Watalii miaka 2014 na 2015

Sasa hao watalii matajiri mnaosema wako wapi?

Watalii wangapi matajiri wamekuja Tanzania mwaka 2015?

Utalii ni sekta changa Tanzania, marketing is needed very much
 
Lakini mkuu The Boss hii 18% VAT itaiingizia serikali tshs bilioni 7.

Hivyo TRA wamegundua hiyo "loophole".

Idadi ya watalii wataongezeka kutoka milioni 1 hadi milioni 2.

Serikali nyingi sasa zinazuia biashara haramu ya nyara za serikali kupitia uwindaji haramu, hivyo utalii kwa njia hii unapungua.

Asilimia 18 ya VAT inayokatwa ni ndogo sana kwenye huduma kama ya kukodisha turubai la kulala porini kwa siku saba au huduma ya wabeba mizigo.

Asilimia 18 haitakatwa kwenye package nzima ya mtalii akija bongo kiasi cha kumfanya huyo mtalii asitishe safari yake.

Mtalii anapofika Arusha na anaanza kutumia huduma za hapo si ndipo anapoambiwa kuwa gharama ya kukodisha turubai imepanda kidogo?

Kwahio kwa mfano mkodishaji turubai ambae ni mlipa kodi kihalali anapaswa kuwa na stakabadhi ya malipo na mashine ya kufanyia malipo ili aweke hesabu zake sawa.

Bila hii kodi serikali inakuwa inakosa pato la bilioni 7.

Hivyo hiyo ndio njia dhahiri ya kukusanya kodi hiyo.

Mkuu Richard, Tanzania haipokei watalii milioni 1 kwa mwaka, idadi ya milioni moja ni jumla ya watu wote waingiao nchini yaani 'arrivals', ikiwemo watokao nchi jirani kwa shughuli mbalimbali..jumla ya watalii wanaokuja hawafiki nusu ya hiyo idadi...
 
jamani huko serengeti hivi sasa kuna utitiri wa watalii. inamaana VAT haijaanza bado?
 
Back
Top Bottom