Tanzania kuna ombwe la uongozi? Zanzibar kuna Taharuki

KISHADA

JF-Expert Member
Oct 18, 2012
2,224
3,290
Kinachoendelea hapa Tanzania si cha kawaida. Tunaweza tukajiliwaza kwamba tuko kwenye mpito kutoka uzembe na ufisadi ULIOPITILIZA KUELEKEA KWENYE MABADILIKO KAMA WATAWALA WANAVYOTAKA TUAMINI lakini nje ya duara hilo kuna masuali hayana majibu.

Kisiasa hali hairidhishi, ni kama nchi ina ombwe fulani. Na ubaya hapatafutwi dawa mujarabu chuki na vitendo vya kuumbuana na maneno yasio staha yametamalaki. Kumejitokeza matendo ya kurudisha nyuma mustawa wa siasa. Kwa kiasi licha ya kukosa maendeleo mengine kama uchumi imara siasa ilijitahidi na kuvumiliana kulikuwa kukubwa jambo lililoendeleza umoja na mshikamano kama taifa licha ya itikadi tofauti za kisiasa. Kwa sasa hali ni mbaya na siasa imerejeshwa na watawala wenyewe kwa kutumia mkakati wa kuinyima demokrasia ya siasa kufanya kazi. Uhai wa vyama vya siasa ni kufanya siasa na hoja za kisiasa hujibiwa na wanasiasa sio kuziba midomo.(ya bungeni ni mfano.

Kiuchumi hali hairidhishi. Unafuu haujapatikana na maisha yamezidi kuwa ghali sana. Licha ya jitihada za watawala za ahadi na kutaka kupewa muda dalili hazionekani. Watu wa uchumi wana kazi ya ziada kuwafahamisha wananchi wanaoelekea kukata tamaa.

Kijamii, watu wanaanza kufarakana kunakosababishwa na hayo hapo juu ya mifarakano ya siasa na kiuchumi. Nchi inaanza kwa taratibu kuingia katika mifarakano kwa wanajamii. Kipindi hiki cha utawala yote hayo yamekuja kwa kasi mno.

ZANZIBAR.
Ikiwa Tanzania kuna au hakuna Ombwe la Uogozi hilo litajulikana baadae, lakini Zanzibar ni wazi kuna taharuki. Ni taharuki ya kisiasa kutokana na uchaguzi wa 2015 kwa mnasaba wa kile kinachoendelea. Kususiana, kutishana, kupigwa watu na kuvamiwa, kuteswa na kunyanganyana mali ndio mfumo halisi wa maisha ya Zanzibar kwa sasa.

Vyombo vya ulinzi vinaendelea na kutoa majibu yasiotosheleza kila pale panapotokea hujuma.
Hakuna kiongozi anaeguswa kwa udhati ni lini hali itarudi kama awali. Hilo suali halipo na hakuna anaeguswa.

Hii ni taharuki ya wazi. Ni taharuki kwa kuwa haijulikani Zanzibar inakwenda wapi na suluhu ya karibu haionekani. Ni taharuki kwa kuwa viongozi wakuu wa kisiasa wa vyama wamesusiana na kutengana kwa muda sasa, Hakuna Ajenda ya kitaifa kwa sasa ni vijembe na kutupiana mpira kila mmoja akimshutumu mwenzake.
Ni taharuki kwa kuwa hata viongozi wa kijamii na kidini wametofautiana na hawana msimamo wa pamoja kuhusu kinachoendelea Zanzibar kwa sasa.

Tanzania kama nchi inahitaji tujitafakari, Tunakoelekea siko.

Nauliza tu, Tanzania kuna ombwe la Uongozi?
 
Kinachoendelea hapa Tanzania si cha kawaida. Tunaweza tukajiliwaza kwamba tuko kwenye mpito kutoka uzembe na ufisadi ULIOPITILIZA KUELEKEA KWENYE MABADILIKO KAMA WATAWALA WANAVYOTAKA TUAMINI lakini nje ya duara hilo kuna masuali hayana majibu.

Kisiasa hali hairidhishi, ni kama nchi ina ombwe fulani. Na ubaya hapatafutwi dawa mujarabu chuki na vitendo vya kuumbuana na maneno yasio staha yametamalaki. Kumejitokeza matendo ya kurudisha nyuma mustawa wa siasa. Kwa kiasi licha ya kukosa maendeleo mengine kama uchumi imara siasa ilijitahidi na kuvumiliana kulikuwa kukubwa jambo lililoendeleza umoja na mshikamano kama taifa licha ya itikadi tofauti za kisiasa. Kwa sasa hali ni mbaya na siasa imerejeshwa na watawala wenyewe kwa kutumia mkakati wa kuinyima demokrasia ya siasa kufanya kazi. Uhai wa vyama vya siasa ni kufanya siasa na hoja za kisiasa hujibiwa na wanasiasa sio kuziba midomo.(ya bungeni ni mfano.

Kiuchumi hali hairidhishi. Unafuu haujapatikana na maisha yamezidi kuwa ghali sana. Licha ya jitihada za watawala za ahadi na kutaka kupewa muda dalili hazionekani. Watu wa uchumi wana kazi ya ziada kuwafahamisha wananchi wanaoelekea kukata tamaa.

Kijamii, watu wanaanza kufarakana kunakosababishwa na hayo hapo juu ya mifarakano ya siasa na kiuchumi. Nchi inaanza kwa taratibu kuingia katika mifarakano kwa wanajamii. Kipindi hiki cha utawala yote hayo yamekuja kwa kasi mno.

ZANZIBAR.
Ikiwa Tanzania kuna au hakuna Ombwe la Uogozi hilo litajulikana baadae, lakini Zanzibar ni wazi kuna taharuki. Ni taharuki ya kisiasa kutokana na uchaguzi wa 2015 kwa mnasaba wa kile kinachoendelea. Kususiana, kutishana, kupigwa watu na kuvamiwa, kuteswa na kunyanganyana mali ndio mfumo halisi wa maisha ya Zanzibar kwa sasa.

Vyombo vya ulinzi vinaendelea na kutoa majibu yasiotosheleza kila pale panapotokea hujuma.
Hakuna kiongozi anaeguswa kwa udhati ni lini hali itarudi kama awali. Hilo suali halipo na hakuna anaeguswa.

Hii ni taharuki ya wazi. Ni taharuki kwa kuwa haijulikani Zanzibar inakwenda wapi na suluhu ya karibu haionekani. Ni taharuki kwa kuwa viongozi wakuu wa kisiasa wa vyama wamesusiana na kutengana kwa muda sasa, Hakuna Ajenda ya kitaifa kwa sasa ni vijembe na kutupiana mpira kila mmoja akimshutumu mwenzake.
Ni taharuki kwa kuwa hata viongozi wa kijamii na kidini wametofautiana na hawana msimamo wa pamoja kuhusu kinachoendelea Zanzibar kwa sasa.

Tanzania kama nchi inahitaji tujitafakari, Tunakoelekea siko.

Nauliza tu, Tanzania kuna ombwe la Uongozi?
Post/Mawazo mazuri, lkn watu wameshaingiwa woga, hakuna aliyetayari kujibu! Let us start- Power vacuum defined: In political science and political history, the term power vacuum is an analogy between a physical vacuum, to the political condition "when someone has lost control of something and no one has replaced them." The situation can occur when a government has no identifiable central power or authority.
Q: Tunakubaliana na definition hiyo? Then from there we will have the same base to start our arguments. If the answer is in the affirmative, then we have power vacuum, and vice versa!
 
Tuna taka Katiba inayotokana inayotokana na rasmu ya Warioba. Rais akipunguziwa madaraka nchi itakwenda.
 
Nyie watu mnashughulika na nini hasa?Mpo sana kimajungumajungu na akili yenu nyepesi kweli.Majungu yenu yalikuwa mengi wakati wa uchaguzi mkuu, lakini hayakuleta tija, bado mmekazana??Nyie ndo wale majizı na mliozoea kujilimbikizia pesa kwa dili bila kufanya kazı.Kikwete aliwalea km wajukuu, kawadekeza mpaka mkawa wajinga, sasa baba karudi na heshima lazima irudi.
 
Post/Mawazo mazuri, lkn watu wameshaingiwa woga, hakuna aliyetayari kujibu! Let us start- Power vacuum defined: In political science and political history, the term power vacuum is an analogy between a physical vacuum, to the political condition "when someone has lost control of something and no one has replaced them." The situation can occur when a government has no identifiable central power or authority.
Q: Tunakubaliana na definition hiyo? Then from there we will have the same base to start our arguments. If the answer is in the affirmative, then we have power vacuum, and vice versa!

Sawa.
Tukijikita hapa "when someone has lost control of something and no one has replaced them." Kwa tafsiri yoyote iwayo, nchi inaelekea siko na kwa sasa ni wazi hakuna anaechukua nafasi ya kuziba mianya hii ya minyukano inayoendelea.

Hakuna wakosoaji na wakemeaji kutoka makundi mengine. Wanaojaribu ni wanasiasa wapinzani lakini nao huandamwa. Utamaduni huu wa kutovumilia ukosoaji unakuwa kwa kasi na unalazimishwa uonekane ndio mfumo wa sasa wa siasa zetu.
 
Dahh kila nikiiangalia znz ndio hasa sijui inaelekea wapi kuna madudu kibao yanafanyika lkn nani aseme waliopiga kelele baraza lao wakilishi wamestopishwa sijui tunaekekea wapi znz ndio giza limetanda hasaa mabucha yanafungwa jumamosi kisa tukanunue nyama ya dhulma kwa lazma kwa wale wanyama walokamatwa na polisi
 
Nyie watu mnashughulika na nini hasa?Mpo sana kimajungumajungu na akili yenu nyepesi kweli.Majungu yenu yalikuwa mengi wakati wa uchaguzi mkuu, lakini hayakuleta tija, bado mmekazana??Nyie ndo wale majizı na mliozoea kujilimbikizia pesa kwa dili bila kufanya kazı.Kikwete aliwalea km wajukuu, kawadekeza mpaka mkawa wajinga, sasa baba karudi na heshima lazima irudi.

Kwa hiyo heshima inarudishwa kwa gharama ya kunyima demokrasia na kuvunja umoja wa watanzania. Inashindikana nini kurudishwa kwa njia za kistaarabu bila kuathiri haki za kisiasa za wengine. Yaani hayo yakiachwa yakienda hivyo tutakuwa ni kama tuna hilo ombwe. Lazima watu wachukuwe nafasi zao kuondowa sintofahamu hii.
 
Dahh kila nikiiangalia znz ndio hasa sijui inaelekea wapi kuna madudu kibao yanafanyika lkn nani aseme waliopiga kelele baraza lao wakilishi wamestopishwa sijui tunaekekea wapi znz ndio giza limetanda hasaa mabucha yanafungwa jumamosi kisa tukanunue nyama ya dhulma kwa lazma kwa wale wanyama walokamatwa na polisi

Hii Kadhia ya NGOMBE niliwahi kuiandiia hapa JF mod wakaiweka vyengine. Vikosi vya SMZ vinashiriki zoezi hili na Polisi wakiulizwa majibu yao hayatoshi.

Zipo taarifa za watu kunyanganywa mifugo yao majumbani mwao na kwenye mazizi. Wakiulizwa wenye dhamana wanasema wanakamata mifugo inayodhurura ovyo barabarani. Tayari watu wameathirika kwa kupigwa risasi na inasemekana baadhi walifariki baadae kwa kadhia hii. Watu walionyanganywa ngombe wanatakiwa wakagombowe mifugo yao kwa Sh. laki tatu(300,000). Wengine wanakwenda hawakuti ngombe wao na hujibiwa ovyo. Zoezi limekwenda kienyeji na ubabe umetumika bila kufuata sheria. Hakuna rikodi za waliochukuliwa mifugo yao na yoyote anaweza kwenda na kugombowa akiaminiwa kuwa ndio mwenyewe.

Hali hio inatia aibu nchi na Serikali ya watu. Imetoka katika misingi yake na vikosi ama Zombie hutumika kufanya uharamia.

Hali hii inanasibishwa na siasa na visasi ndio nikasema Zanzibar kuna Taharuki.
 
Nyie watu mnashughulika na nini hasa?Mpo sana kimajungumajungu na akili yenu nyepesi kweli.Majungu yenu yalikuwa mengi wakati wa uchaguzi mkuu, lakini hayakuleta tija, bado mmekazana??Nyie ndo wale majizı na mliozoea kujilimbikizia pesa kwa dili bila kufanya kazı.Kikwete aliwalea km wajukuu, kawadekeza mpaka mkawa wajinga, sasa baba karudi na heshima lazima irudi.
Umepagawa wewe mambo hayo peleka Lumumba kusoma hukusoma basi hata picha ya mgombea huioni huoni hali ya maisha ilivyo kuwa ngumu au wewe in katika mijizi ya nchi hiii
 
Mioyo ya watu imejaa chuki

Hilo watawala na mawakala wao hawalioni. Wanaendeleza tension na kuifanya siasa kuwa juu bila sababu.
Tulipofika ilitakiwa tusifike ama jitihada za kimkakati kuyamaliza haya ziwe zimepamba moto.

Kwa sababu hatujui ndani kinaendelea nini, huku nje acha tuseme.

Kweli chuki inakuwa kwa kasi Tanzania nzima, na Kwa Zanzibar ni kama kunasubiriwa muda tu jamii iparaganyike zaidi.
 
Kweli kuna power vacuum, tangu pro Lipumba ajihudhuru na Dr Slaa kuajia madaraka ndani ya UKAWA hakuna uongozi, kila mtu kambale, kama kondoo wasio na mchungaji kila mtu na wazo lake
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom