Kampuni ya Serikali ya Korea inayoitwa Korea Resources Corporation imeishauri Serikali ya Tanzania kupitia Wizara ya Nishati na Madini kuanza kuchimba madini ya TUNGSEN (Business Worth USD 600M per annum) pamoja na COBALT.
Hivi karibuni Wizara ilikamilisha uandaaji wa Ripoti ya Aina za madini yaliyopo katika Ardhi ya Tanzania ambapo COBALT na TUNGSEN ni miongoni mwa madini ya thamani yaliyopo nchini, Kampuni mbalimbali za Korea tayari zimeweka nia ya kuanza uchimbaji wa madini hayo nchini, STAMICO imetakiwa kujiandaa kupokea makampuni hayo makubwa kutoka Korea na kufanya nao mazungumzo ya namna ya kushirikiana baina ya Kampuni hizo na STAMICO.
Serikali kupitia Wizara ya Nishati na Madini Imeanzisha kamati maalum ya kuratibu na kusimamia ushirikiano wa nchi mbili hizo, kamati hiyo yenye jina TANZANIA and SOUTH KOREA INTER-MINISTERIAL COMMITTEE ON ENERGY AND MINERALS itahusisha maafisa kutoka wizara inayosimamia nishati na madini ya hapa nchini na ile ya Korea. Miongoni mwa mambo ya msingi ambayo kamati hiyo imeyazingatia na kuanza nayo ni kuratibu na kudhamini Kampuni hasa za Tanzania kupata mtaji na mikopo kutoka AFRICA Fund for ENERGY.
Mipango hii ya Wizara ya Nishati na Madini inalenga kujenga ustawi kwa makampuni ya wazawa ya Tanzania ili kupata mitaji na mikopo ya kuendesha miradi mbalimbali mikubwa na hivyo kunufaika na maliasili za hapa nchini.
Juhudi hizi za Prof Sospeter Muhongo chini ya Wizara yake ya Nishati na Madini zinabatilisha madai ya uzushi na tuhuma ambazo anashutumiwa kuwa anapingana na sera ya Uzawa na kwamba anapendelea makampuni ya nje katika uwekezaji na kunufaika kutokana na rasilimali za Tanzania.
Profesa Muhongo yuko safarini nchini Algeria kwa mwaliko rasmi kutoka kwa Waziri wa Nishati alioutoa October mwaka huu, katika safari yake hiyo tayari kampuni mbalimbali zimeshaingia makubaliano na kampuni za Tanzania kuja kuwekeza katika usambazaji wa gesi ya matumizi ya ndani, kampuni hizo ni pamoja na NAFTAL. Pia nafasi mbalimbali zimepatikana katika vyuo vya mafuta na gesi nchini Algeria na Serikali inategemea kupeleka wanafunzi nchini Algeria mwanzoni mwakani.
Hivi karibuni Wizara ilikamilisha uandaaji wa Ripoti ya Aina za madini yaliyopo katika Ardhi ya Tanzania ambapo COBALT na TUNGSEN ni miongoni mwa madini ya thamani yaliyopo nchini, Kampuni mbalimbali za Korea tayari zimeweka nia ya kuanza uchimbaji wa madini hayo nchini, STAMICO imetakiwa kujiandaa kupokea makampuni hayo makubwa kutoka Korea na kufanya nao mazungumzo ya namna ya kushirikiana baina ya Kampuni hizo na STAMICO.
Serikali kupitia Wizara ya Nishati na Madini Imeanzisha kamati maalum ya kuratibu na kusimamia ushirikiano wa nchi mbili hizo, kamati hiyo yenye jina TANZANIA and SOUTH KOREA INTER-MINISTERIAL COMMITTEE ON ENERGY AND MINERALS itahusisha maafisa kutoka wizara inayosimamia nishati na madini ya hapa nchini na ile ya Korea. Miongoni mwa mambo ya msingi ambayo kamati hiyo imeyazingatia na kuanza nayo ni kuratibu na kudhamini Kampuni hasa za Tanzania kupata mtaji na mikopo kutoka AFRICA Fund for ENERGY.
Mipango hii ya Wizara ya Nishati na Madini inalenga kujenga ustawi kwa makampuni ya wazawa ya Tanzania ili kupata mitaji na mikopo ya kuendesha miradi mbalimbali mikubwa na hivyo kunufaika na maliasili za hapa nchini.
Juhudi hizi za Prof Sospeter Muhongo chini ya Wizara yake ya Nishati na Madini zinabatilisha madai ya uzushi na tuhuma ambazo anashutumiwa kuwa anapingana na sera ya Uzawa na kwamba anapendelea makampuni ya nje katika uwekezaji na kunufaika kutokana na rasilimali za Tanzania.
Profesa Muhongo yuko safarini nchini Algeria kwa mwaliko rasmi kutoka kwa Waziri wa Nishati alioutoa October mwaka huu, katika safari yake hiyo tayari kampuni mbalimbali zimeshaingia makubaliano na kampuni za Tanzania kuja kuwekeza katika usambazaji wa gesi ya matumizi ya ndani, kampuni hizo ni pamoja na NAFTAL. Pia nafasi mbalimbali zimepatikana katika vyuo vya mafuta na gesi nchini Algeria na Serikali inategemea kupeleka wanafunzi nchini Algeria mwanzoni mwakani.